LEGE
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 5,122
- 9,209
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 26
Saa saba na dakika kumi na tisa
Monica aliwasili Jasmina Restaurant
walikopanga wakutane na Dr Marcelo kwa
ajili ya chakula cha mchana.Kitendo
alichokifanya Daniel kumfuata Marcelo na
kumtolea vitisho kilimuudhi sana Monica
na hivyo akampigia simu Dr Marcelo
akamuomba wakutane mchana ili waweze
kuongea kilichotokea.
Monica alishuka katika gari
akaangaza angaza na mara akamuona Dr
Marcelo
akimpungia
mkono
akamfuata.Walikaa sehemu tulivu huku
wakifurahia
mandhari
nzuri
ya
bahari.Muhudumu akafika na kuwasikiliza
wakaagiza chakula na wakati wakisubiri
chakula wakaendelea na maongezi
mengine
“ Dr Marcelo japokuwa sote tuna
shughuli nyingi za kufanya lakini nimeona
ni vyema kama tukakutana mchana huu ili
tuongelee kilichotokea asubuhi.” Akasema
Monica
“ I’m so sorry Monic..” akasema Dr
Marcelo lakini kabla hajamaliza Monica
akamzuia
“ Dr Marcelo mimi ndiye
ninayepaswa kukuomba samahani kwa
kilichotokea.Mimi ndiye chanzo cha haya
yote.I’m
so
sorry
Dr
Marcelo
nimekusababishia matatizo na rafiki yako
mkubwa” akasema Monica
“ Usijali Monica.Mimi na Daniel ni
marafiki wa siku nyingi .Hii ni mara yetu
ya kwanza kukorofishana lakini nina
uhakika tutaelewana tu.” Akasema Daniel
“ Baada ya kutoka kwako Daniel
alinipigia simu na kuniomba msamaha
lakini nikamwambia kwamba aje kwanza
akuombe msamaha ndipo arudi kwangu
kuniomba msamaha,alikuja tena kwako ?
akauliza Monica
“ Hapana hakurudi.Ninamfahamu
Daniel ni kijana mwenye kiburi sana hasa
kutokana na utajiri alionao na katu
hangeweza
kurudi
kuniomba
samahani.Yeye anadai kwamba mimi
ndiye niliyemuingilia katika mahusiano
yake,anadai wewe ni mpenzi wake.Ni
kweli? Akauliza Dr Marcelo na kumfanya
Monica atoe kicheko.
“ Hata kama wanaume wangeisha
kabisa katika dunia hii na angebaki Daniel
peke yake katu hawezi kuwa mpenzi
wangu.Ninamfahamu
vizuri
na
ninazifahamu tabia zake chafu.Ukaribu
wetu ni wa kawaida tu na hakuna zaidi ya
hapo.Kama nilivyokueleza kuwa mimi nay
eye tumekua pamoja toka tukiwa wadogo
na hata familia zetu ni marafiki” Akasema
Monica
Chakula kikaletwa wakaendelea kula
kimya kimya
“ Dr Marcelo ..” akaita Monica.
“ Naomba tafadhali mpuuze Yule
mjinga na maneno aliyoyasema.Yule bado
ni kijana na hana malengo yoyote zaidi ya
kuutumia kwa fujo utajiri wa baba yake
kwa anasa.Ninafurahi sana kukutana na
kijana kama wewe ambaye una malengo
makubwa na pamoja kwamba familia yako
ina uwezo lakini hujatopea katika anasa
na starehe na badala yake umeelekeza kila
shilingi unayoipata katika kuwahudumia
watu wenye matatizo.Endelea na moyo
huo Dr Marcelo na Mungu atakubariki na
atakuzidishia wewe na familia yako.”
“ Ahsante sana Monica kwa maneno
hayo yenye busara” akasema Dr Marcelo
“ Kuna jambo lingine ambalo nataka
nikushauri” akasema Monica
“ Nakushauri uvunje kabisa urafiki
na Daniel.Nimegundua si kijana mzuri na
hafai kabisa kuwa rafiki yako.Wewe na
yeye tabia zenu ni tofauti kabisa. Kifupi ni
kwamba hamuendani.Nakushauri tafuta
rafiki wa karibu mwenye tabia njema na
mwenye malengo makubwa ya maisha
tofauti na Daniel ambaye kila kukicha
yeye anawaza starehe tu” akasema Monica
“ Monica mawazo yako ni kama
niliyonayo kichwani.Nimewaza sana
kuhusu jambo hilo na nimekwisha
dhamiria kwamba mimi na Daniel urafki
wetu uishie hapa .Kwa kitendo
alichonifanyia leo sintaweza kabisa
kuendelea na urafiki naye” akasema Dr
Marcelo
“ Good.Thats a wise decision.”
