QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

SEHEM YA 9

iku ilikuwa ndefu sana na ilipotimu
saa mbili za usiku Monica akawasili
nyumbani kwa wazazi wake ambako
alikaribishwa kwa furaha kubwa .Kwa
pamoja walipata chakula cha usiku na
Monica akafahamishwa kuhusiana na
sherehe itakayoandaliwa pale pale
nyumbani kwao siku inayofuata kwa ajili
ya kumpongeza kwa mafanikio yake na
kubwa zaidi ni kwa yeye kutajwa kuwa
ndiye mwanamke mrembo zaidi barani
afrika.Baada
ya
mazungumo
yaliyowapeleka hadi saa tano za usiku
Monica akaaga na kutaka kuondoka lakini
wakati akielekea katika gari lake mama
yake akaomba waongozane ana jambo
anataka waongee.
“ Jambo gani mama? Akauliza Monica
wakati wakieleka katika gari.
“ Monica kuna jambo moja ambalo
nimekuwa nataka kuzungumza nawe kwa
muda mrefu kidogo lakini kwa kuwa
nafasi inakuwa finyu sana nimeona
niongee nawe sasa hivi.Ni kuhusu Yule
kijana rafiki yako Daniel mtoto wa mzee
Swai”
“ Ndiyo mama nakusikiliza” akasema
Monica
“ Nafahamu kuwa tumekuwa na
ukaribu mkubwa na familia yao,wewe na
yeye mmekuwa marafiki toka mkiwa
wadogo lakini kwa siku za karibuni
nimegundua ukaribu wenu umeongezeka
sana.Hilo ni jambo jema lakini ilinilazimu
kumfanyia uchunguzi ili kumfahamu ni
kijana wa aina gani,kuzifahamu tabia zake
yote hii ni ili kujua kama anaweza
akakufaa kama ukiamua kuingia naye
katika mahusiano .Utanisamehe kwa
kufanya hivyo bila kukutaarifu lakini ni
kwa ajili ya ya faida yako.”
“ Usijali mama hilo ni jambo jema na
zuri kwani si rahisi kumfahamu vizuri kila
mtu anayenizunguka” akasema Monica

Ahsante
Monica.Nilifanya
uchunguzi wangu na nikagundua kwamba
kijana Yule ni mchafu sana wa tabia.Ana
wanawake karibu kila kona ya
jiji.Anautumia utajiri alionao kwa ajili ya
kuwarubuni wanawake na kuwatumia
kimapenzi kisha huwaacha .Ni tabia
mbaya sana aliyonayo na ndiyo maana
nikataka nikuonye mapema ili ujihadhari
naye.Kaa naye mbali hafai kabisa yule
kijana .Jihadhari asije akakurubuni
ukaingia katika mtego wake.Ninafahamu
kuna kitu anakitafuta kwako kwa hiyo kaa
naye mbali kabisa” akasema Bi Janet.
“ Ahsante mama kwa tahadhari hiyo
lakini hata mimi ninamfahamu vizuri
Daniel na nimekwisha chukua tahadhari
kubwa kuhusu yeye.Ninazifahamu tabia
zake ni chafu na ninakuhakikishia
kwamba hapa kwangu amekutana na
mwamba na hataweza kuleta uchafu wake
kwangu.” Akasema Monica
“ Ninashukuru kusikia hivyo
Monica.Chukua tahadhari kubwa na hasa
kwa sasa ambapo jina lako linavuma kila
kona ya dunia,watakuja wanaume wengi
watakaovutwa na umaarufu wako.
Jihadhari nao sana.”
“ Ahsante mama kwa tahadhari hiyo
lakini unanifahamu vizuri msimamo
wangu hakuna yeyote atakayekuja kwa
tamaa zake atakayefanikiwa.” Akasema
Monica na wote wakacheka
“ Lakini Monica kuna jambo lingine
nataka nikuulize”
“ Uliza mama”
“ Ni muda mrefu sasa tumekuwa
tunasubiri taarifa toka kwako lakini
mpaka leo hii kimya”
“ Taarifa gani mama? Akauliza
Monica huku akicheka
“ Kuhusiana na mchumba.Mbona
hutuelezi chochote? Bado hujampata?
Akauliza Bi Janet na wote wakacheka
“ Mama suala hili linahitaji umakini
mkubwa sana katika kufanya uchaguzi
kwani siku hizi watu wamekuwa walaghai
mno na mapenzi ya kweli ni nadra sana
kupata kwa hiyo ninajitahidi kupata muda
wa kutosha kufanya uchaguzi na
uchunguzi wa kutosha kujiridhisha na
yule nitakayekuwa nimemchagua.Sitaki
niumizwe mama na ndiyo maana
nimekuwa makini sana katika
hilo.Endeleeni kusubiri kidogo na pindi
nikiwa tayari wewe utakuwa wa kwanza
kufahamu.” Akasema Monica
“ Nashukuru sana kusikia hivyo
Monica.Basi mimi nakutakia kila la heri na
ufanikiwe kumpata mwanaume bora na si
bora mwanaume.”
“ Ahsante mama nakuahidi
nitakuletea mwanaume ambaye wewe
mwenyewe utamkubali na utampenda pia”
akasema Monica akaagana na mama yake
 
