SEASON 6: SEHEMU YA 2
Vishindo viwili vikubwa
vililitikisa jiji la Dar na kuzua
taharuki kubwa kwa wakazi
wake ambao kwa muda huu wa
jioni wengi walikuwa katika
harakati za kurejea majumbani
kwao baada ya pilika pilika za
kutwa nzima.Moshi mkubwa
mweusi pamoja na vumbi kubwa
vilitanda eneo ulikotokea
mlipuko ule na hivyo kuwafanya
watu wawe na shauku ya
kutaka kufahamu nini
kimetokea .Zilipita dakika tano
baada ya mlipuko kutokea
ving’ora vya magari ya magari ya
polisi na zimamoto vikasikika na
kwa kasi kubwa wakielekea
sehemu ulikotokea mlipuko ule
mkubwa.Bado moshi mzito
uliendelea kutanda eneo
lile.Wananchi walizuiliwa
kulikaribia eneo lile kwa ajili ya
usalama wao.Vikosi viliwekwa
mbali kidogo na eneo lile huku
jitihada za kuuzima moto
ulioendelea kuwaka na kutafuta
manusura zikiendelea.
Wakati jiji la dar likiwa
katika taharuki ile kubwa taarifa
nyingine zikasikika kwamba
jengo la bunge mjini Dodoma
nalo pia limelipuliwa na
hakukuwa na taarifa za awali
zilidai kwamba hakukuwa na
mtu hata mmoja aliyekuwamo
ndani ya jengo lile aliyetoka
hai.Taharuki kubwa ikatanda
nchini.Vyombo vyote vya ulinzi
na usalama vikawekwa katika
tahadhari kubwa .Ofisi na
majengo yote ya umma na
sehemu zile zenye kubeba
mikusanyiko mikubwa ya watu
yakaongezewa ulinzi mkubwa.
Dunia nzima ikaelekeza macho
yake Tanzania na kulaani vikali
mashambulio mawili makubwa
yaliyopelekea vifo vya watu
wengi hasa viongozi .
Hadi ilipofika saa mbili za
usiku bado hakukuwa na taarifa
yoyote iliyotolewa kwa umma
kuhusiana na tukio lile.Vyombo
vya usalama viliwahimiza
wananchi wajitahidi kuwa
watulivu na watapewa taarifa
baadae kuhusiana na tukio
lile.Wananchi waliendelea
kuaswa kuchukua tahadhari
kuepuka mikusanyiko mikubwa
na yeyote mwenye taarifa zozote
zinazoweza kusaidia alitakiwa
kuziwasilisha katika vyombo vya
usalama ili zifanyiwe kazi..
Viongozi wengi wa dunia
waliendelea kumtumia rais wa
Tanzania salamu za rambi rambi
na pole kwa wananchi wa
Tanzania kufuatia
mashambulio yale makubwa
.Wakati dunia nzima ikilaani
mashambulio yale,video
iliyomuonyesha kiongozi mkuu
wa Alshabaab Habib Alzaraq
ilirushwa na kituo kimoja
kikubwa cha runinga kilichopo
huko nchi za kiarabu.katika
video hiyo habib alikiri
Alshabaab kuhusika katika
mashambulio yale mawili
yaliyotokea nchini Tanzania .
“Naitwa Habib
Alzaraq,kiongozi mkuu wa
Alshabaab” ndivyo alivyoanza
katika video hiyo
“Dunia nzima imeelekeza
macho yake nchini Tanzania
kufuatia mashambulio mawili
yaliyotokea jioni ya leo nchini
humo.Nachukua nafasi hii
kuitaarifu dunia kwamba
Alshabaab ndio tuliotelekeza
mashambulio hayo mawili
.Huu ni mwanzo tu wa vita
yetu na Tanzania na
tutaendelea kuishambulia
kila mara hadi pale serikali
ya Tanzania itakapoondoa
wanajeshi wake walioko
katika ardhi ya Somalia
wakilifundisha jeshi la
Somalia .Tumekwisha ionya
mara nyingi serikali ya
Tanzania kuhusiana na
kuwaondoa wanajeshi wake
walioko nchini Somalia
wanaosaidia kulijenga upya
jeshi la Somalia kwa kuwapa
mafunzo lakini wamepuuza
na sasa tumeamua kutumia
nguvu ili kuwashinikiza
kuwaondoa wanajeshi wake
katika ardhi yetu.
