Prof. Samuel Manyele wa Tume ya vinyesi vya Ng'ombe Mto Mara

Prof. Samuel Manyele wa Tume ya vinyesi vya Ng'ombe Mto Mara

Wewe unayemtetea uwezo wako ni kama wake wa kuhongwa hela kubadili ripoti. Of course hata ningekuwa mimi ndiyo professor ningechukua hela ili kulinda uhai wangu. Kipindi hiki serikali inalinda wawekezaji kuliko uhai wa watanzania. Prof angeshupaza shingo wangemuua. Hivyo tumuelewe hiki ndicho kipindi cha hivyo. Hata akina Prof Kabudi au Prof Luoga asingekuwa Dkt Magufuli wangeuawa na ripoti zao za madini na makinikia etc. Kwa ufupi Prof tusimlaumu ila tuwalaumu kundi la mafisadi lililokumbatiwa na serikali. Prof kafanya hivyo kutetea uhai wake.

Unasoma wapi kuwa ninamtetea huyo profesa kiasi cha wewe hata kuujua uwezo wangu wa kuhongwa?

Kuutambua uwezo wake ili kuweza kupambana na ukakasi wa ripoti yake (head on) wewe inakupa taabu mno?

Kwamba hatimaye tukajua Professor Manyele ni nguli kwenye eneo lake la utaalamu.

Kwamba hakukosa wasaidizi wowote ambao angewahitaji. Kwamba alikuwa na access zote katika maabara zozote nchini hadi nje ya nchi, nk nk.

Wewe bado huoni kuwa tuna tatizo kubwa zaidi linalohitaji kujizatiti kweli kweli kukabiliana nalo na kuwa na facts za kutosha ni jambo la muhimu mno?

Ripoti ya Vinyesi vya Ng'ombe mto Mara haishawishi

Nina taabu na ripoti hii labda kuliko hata wewe mjomba.

Habari ndiyo hiyo.
 
Mr. Muchunguzi buana you seem to had aimed where you could not reach. It is not uncommon.

Pole sana.

Kwetu akibobea mtu tunampongeza. Hatuwezi kubobea wote.

Habari ndiyo hiyo.
Andika kiswahili boss! English huiwezi.


Correction:
Mr. Muchunguzi buana you seem to have aimed at where you could not reach
 
Andika kiswahili boss! English huiwezi.
Correction:
Mr. Muchunguzi buana you seem to have aimed at where you could not reach

Umehamia kwenye kusahihisha kiingereza?

Kwani Borris Johnson anakijua Kiswahili?

Kiingereza si ni lugha tu kama ilivyo kwa Kimasai kwa Mmasai na Mhaya?

Huna hoja, huna lolote. Uko kama ling'ombe tu.

Mwenye kukijua kiingereza utakuwa wewe?

Ninakazia wala uwezo huo wa kunisahihisha huna Mr. Muchunguzi.

Bure kabisa!
 
Niko wazi mkuu huyu jamaa yumkini si reja reja.

Alikuwa Mkemia Mkuu wa Serikali huyu mwamba?

Yumkini hawezi kuwa reja reja.
Hiyo "reja reja "umemaanisha nini? Kuna wengine wa "jumla".

Usifikiri msamiati (locution) wako na wenzako mliozoeana nyumbani kwenu basi kila ausomae atauelewa.
 
Ni ndugu yake amekuja kumsafisha

Hivi eeh? Kwa ushahidi upi mkuu? Au kama wa Sirro tu na wale watuhumiwa wa ugaidi?

Kwa mitazamo miepesi miepesi kama hii tunayo safari ndefu sana kuipata katiba mpya.

Yumkini kila mtu ni mtuhumiwa wa usaliti isipokuwa wewe tu?

Hiiiiii bagosha!
 
Hivi eeh? Kwa ushahidi upi mkuu? Au kama wa Sirro tu na wale watuhumiwa wa ugaidi?

Kwa mitazamo miepesi miepesi kama hii tunayo safari ndefu kuipata katiba mpya.

