Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wanyakyusa ukiacha shule unaweza uliwa[emoji23][emoji23]Wanyakyusa wa Tukuyu wanafanana karibu kila kitu na Wahaya
RIP Msomi
Kweli mkuu 😊🤓🤓Usisahau ku enjoy maisha mkuu , maana maisha yetu ni mafupi sana kuyatumia yote kwa kusoma tu
Kuna tofaut ya kuwa na degree tatu? Na kuwa na shahada ya uzamivu? PhD I meanIla mkuu currently watu wana umwa vifua na mafua makali sanaa....
Mm mwenyewe hapa nimeng'ang'aniwa na mafua na kikohozi
AmenTia Nia mkuu inawezekana
Pengine Wana IQ kubwa maana wote wanakula ndizo ambazo zinaphosporousNakubaliana na wewe 100%
Yaan Madigirii yote hayo bado alikuwa AFISA MKUU DARAJA LA 1? Hata Umeneja au Ukurugenzi alikuwa hana.. aisee MAISHA haya.
Kuna watu wanaajiriwa siyo kwa kutafuta fedha,wanaajiriwa Ili kuzitimizia passion zao.Degree Zote hizo halafu alikuwa Kaajiriwa ?
Hata aliyowaachia hazina faida yoyoteSi material pekee ndiyo urithi pengine kawaachia maarifa kama yake na wapo more independent kuliko yeye mwenyewe
Kama carrots kwenu ni nyingi, kunywa juisi kila siku kama hamna tumia mawese mabichi au mbegu zake kwa eingi japo yanachangamoto zake kwa mtu ambae hajayazoea ila ni tiba.Sawa mkuu,
Macho hayana nguvu hasa jicho la kulia naona kabisa limepunguza uwezo wa kuona....
Napo andika hii comment nipo mbele ya computer 💻
This week ntaenda fanya check up ya macho..
🙄🙄🙄🙄🙄🙄Kuna watu wanaajiriwa siyo kwa kutafuta fedha,wanaajiriwa Ili kuzitimizia passion zao.
We una shida opi kati ya hixo mbili.Brother umemjibu huyo lakini wengi wetu ikiwemo mimi binafsi kuna kitu umezungumza nami.
asante sana.
Alitakiwa awe OSHO wa TANZANIA Osho alikuwa na maktaba yenye vitabu karibu 100000 na anadai alivisoma vyote. Baadae akaacha kuvisoma akawa anajibu maswali magumu na kazi zake zimehifadhiwa
Tupe hiyo michongo ya ku-make laki kwa saa kupitia smartphone....Asa unakomaa na hayo makaz ya nn , watu wanamake laki Kwa saa tuu only smartphone
Option ya carrot 🥕🥕🥕 naona itakua the best naanza Leo hiiKama carrots kwenu ni nyingi, kunywa juisi kila siku kama hamna tumia mawese mabichi au mbegu zake kwa eingi japo yanachangamoto zake kwa mtu ambae hajayazoea ila ni tiba.
Jina la ukoo kwa usahihi ni Mafwenga, si Mwafwenga! Poleni sana kwa wafiwa wote.
Aliyekuwa Afisa Usimamizi wa Fedha Mkuu Daraja la Kwanza wa Kitengo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), Profesa Handely Mwafwenga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Mwafwenga aliyekuwa na elimu ya digrii saba na shahada tatu za uzamivu (PhD) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo 19, 2023, wakati akipatiwa matibabu ya figo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.
Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na familia yake kupitia kwa mdogo wake, Innocent Mwafwenga ameeleza kuwa Profesa Handely ambaye ni kaka yake alifariki majira ya saa saba usiku.
“Jana alikuwa amezidiwa ghafla na alipelekwa jengo la wagonjwa mahututi (ICU) na tulipoenda asubuhi ya leo tumemkuta ameshafariki,”amesema Innocent.
Innocent amesema Profesa Mwafwenga kwa muda mrefu alikuwa anasumbuliwa na tatizo hilo japo haikufahamika lakini baada ya kupima ikabainika kwamba anachangamoto ya figo.
“Mwanzoni alikuwa hajagundulika alikuwa anaumwa lakini tulikuwa hatujui kama ni figo lakini baadaye baada ya kupima ikagundulika na figo na alianza kudhohofika kwa kipindi kama cha mwaka mmoja hivi,”amesema.
Innocent amesema kwa kipindi cha nyuma muda mwingi alikuwa analalamika matatizo ya mgongo lakini baada ya kuona tatizo hilo linazidi ndipo alipenda hospitali na kubainika anatatizo hilo.
Hata hivyo, Wizara ya Fedha kupitia kwa Katibu Mkuu, Dk Natu Mwamba imetoa pole kwa watumishi, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu kwa msiba huo.
Innocent amebainisha kuwa Profesa Mwafwenga aliyewai kuwa kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ameacha familia ya watu wa tano, mke na watoto wa nne.
“Watoto wake wote ni wakubwa kuna ambao wameshamaliza elimu ngazi ya vyuo na kuna baadhi wapo kazini,”amesema.
Kuhusu msiba, amesema unafanyika nyumbani kwake Mabwepande na keshokutwa wataanza safari kuelekea Tukuyu mkoani Mbeya kwa maziko.
Ameondoka yeye peke yake, vyeti kaviacha!Da! Hasara sana hii!Bahari Mbaya vyeti havilithiwi,ameondoka na vyeti vyake.
Ushauri mzuri sana, ila jina la ukoo kwa usahihi ni Mafwenga si Mwafwenga!Digrii nyingi Hazinaga urithi kwa watoto labda kama ameacha hazina ya kitaaluma. Ni bora uwekeze kwenye ardhi au viwanda watoto wako watarithi kuliko PhD nyingii za kutishia watu. PhD zote hizo bado ni muajiriwa kashindwa kuanzisha hata kampuni la kuuza utalaam(consultant co).
Mwafwenga ana ombwe ktk modern skill set hasa ktk kuuza ujuzi, ana elimu very traditional ambayo inabidi uajiriwe tu vinginevyo asingekuwa muajiriwa angekuwa ni mmiliki wa makampuni na mwajiri.
We have to learn to adapt modern skill set.
Tuachane na digrii za sifa.
Shaban Robert hakuwa hata na digrii moja lakini ni maarufu kuliko wenye madigrii mengi wa wakati wake.