QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

SEHEM YA 11

Tayari ni
saa kumi na mbili za jioni siku
iliyofuata na wageni walioalikwa katika
sherehe ya kifamilia ya kumpongeza
Monica kwa kutajwa kuwa msichana
mrembo kuliko wote Afrika,walikwisha
anza kuwasili katika jumba la kifahari la
bilionea
mzee
Benedict
Mwamsole.Kulikuwa na bendi ya muziki
ikipiga kuwatumbuiza wageni waliowahi
kuwasili bila kusahau vyakula na vinywaji
vya kila aina.
Saa mbili za usiku muongoza
shughuli akawataarifu wageni walikwa
kuwa muda wa kuanza shughuli ulikuwa
umewadia na hivyo kila mtu anatakiwa
achukue nafasi yake .Huku bendi
ikiendelea
kutumbuiza
Nathaniel
Mwamsole kaka wa Monica akashuka
ngazi
akitokea
ghorofani
akiwa
ameongozana na msichana mmoja
mrembo
sana.Wageni
wakasimama
wakimshangilia na akaelekezwa sehemu
ya kukaa.Baada ya dakika tano Mzee
Benard akiwa ameshikana mkono na
mkewe nao wakashuka ngazi taratibu
wakipita katika zuria jekundu ,watu wote
wakasimama
wakiwashangilia.Mzee
Benard akaelekezwa sehemu yake ya
kukaa iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya
familia
“ Waheshimiwa wageni waalikwa
tunayemsubiri hivi sasa ni malkia wa
Africa ambaye atashuka muda si
mrefu.Naomba mara tu atakapotokea
wote tusimame tumshangilie kwa nguvu
huku tukiongozwa na bendi. “ akasema
muongoza
shughuli.Watu
wote
walioalikwa katika sherehe ile waliopata
zaidi ya mia mbili walielekeza macho yao
mlangoni kumshuhudia mwanamke
mrembo
kuliko
wote
Afrika
atakapotoka.Baada ya kama dakika tano
hivi mlango mkubwa ukafunguliwa
akajitokeza mwanamke mwenye uzuri
usioelezeka na wageni wote wakashangilia
kwa nguvu.Taa zote zikawashwa na eneo
lote likawa jeupe kwa mwanga.Monica
akashuka ngazi taratibu na kutembea
katika zuria jekundu kwa madaha huku
akipunga mkono.Mzee Benard na mkewe
wakampokea Monica na kwenda
kumkalisha
katika
kiti
maalum
kilichoandaliwa kwa ajili yake.Sherehe
ikaanza rasmi.
Ilikuwa ni sherehe nzuri ya kukata
na shoka.Kila aliyekuwamo mle ndani
alisuuzika vilivyo.Kulikuwa na kila aina ya
knywaji na chakula.Ratiba ya mwisho
ilikuwa ni muziki na vinywaji.Baada tu ya
kufungua muziki na watu kujimwaga
kuusakata
muziki,Monica
akaanza
kuzunguka ukumbini akisalimiana na
watu mbali mbali waliohudhuria sherehe
ile na hatimaye akawasili katika meza
aliyokuwa amekaa Dr Marcelo na watu
wengine watatu.Akawasalimu na kuketi
maongezi na vinywaji vikaendelea.
“ Dr Marcelo would you mind if I
show you around? Akauliza Monica na kwa
haraka Dr Marcelo akainuka wakaondoka
pale bustanini wakaelekea katika sehemu
nyingine kulikokuwa na bwawa la
kuogelea.
“ Nyumba yenu ni kubwa sana na
nzuri” akasema Dr Marcelo
“ Hapa ni kwa wazazi wangu mimi
siishi hapa kwa sasa.Ni nyumba kubwa na
hata kama sote tungeamua kuishi hapa
bado tungetosha kabisa kwani kuna
vyumba vya kutosha” akajibu Monica
wakati wakiketi katika meza iliyokuwa
imeandaliwa vinywaji .Dr Marcelo
akamtazama Monica na kutabasamu
“ Hongera sana Monica .Usiku wa leo
umependeza kupita maelezo.Umebarikiwa
uzuri wa ajabu sana na sintachoka kurudia
tena na tena kuwa waliokutaja kuwa
mwanamke mrembo afrika hawakukosea
kabisa.Unastahili heshima hiyo kutokana
na uzuri ulio nao” akasema Dr Marcelo
“ Ahsante sana Dr Marcelo.Hata
wewe umependeza sana nadhani kupita
vijana wote waliohudhuria sherehe hii”
akasema Monica na wote wakacheka
“ Sijamuona Daniel,kwa nini
hajahudhuria?
Dr
Marcelo
akauliza.Monica akanywa funda moja la
mvinyo mwepesi na kusema
“ Daniel hujamuona hapa kwa
sababu sikumualika.” Akasema Monica
“ Hukumualika?!! Dr Marcelo
akashangaa
“ Ndiyo sikumualika.Hii ni sherehe
yangu na ninachagua watu wa
kuhudhuria.Sikutaka Daniel ahudhurie”
akasema Monica
“ Unajua nimeshangaa kidogo kwa
sababu ninavyofahamu wewe na Daniel ni
marafiki wakubwa.Kuna tatizo lolote
limetokea kati yenu? Akauliza Dr Marcelo
“ Hapana hakuna tatizo lolote ila
niliamua tu kutokumualika Daniel”
akasema Monica
“ Dr Marcelo let’s forget about
Daniel, ni masuala yangu mimi na yeye
kwa hiyo yasichukue muda wetu.Kwanza
napenda kukushukuru sana kwa kufika
ingawa nilitegemea ungekuwa na ubavu
wa pili pembeni yako lakini hakuna
kilichoharibika” akasema Monica na wote
wakaangua kicheko
“ Kama nilivyokueleza jana Monica
kuwa bado sijafikia daraja hilo” akajibu Dr
Marcelo
 
SEHEM YA 12

“ Usijali Dr Marcelo hakuna tatizo
lolote unajua suala kama hili halitaki
haraka.Ni suala la kuendea taratibu na
umakini wa kutosha unahitajika kwani
dunia ya sasa mambo yamebadilika
mno.Lakini hata hivyo kwa kijana mwenye
hadhi kama yako ukisema huna mke wala
hata mchumba inakuwa vigumu kidogo
kuamini “ akasema Monica na wote
wakaangua kicheko tena

Ni
kweli
Monica
kama
nilivyokueleza jana kuwa mpaka sasa sina
mke,mchumba au hata rafiki wa kike
kama unaamisha mpenzi japokuwa
marafiki wa kawaida wa kike ninao na
mmojawapo ukiwa wewe.Vipi kuhusu
wewe mbona leo uko peke yako? Yuko
wapi mzee?” akauliza Dr Marcelo na wote
wakacheka
“ Mimi pia ni kama ulivyo wewe
mpaka sasa bado sina mpenzi.” Akasema
Monica huku akitoa kicheko kidogo
“ Usinitanie Monica.Haiwezekani
kabisa msichana kama wewe mwenye
uzuri wa malaika ukose mpenzi.Thats not
true na siwezi kuamini kabisa” akasema
Dr Marcelo
“ Kwani kuna kitu gani kigumu
kuamini Dr Marcelo? Ni kweli sina mpenzi
hadi sasa na huo ndio ukweli” akasema
Monica
“ Nimeshangaa Monica kwa sababu
kwa maisha yetu haya ya sasa wasichana
wengi wazuri wameugeuza uzuri wao
kama mtaji wa kupata unafuu wa maisha
..” akasema Dr Marcelo
“ I’m different Dr Marcelo.Mimi
sifanani na hao kitabia.Mimi ni
mwanamke
ninayejitambua
na
ninaitambua thamani yangu kwa hiyo
siwezi kuutumia uzuri wangu kama mtaji”
akasema Monica
“ Hongera sana kwa hilo Monica
ndiyo maana sintachoka kusema kwamba
waliokutaja kuwa mrembo wa Afrika
hawakukosea.Waliangalia mambo mengi”
“ Ahsante sana Dr Marcelo” akajibu
Monica
Wakati Monica na Dr Marcelo
wakiendelea na maongezi bustanini
,hawakujua kama bi Janet alikuwa
akiwafuatilia toka walipotoka mahala
ilipokuwa inafanyika sherehe.Wakiwa kati
kati ya maongezi mara bi Janet
akajitokeza.
“ Mama !!.akasema Monica kwa
mshangao hakuwa ametegemea kabisa
kama mama yake angefika pale katika
bwawa la kuogelea.
“ Monica samahani kwa kuingia
ghafla kuna jambo nilitaka tuongee lakini
tutaongea baadae,endeleeni na maongezi
yenu” akasema Bi Janet
“ Ahsante mama ila naomba ukutane
na Dr Marcelo Richard.Yeye ni rafiki yangu
na ana hospitali ya kuwahudumia
wagonjwa wenye maradhi ya saratani ya
damu. Ni mmoja kati ya wadau waliojitoa
kwa hali na mali kufanikisha ule mradi
wangu wa shule ya watoto” akasema
Monica na kumgeukia Dr Marcelo
“ Dr Marcelo huyu ni mama yangu
mzazi anaitwa Bi Janet Mwamsole”
Dr Marcelo akainuka na kumsalimu
bi Janet kwa adabu.Kisha salimiana Bi
Janet akaondoka na kuwaacha Monica na
Dr Marcelo wakiendelea na maongezi yao.
“ Dr Marcelo Richard !! akanong’ona
bi Janet wakati akiondoka pale katika
 
