Pugu Boys Secondary School a.k.a Pond boys

Pugu Boys Secondary School a.k.a Pond boys

Mimi nimesoma pale enzi za Mwalimu Mkuu Magambwa, walimu kama Mabagala, Ngola,Mtela nk. Aisee Fungusi walikuwa wananitafuna sana. Siku ya kwanza kufika nikaoga bila kutumia detol. Aisee Fungus walinitafuna ile mbaya hadi kwenye anus.

Tukio la Huzuni ni siku Mwanafunzi mwenzetu alipopigwa risasi. Ilikuwa bado miezi michache amalize form six,alikuwa EGM. RIP

Namkumbuka yule mama aliyekuwa anatuuzia wali pale bondeni, Mama Pendo, Nasikia naye amekufa.

Tukio jingine na Kaka Mkuu aka Mwenyekiti wa Shule ndugu SOSTHENES BAGUME alipovuliwa cheo chake kwa kukitumia kuwanyanyasa wanafunzi hasa wa O'LEVEL.

Napakumbuka Baghdad katikati ya Pugu na Mwisho wa lami, tulikuwa tunaenda angalia Pilau
 
Giro.....umevunja mbavu zangu mpaka noma kweli! Kwenye mboga, maandazi, diet ....namkumbuka mama mmoja alikuwa anaitwa Mama Pendo....du kale Kapendo...machizi walikuwa wanakamendea kweli!
mama pendo keshafariki wakubwa,tulimzika 2009...R.I.P
 
Dah nami 2002-2005. respect kwanza kwa mwl mzava rip. mkuu magambo, mkuu shirimo. nawakumbuka kina jumanne mohamed, peter maha, ernest mtera, shakiri shakifu, deo jonas, ras ben, na 4m 4 leaver 2005. aisee tulinunuaga tshirt za jubilei haikufanyika. afu mnakumbuka shule tulizokuwa tunaletewa wasichana kwa ajili ya disco? respect all.
 
Rwezaura mbona unamsahau na dada zetu akina Kolimba na Mkandawile?Halafu alikuja mzungu mmoja kutoka Uingereza, ali-mreplace Stakes, yeye alikuwa anaitwa Steve, basi akawa anautesa sana moyo wangu, pikipiki lake kubwa halafu mzigo uko nyuma umemkumbatia, halafu na mimi ndiyo nilikuwa nau-mind kishenzi......, matatizo matupu ukikutana nao unaanza kutetemeka hauwezi kuongea hata neno, Steve alivyochukua ika2wa tena shida,...matatizo sana! Alikuwa anafundisha organic Chemistry PCM na alikuwa anaijua sana halafu alikua anajua neno moja tu la kiswahili "hakuna shida".
sure! rwezaula alinipa book store ya maths niisimamie. respect sana.
 
Unawakumbuka walimu wafuatao?Mabagara,Wajimira,Nzoi,Msungu(marehemu),Secondmaster Swai(marehemu),Headmaster Mtera,Mama Mukuru,Mzee Mukuru,Makono(marehemu),Teti,Mkwiche,Grace Chuma,Mamiro,Mama Mtera,Mbulanya,Godfrey Wasiwasi,Kaunda(mwalimu wa michezo 1984-1988),Mzava,Chamuriro,Mugyabuso(marehemu),Bakari Mbonde(Ex-Rufiji Mp)n.k Orodha yao ni wengi sana,waliotangulia mbele ya haki Mungu awaweke mahari panapostaili, aaaammmmmmiiiiiiiiiinnnn.

MKuu inaonekana ww wa kitambo sana mbona kwenye list yako hakuna jina la Mwl. Mkandawile? alipendelea kuwaita pugu boyz! nakumbuka alikuwa akipenda kusema ukiwasimamisha pugu boyz utawajua tu "haziwezi kupita dak2 bila kujikuna sehemu za siri" teh teh!
 
