Tetesi: Professor Lipumba: Lazima tugawane Umeya wa Kinondoni na Ubungo

Tetesi: Professor Lipumba: Lazima tugawane Umeya wa Kinondoni na Ubungo

Ni wazo jema bt hao madiwan aliwapigia yeye kampen au mchango wake ni upi hasa aliwapa kipindi cha kampen.....kumbe anapenda vya kutafuniwaa.......cuf alikuwa anaiua bara wakat wenzie wa Zanzibar wanapambana miaka yote...yy alikuwa anacheza mdaku.....ss hiv kaona utam cuf nao wana halmashaur kadhaa.....s
 
Ameshaanza rasmi kazi aliyoagizwa kuifanya. Ukawa wakiwa wajinga lazima wagawanyike tu.
 
Cuf wakishindwa kumtimua huyo prof.nashaur chadema na vyama vingine wajitoe au waifukuze cuf katka ukawa
 
Ubungo na kibamba Cuf ina madiwani Wawili.....Chadema ina madiwani wengi ubungo na madiwani wote kibamba.

Naamini CCM itachukuwa umea kinondon.....maana Chadema ina madiwani Wengi kuliko CUF na CCM
 
"Nimeona nijikite kwenye kufanya Utafiti wa Ushauri wa masuala ya Uchumi ili kuinua Uchumi wa nchi"
 
Mwenyekiti wa Chama cha CUF Pr. Lipumba kasema ni lazima CUF na CHADEMA wagawane umeya wa Kinondoni na Ubungo kwa kila chama kuchukua halmashauri moja moja na sio madiwani wa CUF kuwa manaibu meya.

Mwenyekiti huyo kasema kuanzia sasa usawa katika kugawana viti lazima uwepo kama kweli umoja huo ni manufaa kwa vyama vyote. Na sio kuburuzwa na chama kimoja

Hali bado ni tete sana ndani ya CUF, kwa hiyo mgawanyo huo utategemea utii wa madiwani husika uko wapi! Kama ni kwa Maalim imekula kwake! Na kama ni kwake amelamba dume!
 
Huyu jamaa tokea mwanzo niliona dalili ya kuupasua ukawa. Ina maana alishindwa fanya kazi ingine kwa muda woote huo huku kusoma kwingine bana
 
Haya sasa. Professor kawakumbusha jambo muhimu kweli. Tunataka kuiona 'Demokrasia ya Kweli' tunayohubiriwa kila siku humu mtandaoni ikifanyika kwa vitendo.[
Lipumba is RIGHT. Ni HAKI kwa CUF kupata meya moja ktk Halimashauri hizo mbili. Siyo naibu tu.
 
Ninagekuwa msajili nisingerehusu neno UKAWA kutumia kama kiashirio cha muungano au ushirikiano wa vyama vya siasa. Neno UKAWA halijasajiliwa popote, hivyo halikutakiwa kutumika mahali popote bila usajili. Hiyo ni sawa na mwenye baa kuandika jina la baa bila kusajili brela
 
Mwenyekiti wa Chama cha CUF Pr. Lipumba kasema ni lazima CUF na CHADEMA wagawane umeya wa Kinondoni na Ubungo kwa kila chama kuchukua halmashauri moja moja na sio madiwani wa CUF kuwa manaibu meya.

Mwenyekiti huyo kasema kuanzia sasa usawa katika kugawana viti lazima uwepo kama kweli umoja huo ni manufaa kwa vyama vyote. Na sio kuburuzwa na chama kimoja

lipumba anaona mbali, Maalim anauwa nguvu za cuf bara, kaingiza cuf kwenye ukawa bara akijua Zanzibar chadema haipo. Sasa umeja gani kinanufaika chadema pekee??
 
Alishiriki vipi kuwapata hata hao madiwani na wabunge wa CUF waliopo?? Hivi le profeseri haoni aibu.
 
Huyu MZEE Lipumba ni mzima kabisa tu...ila kabisa inaonekana kuna agenda ya siri nyuma ya pazia kwenye sakata hili...yote kwa yote ni kuubomoa ukawa na upinzani kwa ujumla wasiposimama kidete....tutarudishiwa enzi za ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA....
 
Back
Top Bottom