Tunatoa nafasi nyingine
kwa seriali ya Tanzania
kuwaondoa haraka sana
wanajeshi wake walioko
nchini Somalia kama
wanataka damu isiendelee
kumwagika.Bila kufanya
hivyo tutaendelea kumwaga
damu ya watanzania kila
uchao hadi pale serikali ya
Tanzania itakapoondoa
wanajeshi wake katika ardhi
yetu.
Kilichotokea leo Tanzania
ni fundisho kwa mataifa
mengine kwamba mzozo wa
Somalia si wa kuingiliwa .Hii
ni vita yetu na mtuachie
wenyewe.Hatutaki taifa lolote
katika ardhi yetu kwa
kisingizio cha kusuluhisha
mgogoro wa Somalia.Yeyote
atakayekanyaga ardhi ya
Somalia na kuisaidia serikali
iliyopo madarakani
tutamuhesabu ni adui yetu na
tutapambana naye bila kujali
ukubwa wala nguvu
zake.Mwisho narudia tena
kuitaka serikali ya Tanzania
na wale wote wenye majeshi
yao Somalia kuyaondoa mara
moja kabla ya damu nyingi
zaidi kumwagika katika nchi
zao”
Ndivyo alivyomaliza Habib
Alzaraq kiongozi mkuu wa
Alshabaab .
SEASON 6: SEHEMU YA 3
Taarifa za mashambulio yale
mawili yaliyotokea dar es salaam
na Dodoma ziliwastua na
kuwachanganya sana Austin na
wenzake.Walisimamisha kazi
zote wakakaa sebuleni
wakifuatilia matangazo ya moja
kwa moja katika runinga
kuhusiana na tukio lile la
kustusha sana.
“ Najaribu kutakakari
kuhusiana na matukio haya
mawili.Ukitazama m uda
yaliyotokea unakaribiana sana
na hii inanipa picha kwamba
yawezekana mshambuliaji
anaweza kuwa mmoja.Dah ! hili
ni shambulio kubwa sana
ambalo halijawahi kutokea
katika historia ya Tanzania na
afrika mashariki kwa ujumla.”
Akasema Austin
Wakati wakiendelea kujadili
juu ya tukio lile mara wakapata
taarifa kuwa katika kituo kimoja
cha runinga cha nje ya nchi
kulionyeshwa video ya kamanda
mkuu wa Alshabaab akijtapa
kuhusika katika mashambulio
yale.Kwa kutumia simu yake ya
mkononi Amarach akaitafuta
video ile na kusikia kile
alichokisema Habib.
“Alshabaab !!! akasema
Austin kwa mshangao
“ Alshabaab ndio
waliohusika na mashambulio
haya? Akazidi kushangaa
“Mbona umestuka Austin
kusikia ni Alshabaa ndio
waliofanya shambulio hili?
Akauliza Job
“ Hainiingii akilini job.Kwa
nini iwe sasa ? Kwa nini
washambulie leo? Vikosi vya
wanajeshi wa Tanzania walioko
nchini Somalia kwa ajili ya
kulifundisha jeshi la Somalia
vina wanajeshi wasiozidi
hamsini na wako nchini Somalia
kwa miaka kadhaa sasa kwa
nini kwa muda huo wote
wasishambulie Tanzania hadi
leo hii? Kingine kinachonifanya
niwe na mashaka ni kwamba
nchi zilizojitolea kujenga upya
jeshi la Somalia si Tanzania
pekee bali kuna Afrika
kusini,Angola na Misri lakini
kwa nini wachague kushambulia
Tanzania pekee? Ndugu zangu
hili jambo linanipa ugumu
kidogo.” Akasema Austin na
kuitazama tena video ile ya
Habib
“ Kwa mujibu wa maelezo ya
huyu anayejiita Habib Alzaraq
kiongozi wa Alshabaab
yawezekana wameamua kuanza
na Tanzania ili kuzifanya nchi
nyingine zenye majeshi yake
nchini Somalia kuyaondoa
kabla nazo hazijashambuliwa.”
