Profesa Muhongo huna credibility ya kuwashauri watanzania kuachana na mradi wa JNHPP na usidanganye watu kuwa Hydro power zimepitwa na wakati

Nakazi kidogo. Ni mtu wa ajabu sana anaweza kujenga mradi mkubwa kama ule kwa kutumia feasibility study ya miaka 50 iliyopita. Prof. Muhongo ni mtu smart aliyejikuta anafanya kazi kwenye nchi alizoita Trump jina lile.
NAwe pia nikuulize; Ni smart wapi? Anavaa vizuri, ananyoa vizuri, au kitu gani?
 


MUHONGO=MUONGO, just simple like that.
 
Hivi CV yake inaeleza alivyokataliwa na mke wake na siku hizi hajulikani anaishi wapi! Baada ya hayo ndo najua kwamba CV ni ya huko darasani. siyo kwenye miradi ya umeme wakati ulisomea jiolojia.

Mbona nawe pia Umeachika na husemi?
 
Hakika Magufuli alikuwa ngangari haswa hawa kima wote type za kina muhongo hatukuwahi kuwasikia wakishauri chochote
 
Duniani kote mabwawa yanajengwa. China, Ethiopia, Uganda, Brazil etc. Hawa wanajiita wasomi ndiyo wamefanya hadi leo tupo kwenye umaskini. Si wakusikilizwa.
Mkuu juzi kulikuwa na kikao gani vile kati ya Ethiopia na Egypt na kikavunjika? Kilihusu Ethiopia kujenga nini vile hadi Egypt kakasirika?
 
Siyo majungu hoja aliyo toa inashangaza sana - kuna jamaa hapa kamu hoji Prof swali zuri tu kwamba anataka kuileza Dunia kwamba Wachina waliojenga a five gorge project ya kuzalisha umeme wa kukidhi mahitaji ya Taifa lao kubwa lenye viwanda chungu nzima kwa nini wali prefer hydroelectric to gas or nuclear ,je Ethiopia na Uganda wote wamejenga DAMS kwenye mto wa Nile kwa lengo la kuzalisha umeme,kwa nini sisi tuwe tofauti.
 
Ethiopia wanajenga bwawa kubwa la umeme hadi wanagombana na Misri kuhusu mto Nile .kweli huyu Ni profesa Muhongo /big lier
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli "UMEME WA MAJI UMEPITWA NA WAKATI" Ikumbukwe ni mara ngapi Mtera, Nyumba ya Mungu... zimeshindwa kuzalisha umeme kutokana na majanga mbalimbali ya kimazingira kama sio mvua kuzidi basi matope nk. Mtu akiambiwa na mtaalamu akaona utaalamu ule ni ujinga mwisho wa siku lazima alipe gharama zake. Akiliccm haijawahi kukubaliana na vitu vyenye akili..m
 
Ameshapitisha vibali vya kazi vitolewa kama karanga, ameshaonesha yupo tayari mkataba wowote kwenye LNG Lindi, kwenye Hellium gas, unataka kuona nini kuwa ameshawishiwa ujinga na kukubali ?
Kwahiyo mlitaka mpaka wasukuma mujue kichimba gesi ndio muanze michakato ya LNG?? Mlikuwa mna mpango wa kujinehemesha tu sukumas sio?

Mama kasema kwenye LNG tuanze na pia tuangalie maslahi yetu. Kama hakuna Investor tuanze wenyewe kwa pesa zetu kama tulivyoanza kwenye SGR..