“ Vipi kuhusu wewe ,? Nina wasi wasi
anaweza akaja kukuletea matatizo pia.”
Akasema Dr Marcelo
“ Hata mimi tayari nimekwisha anza
kuchukua hatua za kumuweka Daniel
mbali kabisa nami.Sitaki kabisa ukaribu
naye.Hata mama yangu amenishauri
nifanye hivyo na ndiyo maana ukaona hata
katika sherehe ile niliyofanyiwa ya
kupongezwa na familia sikumualika,yote
hii ni kwa sababu sitaki tena ukaribu
naye.Usijali hana uwezo wa kunifanya
chochote.Mimi ndiye muamuzi ni mtu gani
ninayetaka awe karibu yangu.” Akasema
Monica
“ Monica ninakuahidi hapa kwamba
Daniel akithubutu kukufanyia jambo
lolote lisilo la kistaarabu I swear I’ll
destroy him.Mimi ni mtu mzuri sana lakini
sintaweza kuvumilia hata kidogo
kumuona Daniel au mwingine yeyote
akikufanyia vurugu. Malaika kama wewe
unapaswa kuheshimika na kila mtu”
akasema Dr Marcelo na kutazamana na
Monica wote wakatabasamu.
“ Wow ! what a gentleman.Macho
yake yanaonyesha wazi anamaanisha
anachokiongea.Ni mapema sana kusema
lakini ninaziona kila dalili za mwanaume
Yule wa ndoto zangu kwa Dr Marcelo.Ana
kila
sifa
ya
mwanaume
bora.Kinachonishangaza ni kwa nini
kijana kama huyu mwenye kila kitu,ana
sura nzuri,ana moyo wa huruma na
anajali,ukiacha yote ni kijana tajiri,mpaka
leo hana mpenzi? Ana tatizo lolote? Nahisi
kuna mambo ya ndani yanayomuhusu
Marcelo ambayo napaswa kuyafahamu.”
Akawaza Monica.
Walimaliza kula kisha wakaendelea
na maongezi kuhusiana na mbio za nusu
marathoni zinazotarajia kufanyika siku
inayofuata.Baada ya kutoka hapo
wakaondoka wote na kuongozana kwenda
kuangalia maandalizi ya mbio hizo
yaliyokofikia.
Saa saba na dakika kumi na tisa
Monica aliwasili Jasmina Restaurant
walikopanga wakutane na Dr Marcelo kwa
ajili ya chakula cha mchana.Kitendo
alichokifanya Daniel kumfuata Marcelo na
kumtolea vitisho kilimuudhi sana Monica
na hivyo akampigia simu Dr Marcelo
akamuomba wakutane mchana ili waweze
kuongea kilichotokea.
Monica alishuka katika gari
akaangaza angaza na mara akamuona Dr
Marcelo
akimpungia
mkono
akamfuata.Walikaa sehemu tulivu huku
wakifurahia
mandhari
nzuri
ya
bahari.Muhudumu akafika na kuwasikiliza
wakaagiza chakula na wakati wakisubiri
chakula wakaendelea na maongezi
mengine
“ Dr Marcelo japokuwa sote tuna
shughuli nyingi za kufanya lakini nimeona
ni vyema kama tukakutana mchana huu ili
tuongelee kilichotokea asubuhi.” Akasema
Monica
“ I’m so sorry Monic..” akasema Dr
Marcelo lakini kabla hajamaliza Monica
akamzuia
“ Dr Marcelo mimi ndiye
ninayepaswa kukuomba samahani kwa
kilichotokea.Mimi ndiye chanzo cha haya
yote.I’m
so
sorry
Dr
Marcelo
nimekusababishia matatizo na rafiki yako
mkubwa” akasema Monica
“ Usijali Monica.Mimi na Daniel ni
marafiki wa siku nyingi .Hii ni mara yetu
ya kwanza kukorofishana lakini nina
uhakika tutaelewana tu.” Akasema Daniel
“ Baada ya kutoka kwako Daniel
alinipigia simu na kuniomba msamaha
lakini nikamwambia kwamba aje kwanza
akuombe msamaha ndipo arudi kwangu
kuniomba msamaha,alikuja tena kwako ?
akauliza Monica
“ Hapana hakurudi.Ninamfahamu
Daniel ni kijana mwenye kiburi sana hasa
kutokana na utajiri alionao na katu
hangeweza
kurudi
kuniomba
samahani.Yeye anadai kwamba mimi
ndiye niliyemuingilia katika mahusiano
yake,anadai wewe ni mpenzi wake.Ni
kweli? Akauliza Dr Marcelo na kumfanya
Monica atoe kicheko.