SEHEM YA 13

bwawa la kuogelea walikokuwa wamekaa
Monica na Dr Marcelo
“Kwa nini Monica aamue kuacha
maeneo yote mazuri kwa kukaa na
kuzungumza akaamua kuja kukaa huku
katika bwawa la kuogelea? Is something
going on between them? Nahisi kuna
jambo linaendelea kati yao na ndiyo
maana wameamua kujitenga huku? Hata
hivyo kwa muonekano wa haraka haraka
Yule kijana anaonekana kuwa ni kijana
mwenye adabu sana na msomi mzuri.Mimi
si mtoto mdogo kwa namna walivyokuwa
wamekaa inaonyesha kabisa kuna kitu
kinachoendelea kati yao .Natakiwa
kumfanyia uchunguzi wa kina huyu Dr
Marcelo ili nimfahamu ni mtu wa aina gani
na kama hana tabia nzuri basi nimkanye
Monica aachane naye angali mapema.Yule
mwingine Daniel sijamuona hapa ninahisi
yale
maneno
niliyomueleza
jana
yamefanya kazi.” Akawaza Bi Janet na
kumtafuta kijana mmoja anaitwa Bakari
ambaye ni mmoja wa vijana anayemtumia
katika shughuli zake nyingi
“ Bakari kuna kazi ninataka
unifanyie na ninahitaji majibu yake kwa
haraka kesho” akasema Bi Janet
“ Kazi gani mama?
“ Unakumbuka niliwahi kukupa kazi
ya kumchunguza Yule kijana rafiki wa
Monica anaitwa Daniel?
“ Ndiyo nakumbuka mama”
“Sasa nataka uifanye kazi kama
ile.Kuna kijana mmoja nataka kupata
taarifa zake za kina.Anaitwa Dr Marcelo
yuko na Monica hivi sasa bustanini
wanaongea.Nataka kazi hiyo uianze usiku
huu wa leo.Wafuatile kila wanachokifanya
na uone kama kuna chochote
kinachoendelea kati yao”
“ Sawa mama nitafanya hivyo
.Tegemea taarifa nzuri yenye kila
unachokihitaji” akasema Bakari
 
SEHEMU YA 14

Taarifa za kuwepo kwa sherehe
kubwa nyumbani kwa akina Monica
zilizoandaliwa na familia yake kwa

ajili ya kumpongeza zilimfikia Daniel na
kumshangaza sana.Hakutegemea kabisa
kama kungeweza kufanyika sherehe kama
ile bila yeye kualikwa au hata kujulishwa
hasa kutokana na ukaribu wake na Monica
na vile vile ukaribu wa familia
zao.Alijiuliza maswali mengi sana na
hakuweza kupata jibu.
“ Haijawahi kutokea hata mara moja
toka kwa Monica kufanya jambo kubwa
namna hii bila kunijulisha.Siku zote
anapokuwa na jambo huwa
ananifahamisha lakini kwa hili
hajanijulisha na wala hajanialika,what
happened? Nini kimesababisha asinialike?
Halafu kingine nasikia Dr Marcelo
alikuwepo.Yaani
mtu
ambaye
amefahamiana jana tu na Monica
amealikwa lakini mimi ambaye nimekuwa
na Monica kwa miaka mingi hata taarifa
sina kwanini Monica ananifanyia hivi?
Kuna kitu gani nimekosea? Akajiuliza na
kuchukua simu akazitafuta namba za
Monica akapiga lakini simu ya Monica
haikuwa ikipatikana.Akapiga namba za
simu za Dr Marcelo lakini hazikuwa
zikipatikana.Akampigia Hidaya msichana
ambaye ni rafiki yake Monica ambaye
anafahamiana naye na ambaye ndiye
aliyemjulisha kuhusiana na sherehe ile
baada ya kutomuona .
“ Hidaya “ akasema Daniel baada ya
Hidaya kupokea simu
“ Unasemaje Danny?
“ Nini kinachoendelea hivi sasa hapo
shereheni?
“ Kinachoendelea hivi sasa ni muziki
na vinywaji?
“ Monica unaweza ukamuona hapo?
“ Monica kitambo sana sijamuona
sijui amekwenda wapi?
“ Dr Marcelo naye unamuona hapo ?
“ Daniel watu ni wengi hapa kwa
hiyo si rahisi kumuona mtu kwa haraka ila
nilimuona hapa kuna wakati alikuwa
anaongea na Monica na hivi sasa kila mtu
amejichanganya kucheza muziki”
“ Basi naomba ukimuona Monica
umpe simu yako niongee naye kwa sababu
nimejaribu kumpigia simu yake
haipatikani”
“ Sawa Daniel nitafanya hivyo mara
tu nitakapomuona” akasema Hidaya na
kukata simu.Daniel akaitupa simu sofani
“ Kwa nini Monica amenifanyia hivi?
Kuna tatizo gani kati yangu naye?
Nimekuwa na ukaribu sana na Monica na
hajawahi kunitenga katika jambo lake
lolote.Lazima kuna kitu kilichosababisha
nisijulishwe au nisialikwe.Nitamtafuta
Monica anieleze nini kimetokea hadi
aniache mimi mtu wake wa karibu na wa
siku nyingi na amualike Dr Marcelo
ambaye amefahamiana naye jana tu.”
Akawaza Daniel akiwa amejawa na hasira
 
SEHEM YA 15

r Marcelo aliwasili nyumbani
kwake saa saba za usiku baada ya sherehe
kumalizika.Uso wake haukukaukiwa
tabasamu .Alikuwa na furaha iliyopitiliza.
“ For he first time in my life I’m
happy.Nina furaha ya ajabu sana leo na
usiku huu wa leo utaingia katika historia
yangu kwani ni usiku wa kwanza
ulionifanya nikawa na furaha na ni usiku
wa kwanza katika maisha yangu I feel I’m
in love.I think I’ve found the woman of my
dreams.Ninaamini
Monica
ndiye
mwanamke wa ndoto zangu kwani kati
yetu kuna muunganiko .We feel connected
to each other .Sijawahi kuhisi kuwa karibu
na mwanamke yeyote kama ilivyonitokea
kwa Monica.Mimi na yeye tumefahamiana
jana lakini utadhani urafiki wetu ni wa
miaka mingi.Nadhani ni wakati sasa wa
kuufungua ukurasa mpya katika maisha
yangu.Ukurasa wa mapenzi.Sihitaji kukata
tamaa kuhusu maisha yangu,nahitaji kuwa
na mawazo chanya kuhusu maisha yangu .I
want to live long because of Monica.”
Akaendelea kuwaza Dr Marcelo
.Akachukua simu yake na kuzitafuta
namba za Monica kwa dhumuni la
kumpigia na kumshukuru kwa usiku ule
mzuri lakini simu ya Monica haikuwa
ikipatikana
“ Nitaonana naye kesho.Lazima
nianze kuchukua hatua za haraka za
makusudi kuupalilia urafiki wetu.Tayari
kuna kila dalili kuwa hata yeye Monica
ananihitaji kuwa rafiki yake.Kitendo cha
kumuacha Daniel ambaye ni rafiki yake
mkubwa na wa siku nyingi akanialika
mimi ni wazi kuwa ananihitaji niwe karibu
yake.Nadhani tayari amekwisha zifahamu
tabia za Daniel na ameanza kujitenga
naye.Hii ni nafasi yangu kuitumia.Najua
Daniel akigundua kwamba nimekuwa na
ukaribu na Monica urafiki wetu
utatetereka sana lakini sijali kuhusu
hilo.Uhusiano wa Daniel na Monica
natakiwa kuuzika kabisa.Monica
anatakiwa awe na mwanaume mwenye
heshima zake kama mimi .” akawaza Dr
Marcelo
 
