QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

SEHEM YA 26



kuanzisha mahusiano nawe na hatimaye
kufunga nawe ndoa lakini anadai aliongea
na baba yako na nina hakika ujumbe wake
ulifika”.Pauline akanyamaza Monica
aliyekuwa anamsikiliza Pauline kwa
makini akakohoa kidogo kurekebisha koo
halafu akasema,
“Pauline kabla sijasema chochote
naomba nikupe pole sana kwa tatizo hili
kubwa ulilonalo.Nimeguswa sana kama
mwanamke kwa hali yako.Nafahamu
mateso anayopitia mwanamke kwa
kukosa mtoto”akanyamaza kidogo halafu
akaendelea.
“Nimeyasilikiza maelezo yako
kwa makini na ninapenda nitumie nafasi
hii kukupongezeni kwa upendo mkubwa
mlio nao ambao umewawezesha
muendelee kuisha kwa amani na
kuzishinda
changamoto
hizi
mnazokumbana nazo.David zumo ni mtu
ambae
ni
maarufu
sana
duniani.Nilimfahamu kutokana na
umaarufu wake huo.Anajulikana dunia
nzima kwa namna alivyoweza kuibadili
nchi ya Congo na sikuwai kuwa na ndoto
ya siku moja kukutana na mtu mkubwa
kama
huyu”.akanyamaza
halafu
akaendelea
“Ninamiliki kampuni ya mavazi
na vile vile ninayo taasisi yangu ambayo
inajishughulisha na kutoa msaada kwa
watu wenye uhitaji hususani wazee
wasiojiweza na watoto.Mwaka huu mimi
na taasisi yangu tuliazimia kuanzisha
mradi mkubwa wa kujenga shule kubwa
ya watoto wenye ulemavu wa kutokuona
na kusikia,ili kupata fedha za
kutuwezesha kuanza ujenzi wa shule hiyo
ilitulazimu tuandae mambo Kadhaa
ikiwemo kuandaa mbio za nusu
marathon.Wakati wa mbio hizo ndipo
nilipokutana na Jean pierre Muyeye
ambaye alitumwa kumuwakilisha David
na akanipa ujumbe aliopewa ulionitaka
nikaonane na David kwani kuna msaada
anahitaji kuutoa.Nilionana na David
akanipa mchango wake mkubwa na
akaniomba siku inayofuata akutane na
wazazi wangu.Nilimkutanisha na wazazi
wangu na tukiwa katikati ya maongezi
nilipata taarifa kuwa rafiki yangu mmoja
alipatwa na matatizo ikatulazimu mimi na
mama kuondoka tukamuacha baba na
David
wakiendelea
na
maongezi.Niliporejea nyumbani baba
akanielezea alichokiongea na David
Zumo.Zilikua ni taarifa zilizonistua sana
na sikuwa na jibu la kuwapa.Wakati bado
nikiwa katika tafakari juu ya suala hilo
David akanipigia simu na kuniambia nije
Congo kwenye kongamano la vijana.kwa
hiyo Pauline mpaka sasa bado sijafanya
maamuzi yoyte kuhusiana na ombi la
David .Nadhani nahitaji muda zaidi
kulitafakari suala hili.Si suala ambalo
ninaweza kulitolea maamuzi ya haraka”
akasema Monica.
“ Nimekuelewa Monica .Hata mimi
kama ningekuwa katika nafasi yako
ningekuwa na woga kama uliokupata.Ni
jambo la kustusha Monica kwa mtu
kuibuka na kutangaza kutaka kukuoa na
hasa mtu mwenyewe akiwa mkubwa kama
David.Nafahamu kila mtu ana malengo
yake katika maisha na kila mtu ana aina
ya mtu anaye muhitaji kama mwenzi wake
kwa hiyo naamini kabisa yawezekana
labda David akawa si mwanaume wa aina
ile ambayo unaitaka lakini ninataka
kukuhakikishia kwamba japokuwa ni
 
