Profesa Mussa Assad: Hasara za Tozo ni kubwa kuliko faida zake, Mawaziri ndio wakatwe kodi

Profesa Mussa Assad: Hasara za Tozo ni kubwa kuliko faida zake, Mawaziri ndio wakatwe kodi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (CAG), Profesa Mussa Assad amezungumzia suala la Tozo wakati akihojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.

Profesa Mussa Assad amesema anaamini suala la Tozo lina hasara kubwa kuliko faida kwa Serikali.

Amesema “Kuna namna nyingine ya kupata fedha, mfano viongozi wanaotumia magari ya Serikali yenye gharama kubwa kwa shughuli za kiofisini na binafsi, hao ndio wanatakiwa kulipa kodi kwa kuwa wanapata faida ambazo si za kifedha.”

Ametoa mfano wanaotakiwa kukatwa kodi ni Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, wakuu wa mashirika ya Umma na kuwa kama wananunua magari iwe ya gharama ya chini kidogo ili nafuu iwe kwa Wananchi.
 
Sisiemu wanachofanya ni sawa na Mnajadili jambo Chumbani na kukubaliana,,,,halafu mnakuja Sebuleni tena kulisema vibaya jambo hilohilo mlilotoka kujadili chumbani......

Serikali (Rais, mawaziri) wanaamua tozo halafu Kamati kuu ya sisemu(Rais, mawaziri) inakuja tena kusema Serikali iziangalie tozo upya...

Blame Society.
 
Sijawahi kuona hata mara moja wazo la kusema mishahara ya mawaziri na wabunge ikatwe kodi halafu serikali ikasema italifanyia kazi hilo wazo, mara zote huwa linayeyuka kama barafu mchana wa jua kali.

Na ajabu zaidi, huwa hatokei mwanasiasa yeyote, kutoka upande wowote, anayekuwa tayari kuhakikisha analisimamia hilo wazo ili kuona linafanyiwa kazi na serikali, wote huwa kimya..

Hawa jamaa sio wenzetu, huwa tunadanganyika tu, sijui wanatumia madawa gani kutupumbaza.
 
Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (CAG), Profesa Mussa Assad amezungumzia suala la Tozo wakati akihojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.

Profesa Mussa Assad amesema anaamini suala la Tozo lina hasara kubwa kuliko faida kwa Serikali.

Amesema “Kuna namna nyingine ya kupata fedha, mfano viongozi wanaotumia magari ya Serikali yenye gharama kubwa kwa shughuli za kiofisini na binafsi, hao ndio wanatakiwa kulipa kodi kwa kuwa wanapata faida ambazo si za kifedha.”

Ametoa mfano wanaotakiwa kukatwa kodi ni Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, wakuu wa mashirika ya Umma na kuwa kama wananunua magari iwe ya gharama ya chini kidogo ili nafuu iwe kwa Wananchi.
Hala Hala msimrambishe tu ASSAD, asinyamazishwe, apewe UWAZIRI Fedha Ili amsaidie kiongozi mkuu kumshauri kuhs Uchumi.
 
Wazo zuri mtu ukimaliza official duty,

Paki gari ya serikali chukua hata boda.

Sasa jamaa wanatanua nazo mpaka shamba huko kuangua nazi.

Juzi i was impressed nilimuona mtu mmoja mzito kapiga pensi yupo kwenye boda.

Safi sana.

Madaraka haya ni ya kuwatumikia wananchi tu na sio zaidi ya hapo.
 
Back
Top Bottom