SEHEMU YA 22
Simu iliyopigwa na balozi wa China
nchni Tanzania ilimkuta rais Ernest Mkasa
tayari amekwisha amka kitambo na
alikuwa anajiandaa kwenda katika
mazoezi ya asubuhi kama kawaida
yake.Ilipata saa kumi na mbili na dakika
tatu za asubuhi.
“ Hallow mheshimiwa balozi”
akasema Ernest baada ya kupokea simu
“ Habari za asubuhi mheshimiwa
rais”
“ habari nzuri mheshimiwa
balozi.Nadhani una habari nzuri za kunipa
asubuhi hii” akasema Ernest
“ Ndiyo meshimiwa rais.Ninazo
taarifa nzuri asubuhi ya leo.Nimetaarifiwa
muda mfupi uliopita na msaidizi wa rais
kuwa kutokana na urafiki mzuri baina ya
China na Tnzania,rais amekubali ombi
lako kwa hiyo tutafanya mabadilishano ya
wafungwa.Kwa hiyo mheshimiwa rais saa
tano kamili leo kwa saa za hapa Tanzania
mfungwa Linda atakabidhiwa kwa ubalozi
wa Tanzania nchini China na kwa taratibu
za mabadilishano zilivyo muda huo huo
wafungwa wa China watakabidhiwa kwa
ubalozi wa China hapa Tanzania.Natumai
tumeelewana meshimiwa rais”
“ Nashukuru sana mheshimiwa
balozi.Siwezi elezea furaha yangu kwa
jambo hili kufanikiwa.Makabidhiano
yatafanyika kama kawaida katika muda
huo.Mheshimiwa
balozi
narudia
kukushukuru tena.Ahante sana” akasema
Ernest na kukata simu.
“Sasa kazi yangu inakwenda
kufanyika kwani Austin hakuwa tayari
kufanya chochote
hadi
pale
atakapohakikisha mdogo wake ametoka
gerezani.” Akawaza Ernest huku
akizitafuta namba za simu za Mukasha na
kumpigia
“ Habari zaa asubuhi mheshimiwa
rais” akasema Mukasha baada ya kupokea
simu
“ Habari nzuri Mukasha.Nimepokea
simu muda si mrefu kutoka kwa balozi wa
China anasema ule mpango umefanikiwa
kwa hiyo saa tano kamili leo kwa saa za
Tanzania mabadilishano yatafanyika
katika balozi zetu.Kwa hiyo lishghulikie
suala hili”
“ Hizo ni taarifa njema sana
mheshimiwa rais.Nitamtaarifu mkuu wa
magereza suala hili ili mchakato uanze
mara moja” akasema Mukasha .
“ Sawa Mukasha,shughulikia suala
hilo na tutawasiliana baadae’ akasema
Ernest na kukata simu akatoka mle
chumbani akasalimiana na walinzi wake
akaelekea katika mazoezi.Mara tu
alipotoka mle chumbani,bi Agatha Mkasa
mke wa Ernest akaichukua simu na
kupekua akaipata namba ya simu ya mtu
aliyekuwa anaongea na rais muda mfupi
uliopita
“ Jing wang Zhu??...akajiuliza
“ Balozi wa China na Ernest wana
mpango gani unaoendelea? Nimemsikia
Ernest akiongelea kuhusu makabidhiano
yatakayofanyika leo,wanakabidhiana kitu
gani? Nahisi kuna jambo Ernest ananificha
kwani nimegundua kwa siku za karibuni
amebadilika ghafla .Ni wazi kuna jambo
linaloendelea chini kwa chini na hataki
kunitaarifu.Nimemuona hata usiku
anakuwa macho muda mwingi ,lazima
kuna kitu kinamsumbua” akawaza
“ Ili nifahamu kinachoendelea lazima
nimchunguze Mukasha kwani ndiye
aliyetumwa kuhakikisha makabidhiano
hayo yanafanyika”
i Agatha akairudisha simu mezani
na haraka akaichukua simu yake
akazitafuta namba Fulani akapiga
“ Hallow “ akasema Agatha baada ya
simu yake kupokelewa upande wa
pili.Baada ya salamu Agatha akasema
“ Muhsin nimekupigia asubuhi hii
kuna jambo nataka nikueleze.Kwa siku
kadhaa nimeona mabadiliko kwa Ernest
nikahisi kuna kitu kinamsumbua.Leo
asubuhi nimemsikia akizungumza na
balozi wa China hapa nchini na walikuwa
wanazungumiza
kuhusu
makabidhiano.Sifahamu ni makabidhiano
gani hayo ila ninaamini kuna kitu
kinachoendelea kati ya Ernest na balozi
wa China.Kuna chochote unachokifahamu
kuhusu Ernest na balozi wa China?
“ Mhh !! hapana sifahamu chochote
.Rais hajanieleza jambo lolote” akajibu
Muhsin.
“Damn you Muhsin,you are a vice
president and its your job to know
everything that’s going on.Tunakutegemea
sana wewe kujua kila kinachoendelea
katika ofisi ya rais.Be smart Muhsin.Find
out whats going on.Kwa kukusaidia kujua
kinachoendelea ni kwamba tuma vijana
wamchunguze Mukasha kwani ndiye
aliyekabidhiwa
kazi
hiyo
aisimamie.Kupitia kwake kuna kitu
tunaweza kukigundua” akasema Bi Agatha
“ Agatha ahsante kwa taarifa
nitaifanyia kazi” akajibu Muhsin
Abdulkareem masoud makamu wa rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania na
kukata simu