SEHEMU YA 16

onica hakurejea nyumbani kwake
baada ya sherehe kumalizika bali alienda
kujipumzisha katika chumba chake
kilichokuwapo katika nyumba ya wazazi
wake.
“ Mama alitaka kuongea nini na mimi
hadi akanifuata kule bwawani nilikokuwa
na Dr Marcelo na alijuaje kama niko kule?
Akajiuliza akiwa amejilaza kitandani
“ Hata hivyo hakuna ubaya wowote
kwani alitukuta tukiwa katika mongezi ya
kawaida.” akawaza Monica na kutabasamu
“ Hakuna siku nimejawa na furaha
katika maisha yangu kama leo.Nina furaha
ya ajabu sana.Sherehe imefana sana kila
mtu amefurahi na kwa hili napaswa
kuwashukuru sana wazazi wangu kwa
kunijali .Kitu kingine kilichonifanya niwe
na furaha ni Dr Marcelo.Nimepata leo
nafasi ya kukaa naye karibu tukaongea
japo kwa muda mfupi lakini ni mtu
ambaye naweza kusema kwamba
amenigusa sana.Ni kijana mwenye tabia
nzuri,ana moyo wa huruma na ana
malengo makubwa .Natamani kama
ningepata muda mrefu zaidi wa kukaa na
kuongea naye...” akawaza na kuinuka
akakaa.
“ Oh no !! I think Im falling in love so
quickly..” akasema kwa sauti ndogo
“ Kwa hili siwezi kubishana na moyo
wangu kuwa tayari nimeanza kumpenda
Dr Marcelo .Hata yeye kuna kitu
nimekigundua kutoka kwake .Kuna kila
dalili kuwa kuna kitu kipo kati yetu
.Naomba Mungu hisia hizi tulizonazo ziwe
za kweli “ Uso wa Monica ukajaa tabasamu
kubwa
“ Siwezi kusema moja kwa moja
kuwa Dr Marcelo is the right guy for me
hadi hapo nitakapomchunguza lakini
lazima nikiri kuwa amenisisimua na
katika kipindi hiki cha masaa machache
tulichofahamiana nimemsoma vya
kutosha na moyo wangu unaniambia
kwamba anaweza akanifaa.Pamoja na
hisia hizi kali nilizo nazo juu yake bado
sitakiwi kuwa na haraka.Natakiwa kwanza
kumfanyia uchunguzi wa kina nimfahamu
ni mtu wa aina gani” Mara akakumbuka
kitu
“ Dr Marcelo amenisaidia niweze
kumuweka pembeni Daniel.Ni kweli mimi
na Danny tumekuwa karibu na kwa
kipindi kirefu lakini kwa sasa simuhitaji
tena karibu yangu.Nimekwisha lifahamu
lengo lake kwangu na sitaki kumpa nafasi
ya kuwa karibu yangu.Sitaki kuzungukwa
na watu wachafu wa tabia kama
yeye.Nitakuwa karibu na Dr Marcelo
ambaye anaonekana ni kijana mwenye
tabia nzuri tofauti kabisa na Daniel.”
Akawaza Monica
 
SEHEM YA 17

Kumekucha
tena
siku
nyingine
imeanza.Saa nne za asubuhi Monica
akawasili ofisini kwake.Akiwa mapokezi
akataarifiwa kwamba Daniel alikuwa juu
ghorofani akimsubiri .Alifika toka saa
mbili za asubuhi.

Huyu
jamaa
anaonakana
atanisumbua sana.I must find a way to
drive him away from me..” akawaza
Monica huku akipanda ngazi kuelekea juu
.Alisalimiana na wafanyakazi wake halafu
akaelekea ofisini kwake akamkuta Daniel
akiwa katika sofa nje ya ofisi yake
akimsubiri.Pembeni yake kulikuwa na
maua mazuri .
“ Daniel “ akasema Monica huku
akijilazimisha kutabasamu
“ Monica” akasema Daniel akiinuka
akamfuata Monica akamkumbatia.
“ Goodmorning queen of Africa”
akasema Daniel
“ Goodmorning Daniel” akasema
Monica huku akiifungua ofisi yake
akamkaribisha Daniel ndani.
“ Daniel karibu sana.You are so early
today” akasema Monica
“ Yes I’m so early today.Nimefika
hapa kama mfanyakazi “ akasema Daniel
na wote wakacheka
“ Hii si kawaida yako Daniel.Kuna
tatizo lolote? Akauliza Monica huku
akipanga vitu vyake mezani halafu
akaenda katika sofa alikokuwa amekaa
Daniel
“ Sikuweza kupata usingizi usiku
ndiyo maana nimewahi sana kuja asubuhi
ya leo” akasema Daniel
“ Kuna tatizo gani Daniel? Kitu gani
kimekukosesha
usingizi?
Akauliza
Monica.Daniel akamtazama Monica kwa
sekunde kadhaa kisha akasema
“ Monica me and you we’re long time
great friends,right?
“ Yeah..We’re great friends” akajibu
Monica
“ Kwa nini ukanifanyia hivi?
“ Nimekufanyia nini Daniel?
“ Kwa nini hukuniambia kama
umefanyiwa sherehe ya kupongezwa na
wazazi wako? Kama hukutaka nihudhurie
lakini
basi
ungenitaarifu
tu
ingetosha.Hujawahi kunifanyia kitu kama
hiki
toka
tumefahamiana
.Nimesononeshwa sana na jambo hili na
ndiyo maana sikuweza kupata usingizi
usiku wa leo .Nimejiuliza maswali mengi
ni kitu gani nimekukosea hadi
ukashindwa kunialika katika sherehe
yako kubwa kama hii ili nifurahi pamoja
nawe? Tafadhali naomba unieleze Monica
kama kuna jambo lolote baya
nimekufanyia ili nikuombe msamaha na ili
siku nyingine usinifanyie jambo kama hili
ulilonifanyia” akasema Daniel.Monica
akamtazama kwa makni na kusema
“ Daniel kwanza naomba unisamehe
sana kwa hiki kilichotokea.Ni kweli jana
kulikuwa na sherehe iliyofanyika
nyumbani kwa wazazi wangu kwa lengo la
kunipongeza kwa mafanikio yangu.Ni
sherehe ndogo iliyoandaliwa na wazazi na
iliandaliwa kwa haraka na hata mimi
sikuwa nimetaarifiwa uwepo wa sherehe
hiyo.It was a surprise na walioalikwa
katika sherehe hiyo karibu wengi
walialikwa na wazazi bila ya mimi
kufahamu” akasema Monica
“ Lakini ulimualika Dr Marcelo.”
Akasema Daniel.Monica akanyamaza
kidogo akavuta pumzi na kusema
“ Nilikuwa na Dr Marcelo jana jioni
tukijadiliana mambo kadhaa kuhusiana na
shughuli ambazo mimi na taasisi yangu
tunakusudia kuzifanya nilipopigiwa simu
na mama akanitaka nifike nyumbani
haraka sana hivyo nikaongozana na Dr
Marcelo na tulipofika kule nikakuta
kumeandaliwa
sherehe.”Monica
akadanganya
“ Ahsante kwa taarifa hiyo lakini
ungenitaarifu kuhusiana na uwepo wa
sherehe hiyo ningekuja hata kama imefika
katikati. “
“ Samahani kwa hilo Daniel.It wont
happen agai......” kabla Monica hajamaliza
alichotaka
kukisema
mlango
ukafunguliwa akaingia Linah msaidizi
wake akiwa amebeba kikapu cha maua
mazuri sana.
“ Madam kuna mzigo wako umeletwa
hapa sasa hivi “ akasema Linah
“ Wow ! what a beautiful
flowers.Yametoka wapi haya? Akauliza
Monica huku akiinuka na kuyapokea maua
yale akayaweka mezani.
“ Kwa mujibu wa mtu aliyeyaleta
anasema ameagizwa na Dr Marcelo”
“ Dr Marcelo ? Daniel akasema kwa
mshangao.Linah akampa karatasi ya
kusaini kwamba amepokea mzigo .Monica
akasaini Linah akatoka .
“ Dr Marcelo amekutumia maua
haya? Akauliza Daniel.
 