SEHEMU YA 27


muda mfupi sana mmeonana na
kufahamiana lakini tayari amekwisha
kupenda na ninamfahamu David akipenda
huwa amependa kweli.Ninakuthibitishia
hilo kwa namna anavyonipenda na
kunifanya nijione niko juu ya wanawake
wengine wote wa dunia.David hapendi
kumuumiza mwanamke na katika kipindi
chote ambacho nimeishi naye hajawah
kunitoa chozi hata mara moja.Ni mtu
anayejali,anasikiliza na akikupenda
chochote ukitakacho utakipata.NI
mwanaume ambaye nikiamua kukueleza
sifa zake naweza kutumia siku nzima.Kwa
kifupi ni mwanaume ambaye kila
mwanamke anaota kumpata.Wanaume wa
aina hii ni wachache sana kupatikana
katika dunia ya sasa.” Pauline akanyamaza
wakatazamana kisha Monica akauliza
“ Kwa nini unaniambia haya yote
Paulie?
“ Ni kwa sababu hauko tayari
kulikubali ombi la David na ndiyo maana
nimeamua kukuambia hata yale mambo
ya ndani ya kumuhusu David ili ufahamu
kwamba hana nia mbaya nawe ,ni mtu
mwema na lengo lake au lengo letu kwako
ni jema sana.Nadhani mimi ninaweza
kuwa mwanamke wa kwanza katika hii
dunia ya sasa kumshawishi mwanamke
mwenzangu akubali kuolewa na mume
wangu.Jambo kama hili ni nadra mno
kutokea katika zama hizi lakini mimi
ninalifanya tena kwa moyo mweupe
kabisa.Monica nakuomba kubali kuolewa
na David .Mimi sina tatizo lolote na suala
hili na niko radhi David awe na mke wa
pili .Nataka umzalie David watoto ambao
watakuwa ni watoto wetu na ndio
watakaokuwa warithi wa utajiri
wetu.Tutakuwa na familia yenye furaha na
upendo mkubwa.Nakuhakikishia kwamba
hautajutia uamuzi wako kama utakubali
kuolewa na David.Utaishi maisha mazuri
na utakuwa kweli malkia wa Afrika .Dunia
nzima
itakufahamu
na
kukuheshimu.David atakufanya mwenye
furaha ,sote tutakuwa na furaha.Maisha
yetu yatakuwa ya furaha kubwa.Monica
naamini unanishangaa sana kwa
msisistizo huu lakini ninafanya hivi kwa
sababu ya furaha ya mwanaume
ninayempenda.Furaha ya David ni yangu
pia na ni wewe pekee ambaye unaweza
ukaifanya furaha ya David ikakamilika
kwa kukubali ombi lake .Nakuhakikishia
Monica mimi binafsi nitakuwa mstari wa
mbele kuhakikisha kuwa unaishi maisha
mazuri na ya furaha.Narudia tena
kukuomba Monica tafadhali kubali ombi la
David”
akasema
Pauline.Monica
akainamisha kichwa na kutafakari
.Ukimya ukatanda.Baada ya kama dakika
tatu Monica akasema
“ Pauline umeniweka katika nafasi
ngumu.Huu ni mtihani mgu....” Akasema
Monica lakini Pauline akamzuia
asiendelee
“ Monica huu si mtihani.Yaamini
maneno yangu na hautajutia maamuzi
yako” akasema Pauline,Monica akabaki
kimya
“ Usiku wa leo” Pauline akaendelea
“ Utakutana na David Zumo .Katika
usiku wa leo atautumia kukueleza wazi
yeye mwenyewe kuhusu jambo
hili.Tafadhali
Monica
naomba
atakapokutamkia kwamba anataka
kukuoa sema ndiyo.Utauvunja moyo
wake,na wangu pia kama ukisema
hapana.Usiku wa leo ni muhimu mno
kwako kwani ndiyo utakaoamua aina ya
maisha unayotaka kuishi.Maisha yako
yanaweza kubadilika kuanzia usiku wa leo
kwa hiyo ulimi wako utafanya kazi kubwa
ya maamuzi kwa kutaamka neno ndiyo au
hapana.Siwezi kukulazimisha ukubali
japo nimejitahidi sana kukushawishi
ukubali ombi la David kwa hiyo wewe
ndiye mwenye maamuzi ya mwisho.Kwa
sasa naomba tuachane na suala hilo na
tuendelee na mamo mengine.” Akasema
Pauline na kuagiza waletewe chakula
wakaendelea na maongezi mengine.
 