Akasema Amarachi
“ Mawazo yako yanaweza
kuwa sahihi Amarachi lakini
kwa upande wangu bado akili
yangu inakataa kabisa
kukubaliana na hiki
walichokifanya
Alshabaab.Wanajeshi wa
Tanzania walioko Somalia ni
wachache sana ukilinganisha na
ukubwa wa mashambulio
waliyoyafanya.Kikosi cha
wanajeshi wasiozisdi hamsini
hakiwezi kusababisha ukalipua
hoteli ile yenye watu wengi
wakiwamo wageni toka mataifa
mbali mbali na kama haitoshi
kulipua pia ukumbi wa bunge
na kwa mujibu wa taarifa za
awali hakuna mbunge ambaye
anasemekana kutoka hai.Hata
hivyo tusubiri taarifa kamili
itakapotolewa kuhusiana na
mashambulio haya na hapo
tutapata mwanga zaidi”
akasema Austin na kuendelea
kutazama matukio katika
runinga ambapo juhudi za
kuuzima moto na kuwatafuta
manusura wa mashambulio yale
mawili ya Dar es salaama na
Dodoma zilikuwa zinaendelea.
“Hawa jamaa wameitikisa
nchi na hiki walichokifanya ni
uchokozi na wanastahili
kuadhibiwa vikali sana.”
Akasema Job.
“ Kuna kitu kinanijia akilini
lakini sina hakika kama
kinaweza kuwa na mahusiano
na hiki kilichotokea leo.Yasmin
aliniambia kwamba rais alifanya
makubaliano na Alshabaab na
moja kati ya makubaliano yao ni
yeye kuachiwa huru.Nini hasa
kilichopelekea rais afanye
makubaliano na Alshabaab hadi
akaamua kumuachia huru mtu
hatari kama Yasmin. Rais wa
nchi unawezaje kuwa na
mawasiliano au hata kufanya
makubaliano na magaidi? Au
walibadilishana wafungwa na
ndiyo maana akamuachia
Yasmin?.”akajiuliza
“Austin !! akaita Amarachi
na kumtoa Austin katika
mawazo mengi
“ Tunaendelea na jambo
gani kwa sasa? Baada ya tuko
hili naona kila kitu
kimesimama.Are we going to
watch this all night? Akauliza
Amarachi
“ We have lots to do lakini
hiki kilichotokea kwa kweli
kimestua kila mtu.Kuna
wabunge zaidi ya mia tatu na
themanini ndani ya bunge lile
na hatujui ni wangapi walikuwa
ndani ya ukumbi wa bunge leo
jioni wakati shambulio hilo
likitokea nina amini ni zaidi ya
mia tatu.Hatujui ni wageni
wangapi waliokuwamo ndani ya
hoteli ile wakati inalipuliwa.Huu
ni msiba mkubwa sana kwa
taifa na maisha ya watu wengi
yamekatishwa kikatili.Hata
hivyo tunaweza kuendelea na
majukumu yetu huku
tukifuatilia kwa karibu
kinachojiri.Kilichokuwa mezani
kilikuwa ni majibu ya kipimo
cha vinasaba ambayo tayari
tunayo mkononi.Rais alidai
kwamba asionyeshwe mtu
mwingine majibu hao isipokuwa
yeye pekee lakini kwa hili
lililotokea leo sina hakika kama
atakuwa na nafasi hata ya
kufuatilia suala hili.Mimi
ushauri wangu tufungue
bahasha hii na tuangalie
kilichomo ndani.Marcelo ni
daktari na atatuambia
kilichoandikwa humu kwani
lugha ya kitabibu huwa ngumu
kidogo kuielewa” Akasema
Austin na kuichukua bahasha
ile yenye majibu ya vipimo vya
vinasaba na kuifungua kisha
akampa Marcelo akaanza
kuipitia.Wakati Marcelo akiipitia
barua ile kukatokea habari
mchepuko katika runinga.
