LEGE
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 5,122
- 9,209
- Thread starter
- #561
SEHEMU YA 23
KINSHASA – JAMHURI YA KIDEMOKRASIA
YA CONGO
Saa ya dhahabu iliyokuwa
inaning’inia ukutani ilionyesha tayari
imekwisha timu saa mbili na dakika tisa za
asubuhi.Taratibu Monica akatoka
kitandani na kusimama katikati ya
chumba kile kikubwa na kutabasamu
.Alivutiwa mno na uzuri wa chumba kile.
“ Jana sikukichunguza vizuri chumba
hiki ..mhh ni chumba chenye uzuri wa
ajabu kabisa.” Akaenda dirishani akafunua
pazia na kuchungulia nje
‘” Wow !! akajikuta akitamka baada
ya kuishuhudia mandhari ya aina yake
kulizunguka jumba lile
“ This house is amazing.Kuna uzuri
wa kipekee kabisa mahala hapa.Panavutia
na unaweza kutamani uishi hapa maisha
yako yote” akawaza na kuvaa nguo zake za
mazoezi akatoka mle chumbani
,akasalimiana na wafanyakazi wa ndani
halafu akaelekea katika chumba cha
mazoezi.Kisha maliza mazoezi akarejea
chumbani akaoga na akiwa katika
kujiandaa kengele ya mlangoni ikalia
akaenda kuufungua mlango akakutana na
mwanadada mrembo aliyejitambulisha
kama mpambaji wake mkuu,akamtaka
waongozane hadi katika saluni
iliyokuwamo ndani ya hilo jengo ambako
Monica akarembwa vilivyo.
Kisha maliza kujiandaa akaenda
katika chumba cha chakula akapata
kifungua kinywa halafu akarejea tena
chumbani kumsubiri Pauline ambaye
alimuahidi kuwa angefika kumchukua
.Wakati akimsubiri Pauline Monica
akatumia simu iliyokuwao mle chumani
kuwapigia simu wazazi wake
akawahakikishia kwamba anaendelea
vizuri na wasiwe na wasiwasi.Kisha maliza
kuwasiliana na wazazi wake akapata wazo
“ Natamani nijue hali ya Dr
Marcelo.Mtu pekee ambaye anaweza
akanipa habari za Marcelo ni Daniel “
akawaza na haraka haraka akaziandika
namba za simu za Daniel kwani
alizifahamu kwa kichwa akampigia.
“ Hallow” ikasikika sauti ya Daniel
upande wa pili wa simu
“ Daniel its me Monica”
“ Monica!! How are you? Umenipigia
kwa namba hi...” akasema Daniel lakini
Monica akamkatisha kabla hajaendelea
zaidi
“Daniel nimekupigia kutaka
kufahamu jambo moja tu.Ni kuhusiana na
Dr Marcelo.Anaendeleaje?
“ Nimetoka kumtazama leo asubuhi
anandelea vizuri lakini bado hajaanza
kuzungumza.Bado anatumia maadishi
kuwasiliana.Amekuulizia nikamdanganya
kuwa umepata dharura nje ya Dar es
salaama na akasema nikukumbushe
kuhusu ombi lake.Hizi ni namba za Congo
KINSHASA – JAMHURI YA KIDEMOKRASIA
YA CONGO
Saa ya dhahabu iliyokuwa
inaning’inia ukutani ilionyesha tayari
imekwisha timu saa mbili na dakika tisa za
asubuhi.Taratibu Monica akatoka
kitandani na kusimama katikati ya
chumba kile kikubwa na kutabasamu
.Alivutiwa mno na uzuri wa chumba kile.
“ Jana sikukichunguza vizuri chumba
hiki ..mhh ni chumba chenye uzuri wa
ajabu kabisa.” Akaenda dirishani akafunua
pazia na kuchungulia nje
‘” Wow !! akajikuta akitamka baada
ya kuishuhudia mandhari ya aina yake
kulizunguka jumba lile
“ This house is amazing.Kuna uzuri
wa kipekee kabisa mahala hapa.Panavutia
na unaweza kutamani uishi hapa maisha
yako yote” akawaza na kuvaa nguo zake za
mazoezi akatoka mle chumbani
,akasalimiana na wafanyakazi wa ndani
halafu akaelekea katika chumba cha
mazoezi.Kisha maliza mazoezi akarejea
chumbani akaoga na akiwa katika
kujiandaa kengele ya mlangoni ikalia
akaenda kuufungua mlango akakutana na
mwanadada mrembo aliyejitambulisha
kama mpambaji wake mkuu,akamtaka
waongozane hadi katika saluni
iliyokuwamo ndani ya hilo jengo ambako
Monica akarembwa vilivyo.
Kisha maliza kujiandaa akaenda
katika chumba cha chakula akapata
kifungua kinywa halafu akarejea tena
chumbani kumsubiri Pauline ambaye
alimuahidi kuwa angefika kumchukua
.Wakati akimsubiri Pauline Monica
akatumia simu iliyokuwao mle chumani
kuwapigia simu wazazi wake
akawahakikishia kwamba anaendelea
vizuri na wasiwe na wasiwasi.Kisha maliza
kuwasiliana na wazazi wake akapata wazo
“ Natamani nijue hali ya Dr
Marcelo.Mtu pekee ambaye anaweza
akanipa habari za Marcelo ni Daniel “
akawaza na haraka haraka akaziandika
namba za simu za Daniel kwani
alizifahamu kwa kichwa akampigia.
“ Hallow” ikasikika sauti ya Daniel
upande wa pili wa simu
“ Daniel its me Monica”
“ Monica!! How are you? Umenipigia
kwa namba hi...” akasema Daniel lakini
Monica akamkatisha kabla hajaendelea
zaidi
“Daniel nimekupigia kutaka
kufahamu jambo moja tu.Ni kuhusiana na
Dr Marcelo.Anaendeleaje?
“ Nimetoka kumtazama leo asubuhi
anandelea vizuri lakini bado hajaanza
kuzungumza.Bado anatumia maadishi
kuwasiliana.Amekuulizia nikamdanganya
kuwa umepata dharura nje ya Dar es
salaama na akasema nikukumbushe
kuhusu ombi lake.Hizi ni namba za Congo