SEHEMU YA 18

.Monica hakujibu
kitu akabaki anayatazama maua yale
mazuri huku akitabasamu
“ Inaonekana mmekuwa marafiki
wakubwa tayari hadi mtumiane maua?
Akauliza Daniel huku sura yake
ikionyesha
wazi
kuwa
hakuwa
amependezwa na kitendo kile cha Dr
Marcelo kumtumia Monica maua.
“ Stop that Danny.Kwani kuna ubaya
gani kwa Marcelo kunitumia maua?
Isitoshe I love flowers” akasema Monica
na mara simu yake ikaita alikuwa ni Dr
Marcelo
“ Hallow Dr Marcelo” Monica
akapokea simu ile mbele ya Daniel
“ Good morning Monica” akasema Dr
Marcelo
“ Good Moring Marcelo.Umeamkaje?
“ Nimeamka salama Monica sijui
wewe”
“ Mimi niko poa kabisa.Ahsante sana
kwa maua mazuri.Nimeyapokea muda
mfupi uliopita” akasema Monica huku
akitabasamu
“ Umeyapenda?
“ Kwa nini nisiyapende? I love
flowers ,nimeyapenda sana maua
uliyoyaleta” akasema Monica na mara
Daniel akainuka na kumfanyia Monica
ishara kuwa anaondoka .
“ Nashukuru sana kama umeyapenda
maua niliyokutumia Monica.Lengo ni
kukushukuru kwa siku ya jana ilikuwa ni
nzuri .Mimi si mtokaji sana wa kuhudhuria
sherehe au kwenda sehemu za starehe
muda mwingi niko kazini lakini kwa siku
ya jana nimefurahi mno.Ahsante sana
Monica”
“ Nafurahi kusikia hivyo Dr
Marcelo.Unajua mara nyingi tunajikuta
tukitumia muda mwingi kwa ajili ya kazi
zetu na kujisahau kama na sisi tunahitaji
kufurahi kama watu wengine. Ni muhimu
kutenga muda walau mara moja kwa wiki
kupumzisha na kuburudisha mwili.”
“ Usemayo ni ya kweli Monica.Basi
naomba nikuache uendelee na kazi zako
tutakutana kesho kutwa katika mbio.”
“Sawa Dr Marcelo.Ahsante sana na
uwe na siku njema” akasema Monica na
kukata simu.Akayatazama tena maua yale
aliyotumiwa na Dr Marcelo
“ Dr Marcelo ni mtu anayenifanya
nitabasamu kila siku.Hiki alichokifanya
anaweza akafikiri kuwa ni kidogo lakini ni
kitu kikubwa kwangu.” Akawaza Monica
na kukumbuka kitu
“ Daniel tayari amekwisha anza
kuwa na wasiwasi kuhusu ukaribu wangu
na Dr Marcelo .Nimeiona sura yake baada
ya kushuhudia maua yaliyotoka kwa Dr
Marcelom hakupendezwa.Najua hili ni
jambo linaloweza kuzua mtafaruku katika
urafiki wao kwani ni marafiki wakubwa
lakini mimi ndiye mwenye kuamua
ninataka kuwa na ukaribu na nani na kwa
sasa nimemchagua Dr Marcelo.Sitaki
kuendelea na ukaribu na Daniel.Nataka
kama ikiwezekana urafiki wangu naye
ufike mwisho.Sina tabia ya kuchagua
marafiki lakini kwa sasa itanilazimu
kufanya hivyo nataka kuwa na marafiki
wasafi wenye tabia na mienendo mizuri ili
niweze kuwa mfano kwa wengine kwani
kwa sasa mimi ni mtu ninayeangaliwa
sana kwa kila ninachokifanya” akawaza
Monica na kumuita Linah akampatia yale
maua aliyokuja nayo Daniel
“ Nenda kayaweke huko na tafadhali
naomba siku nyingine Daniel akija hapa
asiruhusiwe kuja kuingia bila ruhusa
yangu”
“ Sawa Madam” akajibu Linah na
kutoka
 
SEHEMU YA 19

“ Bado siamini eti urafiki wa Dr Marcelo na
Monica umekuwa mkubwa kiasi cha
kufikia
hatua
ya
kutumiana
maua.Nimewakutanisha juzi tu na leo
urafiki wao umekua kana kwamba
wamekutana miaka kumi iliyopita!! That
wont
happen.Halafu
jana
Monica
ameniacha mimi rafiki yake wa miaka
mingi toka utotoni akamualika Marcelo
mtu aliyefahamiana naye juzi kwa nini
lakini? Cha kushangaza zaidi Marcelo
amemtumia Monica maua.Hii ni wazi
urafiki wao unaanza kuota mizizi na kuna
kila dalili kuwa tayari Dr Marcelo
ameanza kuvutiwa na Monica.I wont let it
happen.Natakiwa kufanya kila niwezalo
kuhakikisha kwamba urafiki wao haufiki
kokote.Nikizubaa zubaa hapa nitakosa
kila
kitu.Siwezi
kukubali
kumkosa
Monica.Nimeupalilia urafiki wetu kwa
muda mrefu sana na siwezi kuja
kushindwa sasa labda mimi si Daniel
Swai” akawaza Daniel huku sura yake
ikiwa
imejikunja
akionekana
wazi
kukasirika sana.
“ Kwanza kabisa kuna mambo
ambayo natakiwa kuyafanya kwa haraka
sana.Kwanza natakiwa kuonana na
Marcelo na kumkanya aachane kabisa na
Monica.Najua anaweza akakasirika lakini
hakuna namna lazima nimueleze ukweli
kwamba Monica ni wangu na lazima
aachane naye haraka sana.Kama ni
ukaribu basi uwe ni wa kawada na
asijaribu kabisa kuingiza masuala ya
mapenzi kwa sababu nimekwisha mueleza
toka jana kuwa ninampenda Monica na
niko
katika
harakati
za
kumpata.Sintakubali hata kidogo atokee
na avuruge mipango yangu.Potelea mbali
kama urafiki wetu utavunjika lakini kwa
ajili ya Monica niko tayari kwa hilo “
Daniel akauma meno kwa hasira wakati
akielekea katika hospitali inayomilikiwa
na familia ya akina Marcelo.Alifahamika
sana mahala hapa kwa kuwa amekuwa
akija mara kwa mara ,akapokelewa vizuri
na kutaarifiwa kuwa Dr Marcelo alikuwa
anazungukia
wagonjwa.Hakutaka
kuondoka akaamua kumsubiri hadi
atakapomaliza shughuli zake.
Saa sita za mchana Dr Marcelo
akarejea ofisini kwake huku akionekana
kuwa na kazi nyingi,akastuka alipomkuta
Daniel.
“ Daniel!! Akasema
“ Dr Marcelo” akasema Daniel
“ Karibu sana.Umekuja muda mrefu?
“ Ndiyo nimekuja kitambo kidogo”
“ Karibu sana Danny.Leo niko katika
heka heka kuna wagonjwa wawili hali zao
si nzuri na ndiyo maana nimetumia muda
mrefu wodini.”
“ Ouh usijali Dr Marcelo” akasema
Daniel huku akiketi kitini.
“ Karibu sana Daniel..” akasema Dr
Marcelo baada ya kumuona Daniel akiwa
kimya huku akimtazama kwa macho
makali
“ Dr Marcelo utanisamehe kwa
kuchukua muda wako lakini nitajitahidi
kuongea kwa ufupi sana kile kilichonileta
hapa.”
“ Karibu..” akasema Marcelo
“ Nilitaarifiwa jana na Hidaya
kuhusiana na sherehe aliyoandaliwa
Monica na wazazi wake.nIliambiwa na
wewe ulihudhuria”
“ Yah nilihudhuria ilikuwa nzuri
.Ilifana mno.I wish ungekuwepo” akasema
Dr Marcelo
“ Too bad kwamba sikualikwa achilia
mbali kujulishwa kwamba kuna kitu kama
hicho.”
“ Lakini Monica ni rafiki yako
mkubwa ,kwa nini hakukujulisha kama
kuna sherehe imeandaliwa nyumbani
kwao? Akauliza Dr Marcelo
“ Sifahamu kwa nini lakini naona
kama vile urafiki wetu umeingiliwa na
mdudu na ndiyo maana hakunitaarifu
kama
kuna
shrehe
nyumbani
kwao.Hajawahi kutokea Monica akafanya
jambo
lolote
kubwa
bila
ya
kunitaarifu.Mimi na yeye tumekuwa
marafki kwa muda mrefu toka tukiwa
wadogo .Familia zetu ni marafiki wakubwa
kwa hiyo urafiki wetu haukuanza
jana.Nimestuka
sana
kwa
hiki
alichonifanyia Monica lakini inawezekana
kwa sababu ilikuwa ni sherehe ya
kustukiza ndiyo maana akanisahau mimi
mtu wake wa karibu.” Akasema Daniel
“ Surprise party?!! Dr Marcelo
akashangaa
“ Ndiyo.Anasema hakunialika kwa
sababu ilikuwa ni surprise party”