“Habari za wakati huu
watazamani wetu.Tunaendelea
kuwaleteeni habari mbali
kuhusiana na mashambulio ya
bomu katika hoteli jijini dar es
salaam na Dodoma katika jengo
la bunge,mashambulio
yaliyosababisha vifo vya watu
wengi ambao mpaka sasa bado
haijajulikana idadi kamili ya
vifo.Wakati vikosi vya u okoaji
vikiendelea na juhudi za
kuwatafuta manusura wa
mashambulio hayo ,kuna taarifa
zinazoendelea kusambaa katika
mtandao ya kijamii kwamba rais
wa Tanzania ni miongoni mwa
watu waliokuwamo katika hoteli
iliyoshambuliwa na magaidi
lakini taarifa tuliyoipata hivi
punde kutoka kwa waandishi
wetu walioko katika eneo la
tukio ni kwamba rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania ndugu Ernest Mkasa
alikuwa akienda katika hoteli
hiyo kuhudhuria shughuliya
uchangishaji fedha kwa ajili ya
mradi wa kuwawezesha akina
mama wajasiriamali ,hafla
iliyoandaliwa na mke wa
rais.Kwa mujibu wa taarifa ya
msemaji wa ikulu ni kwamba
shambulio hilo lilitokea wakati
msafara wa rais ukiwa
umebakia mita chache sana
kufika katika hoteli hiyo lakini
walinzi wa rais waliwahi
kumnusuru rais mara tu
shambulio lilipotokea na
kumuondosha eneo la tukio na
msemaji wa ikulu amethibitisha
kwamba rais ni mzima na hana
tatizo lolote .Tunawaomba
wananchi mzipuuzie taarifa
zisizo rasmi zinazoendelea
kusambaa katika mitandao ya
kijamii kuhusiana na matukio
haya.Tutaendelea kuwaleteeni
taarifa za kile kinachoendelea
kadiri tutakavyokuwa
tunazipata.”
Austihn na wenzake
wakatazamana.
“ Inawezekana Alshabaab
walikuwa wanamlenga rais?
Akauliza Amarachi
“Inavyoonekana walikuwa
na lengo hilo na walikusudia
kumuua rais kwani mlipuko
umetokea mita chache kabla ya
rais kuwasili katika jengo
hilo.Inawezekana waliwahi kabla
rais hajaingia katika hoteli hiyo
kwani wangechelewa kidogo na
kusubiri hadi rais aingie hotelini
hivi sasa tungekuwa
tunazungumza mambo
mengine.” Akasema Job
Austin aliyekuwa
ameinamisha kichwa akiwaza
akainua kichwa akamtazama
Marcelo
“ Marcelo tueleze
kilichoandikwa katika karatasi
hizo” akasema
Marcelo ambaye tayari
alikwishayapitia majibu yale
akasema
“Ndani ya report hii kuna
barua iliyoeleza kwa ufupi
kuhusiana na matokeo ya
vipimo na mwisho wa barua hii
wamesema kwamba kutokana
na uchunguzi walioufanya
asilimia 99.9999 inaonyesha
kwamba mlengwa ni baba wa
mtoto.Kwa hiyo Rasmi Monica ni
mtoto wa rais Ernest Mkasa.”
Akasema Marcelo na wote
wakawa kimya kisha Austin
akasema
“ Hizi ni taarifa nzuri kwa
rais lakini zimekuja kwa wakati
mbaya ambao anakabiliwa na
jambo zito .Kitu cha msingi kwa
sasa ni kuiweka taarifa
hiipembeni na kuendelea na
mambo mengine.Tunamsubiri
Yasmin apige simu kama
tulivyokubaliana lakini mpaka
sasa bado hajapiga.Hata hivyo
kuna jambo moja ambalo
linaniumiza mno kichwa na
ambalo nataka kuwashirikisha
na ninyi” akanyamaza kidogo
halafu akaendelea.
“ Tulikuwa wote wakati
nazungumza na Yasmin na
alisema kwamba aliachiwa huru
kutokana na makubaliano kati
ya rais na Alshabaab.Mpaka
sasa bado haijaniingia akilini
iweje rais wa nchi afanye
makubaliano na magaidi? Ni
makubaliano gani hayo hadi
akaamua kumuachia huru
Yasmin ambaye amefungwa
mahala pa siri kwa miaka zaidi
ya kumi? Sitaki kuunganisha
moja kwa moja hiki kilichotokea
leo na haya mahusiano ya rais
na Alshabaab lakini kuna hisia
zinakuja kwamba kuna jambo
limejificha hapa na endapo
kama tukimpata Yasmin
angeweza kutueleza ni kitu gani
kinachoendelea kati ya rais na
Alshabaab.Nimejiuliza labda
kulikuwa na mabadilishano ya
wafungwa lakini kama ingekuwa
hivyo vipo vyombo husika
ambavyo vingeshughulikia suala
hili lakini hapa anaonekana rais
mwenyewe ndiye
amelishughulikia jambo hili na
hadi akadiriki kutaka
kutuzunguka ili amchukue
Maria na kumkabidhi kwa
mama yake.Jamani hebu
jaribuni kupanua akili zenu na
tuliangalie hili suala kwa
mapana yake.” Akasema Austin.
