Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

Wakati fulani, rafiki yangu alikwama kuingiza vifaranga vya samaki kwa muda, sijui kama aliweza. Deep down, tusipolinda vya kwetu vilivyopo tutajalia. Ila kama ni breed mpya sawa ije, lakini kama breed hiyo ipo ndani ya nchi kwa nini tuingize toka nje? Tutasema vilivyopo havitoshi, ni sawa, sasa nani mwenye wajibu wa kutafuta njia ili vitoshe kama siyo sisi wenyewe? maswali ni mengi mno, bahati mbaya wa kujibu hayupo.
 
View attachment 2466380
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.


Kukamatwa kwa vifaranga vilivyokuwa vikiingizwa nchini kumeibua masuala ya uwajibikaji na kutofuata sheria miongoni mwa viongozi wa Serikali na wadau wa sekta ya ufugaji wa kuku.

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.

Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.

Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.

Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.

“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.

“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.

Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.

“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.

Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.

“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
Imagine kule Arusha kuna mwekezaji aliteketeza vifaranga vya kuku mwezi Jana December kwa kukosa soko. Hizi paradox zikoje na zinamhusu nani
 
Tujifunze kufata utaratibu

Tujifunze kupanga mambo yetu vizuri kabla ya kuanza utekelezaji.

Tujifunze pia kujua "utamaduni" wa taasisi na vyombo vyetu vya maamuzi.

Haya yanaweza kutusaidia KUYOKUOATA HASARA zinazoweza kuepukika.
Huo utaratibu ndo shida unaweza chukua mwaka kukamilisha utaratibu. Nikupe mfano mdogo tu. Nimelipia umeme tangu mwaka 2021 November. Hadi Sasa sijafungiwa. 2023. Hapo utaratibu uko wapi Sasa?
 
Huo utaratibu ndo shida unaweza chukua mwaka kukamilisha utaratibu. Nikupe mfano mdogo tu. Nimelipia umeme tangu mwaka 2021 November. Hadi Sasa sijafungiwa. 2023. Hapo utaratibu uko wapi Sasa?
Time wastage because of UTARATIBU na ndiyo maana matajiri walio wengi ni wale wenye Elimu ndogo kwa sababu UTARATIBU kwao ni kupoteza muda ndiyo maana wametoboa maisha,huyo anayeng'ang'ania utaratibu akistaafu ni miaka miwili tu amefilisika na utaratibu wake unaisha anaanza kuomba hela kwa wale aliokuwa anawanyanyasa.
 
Huo utaratibu ndo shida unaweza chukua mwaka kukamilisha utaratibu. Nikupe mfano mdogo tu. Nimelipia umeme tangu mwaka 2021 November. Hadi Sasa sijafungiwa. 2023. Hapo utaratibu uko wapi Sasa?
Huko ndo kabisa, nakumbuka miaka ile ilizaliwa kampuni fulani, Vishoka Tanzania Ltd.
 
View attachment 2466380
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.
Chanzo: Mwananchi

Mbona kwenye picha ni kama babu wa Bumbuli
 
View attachment 2466380
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.


Kukamatwa kwa vifaranga vilivyokuwa vikiingizwa nchini kumeibua masuala ya uwajibikaji na kutofuata sheria miongoni mwa viongozi wa Serikali na wadau wa sekta ya ufugaji wa kuku.

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.

Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.

Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.

Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.

“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.

“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.

Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.

“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.

Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.

“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi

Havikuwa vya walamba asali na bila shaka ilihitajuka rushwa iliyoshiba. Hii nchi ngumu sana kwamba ikibidi wacha hata vifaranga vife.
 