SEHEMU YA 28


DAR ES SALAAM – TANZANIA
Saa tano na dakika kumi,simu ya
Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania ikaita.Alikuwa
balozi wa China Jing wang Zhu.Hii ni simu
ambayo Ernest alikuwa anaisubiri sana
hivyo akaipokea haraka haraka
“ Hallow Balozi.” Akasema Enest
“ Mheshimiwa rais nimekupigia
kukutaarifu kwamba makabidhiano yetu
yamekwenda vizuri.Wafungwa raia wa
China wamekabidhiwa kwangu saa tano
kamili juu ya alama wakiwa na afya njema
kabisa.Katika muda huo h uo mfungwa
Linda January raia wa Tanzania aliyekuwa
amefungwa nchini China amekabidhiwa
kwa ubalozi wa Tanzania nchini
China.Unaweza kuwasiliana na balozi wa
Tanzania China kwa uhakika
zaidi.Hongera mheshimiwa rais kwa
kulifanikisha jambo hilo “ akasema Jing
wang
“ Ahsante sana mheshimiwa balozi
kwa kulifanikisha suala hili.Nifikishie
shukrani zangu nyingi kwa rais wa China”
akasema Ernest akaagana na balozi
.Alipokata simu haraka haraka akazitafuta
namba za balozi wa Tazania nchini China
akampigia.
“ habari yako mheshimiwa balozi “
akasema Ernest baada ya Edger Chuswa
balozi wa Tanzania nchini China kupokea
simu.
“ Habari nzuri mheshimiwa
rais.Nilikuwa katika harakati za kutaka
kukupigia simu na kukupa taarifa za suala
lile ulilonieleza.Yule msichana tayari
amekabidhiwa hapa ubalozini ,akiwa na
afya njema.Nitamuhifadhi nyumbani
kwangu wakati nikisubiri maelekezo toka
kwako mheshimiwa rais” akasema balozi
Edger
“ Ahsante Edger.Nitakupa maelekezo
nini cha kufanya .Kitu pekee
ninachopenda kukukumbusha ni kwamba
suala hili halipaswi kusambaa kwani ni
suala la siri kubwa.”
“ Nalifahamu hilo mheshimiwa rais
nakuomba usihofu kabisa”
“ Ahsante Edger ,naomba umpe
uangalizi wa hali ya juu sana huyo
msichana .Baadae mida ya saa tatu usiku
kwa saa za afrika mashariki ambayo
itakuwa ni saa nane usiku kwa saa za
China nitakupigia nitataka kuongea na
Linda.”
“ Sawa mheshimiwa rais,nitajitahidi
kuhakikisha anakuwa macho mida hiyo ili
uweze kuzungumza naye”
“ Ahsante sana balozi ,tutawasiliana
hapo baadae” akasema Ernest na kukata
simu
“ Nimelazimika kutumia madaraka
yangu kama rais kuweza kulifanikisha
ombi la Austin.Hili ni suala zito na
linaweza kuniletea matatizo likijulikana
kwani ni kinyume na sheria za nchi na
nimetumia vibaya ofisi yangu lakini
sikuwa na nama nyingine ya kufanya
.Nahitaji Austin anifanyie kazi yangu na
asingeweza kuifanya bila ya sharti lake
hilo kutimizwa.Hakukuwa na namna
nyingine ya kuweza kumtoa Linda
gerezani bila kubadilishana wafungwa.”
Akawaza Ernest.
 