“ Hata mimi ninaona kitu
Fulani katika hoja ya
Austin.Huyu Yasmin Esfahani
alikamatwa na kufungwa
mahala pa siri akiwa katika
jitihada za kukipanua kikundi
cha IS katika ukanda wa afrika
mashariki.Lazima rais
anafahamu kabisa kwamba
Yasmin ni mfuasi wa IS ambalo
ni kundi hatari kabisa la kigaidi
duniani kwa sasa lakini pamoja
na kufahamu huko bado
akaamua kumuachia
huru.Kama haitoshi akakusudia
kumuachia huru pia Maria
mtoto wa Yasmin akiwa
anafahau kabisa kwamba
tunamshikilia kwa mahojiano
baada ya kutaka kumuua
Austin.Yote hayo ameyaweka
pembeni lakini lengo lake ni
moja tu kutaka mpango wake
wa kumuachia Yasmin
ukamilike.Hapa kweli kuna
jambo ” Akasema Amarachi
“ Kwa kawaida mimi
hupenda kulitazama jambo
lolote ninalolitilia shaka kwa
mapana yake.Muda mfupi
uliopita tumetoka kutazama
habari inayosema kwamba
shambulio lilitokea wakati rais
akiwa mita chache toka hoteli
hiyo.Inawezekana labda
mlengwa wa shambulio la Dar
alikuwa ni mheshimiwa rais.Kwa
mtazamo wa kawaida unaweza
kuamini hivyo lakini mimi bado
nina mashaka.Kwanza mke wa
rais alikuwa ni mfuasi wa
Alberto’s ambao tayari rais
amewaasi na kama kungekuwa
na hafla h iyo ya kuchangisha
fedha aliyoiandaa mke wa rais
basi lazima kungekuwa na
Alberto’s wengi sehemu hiyo na
rais asingeweza kwenda kwani si
mwenzao tena na wana
uhasama mkubwa.Swali la
kujiuliza rais alikwenda
kutafuta nini katika hoteli hiyo?
Jambo lingine ni kwamba kwa
mujibu wa Yasmin,rais na hawa
jamaa waliojitangaza kuhusika
katika msahambulio yote mawili
ni watu wanaofahamiana na
wamefikia hadi hatua ya
kufanya makubaliano na
akamuachia huru mtu hatari
kwa usalama wa taifa na Afrika
mashariki ambaye ni Yasmin
Esfahani.Iweje watu hao hao
watake kumuua rafiki yao? Je
kuna makubaliano amekiuka?
Kama shambulio la dar es
salaam lilimlenga rais,lile
shambulio la Dodoma ambako
idadi kubwa ya wabunge
inasemekena wamepoteza
maisha mlengwa ni nani?
Akauliza Austin
“ Austin unanifurahisha
sana kwa namna
unavyochambua mambo na
hata mimi unanifanya nianze
kupata picha Fulani ya kile
unachokisema.Kwa mtazamo
huo ulioutoa ni wazi hapa kuna
jambo limejificha.Tukio hili
halijatokea kwa bahati mbaya
.Lazima limepangwa.Kama
ulivyosema awali kwamba kwa
nini Alshabaab washambulie
sasa wakati wanajeshi wa
Tanzania wako Somalia kwa
miaka kadhaa ? Hapa lazima
kuna sababu nyingine na si hiyo
ya kuitaka Tanzania iondoe
wanajeshi wake
Somalia.Tukifanikiwa kumpata
Yasmin tutafahamu mambo
mengi” akasema Job
“ Ni kweli Job,kama
tungeweza kumpata Yasmin
tungefahamu kuhusu uhusiano
wa rais na Alshabaab.Mwenendo
wa rais umebadilika na ananipa
shaka sana.Ni Jana tu ambapo
tumefahamu kuhusu
makubaliano yake na Alshabaab
na leo haohao Alshabaab
wanafanya mashambulio
makubwa na kumwaga damu
nyingi.” Akasema Austin
“Kwa hiyo unashauri nini
kifanyike Austin? Akauliza
Amarachi
“ Tusubiri kwanza taarifa
rasmi ya tukio hili itoke halafu
tutajua nini cha kufanya,lakini
rais ni mtu ambaye tunapaswa
kumuwekea alama ya
kiulizo.Kuna maswali ambayo
anahitaji kutupatia majawabu
yake.Najua kwa sasa inaweza
kuwa vigumu kuonana naye au
hata kuwasiliana naye kutokana
na hili lililotokea lakini ripoti hii
ya kipimo cha vinasaba
itamfanya atutafute .Kwa sasa
tupumzikeni na tuendeleeni
kufuatilia tukio hili kwa karibu
.” akasema Austin na kuwaacha
wenzake sebuleni akaelekea
chumbani kupumzika.
