Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo?

je hiyo wil naituiaje??
kwanza ni nini manake nikiitafsiri najua ni kama vile "amua" sasa ni amue nini??
je naweza kuamua kuendesha vogue?? na ikaja vogue??
unless am missing something here
 
Mkuu pasco naomba uniambie na mimi huwa nina experience mambo haya yafuatayo je nina uwezo gan?

1. Kama niki set alarm kwa ajili ya kuamka naamka dakika moja kabla ya alarm kuita na siku nyingine nakuta alarm set off wakati nilihakikisha kabisa nimeset na ikastart counting down

2. Usiku huwa ninashtuka saa 8 au 9 na kuhisi kuna kitu kilikiwa kinafanyika nahisi ni wachawi au wanga

3. Kuota ndoto afu inakija kitokea ila huwa siikimbuki hadi siku tukio linatokea na linapotokea najua baada ya hiki kinafatia hiki na ninafanya sawia kama kwenye ndoto

4. Nilishawah kuota uncle wangu ambaye alikuwa baada ya siku mbili anasafiri kuelekea moshi kapata ajali na kweli alivyosafiri akapata ajali

Na huyu house girl wetu aliniambia kuwa kila jambo analomuambia mtu in hostile way basi litamtokea huyo mtu mi
namuona kama mchawi maana kuna kijana alimwambia "tuone kama utapata kazi" hado leo hii hajapata kazi je nae ana psychic powers??kama ndio mtu asiye na psychic power anawezaje kujilinda dhidi ya watu kama hawa wanaonuwia kitu na kinatokea kwa watu wengine?
 
baadhi ya watu ni bora wasijue kabisa kwani badala ya kuwasaidia inaweza kuwa tatizo kwao au jamaa!

safi sana kwa elimu hii!
 
Like Like

Pure abracadabra

Ginning gobbledegook gibberish with hocus-pocus, hoi-polloi hogwash.

Abrasive abracadabra.

Pure manure would be better for sure, at least with it you can fertilize the ground for farming.
 

Hiyo unaitwa de javu
 
Last edited by a moderator:
Pasco haya mambo yanaogopesha wakati mwingine
umeyasomea wapi yote haya?
Mimi nshajiuliza sana kwanini inanitokea nikimkumbuka mtu ambae sijamwona siku nyingi ndani ya muda wa wiki hiyo hiyo huo ntaambiwa anaumwa sana au ameshafariki
Nimjearibu kuwaza kuna connection gani sijapata jibu hadi leo.
na ni kwanini mawazo hayo hunijia.

Kingine watu wengi wanapenda kunishirikisha matatizo na shida zao
sijui kinachowatuma wanieleze hata kwa watu wageni na nsiowajua.
mfano nikiwa ofisini Tanzania watu wanaofika na shida zao baada ya muda hurudi tena na kunishirikisha hata ambayo hayahusiani na kazi ninayofanya, kiofisi changu sipendi wanyimwe kuingia.
majibu ninayowapa wananijulisha yamefanya kazi na hali imetengamaa matatizo yameisha
ukiniuliza nimewapa ushauri gani wa maana kiasi cha wao kunishukuru sijui hata nikakoutoa na sijui kama ninachokisema kina umuhimu kwao kwani huwa napenda kuongea kawaida na kwa ucheshi mtu anajikuta akicheka hata kama alikuwa na huzuni kubwa kwa muda mrefu.
Nikijiangalia na umri wangu na jinsi hata watu wazima wanavopenda kunieleza yanayowakumba kwa kweli sielewi
sielewi kama nina hizo nguvu au kipaji umekitaja.
Unaweza kujibu kwa ufupi nini kinasababisha?
 
Kwa kifupi huu ni mwanga sana kwa wale ambao wapo njia panda hasa kwenye maswala ya kiimani wengi walikua wanaamini kama wewe sio muumini wa dini tulizorisishwa na wazazi wetu,huwezi kua na imani
 

That's why nakuadmire Pasco there something very special in you man.
 
Last edited by a moderator:
Daah!! Hatarii !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…