A free advice.
Badala ya kwenda na kurudi na hawa Wachina, Tanzania isipange kupata tumisaada-saada twa dola milioni 50, 100, 300, 5000.... Ipange karata zake iingie kichwa kichwa na Wachina katika 'strategic partnership'. Kila miaka miatano China iipatie TZ bilioni 10 $ kwa muda wa miaka 50 ijayo. Tanzania ianze kulipa baada ya miaka 20 kwa faida ya 2%
Wachina, wakielezewa vizuri, watakubali, maana wanatafuta mahali penye Amani na Rafiki pa kuhifadhi ma trilioni yao ya dola ambayo sasa yanatishiwa 'kutaifishwa' na Marekani inayofilisika. Tanzania imeisaidia sana China, bila ya faida yeyote ya kueleweka. China iko tayari kuingia na Iran mkataba kama huo, sembuse TZ? Halafu tuna Wachina wengi waliopo serikalini wa kututetea. Chukua kwanza mfano wa balozi aliyepita Dr. Lu Youqing.
Huku kukatiwa vijidola hamsini kila mara hakutatufanya tuendelee. Tunahitaji 'a huge infusion of capital' ku revamp kabisa elimu yetu na agriculture, kabla hatujaendelea. Hii maneno ya "Uchumi wa Kati" tulionao ni 'smokescreen' tu. Mwaka huu huu tutarudi kuwa uchumi maskini. Uchumi wa kati haumaanishi tumeshafika basi tutabaki hivyo hivyo. Kwanza uchumi wa kati wenyewe ni "Kati ya chini" siyo "Kati ya juu" kama Kenya. Ila hawawatangazii raia hivyo, wanawaacha waimbe tu!
Alas! Hatuna 'strategic thinkers' katika tabaka la viongozi wetu. Hatuna hata 'long-term mapping' ya maendeleo yetu. Twategemea matamko ya rais tu kuwa mwongozo! Chukua mfano kauli mbiyu ya 'Uchumi wa viwanda' Inasemwa tu. Hakuna aliyeuliza viwanda gani? Wapi watatokea wajenzi Watanzania wa viwanda hivyo? Tuna mainjinia, ma project managers, ma machine operators, ma programme builders........wa kutosha? Tunataka kiasi gani cha hao watoke kila mwaka katika Vyuo vyetu vikuu?
Hii siyo lele mama! Walioendelea walipanga!