Hapana
haikuwa
surprise
party.Mbona mimi amenialika usiku wa
kuamkia jana? Kama ingekuwa ni surprise
asingenialika
siku
moja
kabla
 
SEHEMU YA 20

Inawezekana kabisa labda hakutaka
uhudhurie na ndiyo maana hakukutaarifu”
akasema
Dr
Marcelo.Maneno
yale
yalionekana kumchoma sana Daniel
ambaye aliinama akafikiri kidogo halafu
akainua kichwa na kusema
“ Inawezekana hayo unayoyasema ni
ya
kweli
.Inawezekana
hakutaka
nihudhurie katika sherehe hiyo lakini
pamoja na hayo bado Monica ndiye
mwanamke peke ninayempebnda kuliko
wote.Yawezekana alikuwa na sababu zake
na ndiyo maana akafanya hivyo
alivyofanya lakini siwezi kumchukia kwa
hilo wala kumlaumu kama kuna tatizo
atanieleza.” Akasema Daniel
“ Yah “ akajibu Dr Marcelo
“ Kabla ya kuja hapa nimetoka ofisini
kwa Monica nimeonge a naye na
tumeweka mambo sawa .Wakati nikiwa
pale ukaingia mzigo wa maua ukitokea
kwako.Nikastuka
kidogo
kwamba
mmefahamiana juzi tu na Monica halafu
leo hii tayari mmeanza kumtumia
maua.Nimejiuliza maswali mengi maua
yale yalikuwa kwa ajili gani? Ni ya
pongezi,au ya nini? Usije ndugu yangu
ukaanza kunizunguka wakati nimekwisha
kueleza kwamba mimi Monica ndiye
mwanamke ninayemtaka na nimeupalilia
urafiki wetu kwa miaka mingi na
nimekwisha
weka
ahadi
lazima
nihakikishe nimempata.” Akasema Danel
huku
akicheka
kidogo.Dr
Marcelo
akastuka sana kwa kauli ile ya Daniel
“ Unajua uuhh..nilimtumia maua
yale..you
know
me..ninapenda
kushukuru..” akasema Dr Marcelo.
“ Ni vizuri kama itakuwa hivyo na si
vinginevyo.Marcelo naomba nirudie tena
kukuweka wazi kwamba ninampenda
Monica sana zaidi ya ninavyoweza
kukueleza na kwa hiyo niko tayari
kufanya jambo lolote lile kwa ajili ya
kuhakikisha ninampata kwa hiyo basi
naomba ulifahamu hilo na usithubutu
kufanya mchezo wowote wa kujaribu
kunizunguka.Nikigundua
kama
unanizunguka I swear I’ll forget that you
are my friend and we’ll become
enemies.Umenielewa Marcelo? Akauliza
Daniel .Marcelo hakumjibu kitu akabaki
anamtazama.
“ Umenielwa Marcelo? Akauliza
Daniel safari hii kwa ukali kidogo
“ Daniel kuna kitu sijakielewa
hapa.Unadai kwamba Monica ni msichana
wako nikimpigia simu sasa hivi atakiri
hilo? Akauliza Dr Marcelo ambaye naye
alionekana kukereka sana na maneno yale
ya Daniel
“ Unataka kumaanisha nini Marcelo?
Akauliza Daniel uso ukiwa umejikunja
“ Ninataka nipate uhakika wa hayo
unayoyasema kama kweli Monica ni
mpenzi wako”
“ Sijasema kwamba Monica ni
mpenzi
wangu
nimesema
kwamba
ninataka awe mpenzi wangu na sijaanza
leo nimeanza kuipalilia njia miaka mingi
iliyopita na kuna kila dalili za kuelekea
katika kulifanikisha hilo hivi karibuni kwa
hiyo nakuomba usiwe kikwazo cha mimi
kushindwa
kulifanikisha
hilo.Toka
nimekutambulisha juzi naona kumekuwa
na mabadiliko makubwa kwa Monica.”
Akasema Daniel
“ Daniel kuhusu maelewano yako na
Monica kubadilika ghafla mimi si wa
kulaumiwa kwani siwezi kuingia ndani ya
moyo wa mtu na kujua anawaza nini .Hayo
ni masuala yenu ninyi wawili mkae na
mtafute namna ya kuyatatua na ninaomba
mimi nisihusishwe kabisa.Halafu hata
kama nikitaka kuanzisha mahusiano ya
kimapenzi hakuna wa kunizuia kwani
Monica yuko huru na hafungwi na
mahusiano yoyote” Akasema Dr Marcelo
kwa sauti ya juu
“ Marcelo naomba usijaribu kutafuta
ugomvi na mimi .Mmi ni mtu mbaya sana
nikikasirishwa kwa hiyo kama unataka
kuziona hasira zangu basi endeleza
mahusiano
na
Monica.Nimekwisha
kwambia kwamba Monica ni wangu .”
“ Daniel naomba tafadhali usijaribu
kunitisha.Huna uwezo wa kunizuia nisiwe
na Monica.Mwenye uwezo huo ni Monica
peke yake kwa hiyo kama huna jambo
lingine la kuniambia tafadhali naomba
uondoke ofisini kwangu kabla sijaita
walinzi wakutoe kwa nguvu.” Akasema Dr
Marcelo kwa ukali huku akisimama.Daniel
naye akasimamana kumkaribia
“ Please Marcelo don’t try me!!!
Akasema Daniel kwa hasira
“ Kwenda zako Daniel huna lolote la
kunitisha .Kama ungekuwa kidume kweli
kwa miaka hii yote uliyokuwa na ukaribu
na Monica basi ungekwisha mpata lakini
pale umegonga ukuta kwani Yule si kama
hao
makahaba
ambao
umezoea
kuwarubuni kwa vihela vyako.” Akasema
Dr Marcelo na ghafla Daniel akamvuta koti
na kutaka kumkaba lakini Dr Marcelo
akamsukuma kwa nguvu akaanguka chini.
“ Get out of my office right now kabla
sijakuharibu sura yako ..!!! akasema Dr
Marcelo kwa ukali
“ Marcelo hvi ni wewe unayethubutu
kunifanyia hivi kweli??? Akauliza Daniel
akiwa bado amekaa chini
“ Daniel naomba uinuke haraka sana
uondoke kabla hasira zangu hazijapanda
nikajikuta nimekufanyia kitu kibaya
ambacho nitakijutia !!! akasema Marcelo
kwa ukali.Taratibu Daniel akainuka