“ Hata kama wanaume wangeisha
kabisa katika dunia hii na angebaki Daniel
peke yake katu hawezi kuwa mpenzi
wangu.Ninamfahamu
vizuri
na
ninazifahamu tabia zake chafu.Ukaribu
wetu ni wa kawaida tu na hakuna zaidi ya
hapo.Kama nilivyokueleza kuwa mimi nay
eye tumekua pamoja toka tukiwa wadogo
na hata familia zetu ni marafiki” Akasema
Monica
Chakula kikaletwa wakaendelea kula
kimya kimya
“ Dr Marcelo ..” akaita Monica.
“ Naomba tafadhali mpuuze Yule
mjinga na maneno aliyoyasema.Yule bado
ni kijana na hana malengo yoyote zaidi ya
kuutumia kwa fujo utajiri wa baba yake
kwa anasa.Ninafurahi sana kukutana na
kijana kama wewe ambaye una malengo
makubwa na pamoja kwamba familia yako
ina uwezo lakini hujatopea katika anasa
na starehe na badala yake umeelekeza kila
shilingi unayoipata katika kuwahudumia
watu wenye matatizo.Endelea na moyo
huo Dr Marcelo na Mungu atakubariki na
atakuzidishia wewe na familia yako.”
“ Ahsante sana Monica kwa maneno
hayo yenye busara” akasema Dr Marcelo
“ Kuna jambo lingine ambalo nataka
nikushauri” akasema Monica
“ Nakushauri uvunje kabisa urafiki
na Daniel.Nimegundua si kijana mzuri na
hafai kabisa kuwa rafiki yako.Wewe na
yeye tabia zenu ni tofauti kabisa. Kifupi ni
kwamba hamuendani.Nakushauri tafuta
rafiki wa karibu mwenye tabia njema na
mwenye malengo makubwa ya maisha
tofauti na Daniel ambaye kila kukicha
yeye anawaza starehe tu” akasema Monica
“ Monica mawazo yako ni kama
niliyonayo kichwani.Nimewaza sana
kuhusu jambo hilo na nimekwisha
dhamiria kwamba mimi na Daniel urafki
wetu uishie hapa .Kwa kitendo
alichonifanyia leo sintaweza kabisa
kuendelea na urafiki naye” akasema Dr
Marcelo
“ Good.Thats a wise decision.”
“ Vipi kuhusu wewe ,? Nina wasi wasi
anaweza akaja kukuletea matatizo pia.”
Akasema Dr Marcelo
“ Hata mimi tayari nimekwisha anza
kuchukua hatua za kumuweka Daniel
mbali kabisa nami.Sitaki kabisa ukaribu
naye.Hata mama yangu amenishauri
nifanye hivyo na ndiyo maana ukaona hata
katika sherehe ile niliyofanyiwa ya
kupongezwa na familia sikumualika,yote
hii ni kwa sababu sitaki tena ukaribu
naye.Usijali hana uwezo wa kunifanya
chochote.Mimi ndiye muamuzi ni mtu gani
ninayetaka awe karibu yangu.” Akasema
Monica
“ Monica ninakuahidi hapa kwamba
Daniel akithubutu kukufanyia jambo
lolote lisilo la kistaarabu I swear I’ll
destroy him.Mimi ni mtu mzuri sana lakini
sintaweza kuvumilia hata kidogo
kumuona Daniel au mwingine yeyote
akikufanyia vurugu. Malaika kama wewe
unapaswa kuheshimika na kila mtu”
akasema Dr Marcelo na kutazamana na
Monica wote wakatabasamu.
“ Wow ! what a gentleman.Macho
yake yanaonyesha wazi anamaanisha
anachokiongea.Ni mapema sana kusema
lakini ninaziona kila dalili za mwanaume
Yule wa ndoto zangu kwa Dr Marcelo.Ana
kila
sifa
ya
mwanaume
bora.Kinachonishangaza ni kwa nini
kijana kama huyu mwenye kila kitu,ana
sura nzuri,ana moyo wa huruma na
anajali,ukiacha yote ni kijana tajiri,mpaka
leo hana mpenzi? Ana tatizo lolote? Nahisi
kuna mambo ya ndani yanayomuhusu
Marcelo ambayo napaswa kuyafahamu.”
Akawaza Monica.
Walimaliza kula kisha wakaendelea
na maongezi kuhusiana na mbio za nusu
marathoni zinazotarajia kufanyika siku
inayofuata.Baada ya kutoka hapo
wakaondoka wote na kuongozana kwenda
kuangalia maandalizi ya mbio hizo
yaliyokofikia.