Kosa la maafisa wa airport nini? Mlitaka waruhusu vifaranga viingie bila vibali? Yani mijitu inatanguliza vifaranga bila hata vibali,,alafu muje muwalaumu maafisa
Wewe una akili timamu kweli?Hivi kulikuwa hakuna namna nyingine ya huduma wakati wakisubiria utaratibu?Kwa nini havikurudishwa vilikotoka kama viliingia bila utaratibu?Ni mwehu yupi anaweza safirisha vifaranga from Belgium to Tanzania kwa njia isiyo halali kwenye Viwanja vya Ndege na Bandari kuna sheria zinazofanana?Acheni ujinga wa kutetea maovu,vifaranga nao ni viumbe wa Mungu.
 
Wewe una akili timamu kweli?Hivi kulikuwa hakuna namna nyingine ya huduma wakati wakisubiria utaratibu?Kwa nini havikurudishwa vilikotoka kama viliingia bila utaratibu?Ni mwehu yupi anaweza safirisha vifaranga from Belgium to Tanzania kwa njia isiyo halali kwenye Viwanja vya Ndege na Bandari kuna sheria zinazofanana?Acheni ujinga wa kutetea maovu,vifaranga nao ni viumbe wa Mungu.
wewe huna akili, unatangulizaje kitu huna kibali cha kuingiza? huo si upumbavu... kama una huruma na vifaranga mbona unavila wakiwa wakubwa. Nyambaf! ungeenda kuwalisha basi airport
 
Kosa la maafisa wa airport nini? Mlitaka waruhusu vifaranga viingie bila vibali? Yani mijitu inatanguliza vifaranga bila hata vibali,,alafu muje muwalaumu maafisa
Ni ujinga mtupu unaofanywa na watumishi wa Serikali. Mpaka siku Serikali itakapoamua kila sehemu kuajiri the best best, ndiyo matatizo kama haya yataisha.

Kuna watemdaji wa Serikali ambao ni wajinga kupindukia. Wanadhani Serikali kazi yake ni kuumiza wananchi. Wanashindwa kuelewa kuwa Serikali inatakiwa kuwa mwezeshaji.

Hao maofisa wa Serikali walitakiwa kujiuliza wafanye nini ili muingizaji vifaranga asiingie hasara lakini pia nchi iwe salama.

Wangeweza kuruhusu vifaranga kuingia wakapelrkwa shambani kwake kwa ysimamizi maalum. Na huko wawekwe karantini, na walindwe kwa gharama ya mwingizaji. Wapimwe kwa gharama ya mwingizaji. Wakionekana hawana tatizo, aendelee na ufugaji, lakini apigwe faini.

Lakini kwa upande mwingine ilitakiwa kuangalia kama aliomba kibali cha kuingiza, aliomba lini, kwa nini watoa vibali hawakutoa vibali. Na kama walishindwa kutoa vibali kwa sababu ya uzembe au kutengeneza mazingira ya rushwa, basi hao maofisa wa wizara ya kilimo, wafukuzwe kazi na kupoteza stahiki zao zote.
 
wewe huna akili, unatangulizaje kitu huna kibali cha kuingiza? huo si upumbavu... kama una huruma na vifaranga mbona unavila wakiwa wakubwa. Nyambaf! ungeenda kuwalisha basi airport
Wewe ni mmojawapo wa wapumbavu wenye vikwazo visivyo na tija tunapoongelea hayo hatuongei eti kwa sababu hatuna utaratibu bali kuna visheria vya hovyo hovyo hasa Wizara ya Kilimo.
 
Ni ujinga mtupu unaofanywa na watumishi wa Serikali. Mpaka siku Serikali itakapoamua kila sehemu kuajiri the best best, ndiyo matatizo kama haya yataisha.

Kuna watemdaji wa Serikali ambao ni wajinga kupindukia. Wanadhani Serikali kazi yake ni kuumiza wananchi. Wanashindwa kuelewa kuwa Serikali inatakiwa kuwa mwezeshaji.

Hao maofisa wa Serikali walitakiwa kujiuliza wafanye nini ili muingizaji vifaranga asiingie hasara lakini pia nchi iwe salama.