SEHEMU YA 29


aa saba za mchana Daniel aliwasili
hospitali kwa ajili ya kumjulia hali Dr
Marcelo.Alishuka garini na kutembea
taratibu kuingia katika wodi alikolazwa
Marcelo.Kichwa alikiinamisha chini
ilionyesha wazi alisongwa na mawazo.
“ Sijui nitamjibu nini Marcelo endapo
ataniuliza kuhusu Monica.” akawaza
Daniel
“ Ni wazi Monica amekwisha nitoa
kabisa katika akili yake.Zamani kila
akitaka kusafiri iwe ndani au nje ya nchi
alikuwa ananijulisha lakini kwa sasa hana
habari tena na mimi.Nini kimetokea na
kumbadilisha Monica namna hii?Lakini
haya yote yameanza ghafla tu baada ya Dr
Marcelo kutokea.Anyway ngoja niachane
na mawazo haya” akawaza wakati
amekaribia
wodi
alimolazwa
Marcelo.Ndani ya wodi walikuwemo watu
kadhaa waliokuja kumjulia hali Marcelo
na kwa kuwa chumba hakikuwa kikubwa
sana iliwalazimu wengine kukaa nje
kusubiri zamu yao ifike.Wakati akiwa nje
akisubiri kuingia,akatokea Julieth dada wa
Marcelo,wakasalimiana
“ Nimefurahi umefika Daniel.Marcelo
aliniuliza kama umekuja nikamjibu bado”
akasema Julieth
“ Nimefika muda si mrefu “ akajibu
Daniel
“ Where is Monica? Sijamuona jana
na hata leo.Si kawaida yake kutoonekana
hapa hospitali toka Marcelo alipopata
matatizo”
“ Monica amepata safari ya dharura
lakini kesho atarejea” akasema Daniel na
mara watu waliokuwa ndani ya chumba
wakatoka Daniel hakutaka tena maongezi
na Julieth akaingia ndani.Bado Marcelo
alikuwa anawasiliana kwa ishara na
hakuwa ameweza kuzungumza.
“ Monica yuko wapi? Marcelo
akauliza kwa njia ya maandishi
“ Monica amepata dharura na
ametoka nje ya Dar es salaam lakini muda
si mrefu atarejea” Daniel akamjibu kwa
maandishi
“ Call and tell her to hurry”
“ Sawa nitamueleza” akajibu akajibu
Daniel kwa maandishi na kutoka mle
chumbani
“ Kuna kitu gani kati ya Monica na
Marcelo?Toka jana Marcelo amekuwa
ananisisitiza kuhusu Monica.Nadhani
hakuna tena ulazima wa mimi kuja hapa
tena kama Monica hayupo.Sitaki
kuendelea kudanganya kila siku.Kingine
kinachoniumiza zaidi ni kwamba Marcelo
ameharibu mahusiano yangu na
Monica.Nadhani itakuwa vyema nikiweka
pembeni niwaache waendelee.” Akawaza
Monic
 