Marcelo
this
isn’t
over...Umeuwasha moto ambao hutaweza
kuuzima.Mimi na wewe hivi sasa ni
maadui wakubwa na sasa utanifahamu
kama mimi ndiye mwenye jiji hili.”
Akasema Daniel
 
[emoji134] [emoji134] [emoji134] [emoji134] ngoja nirudie tena kuanzia mwanzo, sehemu ya kwanza,


Maanake LEGE alisema ni bampa tu bampa kumbe anaishia hapa leo
 
[emoji134] [emoji134] [emoji134] [emoji134] ngoja nirudie tena kuanzia mwanzo, sehemu ya kwanza,


Maanake LEGE alisema ni bampa tu bampa kumbe anaishia hapa leo
kama umemaliza na unakesha mm nakuwekea muziki .kama unaweza kukesha mpaka mida ya wanga
 
SEHEMU YA 21

Hunitishi Daniel.Tena ninakuonya
kwamba kaa mbali kabisa na Monica na
usithubutu kumsogelea.Hakutaki kabisa
karibu yake wewe mchafu wa tabia.If I
ever see you near Monica agan it’ll be you
or me..!! akasema Marcelo .
“ Get prepared Marcelo!!! Akasema
Daniel na kutoka akiwa amejaa hasira.Dr
Marcelo akavuta pumzi ndefu na kuketi
kitini
“ Nilijua tu jambo kama hili lazima
litatokea.Lakini ni bora nikaingia katika
mgogoro na Daniel kuliko kumuacha
akawa karibu na Monica.Niko tayari kwa
lolote kwa ajili ya Monica.Yule ni mtu
mwenye heshima kubwa sana na siko
tayari kuona akiingia katika ulaghai wa
mtu kama Daniel.Ni bora nikayapoteza
maisha yangu katika kumpigania Monica
kuliko kukubali akawa katika mapenzi na
Daniel.Mimi simuogopi na hawezi
kunifanya chochote” akawaza Dr Marcelo
na kuchukua simu akampigia Monica
“ Hallow Dr Marcelo” akasema
Monica
“ Monica samahani sana kwa
kukusumbua tena”
“ Bila samahani Dr Marcelo”
akasema Monica
“ Daniel was here.Kumetokea
mtafaruku kati yetu”
“ oh my God !! is everything ok? Are
you ok? Akauliza Monica kwa wasi wasi
“ Usijali Monica hakuna tatizo
tulipisha tu kauli.” Akasema Marcelo
“ Alikuwa anataka nini Daniel?
“ Alikuja kunikanya nisiwe karibu
nawe kwa sababu anakusudia uwe
wake.Wewe nay eye mna mahusiano
yoyote ya kimapenzi?
“ Hapana mimi na Daniel hatuna
mahusiano yoyote yale ya kimapenzi ni
marafiki wa kawadia toka tukiwa
wadogo.Tafadhali naomba asikusumbue
huyo” akasema Monica kwa ukali
“ Hata mimi nilimwambia kwamba
hawezi kunizuia nisiwe karibu nawe bali
wewe ndiye mwamuzi kama niwe karibu
nawe au vipi.Ameondoka na hasira na
vitisho vingi.”
“ Pole sana Dr Marcelo na samahani
sana kwa kilichotokea.” Akasema Monica
“ Usijali Monica.Hili si tatizo kubwa
kwangu ila nimeona ni vema kama
nitakutaarifu
kilichotokea
na
kinachoendelea kati yangu na Daniel ili
usisikie kwa watu ukashangaa” akasema
Dr Marcelo
“ Ahsante Dr Marcelo .Again I’m so
sorry and dont worry I’m gong to handle
it”
“ Thank you Monica.Have a good
day”
“ You too “ akajibu Monica na kukata
simu
“ Huyu Daniel sasa amefika
pabaya.Kitendo cha mimi kuwa karibu na
Dr Marcelo kimemuumiza sana.Kumbe
lengo lake la kuwa karibu nami ni
kuniweka katika orodha ya wanawake
aliotembea nao.Hapa kwangu amekwaa
kisiki.Lazima nimkanye asimfuate kabisa
Dr Marcelo.Anatakiwa apambane na mimi
na si Dr Marcelo..” akawaza Monica na
kuchukua simu akampigia Daniel
“ Hallow Monica” akasema Daniel
baada ya kupokea simu
“ Daniel nataka unieleze kitu kimoja
tu,ulikwenda kufanya nini kwa Dr
Marcelo?? Akauliza Monica kwa ukali
“ Calm down Monica..”
“ Calm down?!! Nataka unieleze
umekwenda kufanya nini kwa Dr Marcelo?
“ Monica I’m sorry.Real I am.Naomba
tuzungumze suala hili wakati umetulia.Let
us find sometime and we can talk”
“ Nataka unieleze sasa hivi kwa nini
umemfuata Dr Marcelo na kumtusi pamoja
na kumtolea vitisho?
“ Monica taarifa ulizopewa si za
kweli,sijamtusi wala kumtisha lakini hata
hivyo naomba tuzungumze jambo hili
wakati tumetulia.Hivi sasa mimi nina
hasira na wewe una hasira pia kwa hiyo
hatuwezi
kuzungumza.Nitakutafuta
wakati umetulia na tutaongea ila I’m sorry
for what happened “
“ Wa kumuomba samahani si mimi
bali Dr Marcelo ambaye ulimfuata na
kumtolea vitisho kwamba asiwe karibu na
mimi.Wewe ni nani hadi unipangie watu
wa kuwa karibu nao.Umeniudhi sana
Daniel”
“ I’m so sorry Monica.Ndiyo maana
nikasema kwamba nitatafuta nafasi
wakati sote tumetulia tutaongea kuhusu
suala hili,ila naomba samahani sana kama
nimekuudhi Monica”
“ Ni kweli nimechukia lakini wa
kumuomba samahani si mimi bali ni Dr
Marcelo ambaye umemfuata na kumtolea
vitisho.Ukitaka nikusamehe nenda
kwanza kwa Dr Marcelo na umuombe
msamaha ndipo na mimi nitakusamehe”
akasema Monica na kukata simu
“ I’ll never say sorry to that
bastard...Sintaweza kumuomba msamaha
Dr Marcelo wakati yeye ndiye
aliyenichokoza kwa kuingia kwenye anga
zangu.Narudia tena I’ll never say sorry to
him na Monica lazima nitampata tu.Hana
ujanja kwangu.” Akasema Daniel kwa
hasira
 