SEASON 6: SEHEMU YA 4
Yasmin Esfahani na Tariq
walikuwa katika chumba cha
hoteli walimofikia wakifuatilia
habari za kile kilichotokea jijini
Dar es salaam na Dodoma jioni
ya siku hiyo.Walikuwa
wanatazama chaneli moja
inayotangaza kwa lugha ya
kiarabu. Yasmin alikuwa
ameketi katika zuria
laini,pembeni yake kukiwa na
chupa kubwa ya mvinyo .Tariq
yeye alikuwa sofani akiwa na
pakiti la sigara akivuta moja
baada ya nyingine.Mara katika
chaneli ile kukaonyeshwa video
ya Habib akitangaza Alshabaab
kuhusika katika mashambulio
yale mawili yaliyotokea
Tanzania. Video ile ilimstua
sana Tariq
“ Kumbe ni Alshabaab ndio
waliotekeleza mashambulio haya
!! akasema kwa mshangao.
“Kwa miaka kadhaa
sijamuona Habib.Nimestuka
sana nilipomuona .Hajabadilika
na hata sura yake bado ina lile
tabasamu lake la kikatili.”
Akasema Tariq huku akiwasha
sigara nyingine na kuvuta kwa
fujo
“Umeshuhudia Alshabaab
walichokifanya leo.Mamia ya
watu wasio na hatia wamepoteza
uhai .Faida gani inayopatikana
kwa kuua watu wengi hivi wasio
na hatia ? Ndani ya hoteli ile
kulikuwa pia na watoto wadogo
hao wamekosa nini? Kwa hiki
tunachokishuhudia bado kuna
sababu ya kuendelea kuwa
wafuasi wa makundi haya? Bado
unatamani kuendelea kuua
watu wasio na hatia? Huu ni
unyama uliopitiliza.!!! Akasema
Yasmin.Tariq akapuliza moshi
mwingi hewani na kusema
“ Yasmin kuna jambo
ambalo limekuwa linaniumiza
kichwa changu toka jana
ambalo naomba unisaidie
kupata jibu lake kama
unalifahamu.”
“Uliza” akajibu Yasmin
“ Rais alinifuata gerezani
akaniambia kwamba anataka
kuniachia huru lakini atafanya
hivyo iwapo nitamsaidia kupata
mawasiliano ya
Habib.Nilishangaa sana kwa rais
wa nchi kutaka kuwasiliana na
kamanda mkuu wa Alshabaab.
Kwa kuwa nilikwisha choka
kukaa gerezani nilimsaidia rais
na akafanikiwa kuzungumza na
Habib .Sikujua waliongea
nini,hadi jana usiku nilipotolewa
gerezani nikaambiw akwmaba
niko huru na kukabidhiwa kwa
vijana wale walionileta katika ile
nyumba tuliyolala.Wewe
umekuwa unazungumza na rais
kwa muda mwingi na katika
maongezi yenu nimesikia
kwamba kuna makubaliano
yamefanyika kati ya rais na
Alshabaab.Nataka kufahamu
wamekubaliana nini?Nijibu
tafadhali kama unafahamu
chochote” akasema Tariq
“ Tariq ,hata mimi kama
ilivyokuwa kwako rais alinifuata
gerezani akaniambia kwamba
amekuja kuniachia
huru.Nilimuuliza kwa nini
anataka kuniachia huru
akasema kwamba amefanya
makubaliano na Habib na moja
kati ya makubaliano yao ni mimi
kuachiwa huru.Nilishangaa
sana kwani sikuwa
nikimfahamu huyo Habib ni
nani hadi pale aliponitajia
kwamba ni kiongozi wa
Alshabaab.Baada ya kutoka pale
gerezani akanipeleka katika ile
nyumba tuliyolala na
nikafanikiwa kuzungumza na
Habib kwa mara ya kwanza ,
akaniambia kwamba yeye
hanifahamu lakini ameelekezwa
na IS kwamba moja kati ya
makubaliano yake na rais ni
mimi kuachiwa huru.Kitu cha
pili ambacho walikitaka ni hati
ya muungano wa Tanganyika na
Zanzibar hii ambayo tunayo
hapa.” Akamimina pombe katika
