Profesa Assad: Katiba Mpya sawa ila isitupe mtu ambaye hawezi kumsikiliza mtu yeyote kama ilivyokuwa

Huyu mzee anasononeko la moyo mpaka linamkereketa.huyu Mzee anatakiwa kukubali Rais ni cheo kikubwa Sana na anakuwa anajidhalilisha kuzungumzia kitu kinachomtesa.

Na inaonyesha Magufuri alimjua kwamba ni mnafiki ndo mana wabunge walimtimua na makaratasi yake!!!
 
Tatizo la watanzania hawataki kukubali kwamba kiongozi mzuri anaongoza kwa mawazo yake na ahadi alizotoa kabla ya kuchaguliwa. Sasa kila mtu anataka ajizukie eti kumshauri. Ushauri ukikataliwa ooh hakubali ushauri. Hakubali ushauri wako kwani wewe ndio umechaguliwa kua rais?
Kwa mfano jpm alikua anasikiliza sana maoni ila alifuata maoni aliyoona yanafaa kufuatana na staili yake na jinsi yeye aliona sawa.
Yeye alijali maslahi ya umma. Kwa hivyo aliona mawazo yenye kuleta maendeleo ya umma ndio bora. Sasa kuna watu ushauri wao ni kupata suluhu ya maslahi yao binafsi rais akiwatolea nje ndio utasikia ooh sio msikivu.
 

Katiba mpya lazima isimike uhuru (independence) wa Bunge na mahakama [emoji817], imweke Rais na familia yake chini ya utawala wa sheria na kuwe na taasisi huru (autonomous commissions) za utumishi wa vyombo vya dola zitakazosimamia teuzi, vyeo na nidhamu za maafisa na viongozi wa vyombo vya dola kwa kushirikiana na kamati ya Bunge ya ulinzi na usalama wa taifa. Rais awe anapelekewa mapendekezo kuidhinisha tu.

Hiyo ndiyo namna pekee ya kuepuka Rais kuwa mtu wa hatari nchini. Short of that hata mchague malaika, nchi imejaa waroho wanaovizia fursa za kifisadi watakaohakikisha “mtu wao” anakamata dola sawa sawa na kuhakikisha hakuna mtu anayefurukuta mbele ya “wenyewe”. Katiba isipozingatia hayo ni bora kuachana kabisa na zoezi hilo status quo iendelee.

Man, devoid of constraints, is never rational.
 

Na kwa wanaomsifu? Kinyaa pia?
 
nimesikia kama Magufuli amechambuliwa. Naungana na Prof nchi ilipoteza uelekeo
 
Prof anazungumzia katiba kwa kutoa mifano hai katiba iliponajisiwa. mnapenda msikie mifano ya Rwanda hamtaki kusikia yenu?
 
Sahihi Mkuu

ndio hoja kuu ya Prof Assad na mawazo haya yanafanana na ya Bobywine alipozungumza kwenye Hadhara kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)

Tatizo letu kubwa ni watu kutoheshimu katiba kuliko udhaifu kwny contents za Katiba yenyewe



Kwa lugha nyepesi "je uwezo wa Watu Kuisimamia katiba mpya upo?" Kama tunao uwezo tutafaidika sana na katiba mpya, lau kama hatuna watu wa kusimamia na kuitekeleza kinaweza kuwa kiroja!
 
Ndio mtaelewa kwamba Katiba sio jibu la kila kitu
 
2025 tungetest mitambo kwa Prof Assad angalau miaka 5 tu. Anaupiga mwingi sana
 
Ili tuendelee tunahitaji wananchi wenye uthubutu wa kuwashughulikia viongozi ili viongozi wawatumikie wananchi.
Kwa sasa viongozi wanafanya wanalotaka kwa udanganyifu kuwa ni maslahi ya uma.
 
Prof. kasema vizur. Swali dogo tu. Hao watu/viongozi watakaosimamia utekelezaji wa katiba watapatikanaje na katika mazingira yapi ya kisheria na kisiasa kwa ajili ya kuwalinda katika utekelezaji wa majukumu hayo mazito.

Tusipuuze ukweli kwamba mpaka sasa tunayo katiba na mihimili yake - Serikali, Bunge na Mahakama. Tumekwama wapi mpaka tuanze kuzungumzia Katiba Mpya wakati zoezi la 2014 la katiba mpya yalijahitimishwa.
 
Mbona Nyerere anazungumzwa??
 
Hitler, Idd Amin, Mobuttu, Bokassa wanasemwa mpaka leo sembuse magufuli.?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…