Mkuu Eiyer, nakuomba sana usilazimishe mambo!
Nimelazimisha mambo gani?
, hapa sio nyumba ya ibada!,
Who said so?
naomba tufanye appontment kule jukwaa la dini, nikupige somo!,
Kwanini?
Naanza kuapta wasiwasi na uwezo wako wa kuelewa
Napata wasiwasi kwasababu nashindwa kuelewa ni kwanini unashindwa kuliona tatizo lililoko kwenye mada yako
Alietakiwa kwenda huko kwenye hilo jukwaa ni wewe pamoja na hii mada yako na sababu nimezieleza hapo kwenye post yangu uliyoi quote,au hujaisoma?
Unaponiambia nalazimisha mambo bila kusema ni mambo gani na bila kueleza vile ninavyolazimisha mambo utaonekana ni kituko tu
Pia sio mimi peke yangu niliekuambia hayo,lakini ajabu huelewi
usijekujikuta na wewe ndio hao wamuabidia shetani aliyejidisguised kama Mungu,
Hili ni sehemu ya mada yako?
ndio maana unababaika sana!.
Kubabaika maana yake nini?
Nimebabaika wapi?
Issue ya shetani aliumbwa na nani usiifanye a very big deal!,
Wewe huoni kama ni big deal?
Hujui umuhimu wa kumjua shetani kwenye imani ya Kikristo?
Au wewe ulikua unaandika ukidhani ni kitu kidogo sana?
Unazidi kuonesha namna usivyojua mambo
nilikuuliza huko nyuma, jee unaujua mwanzo wa Mungu?!, jee unaijua source of powers za Mungu?!,
Utaendelea kushangaza kama utakuwa huelewi uzito wa haya unayoongea hapa
Na nakuambia huenda kukawa kuna watu walikuwa wamevutiwa na hii mada yako na watakapoona unazungumza mambo kama haya watagundua tu kuwa hayo uliyoandika hapo hukutoa kichwani mwako kwa kutafakari bali umekopi mahali tu
Unaulizaje kuhusu kuhua mwanzo wa Mungu na nguvu zake?
Hivi unamjua Mungu wewe?
Unaweza kumtafakari akaweza kuenea kwenye mawazo yko yenye ukomo?
Hebu niambie huo mwanzo wa Mungu ni upi ili uwe umethibitisha kuwa alisema uongo aliposema hana mwanzo wala mwisho.tuambie hicho chanzo cha nguvu za Mungu ili wewe uwe ndie Mungu
Usichokijua ni kwamba unayosema na kujidai kufundisha hapa ni pure satanic na wewe hujui tu au unaamua kudanganya kwa makusudi
Dhana ya kutaka kufanana na Mungu aliianzisha shetani mwenyewe huko mbinguni na wewe unaiendeleza hapa kwakudai kujua mwamnzo wa Mungu na nguvu zake
Trust me hutakaa ujue na haitatikea binadamu yoyote akajua mwanzo wa Mungu wala nguvu zake kwakuwa hazina mwanzo na yeye ni zaidi ya huo mwanzo
Ni sawa na kijiko kitake kijue mwanzo wa aliyekitengeneza,inawezekana hilo?
Japokuwa aliyekitengeneza kijiko ana mwanzo lakini kijiko hakiwezi kuujua,sijui wewe kutaka kujua mwanzo wa asiyekuwa na mwanzo utaujuaje
Jee unaujua mwanzo wa shetani?!,
Simple,
Aliumbwa na Mungu
kama ulifundishwa kuwa shetani aliumbwa na Mungu, na ndiye aliyempa hizo nguvu za kushetani tufuindishi na sisi tujue!.
Nishakujibu tayari
Nilikuuliza baada ya shetani kuasi kule kwa Mbinguni, jee unajua ni kwa nini Mungu hakumuangamiza?!.
Kwani hujui ni adhabu gani Mungu aliyomuandalia?
Kwanini wewe unadhani alitakiwa amuangamize?
Hujui kuwa Mungu hakuona busara kuwa dikteta?
Ile haki yake ya kuishi aliendelea kumpatia na huo ndio upendo
Lakini pia hujui kuwa unajikinza?
Wewe ulisema hapa kuwa shetani hakuumbwa na Mungu,sasa Mungu atakuwaje na mamlaka ya kuangamiza ambacho hata hakuhusika na mwanzo wake?
Hayo mamlaka aliyatoa wapi?
Nilikuuliza maswali kuhusiana na hili lakini hukujibu
Jee unajua Mungu alituumba sisi binadamu kwa mfano wake?!,
Najua hilo
Halafu wakati mwingine naona unauliza maswali ambayo hata sijui na sioni mantiki yake iko wapi
Au unauliza tu bila kujua lengo la swali lako?
jee huyo shetani baada ya kumdanganya mama Yetu Eva na kumshawishi kumuasi Mungu!, unajua alifanywa nini?!.
Hakuna alichofanywa
Tayari adhabu yake ilishaandaliwa tangu mwanzo na ni hiyo hiyo wafuasi wake watakayoipata pamija nae
Kilichoadhibiwa ni kile kiumbe ambacho shetani alitumia umbo lake kumuendea Hawa na kumdanganya pamoja na binadamu aliekubali kudanganywa
Baada ya Kaini mtoto wa kwanza wa Eva, kumuua ndugu yake Abeli, unajua alifanywa nini?!.