Nyie wapumbavu mbona hamuongelei ATCL ilikuwa inapiga hasara na huyo shujaa wenu akawa anatangaza hadharani eti inapata faida? The guy was a complete selfish thief, ndio maana alijaza wezi wenzake waibe kimya kimya na kulazimisha ATCL ianze safari za kwenda Chato Airport kitu ambacho afisa masoko wa ATCL kakiri huyo ruti ni hasara tu hakuna biashara
 
Dunia nzima inaenda kwenye nuclear, gas na solar. Sisi bado tumegomea kwenye maji
Dunia nzima haina maji ya kuzalisha umeme...., Nuclear disposing ya wastes ni tatizo, gas sio renewable na solar inahitaji storage (ambayo bado is not up to standard)
 
Ni ushenzi mkubwa kufyeka miti hekta milioni mbili kwa ajili ya mradi wa maji ambao ungeweza kutekelezwa kwingineko bila kuharibu Eneo la hifadhi ya dunia
 
Mzee unafeli kumuita Muhongo mtaalam wa Nishati huyo ni Geoligist, ambae hajui hata umeme, Iko ivi dunia inapambana kurudi kwenye renewable sources kama jua au maji mana running cost ni kidogo sana compare izo non renewable source, Hata polution ni very less regardless kuwepo na high initial cost, Muhongo ni wakupuuza wakati gesi inachibwa mtwara alisema mgao wa umeme utakuwa historia
 
Umetumia vizuri fasihi.

Mimi katika nyuzi zangu kadhaa nimekuwa nasema kuwa watanzania tumegawanyika kambi mbili tu bila kujali vyama vyetu, nazo ni:
1. Majizi, mafisadi na mashabiki wao.
2. Wazalendo wanaopinga wizi na ufisadi.
Jinsi mtu anavyochangia unaweza kujua mlengo wake ni upi ndio maana unashangaa ntu anashindwaje kuona smple fact! Wanaweza kuwa watu wawili mmoja ana elimu ya chuo kikuu mwingine darasa la saba lakini huyo wa chuo kikuu unashangaa jinsi alivyo bogus kuliko wa darasa la saba.
 
Nimeisikiliza hotuba yote ya Muhongo leo. Hakuna popote aliposhauri kuwa mradi wa bwawa la umeme la Nyerere haufai au uachwe. Na watu wengi humu wamerukia kumlaumu hata bila kujua alichosema. Amesema kuwa umeme wa maji kwa ujumla wake hautabiriki kwa sababu ya kutegemea mvua na kuathiriwa na shughuli zingine za binadamu. Kinachotakiwa ni kuendeleza vyanzo vyote vya umeme, ikiwemo gasi asilia ambayo inaonekana kutelekezwa. Rudi ukamsikilize tena.
 
Mbona nawe pia Umeachika na husemi?
KWa hiyo wote sisi ni hovyo na Muhongo wako au? Usirudie kusifu dume zima bila sababu. MWenzio analilia bila kujua alale wapi, wewe unasifu kichwa chake.
 
Hivi Ethiopia na Misri ule mgogoro umeisha

Gesi tunayo Maji nayo bwelelee sasa nikuangali gharama za ujenzi na enviromental impact ya ya hiyo miradi miwili
Misri wanataka kutuma midege ya jeshi kuja kuokoa maji yao! Kwa kubomoa bwawa!
Ila Misri imebaki maneno tu!!
 
Tanzania inahitaji wasomi wenye damu changa sasa, hawa wenzangu na mimi waliozaliwa miaka ya 50 mpaka 60 waondoke tu madarakani na wasiuone mlango wa jengo la watunga sheria tena, leo tumemsikia mtu anaeitwa Ndugai na ushauri alioutoa kwa wabunge... Lakini hata kabla hatujatafakari mtazamo wa Spika tunapata dozi nyingine ya Profesa mmoja wa kizamani wa madini!!....Kwamba umeme wa gesi ndio mpango mzima kwa sasa, nadhani anatoa msisitizo tu kwani aliishasema.

Hivi Kinyerezi si kuna mitambo ya kuzalisha umeme kwa gesi? Atuambie sasa ni kwa nini kila siku umeme unakatika hasa maeneo yanayopata umeme kupitia Kinyerezi.😳 Nashauri vijana wa sasa waliosoma na hata wasiosoma wajitokeze kuchukuwa nafasi za utumishi Serikalini ili hawa wazee waliojichokea kama mimi wakafungue miradi yao binafsi au wakatumie muda wao mwingi kulea wajukuu.... Aibu!!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…