Mzee wa shamba was a legend, hivi wale akina amanda walipotelea wapi... hiyo ilikua miaka ya 1992
 
eeh ngomani nani amewahi hudhulia zile za usiku-disco vumbi.
 
Hii thread inanikumbusha mbali sana, kuna msela wangu alikuwa anasoma pugu, kila weekend alikuwa anakuja kibaha boyz kuja kuoga. Alikuwa ananichekesha sana alipokuwa ananiambia "nimechoka kupiga pond mzee!" jamaa akiingia chooni kuoga hatoki! alkitoka chooni utamsikia ebwana hapa ni Chuoni au UD?
 
Dah!! Umenikumbusha mbali sana. Mi nlipita pugu 1998-2000(A-LEVEL).
Naikumbuka sana mihogo ya sh 20, ilitusevu ingawa tulikuwa tunasinzia darasani.
Nakumbuka pia jinsi nlivyokuwa nkila ugali wa jana asubuhi kwa maharage ya jana kama kitafunwa cha chai iwapo sh 20 ya kunnua mihogo ilikosekana. Wenyewe tulikuwa tukiuita mchanganyiko wa ugali na maharage ya jana kwa jina la PROCESS. Sidhani kama kizazi hiki cha ubongo wa fleva kitayaweza maisha yale. Watoto wa mama walikuwa kila weekend wanadrop kwenda town kuchenji dayati, mwalimu mkandawile aliwatunga jina la DAYATI (DIET) BOYS.
Nakumbuka pia jinsi nyama ilivyokuwa adimu, ilipikwa tarehe 15 na 30 kila mwezi. Siku ya kupewa machungwa palikuwa hapatoshi, fujo mtindo mmoja. Mi nlikuwa napozi bweni la ujamaa.
Katika siku nnazozikumbuka ni hii: siku moja ulipikwa ugali kwa unga uliooza mchana. Kumbe unga ule tulikuwa tukiula usiku ndo maana hatukujua kuwa umeoza, sa that day walikosea wakapika mchana, palikuwa hapatoshi, ikabidi tule wali mchana kitu ambacho ni nadra sana kula wali mchana.
Nakumbuka tulipokuwa form 5, dent mwenzetu alianguka uwanjani na kufa papo hapo wakti wakicheza mpira.
Nakumbuka siku ya kufanya mtihani wa mwisho ilikuwa ni siku ya kumaliza physics paper 2, ndio siku alokufa mwalimu msungu, mtaalam wa network ya mabomba pugu. Masikini wanafunzi wengi hawakumzika msungu kwani walikuwa wameshaondoka, msungu alifariki mida ya saa 9 mchana.
Mwalimu wasiwasi nlisikia alikuwa ud kuongeza elimu, baadae nkawa namuona luningani katika maigizo na matangazo ya biashara.
Namkumbuka ticha wa bios, mama mbulanya na ticha wa physics practical, ticha nzoi.
Aiseee!!!! Nmekumbuka mbali. Wale ma-pcb boys mnawakumbuka mkandawile, kambwili na mzezele??????? Hao ni walimu binafsi, walitupiga tafu kusaka principles




Duh!!! jamaa alikuwa muongeaji kinoma, akachukua uhead boy.



Washikaji wengine walikuwa wakijiandikia barua wenyewe na kujitumia ili waonekane nao waakumbukwa.
Je, wee ndo yule seleman mfupi?????, alikuwa na ndoto ya kuwa daktari???? Tulikuwa class 1, 5G/6G kama sikosei. Kama ndo wee unakumbuka ulivyokuwa ukilia baada ya kutoka katika physics paper 2???. Unamkumbuka some body buberwa????, saa hizi ni mganga mkuu msaidizi tmk hospital, dsm.

Duh! Buberwa kumbe naye pugu boyz?
 
Ninajua kunawadau wengi sana ambao katika maisha yao watakuwa wamepitia pale Pugu Secondary School kama wanafunzi, wafanyakazi, wakazi etc. Wadau hawa sasahivi wametawanyika sehemu mbalimbali ya nchi yetu na duniani kote.

