Profesa Tibaijuka: Mikataba yote tunayoambiwa ni ya Siri ni mibovu. Ashangaa kwanini wananchi wapo kimya

Huyu mama atulie ale utajiri wake aache kuwa enjoy watanzania
Wakati ukifika mabadiliko yataletwa na watanzania wananchi na siyo wanasiasa

Ova
 
Kwanza tunadai mkataba na DPW tuwekewe mkeka wazi tuone nini wamesaini. Wanajidai eti wamezingatia yote wananchi wamepinga kwenye ule mkataba na dubai lakini mkataba wenyewe umebakia siri. Hatuwezi kuiamini serikali hii ya samia. Kama walisaini ule mkataba kuipa dubai bandari zetu zote hadi za mito na speaker kinyemela akahakikisha bunge linapitisha mkataba huo kwa nini tuwaamini. Mkataba huo na dubai ni wa ovyo hadi kigogo mmoja serikalini alisema haufai hata kulumangia ugali. Mkeka wa mkataba huo na dubai uliwekwa kwenye mitandao kwa hisani ya kigogo mwananchi mzalendo. Mungu ambariki na kumpa uzima wa milele🙏
 
Wakati yeye yupo Bungeni haikuwa Siri ?

 
ni jambo la kushangaza sana kwa Prof. wa kiTanzania kulalamikia wananchi🐒

muda ukikutupa mkono kwenye siasa na utawala unaweza kujikuta unalaumu wanyonge na wasiostahili kulaumiwa...


maisha hayana extra time Prof.
kila zama n kitabu chake 🐒
 
Huyu Mama naye...!, mkataba ni wa siri, wanasheria wenyewe wanaojua sheria wako kimya, unategemea nini kwa mwananchi wa kawaida?.
Hebu atuache...!.
Tuko hapa ukumbini tunamsubiri Mama tusemezane.
P
Mama anatumegea ili sisi kama sisi tujadili nini cha kufanya na ikiwa kwa wakati wake alishindwa kufanya chochote haimaanishi basi wote tuwe kama wao kuna cha kujadili na kuchukua hatua kwa wakati wetu kuna mambo katika ujana wako ulishindwa kuyafanya watakuja vijana watafanya mimi sioni kosa kwake na ndio maana watz hatubadiliki tumekuwa rigid.
 
Profesa Tibaijuka nilimkubali sana pale aliporudi kutoka huko Umoja wa Mataifa na kusema kwamba kipo kitengo huko UN kinacho zisaidia Nchi zile zilizo ingizwa chaka kwenye mikataba ya madini ili zisipunjwe katika mapato ya migodi ya madini hasa hasa Dhahabu !

Lakini cha ajabu siku ya pili yake alihojiwa tena na Redio ile ile akabadilisha kabisa maelezo yake na kuwataka watu waamini kwamba mikataba iliyopo haikuwa na matatizo yeyote. 😅😅🤦🏽‍♂️

Baada ya siku chache tukasikia Professor ameshakuwa Mheshimiwa 😅😅🤠😇

You can imagine hii mambo inakuwaje !!
Huwa nakosa majibu nabaki kujisemea Hiiii - kweli kila mtu abebe mzigo wake 😳🙌👍
Tutafika mbinguni tumechoka sana
These people are not trustworthy,
Leo atasema hivi na kesho atasema vile ,
They are always dancing according to their tunes !
 
Tuliandaliwa kuto kuhoji na tatizo la kuto kuhoji linaanza kwenye ngazi ya familia
 
Ule mgao aliopewa Tibaijuka, ukamng'oa uwaziri, alikuwa na mkataba na Singa, Ruge au Tanesco?
 
Kila mtu apambane na hali yake
 
Nchi hii watu waliopo Kwenye madaraka, hawana huruma hata kidogo na Taifa, badala yake wanatumia nafasi hizo kutuibia bila huruma😎
Yaani uonewe huruma kivipi ilhali huonyeshi kukereka na madudu yanayofanywa na wale waliopewa dhamana?
Ukiambiwa onyesha kukerwa hata kwa kufanya maandamano ya amani,unasema mimi mambo ya siasa sipendi,au unasema acha Mbowe na wenzake waandamane,mimi sihusiki.
Acha wale wanavyotaka,usilalamike,muhimu hakikisha unalipa kodi kwa uaminifu mkubwa,ili pesa zitumike na wajanja kwenda jusaini mikataba ya hovyo.
 
Hivi lile sakata lake la kumuuzia George Bushi wilaya nzima ya Kigamboni liliishaje?
 
Ptofesa Tibaijuka alijipatia $1,000,000 kutoka kwenye mgao wa Escrow.
Na kwa dharau alidai hiyo ni hela ya mboga.
Arudishe hizo hela kwanza ili tuone uaminifu wake kwa nchi hii.
 
Hivi lile sakata lake la kumuuzia George Bushi wilaya nzima ya Kigamboni liliishaje? Ule mkataba hatujawahi kuuona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…