Mmekuja wote[emoji16] [emoji2] [emoji2] [emoji2]

Kumbe mna selected readers, kwanini msiwatumie PM badala ya kuweka public... Au mngetangaza kama kuna kulipia kabla hujaiweka story ili kuchuja wakina sisi.. Tatizo mnajikuta BRAND

nipe yote safi kwa kuliona hilo

[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
wakuu dozi inaendelea 10 za jioni za kulalia asubuhi tena 10 mchana pia 10 mda ukipatikana ratiba ndio hiyoo mkiona kimyaa msilalamike sana .siumnajua tena kazi na dawa
 
WAKUU STORY NAIKATA JUU KWA JUU ILI ISIWE NDEFU SANA NIKISEMA NIWEKE MPANGILIO MZURI WA KUSOMEKA TUTAKESHA ITABIDI KUSUBILIA KWA SIKU KADHAA,hivyo msishangae kuona vipande vyake havina mwelekeo mwendelezo wa sentens unaishia kwenye sehem nyingine
Umeanza yale yale ya penela
 
SEHEM YA 10

akaingia garini na kuondoka kuelekea
nyumbani kwake
“ Kumbe hadi mama tayari
amegundua kuhusu tabia chafu za
Daniel.Natakiwa kuanza kukaa naye mbali
ili asije haribu sifa yangu.Ukaribu wetu
unaweza kuzua maswali mengi kwa jamii
na wakadhani labda tuna mahusiano
.Natakiwa haraka sana kupunguza mazoea
naye “ akawaza Monica akiwa garini
kurejea nyumbani kwake.
Alifika nyumbani kwake na
kuwajulia hali watumishi wake wote na
kisha akaingia chumbani kwake akaoga na
kujitupa kitandani.Kichwa chake kilijaa
mawazo
“ Jambo aliloliongea mama ni jambo
la msingi sana.Ni wakati sasa wa mimi
kumtafuta mwanaume wa maisha
yangu.Umri unakwenda kwa kasi na
wakati wa kumpata mwanaume wa ndoto
zangu ni sasa.Nimezungukwa na wanaume
wengi wazuri wenye sifa na tabia nzuri
lakini si kazi nyepesi kujua ni yupi
anayeweza kunifaa.Umakini mkubwa sana
unahitajika katika hili.” Akawaza Monica
halafu sura ya Dr Marcelo ikamjia
akatabasamu
“ Dr Marcelo ni kijana mpole
mtanashati na mpenda watu.Katika
wanaume wote niliokutana nao na
walionizunguka yeye namuona yuko
tofauti sana.Nilimtazama machoni wakati
tukiongea pale ofisini kwangu nikagundua
kitu katika macho yake kwa namna
alivyokuwa ananitazama. Jicho lile
linanipa picha Fulani kwani mimi si mtoto
mdogo kufahamu mtu ambaye anahitaji
kitu Fulani toka kwangu.Siwezi pia
kuudanganya moyo wangu lakini kwa
kweli lazima nikiri kuwa hata mimi
nilihisi moyo wangu umestuka sana pale
nilipomuona .Kwa kweli amenigusa sana
moyoni na kuna kila dalili kwamba kuna
kitu kinazunguka kati yetu.Hata hivyo
sipaswi kuwa na haraka sana
ninachotakiwa kukifanya kwa sasa ni
kumchunguza Marcelo ni mtu wa aina gani