SEHEMU YA 30


KINSHASA – JAMHURI YA KIDEMOKRASIA
YA CONGO
Tayari ni saa moja kasorobo za jioni
jijini Kinshasa.Kwa zaidi ya saa moja sasa
Monica alikuwa katika saluni iliyokuwamo
ndani ya jumba anamoishi na akina dada
wapatao wanne wakifanya kazi ya
kumremba kwa ajili ya usiku a kipekee
ambao angekutana na David Zumo.Wakati
akiendelea kurembwa bado mambo
aliyozungumza na Pauline mchana
yaliendelea kumjia kichwani.Bado
aliendelea kuisikia sauti ya Pauline
masikioni mwake ikimtaka akubali ombi
la David Zumo.Kwa siku nzima jambo hili
lilimuumiza sana kichwa.
Baada ya kurembwa akarejea
chumbani kwake kujiandaa na alipoingia
chumbani akakuta kuna gauzi zuri sana
limewekwa kitandani pamoja na vito vya
thamani kwa ajili ya kuvaa usiku
ule.Akatabasamu
“ maisha haya ni mazuri mno.Unaishi
kama malkia,unahudumiwa kwa kila
kitu.Nimeanza kuyapenda maisha haya na
endapo usiku wa leo nitamkubalia David
Zumo ombi lake basi haya yatakuwa ndiyo
maisha yangu ya kawaida.Hata hivyo bado
moyo wangu haujafanya maamuzi kama
nikubali au nikatae kuolewa na David
Zumo .Natamani niombe ushauri kwa mtu
lakini suala hili linahusu maisha yangu na
siwezi kutegemea mtu anishauri.Wazazi
wao tayari wamekwisha amua wanataka
nikubali” akakaa kitandani na kukumbuka
kitu
“ Ngoja nimpigie Daniel nimuulize
maendeleo ya Marcelo.Sijui atakuwa
katika hali gani hivi sasa.Naomba Mungu
aendelee kumlinda hadi hapo
nitakaporejea ili nitafute namna ya
kumsaidia.” Akawaza Monica huku
akiziandika namba za Daniel katika simu
akapiga.Baada ya muda Daniel akapokea.
“ hallow “ akasema
“ Hallow Daniel its me Monica”
“ Monica,nafurahi kuisikia tena sauti
yako.Lini unarudi?
“ Nitarudi muda wowote
Daniel.Nimekupigia kufahamu hali ya Dr
Marcelo,anaendeleaje?
“ Anaendelea vizuri .Nilikwenda
kumtazama mchana wa leo.Bado hajaanza
kuzungumza ila amenipa tena ujumbe
nikufikishie
anasema
ufanye
haraka.Hakutoa maelezo mengine zaidi ya
hayo.Monica jitahidi umletee kitu
anachokihitaji kwani nimechoka
kumdanganya kila siku.Kama itakuchukua
muda mrefu kurejea itakuwa vyema
endapo tutamueleza ukweli kwamba
haupo nchini ili awe akifahamu” akasema
Daniel
“ Daniel please naomba usimueleze
chochote kama niko nje ya nchi.Usiache
kwenda kumtembelea na tafuta namna ya
kuendelea kumdanganya .Leo namalizia
mambo
yangu
na
kesho
nitarejea.Tafadhali Daniel nakuomba
fanya hivyo” akaomba Monica .Baada ya
sekunde chache Daniel akajibu
Sawa Monica nitafaya hivyo lakini
usichelewe sana kurudi tafadhali’
akasema Daniel
“ Ahsante Daniel.Nitakupigia tena
asubuhi.” Akasema Monica na kukata
simu,akavuta pumzi ndefu.
“ What am I going to do to help him?
Akajiuliza na kuinamisha kichwa
 
SEHEMU YA 31


Kesho lazima nirejee Dar es
salaam.Marcelo
needs
my
help.Nisipomsaidia kwa haraka kama
alivyoomba anaweza akauawa.” Akawaza
Monica na kuinuka akaanza kuvaa
Alimaliza kuvaa na kujitazama
katika kioo akatabasamu
“ Sipendi kujisifu lakini mimi ni
mzuri.Naamini usiku huu David Zumo
atapag.....” Monica akastuliwa toka
mawazoni
na
kengele
ya
mlangoni.Akaenda kuufungua akakutana
na mfanyakazi wa mle ndani akiwa na
mwanamke mmoja mwenye umbo kubwa
“ Mama Monica huyu ni mbunifu wa
mavazi anaitwa Sheris.Alitakiwa kuwasili
hapa kitambo lakini alipata tatizo njiani
ndiyo maana amechelewa”
“ Hallow Sheris” Monica akamsalimu
Yule mwanamama.
“ Hallow Monica.Nimefurahi sana
kukuona.Nilitakiwa kufika hapa muda
mrefu uliopita lakini niliharibikiwa na
gari njiani.Nimepewa kazi ya kukuvalisha
kwa usiku wa leo” akasema Sheris na
kuingia chumbani akaanza kumkagua
Monica kuanzia juu hadi chini akamfanyia
marekebisho kadhaa
“ Sasa uko tayari kukutana na
mtukufu rais usiku wa leo” akasema
Sheris baada ya kumaliza kumfanyia
Monica marekebisho
Saa mbili kamili juu ya alama
kengele ya mlangoni ikalia,Monica
akaufungua na kujikuta anatabasamu
“ Pierre Muyeye” akasema kwa
furaha
“ Monica” akasema Muyeye
wakasalimiana
“ Monica umependeza sana kweli
wewe ni malkia wa Afrka” akasema
Muyeye na wopte wakacheka
“ nadhani uko tayari”
“ Niko tayari Muyeye” akasema
Monica kisha Muyeye akamuongoza
kushuka chini hadi katika gari zuri la
kifahari akafunguliwa mlango akaingia na
msafara wa magari zaidi ya kumi uliokuja
kumchukua ukaondoka ukitanguliwa na
piki piki za polisi.Magari yote katika
barabara ulikopita msafara yakawekwa
pembeni kuupisha msafara wa Monica
upite.Monica hakutaka kuonyesha furaha
yake usoni lakini moyoni alifurahi kupita
maelezo.Hakuwahi kuota kama siku moja
atapewa heshima kubwa namna ile kiasi
cha magari barabarani kuwekwa pembeni
kumruhusu apite.
 
