SEHEMU YA 84
Tanzania.Mimi ni miongoni mwa watu hao
kumi”
“ Oh my God !! akasema Ernest kwa
mshangao
“ Ernest naomba usiongee chochote
kwanza hadi nitakapomaliza.Naomba
uendelee kunisikiliza.” Akasema Agatha
“ Mimi na wenzangu tuliochaguliwa
,tumekula kiapo mbele ya mkuu Alberto
wa tatu kuhakikisha kuwa tunafanya kila
tuwezalo kuondoa vizingiti vyote
vinavyofanya Alberto’s washindwe
kupenya na kufanya kazi zao nchini
Tanzania.Tumepewa nguvu ya kufanya
mambo ambayo binadamu wengine
hawawezi kuyafanya.Nimekuwa mtu mpya
.Nimeweka agano mbele ya Alberto mkuu
la kuwa mtiifu na kufuata maelekezo yote
anayoyatoa.Kwa hiyo basi tumepewa kazi
kubwa ya kufanya na kazi ya kwanza
ambayo tunatakiwa kuifanya ni
kutengeneza serikali.Tunataka rais
,makamu wa rais ,waziri mkuu na
mawaziri wote wawe ni Alberto’s
.Tukilifanikisha hilo basi tutakuwa
tumeotesha mzizi na Tanzania
itabadilika.Tunataka Tanzania mpya.”
Agatha akanyamaza akamtazama
mumewe ambaye uso wake ulijikunja
kqwa hasira .Agatha hakujali akaendelea
“ Ernest nafahamu jambo hili
limekustua sana lakini ni suala ambalo
lina manufaa makubwa si kwetu pekee
bali kwa nchi na dunia kwa hiyo nakusihi
usikasirike mpendwa wangu kwani kuna
jambo kubwa umeandaliwa na ambalo
hukuwa umelitarajia kabisa” akanyamza
kidogo akaendelea
“ Baada ya kupewa jukumu la
kuhakikisha tunaandaa serikali ambayo
itakuwa
chini
ya
Alberto’s,nimekupendekeza wewe uwe
rais mpya wa Tanzania.”
“ Nini ?? Akauliza Ernest kwa
mshangao
“ Nimekupendekeza uwe rais wa
Tanzania.Utaongoza serikali itakayokuwa
chini yetu.Wew................”
“ Stop Agatha!!!..stop!!...!! akasema
Ernest kwa hasira
“ Wewe na hao mashetani wenzako
ni mataahira.Agatha kitu gani umekosa
hadi ukaingia katika mambo haya ya
kishetani? Please Agatha toka huko
ulikoingia haraka sana.I need back my old
Agatha,the one I married and not you!!
Akasema Ernest kwa ukali
“ Ernest I’m still the same Agatha,
your one and only wife.From now you are
going to listen to me and do whatever I tell
you to do.You here me? Akasema Agatha
kwa ukali
“ Mimi ndiye mwenye amri ya
mwisho ndani ya nyumba hii na
utanisikiliza mimi pekee.Nataka uchukue
simu na uwapigie hao mashetani wenzako
uwaambie kwamba hutashiriki tena
katika mambo yao ya kishetani na baada
ya hapo hautaruhisiwa tena kutoka nje ya
nyumba hii.Umenisikia Agatha? Akasema
Ernest huku mwili ukimtetemeka kwa
hasira
“ Una dakika mbili za kuchukua simu
na kuwapigia hao wenzako ama sivyo
uchukue kila kilicho chako na uondoke
katika nyumba hii.Nadhani umenielewa
vizuri na wala sitishwi na huo uchawi
wako .Nitahakikisha kila mtu anafahamu
ni mambo gani wewe na hao mashatani
wenzako mnayafanya.” Akasema Ernest