SEHEMU YA 106
onica aliingia chumbani kwake na
kuketi sofani .Alihisi kichwa kizito
kutokana na kujawa na mawazo
mengi.Jambo aliloelezwa na wazazi wake
usiku ule lilimchanganya mno akili yake
“ Sikutegemea kabisa kusikia hiki
nilichokisikia usiku wa leo toka kwa
wazazi eti Davi Zumo anataka kunioa”
akawaza halafu akavua viatu na kujilaza
sofani
“ David Zumo ni mtu mkubwa,ni rais
mwenye nguvu na tajiri namba moja
Afrika.Kusema kwamba amenipenda na
anataka kunioa si kitu kidogo.Hili ni
jambo kubwa kwake,kwangu na kwa nchi
zetu pia.Ninatakiwa kutafakari kwa
makini sana kuhusu suala hili na
kuchukua maamuzi yenye kufaa.Oh m y
gosh ! kichwa changu nahisi kimejaa na
kinashindwa kufikiri sawa sawa”
akainuka akabadili mavazi akatoka na
kuelekea katika bwawa la kuogelea
akajitumbukiza
majini
akaanza
kuogelea.Mara nyingi awapo na jambo
kubwa linalomsumbua kichwa chake
hupenda sana kuogelea.Wakati akiogelea
bado kichwa chake kiliendelea kujaa
mawazo kuhusiana na David Zumo.
“ Nilijiuliza sana sababu ya David
Zumo kutoa msaada ule mkubwa kumbe
alikuwa na lengo lake na msaada ule
alionipa ni moja kati ya njia za kutaka
kufanikisha lengo lake la kuanzisha
mahusiano na mimi.Amenifahamu kwa
muda gani hadi afikie hatua ya kufanya
maamuzi ya kutaka kunioa? Nia yake ya
kutaka kunioa inatoka moyoni au
amevutiwa tu na uzuri wangu? Ninahisi
yawezekana akawa amevutiwa na uzuri
wangu na hasa baada ya kutangazwa
mrembo zaidi Afrika na anataka kutumia
jina na utajiri wake kunipata.Endapo
angekuwa na nia ya dhati kwangu
angeweza kuieleza mimi mwenyewe wazi
wazi lakini hakufanya hivyo na badala
yake akawaeleza wazazi ili wao
wanishawishi mimi nikubali kuolewa
naye.Thats an old style.Wazazi nao kwa
tamaa ya utajiri walioahidiwa
wanajitahidi kufanya kila wawezalo
kunishawishi nikubali kuolewa na
David.Sijawahi kubishana nao hata mara
moja na wanaitumia fursa hiyo
kunishawishi.I’m confused and I don’t
know what to do” akawaza na kuzama
chini halafu akaibuka
“ Kwa mara ya kwanza katika maisha
yangu
nitatofautiana
na
wazazi.Sintakubaliana nao kwa hiki
wanachotaka nikifanye” akawaza na
kuzama tena chini ,akaibuka
“ Simfahamu David Zumo
kiundani,sizifahamu tabia zake,sifahamu
ananipenda kiasi gani.Ninafahamu kitu
kimoja tu kuhusu David kwamba ni tajiri
namba moja Afrika.Zaidi ya hilo sifahamu
chochote kuhusu yeye na siwezi kukubali
au kufurahia kuolewa na bilionea huyu
ambaye bado simfahamu vyema.”
Akaendelea kupiga mbizi kuzunguka
bwawa.
“ Suala la ndoa si suala rahisi kama
wao wanavyolichukulia.Ni jambo
linalohusu moyo zaidi kuliko mali .Kama
isingekuwa matatizo yaliyomtokea Dr
Marcelo ,ni mwanaume ambaye tayari
nilikwisha aanza kuvutiwa naye .Ana sifa
nyingi kati ya zile ninazozihitaji kwa
mwanaume wa maisha yangu,lakini naye
kama ilivyo kwa David Zumo bado
simfahamu vyema na kuna mambo mengi
ambayo nahitaji kuyafahamu kuhusu yeye
lakini kwa sasa its already late.kwa
mambo yaliyotokea mimi na yeye
tutaendelea kuwa marafiki wa kawaida
tu.Namuomhea aweze kupona na aendelee