SEHEMU YA 32

DAR ES SALAAM - TANZANIA
Inakariabia saa mbili na nusu jijini
Dar es salaam rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Ernest mkasa
yupo katika chumba chake maalum ndani
ya hoteli hii anayoimiliki .
“Mukasha nadhani ni muda
muafaka sasa wa kwenda kuonana na
Austine”Ernest akamweleza Mukasha
aliyekuwa naye mle chumbani
wakijadiliana mambo kadhaa,akainuka na
kurejea katika chumba cha kulala na kama
alivyofanya siku iliyotangulia akabadili
muonekano wake.akajitazama na
kutabasamu.
“ Austin amenifanya nikumbuke
mbali sana enzi za ujana wangu.Nimepitia
mambo mengi sana na siamini eti leo hii
mimi ni rais a jamhuri ya muungano wa
Tanzania.Kweli maisha yana maajabu
.Najikubali kwa historia ya maisha yangu
sikuwa na vigezo vya kuniwezesha
kushika nafasi kubwa na nyeti kama hii
.I’m a monster,lakini tazama nilipo
sasa,niko katika ofisi kubwa kuliko zote
nchini.Kweli hakuna kisichowezekana
chini ya jua” akawaza Ernest na kutoka
mle chumbani na kama ilivyokuwa usiku
uliopita akaongozana na Mukasha na
Evans mlinzi wake wakazunguka upande
wa nyuma ambako kuna njia ya siri ya
kupita wakaingia katika magari na
kuondoka.
Waliwasili katika nyumba anayoishi
Austin.Evans akashuka na kubonyeza
kengele ya getini baada ya dakika tatu geti
likafunguliwa na gari zile mbili zikaingia
ndani.Rais akafunguliwa mlango akashuka
“ Hallow Austine” akasema Ernest
“ Karibu sana mheshimiwa rais”
akasema Austin na kugeuka akaanza
kupiga hatua kuelekea ndani.Mukasha
,Evans na wale walinzi wengine wawili
wakaambatana
nao.Mara
Austin
akageuka.
“ Namuhitaji rais peke yake humu
ndani.Wengine mtasubiri nje”
“ Hilo halitawezekana kaka.Huyu ni
rais wa nchi na jukumu letu ni kumlinda
katika sehemu anayokwenda .Hatuwezi
kumuacha peke yake hata sekunde moja.”
Akasema Evans.Austin akamuelekezea
macho Ernest
“ You want to talk to me ? Waambie
watu wako wabaki nje “ Austin
akamwambia Ernets ambaye aliwataka
walinzi wabaki nje akaingia ndani na
Austin
“ Karibu mheshimiwa rais” akasema
Austin na kumkaribisha rais sofani
“ Ahsante Austin lakini hukupaswa
kufanya vile,wale ni walinzi wangu
walioapa kuyatoa maisha yao kunilinda
,wanastahili heshima”
“ I’m sorry mr President ,that’s how I
work.I don’t trust people so easily.Ukitaka
kufanya kazi na mimi lazima ukubali tabia
zangu”
“ Sawa hakuna tatizo.Umeshindaje
leo?
 
Back
Top Bottom