Mimi binafsi ni mojawapo ya watu waliopitia pale kama dent wa high school...(form 5 to 6), ningependa tujikumbushe mambo mbalimbali kuhusu shule ile ambayo ina historia ndefu sana kwa Taifa letu. Ni shule ambayo viongozi wetu mbalimbali walishapitia pale kama wanafunzi au walimu kama vile Mwal. Nyerere, Mkapa (kama sikosei) na wengine wengi tu.

Kwa kuanza kabisa mimi nakumbuka wakati tukisoma pale, maji yalikuwa upatikanaji wake wa shida sana, kulikuwa na wadudu wa malaria na tryphoid sana, kulikuwa na Fungus acha kabisa....yaani tulikuwa tunakamatwa na fungus kiasi cha kushindwa kutembea au kutembea as if one has STDs.....jamaa mtaani mpaka wakawa wanatuita FUNGUS BOYS Mabafu halikuwa haba sana na machafu...so option ilikuwa kwenda kuogea kule mtoni tulikuwa tunakuita POND....hence tukawa tunaitwa POND BOYS.....!

Anything you remember here?

Daaah life ya pugu wakati mwingine huwa sitaki kulikumbuka...naona ni baya sana,nadhani ni moja ya sehemu nilizoishi vibaya so far.
Nakumbuka tulikuwa tukienda kujisaidia chooni tunaacha mashati nje ili kuepuka harufu isibaki kwenye shati.
Chai ikipoa tu ujue huinywi,ina test kama klorokwini-maji ya POND hayo
Mwalimu mabagala naye-MABAGUS
Kwenda shule tunapanda malori ya mchanga(nilisoma O level na A level)

Wazee mlosoma O level 1995-1999 mnamkumbuka jamaa alikuwa anajiita WASAPE (WATSUP)? jamaa alikuwa natesa form one sana yule
 
nimefurahi sana kusikia baghdad!!!!! niliacha kiatu pale masela waliomba hela ya ndumu na mimi nikawa hata 100 ya kupanda gari za chanika sina, pia kwa wale waliokuwepo till 2000 wanakumbuka jamaa mmoja alikua anaitwa Mabagala? anakukimbiza hata ukiwa uchi.
hahahaha!! mabagala alikuwa mwalimu pale pugu, alitukosesha raha sana kule kwenye bweni la MAPINDUZI
 
Mzee wa shamba was a legend, hivi wale akina amanda walipotelea wapi... hiyo ilikua miaka ya 1992

Mkuu umenikumbusha mbali, Amanda kila mtu alikuwa anamtaka yule demu!! sijui yupo wapi siku hizi...
 
sure! rwezaula alinipa book store ya maths niisimamie. respect sana.
mkuu umenikumbusha mbali sana, rwezahula, mnongalingi, baba nzoi,mkandawile, hawa walitusaidia mno "DY/DX- BOYS"(PCM)
 
..............daah, nimefurahi sana kusikia PUGU boys mpo jamvini. mimi ni ex-pugu boys...form 6 leaver 2005. ni daktari Masters degree holder kwa sasa. DOCEBIT VOS OMNIA ni TEACH THEM EVERYTHING.
mkuu mbona unataka kutuharibia mudi sasa? unaijua vizuri miaka ya kusomea udaktari? acha kuleta ubabaishaji hapa!
 
Hapo nilikosea mkuu 21% ilkuwa ...daah niliconfuse kabisa, O level wakati huo nilikuwa kipanga wa namba aisee, nilijiona mdogo kama piliton aisee.....bt thanks, ilinipa nguvu sana ya kula ma Backhouse, ma Shayo etc...at the end of the story katoka na B!
mkuu lakini huyu rwezaula si alikuwa anafundisha Advanced Maths A -Level??
 
Back
Top Bottom