Yumkini kila mtu ni mtuhumiwa wa usalitiisipokuwa isipokuwa wewe tu?

Hiiiiii bagosha!
Sawa
 
Hiyo "reja reja "umemaanisha nini? Kuna wengine wa "jumla".

Usifikiri msamiati (locution) wako na wenzako mliozoeana nyumbani kwenu basi kila ausomae atauelewa.

Ulitaka nitumie msamiati wako bibie? Kwetu usukumani kwao jiwe. Ndiyo lugha zetu hizo ati.

Hiiiiii bagosha!
 
Unaweza kuwa umeona katika maandiko yangu kwenye uzi huu. Ripoti ya Professor ina ukakasi wa kutosha. Ila sasa namna ya kumwingia inabidi kujipanga.

Ndiyo maana kumekuwa na background checks, fact checks na maboresho ya hapa na pale kila ilipobidi (credit kwako fizoG).

Hizi hapa ni facts:

"Ng'ombe wa beberu aliyenona vilivyo (540kg) anakula takribani 15kg tu kwa siku.

Determining How Much Forage a Beef Cow Consumes Each Day
Mkuu una uhakika na uchoongea ?, Kumbuka hao wanaongea forage (yaani nutritious forage /yenye virutubisho) na hio kwa wewe unayewalisha its to your advantage kuwapa as less as possible...

Sasa kama wanakula makapi (garbage in garbage out) huenda ikahitajika content nyinzi zaidi ya makapi ili kupata nutrient ile ile...., Sasa tukija kwenye how much kgs can an average cow excrete ?, Ngoja ni-contact google kama ulivyofanya...., na hapo utaona figure iliyotolewa sio ya ajabu...,


 
Mkuu wangu hapa chini ni bandiko langu jana punde baada ya kusikia habari hizi:

View attachment 2158036

Uzi:

Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndiyo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini

Kimsingi nilikuwa na usongo mkubwa na huyu mwamba ndiyo kisa katika kujizatiti nikayakuta na haya:

Mkemia Mkuu Ato Siri ya Kupimwa Mkojo kwa Wahalifu

Ukikuta hayo kimsingi unafanya je ukigundua kumbe maji ni marefu?

Kiungwana tunatafuta inputs zaidi.

Au nasema uongo ndugu Kennedy ?
Hii comment iko wapi niigongee like.

"Hivi wale Nyumbu, Simba, etc huwa hawajisaidii ni mbuzi, n'gombe na kondoo tu"
 
Ambao mnabisha pelekeni hoja zenu pia na facts.....

Prof wa kinyesi cha ng'ombe ndio amesha wasilisha findings zake,,, na nyie pelekeni zenu
 
Kwa kweli mkuu inashangaza sana... Yaani kinyesi cha Ng'ombe kiue samaki?

Report ya Profesa ni batili....
Watu wanafuga samaki na kutumia kinyesi cha ng'ombe kama source ya chakula chao. Hii haieleweki inantaka ufafanuzi zaidi
 
Ambao mnabisha pelekeni hoja zenu pia na facts.....

Prof wa kinyesi cha ng'ombe ndio amesha wasilisha findings zake,,, na nyie pelekeni zenu

Option iliyopo si kuleta zetu tu. Kuna utafiti huru au hata wa kutumia wataalamu wengine.
 
Watu wanafuga samaki na kutumia kinyesi cha ng'ombe kama source ya chakula chao. Hii haieleweki inantaka ufafanuzi zaidi
Hao wao wanaweka kinyesi kiasi gani lorry zima kwenye ukubwa wa Bwawa la Wastani ?

Kumbuka samaki wanachokula ni algae, kinyesi ni mbolea ya hao algae..., ukiweka kingi kupita kiasi na algae waka-bloom kuliko consumption wakati hakuna photosynthesis na algae wana-consume oxygen hivyo kinachopelekea ni less dissolved oxygen hapo ukiamka asubuhi unakuta samaki wote matumbo juu Also Known As Belly - Up, AKA Dead....
 
Back
Top Bottom