Profesa Mussa Assad: Hasara za Tozo ni kubwa kuliko faida zake, Mawaziri ndio wakatwe kodi

Profesa Mussa Assad: Hasara za Tozo ni kubwa kuliko faida zake, Mawaziri ndio wakatwe kodi

Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (CAG), Profesa Mussa Assad amezungumzia suala la Tozo wakati akihojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.

Profesa Mussa Assad amesema anaamini suala la Tozo lina hasara kubwa kuliko faida kwa Serikali.

Amesema “Kuna namna nyingine ya kupata fedha, mfano viongozi wanaotumia magari ya Serikali yenye gharama kubwa kwa shughuli za kiofisini na binafsi, hao ndio wanatakiwa kulipa kodi kwa kuwa wanapata faida ambazo si za kifedha.”

Ametoa mfano wanaotakiwa kukatwa kodi ni Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, wakuu wa mashirika ya Umma na kuwa kama wananunua magari iwe ya gharama ya chini kidogo ili nafuu iwe kwa Wananchi.
Wadanganyika mutaisoma namba kweli na mtamkumbuka Rais Magufuli alisema akiondoka yeye kila kitu kitarudi kama zamani sasa muisome namba wabongo poleni sana.
 
Sijawahi kuona hata mara moja wazo la kusema mishahara ya mawaziri na wabunge ikatwe kodi halafu serikali ikasema italifanyia kazi hilo wazo, mara zote huwa linayeyuka kama barafu mchana wa jua kali.

Na ajabu zaidi, huwa hatokei mwanasiasa yeyote, kutoka upande wowote, anayekuwa tayari kuhakikisha analisimamia hilo wazo ili kuona linafanyiwa kazi na serikali, wote huwa kimya..

Hawa jamaa sio wenzetu, huwa tunadanganyika tu, sijui wanatumia madawa gani kutupumbaza.

Hili tunapaswa kulisimamia sisi wananchi. Mishahara na marupurupu makubwa bila ya kulipa kodi ndiyo kulamba asali kwenyewe.

Kumbuka hakuna mwanasiasa bungeni aliyelivalia suala la malipo ya kufuru wanayolipwa kuliganisha na mzigo anaotwishwa mlipa kodi.

Kwa hakika tunataka serikali itakayolipa watendaji wake ikizingatia maslahi kamili ya mlipa kodi.

Hii ni kote bila kujali atakayekuwa madarakani.
 
Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (CAG), Profesa Mussa Assad amezungumzia suala la Tozo wakati akihojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.

Profesa Mussa Assad amesema anaamini suala la Tozo lina hasara kubwa kuliko faida kwa Serikali.

Amesema “Kuna namna nyingine ya kupata fedha, mfano viongozi wanaotumia magari ya Serikali yenye gharama kubwa kwa shughuli za kiofisini na binafsi, hao ndio wanatakiwa kulipa kodi kwa kuwa wanapata faida ambazo si za kifedha.”

Ametoa mfano wanaotakiwa kukatwa kodi ni Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, wakuu wa mashirika ya Umma na kuwa kama wananunua magari iwe ya gharama ya chini kidogo ili nafuu iwe kwa Wananchi.
Wawapige ban na Clouds sasa maana Dar tv wamepigwa faini kisa Afande Sele kupinga tozo.
 
Wazo zuri mtu ukimaliza official duty,

Paki gari ya serikali chukua hata boda.

Sasa jamaa wanatanua nazo mpaka shamba huko kuangua nazi.

Juzi i was impressed nilimuona mtu mmoja mzito kapiga pensi yupo kwenye boda.

Safi sana.

Madaraka haya ni ya kuwatumikia wananchi tu na sio zaidi ya hapo.
Unaijua viete wewe [emoji1]

Ac unapigwa mpk unyayoni

Ova
 
Maisha ya watanzania ni kama kitendawili, ukishindwa kupata jibu unampa mji mtoa Kitendawili bila ya wakazi wa huo mji kujulishwa kama kuna mtu kapewa mji wao ili atoe jibu la Kitendawili.
 
Sijawahi kuona hata mara moja wazo la kusema mishahara ya mawaziri na wabunge ikatwe kodi halafu serikali ikasema italifanyia kazi hilo wazo, mara zote huwa linayeyuka kama barafu mchana wa jua kali.

Na ajabu zaidi, huwa hatokei mwanasiasa yeyote, kutoka upande wowote, anayekuwa tayari kuhakikisha analisimamia hilo wazo ili kuona linafanyiwa kazi na serikali, wote huwa kimya..

Hawa jamaa sio wenzetu, huwa tunadanganyika tu, sijui wanatumia madawa gani kutupumbaza.

Waliondolewa Kodi lini jamani?
 
Watanzania tunasema wajibu wa kuijenga nchi yetu upo mikononi mwetu, Anataka Nani atujengee nchi yetu? Anataka tukope mpaka lini? Sisi tutajifunza lini kujitegemea? Kwani yeye hajaona miradi iliyotekelezwa na kufanyika kutokana na tozo zetu? Nani kakwambia tozo zinanunua magari? Au anabeba kauli za uzushi wa watu wanajifanya upotoshaji
 
Mikopo ilipozidi walitujibu hata kama wakikopa sana hakuna mwananchi atakae gongewa mlango ili atoe hela alipe

Sasa hivi wameweka tozo kila sehem mishahara inakatwa Kodi zaidi ya Mara 3 na unaambiwa Kama hutaki hamia Zimbabwe

Mimi naamini mwisho upo karibu sana hata paka ni mpole ila ukimpiga ukiwa umemfungia chumbani akakosa pakujitetea ndio utajua ukali wake
 
Back
Top Bottom