SEHEMU YA 22

KINSHASA – JAMHURI YA
KIDEMOKRASIA YA CONGO.
Msafara wa magari zaidi ya kumi na
tano uliwasili katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa N’djili jijini Kinshasa.Ni
msafara wa rais wa jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo.Ulinzi ulikuwa
mkali hapo uwanjani kama ilivyo kawaida
ya rais huyu ambaye huwa na ulinzi mkali
sana.Taratibu za kiusalama zikafuatwa na
mlango wa gari la kifahari la rais ambalo
ni la kipekee kwa marais wa afrika
ukafunguliwa ,akashuka akiwa mwingi wa
tabasamu na kisha akaanza kutembea
katika zuria jekundu akisalimiana na
viongozi mbali mbali waliojipanga mstari
kumuaga.Kisha agana na viongozi
mbalimbali rais akaingia katika dege lake
kubwa la kifahari aina ya Boeing 747
tayari kwa safari ya kuelekea nchini
Tanzania kwa ajili ya mkutano wa wakuu
wa nchi za maziwa makuu.
David Bikumbi Mukaya Zumo ni rais
anayeongoza taifa kubwa la jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo.Ana umri wa
miaka 43 na anatajwa kuwa rais kijana
zaidi barani afrika.Anatokea katika
familia ya kitajiri sana.Baba yake mzee
Patrice Mukaya Zumo ni mmoja kati ya
matajiri wa kubwa sana na
wanaoheshimika nchini Congo na
afrika.Toka akiwa mdogo David aliishi na
kupata elimu yake nchini Ufaransa na hadi
alipohitimu sahahada yake ya uzamivu
katika masuala ya uchumi ndipo
aliporejea nchini Congo na kwa ushawishi
wa baba yake ambaye alimtaka arudi
Congo na ajihusishe katika masuala ya
siasa.David hakuwa mtu anayefahamika
sana nchini Congo lakini kwa ushawishi
wa baba yake ambaye ni tajiri
anayejulikana na kuheshmika sana nchini
Congo David alijulikana na kukubalika
kwa haraka na hatimaye ulipofika
uchaguzi David akachaguliwa kugombea
na kwa mshangao wa wengi aliibuka
mshindi kwa kura nyingi.
David Zumo ni rais ambaye anatajwa
kufanya mambo mengi makubwa katika
nchi ya Congo kwani toka aliposhika
madaraka uchumi wa Congo umepaa kwa
kiwango cha kushangaza.Kumejengwa
viwanda vingi ambavyo vimetengeneza
ajira nyingi.Huduma za elimu na afya
zimeboreka kwa kiwango cha juu
mno.Miundo mbinu imeboreshwa kwa
kiwango kikubwa kwani wakati akiingia
madarakani alikuta kukiwa na kilometa
chini ya 3500 za lami na ameboresha hadi
kufikia kiasi cha kilometa zaidi ya 30000
za lami kwa nchi nzima.Anatajwa kuwa
rais pekee ambaye katika kipindi cha
uongozi wake ameweza kuleta amani
nchini Congo kitu ambacho wananchi wa
Congo walikuwa wanakihitaji kwa muda
mrefu.Ameweza kukaa na makundi ya
waasi wakakubaliana kusitisha mapigano
na kuufungua ukurasa mpya wa watu wa
Congo kuijenga nchi yao.Ni rais ambaye
anatajwa na tafiti mbali mbali
zilizofanyaka kuwa katika maraisi wote
waliowahi kuitawala nchi hii tajiri David
Zumo ndiye ndiye rais anayependwa zaidi
nchini Congo hasa kutokana na mambo
aliyoyafanya.Amefanikiwa kulifanya taifa
la Congo kuwa taifa kubwa na lenye nguvu
kiuchumi na kijeshi.
Pamoja na kazi kubwa ya kuibadili
Congo aliyoifanya David Zumo na kuifanya
iwe mojawapo ya nchi inayoongoza kwa
uchumi mkubwa lakini kuna mambo
mengine makubwa aliyoyafanya ambayo
yaliweka doa katika utawala
wake.Kikubwa alichokifanya David
ambacho kilimuwekea doa kubwa na
kumfanya apigiwe kelele na jumuiya za
kimataifa ni kitendo cha kukutaka
kuibadili Congo kuwa nchi ya kifalme nay
eye kutawazwa kuwa mfalme wa kwanza
wa Congo.Tayari maandalizi ya jambo hilo
yamekwisha kamilika na kilichokuwa
kinasubiriwa ni wananchi kupiga kura ya
maoni kuamua jambo hilo.
Ukiacha hilo la kutaka kuibadili
Congo kuwa nchi ya kifalme David ni
mmoja wa marais wachache matajiri
wakubwa
duniani
anayetajwa
kujilimbikizia kiasi kikubwa cha mali.Ni
raisi ambaye anaongoza kwa utajiri barani
afrika.Anatajwa kuwa tajiri wa kwanza
Afrika.Ndiye rais pekee afrika mwenye
ndege yake binafsi kubwa na ya kifahari
aina ya Boeng 747 iliyogharimu kiasi cha
dola milioni 530 za Marekani.Ni ndege ya
kifahari mno.Ukiacha hiyo ndege
anamiliki pia shirika lake kubwa la ndege
la Dav air lenye ndege kubwa zaidi ya
hamsini zinazofanya safari ndani na nje ya
Congo.Anamiliki pia mahoteli na biashara
nyingine kubwa kubwa nje ya Congo . Ni
rais anayeishi maisha ya anasa kubwa
pengine kuliko wote afrika.
 
SEHEMU YA 23

aada ya kuingia ndegeni
alisalimiana na walinzi wake pamoja na
wasaidizi wake akaenda pia katika
chumba cha marubani akasalimiana nao
na moja kwa moja akaelekea katika
chumba maalum cha rais kiilichokuwa na
kila kitu kuanzia ofisi,ukumbi wa
mikutano chumba cha kulala n.k.Baada ya
dakika chache dege likapaa kuelekea Dar
es salaam.
Akiwa katika chumba chake cha
mikutano alijadiliana mambo kadhaa na
wasaidizi wake alioambatana nao kisha
akawaomba wamuache apumzike
kidogo.Baada ya wasaidizi wale kundoka
akamuita Jean Pierre Muyeye mmoja wa
wasaidizi wake anayemtumia katika
mambo yake mengi binafsi. Haraka haraka
Muyeye akafika .David alikuwa
ameelekeza macho katika kompyuta yake
ndogo baada ya kama dakika mbili hivi
akainua kichwa na kumtazama Muyeye.
“ Muyeye tunakwenda Dar es salaam
lakini tukiwa huko kuna jambo ambalo
nataka ulifanye.” Akasema David
“ Niko tayari mkuu” akajibu Jean
Pierre Muyeye kwa adabu.David
akamgeuzia Muyeye kompyuta ile ndogo
ambayo kulikuwa na jalada la jarida la The
Face lililopambwa kwa picha ya
mwananke mmoja mrembo sana
aliyekuwa ndani ya tabasamu pana
“ Umemuona huyo mwanamke
katika hilo jarida? Akauliza David
“ Ndiyo mzee nimemuona.”
“ Vizuri.Jina lake anaitwa Monica
Benedict Mwamsole ni mtanzania.Ni mtoto
wa mfanya biashara mmoja mkubwa pale
jijini Dar es salaam anaitwa Benedict
Mwamsole”
David
akanyamaza
akamtazama Muyeye na kuendelea
“ Tukifika Dar es salaam wakati
ninaendelea na kikao wewe utakuwa na
kazi moja tu nataka ukusanye taarifa za
kumuhusu huyu msichana.Nataka mpaka
jioni ya leo uwe umepata taarifa sahihi na
za kutosha kuhusu Monica. Tafadhali
Muyeye jambo hili ni muhimu sana
kwangu na kazi hii unatakiwa uifanye kwa
umakini na kwa usiri mkubwa.Baada ya
kuzipata taarifa hizo nitakuelekeza nini
cha kufanya” akasema David Zumo na
baada ya maelekezo machache Muyeye
akatoka na kumuacha rais peke yake mle
ofisini.David akaelekeza tena macho
katika kompyuta yake akaanza
kuzitazama picha mbali mbali za Monica
alizozikuta mtandaoni
“ Monica Benedict Mwamsole..”
akasema kwa sauti ndogo
“ Hakika huyu msichana ana uzuri
wa kipekee sana na anastahili kuwa
mrembo kuliko wote Afrika.” Akawaza na
kupiga funda kubwa la mvinyo mkali
“Katu siwezi kukubali msichana
mrembo kama huyu akanikosa.Ugonjwa
wangu mimi ni wanawake wazuri kama
hawa.Lazima nifanye kila linalowezekana
kuhakikisha ninampata .Lazima awe mke
wangu.Kama yeye ni malkia wa afrika basi
mimi ndiye mfalme wa Afrika.Monica
anastahili kuwa na mtu kama mimi ili
aishi kweli yale maisha ya kimalkia.”
Akawaza David na unywa tena funda
lingine la mvinyo
“ Macho yangu yameona wanawake
wengi lakini si kama huyu.Monica ni
mwanamke wa tofauti sana.Wanawake
wenye sura kama hizi tumezoea kuwaona
katika michoro ya wachoraji mahiri lakini
kumbe kuna wengine wapo kweli na
mmoja wao ni huyu Monica.I swear lazima
nimpate huyu mwanamke.Kwa namna
yoyote ile lazima nimpate ” Akaendelea
kuwaza David huku dege lake likiwa
angani kuelekea Dar es salaam.
 