Wangeweza kuruhusu vifaranga kuingia wakapelrkwa shambani kwake kwa ysimamizi maalum. Na huko wawekwe karantini, na walindwe kwa gharama ya mwingizaji. Wapimwe kwa gharama ya mwingizaji. Wakionekana hawana tatizo, aendelee na ufugaji, lakini apigwe faini.

Lakini kwa upande mwingine ilitakiwa kuangalia kama aliomba kibali cha kuingiza, aliomba lini, kwa nini watoa vibali hawakutoa vibali. Na kama walishindwa kutoa vibali kwa sababu ya uzembe au kutengeneza mazingira ya rushwa, basi hao maofisa wa wizara ya kilimo, wafukuzwe kazi na kupoteza stahiki zao zote.
yani wabongo mnajifanyaga mnajua mambo kwasababu ya Hindsight. Nchi ina sheria na maofisa lazima wafuate sheria. Hivi ingekua Marekani au nchi nyingine inayojielewa hao vifaranga wangechomwa kitambo, kwanza hao waBelgiji wasingehata thubutu kuwaweka kwenye ndege kabla vibali havijarudi
 
Ni ujinga mtupu unaofanywa na watumishi wa Serikali. Mpaka siku Serikali itakapoamua kila sehemu kuajiri the best best, ndiyo matatizo kama haya yataisha.

Kuna watemdaji wa Serikali ambao ni wajinga kupindukia. Wanadhani Serikali kazi yake ni kuumiza wananchi. Wanashindwa kuelewa kuwa Serikali inatakiwa kuwa mwezeshaji.

Hao maofisa wa Serikali walitakiwa kujiuliza wafanye nini ili muingizaji vifaranga asiingie hasara lakini pia nchi iwe salama.

Wangeweza kuruhusu vifaranga kuingia wakapelrkwa shambani kwake kwa ysimamizi maalum. Na huko wawekwe karantini, na walindwe kwa gharama ya mwingizaji. Wapimwe kwa gharama ya mwingizaji. Wakionekana hawana tatizo, aendelee na ufugaji, lakini apigwe faini.

Lakini kwa upande mwingine ilitakiwa kuangalia kama aliomba kibali cha kuingiza, aliomba lini, kwa nini watoa vibali hawakutoa vibali. Na kama walishindwa kutoa vibali kwa sababu ya uzembe au kutengeneza mazingira ya rushwa, basi hao maofisa wa wizara ya kilimo, wafukuzwe kazi na kupoteza stahiki zao zote.
Ubarikiwe sana kwa ufafanuzi mzuri,Plan B inahitajika kwenye kazi yoyote inapotekea kuna mkwamo.
 
Wewe ni mmojawapo wa wapumbavu wenye vikwazo visivyo na tija tunapoongelea hayo hatuongei eti kwa sababu hatuna utaratibu bali kuna visheria vya hovyo hovyo hasa Wizara ya Kilimo.
na ww unajifanya unajua kwasababu yameshatokea.. Unatumaje vifaranga kwenye ndege bila kibali chochote, hiyo si dharau. Na huwezi jua pengine ndio kawaida yao, wanaingia bila vibali airport watu wanapiga rushwa maisha yaendelee, ni bahati unakuta siku hiyo kuna ki-system kilitumwa kichunguze kikakutana na huo ujinga
 
Kosa la maafisa wa airport nini? Mlitaka waruhusu vifaranga viingie bila vibali? Yani mijitu inatanguliza vifaranga bila hata vibali,,alafu muje muwalaumu maafisa
ndicho cha kushangaza na vingepita vikaja leta madhara ungesikia tena maofisa wa hovyo waondolewe.Tararatibu zipo wazi na siyo Tanzania tu na nje ya Tanzania huwezi ingiza bidhaa za nyama bila vibali hata kama ni nyama choma.Tumeshasikia sana mafua ya ndege sasa mlitaka mtu ajiletee tu vifaranga bila pewa kibali?
 
Back
Top Bottom