,ana tabia gani na kama anaweza kunifaa
kwani kuna kila dalili kwamba ameugusa
moyo wangu” akawaza Monica akainuka
na kukaa
“ Tena itakuwa vizuri kama
nitamualika
katika
sherehe
niliyoandaliwa nyumbani kesho.Nikiwa
naye karibu nitaweza kumfahamu vizuri
sana ni mtu wa aina gani “ Monica
akatabasamu kidogo
“ That’s a good I dea.Natakiwa
kumualika Dr Marcelo katika sherehe ya
kesho nyumbani kwetu.Lakini tatizo ni je
amekwisha oa? Kama ana mke lazima
ataambatana naye na mimi ninahitaji awe
peke yake ili nipate nafasi nzuri ya
kumfahamu.” Akawaza Monica
“ Inawezekana kweli Dr Marcelo
akawa ana mke? Nakumbuka sikuona pete
ya ndoa katika kidole chake lakini hata
hivyo kuna njia moja tu ya kufahamu
kama ameoa ama vipi.Natakiwa kumtumia
ujumbe wa kumualika katika sherehe ya
kesho aje na mke wake.Kama hatakuwa na
mke atanijulisha.” Akawaza Monica na
kuchukua simu yake akamuandikia
ujumbe wa mualiko Dr Marcelo na
kumtumia .Baada ya kama dakika tatu hivi
toka autume ujumbe ule ukaingia ujumbe
katika simu yake uliotoka kwa Dr Marcelo
akaufungua haraka haraka.
“ Monica ahsante sana kwa
mwaliko.Nitafika bila kukosa” ndivyo
ulivyosomeka ujumbe toka kwa Dr
Marcelo.Baada ya kuusoma Monica
akatabasamu na kuandika tena ujumbe
mwingine
“ Usisahau kuja na wifi yangu”
Baada ya dakika moja ukaingia
ujumbe
“ Wifi yako hayupo niko mwenyewe
bado sijaingia katika daraja la ndoa”
“ Wow !! Kumbe bado hajaoa.”
Akawaza
Monica
huku
akitabasamu.Akaandika tena ujumbe
mwingine
“ I hope utakuwa tayari na mchumba
naomba uje naye.Itapendeza sana kama
ukiongozana naye”
Baada ya sekunde kadhaa ukaingia
ujumbe toka kwa Marcelo
“ Bado sina mchumba,siko katika
mahusiano yoyote ya kimapenzi kwa sasa”
“ Mhh !! hiki anachokisema Dr
Marcelo ni cha kweli? Inawezekanaje
akakosa mke au hata asiwe katika
mahusiano yoyote? Ni nadra sana
kukutana na kijana mzuri kama Yule
halafu akawa hana mchumba wala
mahusiano.Kuna haja ya kumchunguza na
kumfahamu Dr Marcelo kwa undani kama
ni kweli anachokisema basi lazima
atakuwa na tatizo..” akawaza Monica na
kuandika ujumbe mwingine wa kumjibu
“ Ahsante kwa kukubali mwaliko
wangu.Tafadhali ufike bila kukosa.Usiku
mwema” akautuma na baada ya muda
ukaingia ujumbe mwingine toka kwa
Marcelo
“ Ahsante nashukuru .Usiku mwema
nawe”
“ Dah !! kuna kitu ninahisi cha tofauti
sana kila ninapowaza kuhusu Dr
Marcelo.Kesho nitamfahamu vizuri zaidi”
akawaza Monica na kuzima simu zake
akalala
 
Back
Top Bottom