SEHEMU YA 24


Daniel hakutaka kuelekea sehemu
nyingine yoyote baada ya kutoka kwa Dr
Marcelo akanyoosha moja kwa moja kwa
Muktar rafiki yake anayefanya biashara ya
kuuza vipuri vya magari na ambaye huwa
wanashirkiana mambo mengi.
“ King Daniel !! akasema Muktar
baada ya kumuona Daniel akiingia dukani
kwake
“ Leo kulikoni asubuhi namna hii?
Gari
lina
matatizo?
Akauliza
Muktar.Hakuwa amezoea kuonana na
Daniel mida kama ile.
“ Kwani kuna ubaya nikija dukani
kwako asubuhi Muktar? Akauliza Daniel
“ Hakuna ubaya Danny lakini
nimeuliza tu kwa sababu sijazoea kukuona
maeneo haya asubuhi. Karibu sana
Daniel..” akasema Muktar na kumtazama
Daniel usoni akagundua kuwa kuna kitu
hakiko sawa
“ Daniel kuna tatizo? Akauliza
Muktar
“ Daniel nimekuja kwako unishauri .”
akasema Daniel na Muktar akamuongoza
hadi katika ofisi yake .
“ Kuna tatizo gani Daniel?
Akauliza.Daniel akavuta pumzi ndefu na
kusema
“ Muktar nadhani unamfahamu
Monica”
“ Monica Yule rafiki yako?
“ Ndiyo”
“ Ninamfahamu vizuri.Nini
kimetokea?
“ Muktar wewe unanifahamu vizuri
mimi ugonjwa wangu ni vimwana
warembo.Nimekuwa na ukaribu na
Monica kwa muda mrefu sasa na sikufichi
ndugu yangu Yule mtoto amenichanganya
mno.Sijawahi kuchanganyikiwa kwa
mwanamke kama ilivyonitokea kwa
Monica.Pale akili yangu imefika mwisho
,ninampenda Monica zaidi ya ninavyoweza
kueleza.Monica ana mradi wake mkubwa
anataka kuuanzisha anataka kujenga
shule ya watoto walemavu kwa hiyo
anahitaji fedha nyingi.Ameandaa mbio za
nusu marathoni ili kukusanya fedha toka
kwa watu mbali mbali.Kuna Yule rafiki
yangu Dr Marcelo naye baada ya kusikia
kuhusu jambo hilo akataka kuchangia
nikamkutanisha na Monica wakaongea na
akatoa mchango wake lakini mara ghafla
naona mambo yamebadilika.Monica na Dr
Marcelo wamekuwa na ukaribu mkubwa
sana.Jana
kulikuwa
na
sherehe
iliyoandaliwa nyumbani kwa wazazi wa
Monica
kumpongeza
lakini
cha
kushangaza kwa mara ya kwanza toka
nimekuwa na ukaribu na Monica
hakunialika katika sherehe hiyo na badala
yake akamualika Dr Marcelo.Nilipopata
taarifa hizo nilishangaa sana na asubuhi
ya leo nikawahi ofisini kwa Monica ili
anieleze ni sababu gani iliyopelekea
asinialike katika sherehe yake lakini
wakati tukiongea akaingia msaidizi wake
akiwa na kikapu cha maua yaliyotoka kwa
Dr Marcelo.Nilikasirika nikaondoka bila
hata kumuaga nikaelekea moja kwa moja
kwa Dr Marcelo kumuonya akae mbali na
Monica kwani Monica ni wangu .Sikuweza
kuelewa na Dr Marcelo na tukataka
kugombana.Ameniudhi sana Yule paka na
hapa nilipo nina hasira kama za Mbogo.Dr
Marcelo ameonyesha kila dalili kuwa
anamtaka Monica na hata Monica
ameonyesha dalili za kuvutiwa na
Marcelo.Muktar nimechanganyikiwa and I
don’t know what to do.Tafadhali naomba
unishauri nini cha kufanya? Akasema
Daniel.Muktar akatoa sigara akawasha na
kupiga mikupuo kadhaa kisha akasema
“ Una hakika Monica anaweza akawa
amevutiwa na Marcelo au ni urafiki wa
kawaida tu?
“ Muktar laiti ungemuona namna
Monica alivyotabasamu baada ya kupokea
maua
yaliyotoka
kwa
Daniel
ungekubaliana nami kuwa tayari ameanza
kuvutiwa na Yule mjinga.I swear I’m going
to destroy that bastard !!!..akasema Daniel
na kugonga meza
“ Daniel punguza hasira kidogo ili
tujadili namna ya kulimaliza suala hili.”
“ Muktar nina hasira sana na
ninaweza kufanya chochote kile kwa aili
ya Monica.!! Akasema Daniel
“ Kibaya zaidi Marcelo amempigia
simu Monica na kumueleza kwamba
nimemfuata na kumtishia maisha yake
jambo ambalo limemkasirisha sana
Monica.Muktar sikutaka kabisa kumuudhi
Monica.I don’t know what to do” akasema
Daniel na kuinama chini
 
SEHEMU YA 25

Daniel siku zote ninakuelezaga
kwamba wewe ni mtu mwenye hasira
nyingi kwa hiyo jitahidi siku zote kudhibiti
hasira zako.Kitendo ulichokifanya cha
kumfuata Marcelo ni wazi hakikuwa
kizuri.Kwa hapa jambo hili lilipofika
inahitajika busara zaidi kuweka mambo
sawa””
akasema
Muktar
,Daniel
akamtazama kwa macho makali
“ Unataka kumaanisha nini Muktar?
Akauliza
“ Namaanisha kwamba tayari
ulikwisha jenga mahusiano mazuri na
Monica na njia ilikuwa nyeupe kumpata
lakini kwa hiki ulichokifanya cha
kumfuata Marcelo tayari kimetia doa ile
taswira nzuri uliyoijenga kwa Monica.Ili
kuijenga tena taswira nzuri kwa Monica
unatakiwa kufanya jambo ambalo naamini
kwako litakuwa gumu lakini lazima
lifanyike.Unatakiwa
ukamuombe
msamaha Monica “ akasema Muktar
“ Tayari nimekwisha fanya hivyo
lakini imeshindikana,amenipa sharti
ambalo ni gumu kwangu” Akasema Daniel
“ Amekupa sharti gani Monica?
“ Amesema eti nikamuombe
msamaha Marcelo jambo ambalo katu
siwezi kulifanya” akasema Daniel na
kuukunja uso.Muktar akamtazama na
kusema
“ Kama Monica ndivyo anavyotaka
please do it..”
“ No !! No !! no.!!.siwezi katu kufanya
kitu kama hicho .Siwezi katu kumuomba
msamaha Marcelo wakati ni yeye ndiye
aliyeingia katika anga zangu .Kama Monica
hatanisamehe kwa sababu tu sijamuomba
msamaha Marcelo let it be ila siko tayari
kabisa kabisa kwenda kumpigia magoti
Yule mbuzi na kumuomba msamaha.But I
swear I’ll destroy him....!! Atanitambua
mimi ni nani!! Siwezi kumkosa Monica
kwa sababu yake!!! Akasema Daniel huku
akigonga meza kwa hasira na kuinuka
“ Daniel tafadhali punguza hasira na
usifanye
hicho
unachodhamiria
kukifanya.Usijingize tena katika matatizo
mengine yasiyokuwa na msingi.Tafuta njia
nyingin......” akasema Muktar lakini kabla
hajamaliza Daniel akasema kwa sauti kali
“ Huna chochote cha kunishauri
Muktar.Wewe nawe ni kama wao tu.I wont
come to you again for advice.....!! akasema
kwa ukali na kuondoka
“ Kama ni kumkosa Monica acha
nimkose lakini si kumpigia magoti Yule
mshenzi Marcelo.Yeye ndiye sababu ya
mimi kumkosa mwanamke ninayempenda
kuliko wote and I’m going to show him
who I real am.Nitamuonyesha kwamba hili
jiji ni langu..!! akawaza huku akiuma meno
kwa hasira baada ya kuondoka dukani
kwa Muktar
 
Back
Top Bottom