Narudia tena haya maswali yako hayaeleweki lengo lake
Huenda ukiniambia leng lake kwenye mjadala huu na maswali niliyokuuliza naweza kupata hamu ya kukujibu
Kwa maana hiyo jinsi Mungu aliupenda ulimwengu, hadi akamtoa mwanaye mpendwa wake anayependezwa naye kuja kuuokoa ulimwengu from what!,
Sababu si umeiandika mwenyewe hapo juu?
Au umesahau?
yaani huyu shetani ni nani haswa hadi Mungu kumtoa kafara mwanaye?!,
Your mixing things here
Sababu ya Mungu kumtoa mwanae wa pekee sio shetani bali ni upendo wa Mungu kwa binadamu
Wewe ni mkristo kweli?
kwa nini asingemuangamiza shetani na yote yakaisha!.
Hili swali linaonesha wewe hujui ukristo kabisa
Halafu aina la hili swali lineulizwa na atheist ningeelewa,lakini linapoulizwa na mtu anaesema kuwa yeye ni mkristo napata wasiwasi na maelezo yake na nina kila sababu ya kumuita mpinga kristo
Kuhusu sababu ya Mungu kutokumuangamiza shetani nimekujibu hapo juu
Soma
Nakushauri kwa mambo usiyoyajua ukidhani unajua, bora jikalie kimya, acha watu tufungulie watu milango ya kumtambua shetani na kumuepuka!, huku tukiwaacha watu mliojifungia katika box la shetani, akiwaaminisha yeye ndio Mungu,
Sitaki ushauri wako
Anza wewe kujishauri kwanza
Hakuna unachokijua kinachoweza kumpeleka mtu mbali na shetani badala yake wewe unawasogeza watu karibu na shetani
Hivi mtu unasema kuwa nguvu inayotumika kufanya mabaya na mema ni ileile ila inapotumika kutenda maovu huhesabika kama shetani na inapotumika kutenda mema inahesabika kuwa ni Mungu unakuwa unawasogezaje watu mbali na shetani?
Ndi maana nakuambia ushauri wako kaa nao mwenyewe
huku mkiamini!, bila kuwa elightened!, utajikuta unamtumikia shetani bila kujijua!.
Hizi trick zako tunazijua
Huko kuwa enlighted sikutaki na sitakutaka hata Illuminati nao hudai hivyo
Huo mwangaza wako kaa nao mwenyewe
Wewe unachokifanya wewe ni kuwafanya watu wamtumikie shetani kwa uhakika kabisa
Sio lazima kuchangia, fuatilia tuu uzi huu ukifunguka, utakuja kunishukuru nimekuokoa!.
Nilichokifanya na ninachokifanya mimi na wengine kuwafunulia watu udanganyifu wako na wapo waliokuja kushukuru hapa
Acha danadana
Kipimo cha kwanza kwa wanaomwabudu shetani bila kujijua, Yesu wa ukweli akitajwa, watataka kukuzuia usimtaje!.
Yesu wa kweli ni Yupi?
Ana sifa gani?
Huyo Roho Mtakatifu mnaotaka kuzuia tusimtaje ndio hizo powers zenyewe na kufanya kila kitu!,
You may be right here,lakini usichokijua wewe ni kuwa unadhani kuna nguvu zinazotumika tu hovyo hovyo biula kutumia kanuni
Huyo anaitwa Roho mtakatifu,maana yake ni takatifu,smoja kati ya sifa kubwa ya kitu kitakatifu ni kuwepo palipo patakatifu
Sasa wewe unadai kuwa mtu yoyote anaweza kuitumia hiyo nguvu,yaani haijalishi kama ni mtakatifu ama laa yaani mtu wa imani yoyte ile anaweza kuitumia hiyo nguvu
Hapo umedanganya sana
Njia pekee ya binadamu kuwa mtakatifu ni kusafishwa kwa damu ya Yesu kwa kumkiri Kristo kuwa mwokozi wake na kuacha dhambi,sasa hao walioko kwenye imani zisizokubaliana na hayo na wala huyo roho mtakatifu watawezaje kuitumia?
Ni sawa utake kuupitisha umeme kwenye kamba ya katani,itawezekana kweli?
neno Roho Mtakatifu likiwa ni jina tuu, the essence is powers!.
Nguvu gani zinazotumika bila utaratibu?
Humu duniani kuna nguvu zinaoendana na kutokuwa mtakatifu na kuna nguvu zinazoendana na kuwa mtakatifu,na nguvu hizi zina vyanzo tofauti kulingana na hizo sifa[utakatifu na kinyume chake]
Hivyo napenda kuwaambia wana JF kuwa wasijidanganye kuwa hata ukitoka kuzini huko unaweza tu kuzitumia nguvu za Mungu kwa kupitia roho mtakatifu
Kama kutakuwa na nguvu unayoitumia hiyo itakuwa ni ile inayoendana na huo uchafu wako[shetani]
Nitamtaja Mungu!, Nitamtaja Yesu, Nitamtaja Roho Mtakatifu kwa ajili ya wale waaminio, na kwa kwa wasio waaminia, nitawaruhusu kuitumia imani yoyote wanayoiamini kuifungua milango ya "powers from within!".
Go on brother,i can not stop you because i don't have that authority
Lakini huyo mwenye hizo nguvu na mamlaka unazozipotosha hapa iko siku na saa atakuzuia na utazimika kama umeme wa tanesco
Kuwa makini sana
Mungu wetu wa mbinguni akuhurumie!