glasi akanywa halafu akatikisa
kichwa na kusema
“ Nilifanikiwa kuzungumza
na viongozi wangu wa IS
wakaniambia kwamba rais wa
Tanzania anataka Alshabaab
wamfanyie kazi Fulani nchini
kwake na Alshabaab
wakawasiliana na IS ambao
walitoa masharti hayo
mawili.Endapo Alshabaab
wangefanikisha kupatikana kwa
vitu hivyo viwili basi IS
wangewalipa pesa nyingi na vile
vile wangeunganisha nguvu na
kuanzisha mapambano ili
kuhakikisha wanaiangusha
serikali ya Somalia kitu
ambacho Alshabaab wamekuwa
wakikitafuta kwa miaka
mingi.Kwa sasa IS ni kikundi
cha kigaidi chenye nguvu kubwa
duniani.Alshabaab
walikubaliana na matakwa hayo
ya IS na wakampa masharti rais
wa Tanzania akakubali.Kuhusu
makubaliano ya rais wa
Tanzania na Alshabaab mimi
siyafahamu lakini yawezekana
walikubaliana kuhusu
mashambulio haya ya leo kwani
si mara moja rais wa nchi
kutumia vikundi vya kigaidi
katika kufanikisha mambo yao
Fulani Fulani na inawezekana
kabisa katika mashambulio
haya mawili yaliyotokea leo hii
hata rais wa Tanzania anaweza
kuwa anahusika japokuwa sina
uhakika na hilo ” akasema
Yasmin .Kama madirisha ya
chumba kile yasingekuwa wazi
chumba chote kingejaa moshi
kutokana na sigara mfululizo
alizokuwa anavuta Tariq.
“ Maelezo yako yamenipa
picha kamili ,kweli nilikuwa
gizani na sikujua chochote
kinachoendelea.Bado kuna kitu
kimoja nahitaji kukifahamu.IS
wanaitaka hati ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar kwa
kusudi gani? Akauliza
Tariq.Ilimchukua Yasmin zaidi
ya dakika mbili kujibu.
“Baada ya kupata upinzani
mkubwa katika nchini nyingi za
mashariki ya kati ,ulaya na
Amerika Is wameamua
kuwekeza na kuliimarisha zaidi
kundi lao barani Afrika,hivyo
wakanituma mimi nije afrika
mashariki kuweka sawa
mipango ya kuanzisha kwa tawi
la IS katika ukanda huu.Kwa
muda wa miaka kumi na nne
nimeishi katika sehemu mbali
mbali za afrika mashariki
nikifanya uchunguzi na mipango
ya kueneza kundi la IS na
namna tutakvyoweza kufanya
kazi.Pamoja na kuzunguka
sehemu mbali mbali za afrika
mashariki makao yangu makuu
yalikuwa Dar es salaam
Tanzania ambako nilifanikiwa
kumpata mwanaume mmoja
aliyekuwa anajishughulisha na
biashara ya dawa za kulevya
nikazaa naye mtoto
mmoja.Huyu alinisaidia sana
bila yeye kufahamu mimi ni
nani.Baadae nikakamatwa na
kufungwa gerezani .” akatulia
kidogo akamimina pombe katika
glasi na kunywa .
“ Niliyakosa sana maisha
kama haya .Nilikuwa na kiu ya
mvinyo huu ” akasema Yasmin
na kunywa tena pombe nyingine
halafu akaendelea.
“Katika uchunguzi wangu
niligundua kwamba IS
tungekuwa na mafaniko
makubwa na tungeweza kufanya
kazi zetu kwa uhuru zaidi iwapo
tungefanikiwa kukimiliki kisiwa
cha Pemba.Tungefanikiwa
kukipata kisiwa hiki tungeweza
kulitawala eneo la bahari na
hata eneo zima la afrika
mashariki.Niliwasilisha
mapendekezo hayo kwa wakuu
wangu wakakubaliana nayo
lakini tatizo likawa ni namna ya
kuweza kukipata kisiwa hicho
kwani kiko ndani ya jamhuri ya
muungano wa Tanzania .Kitu
pekee ambacho kingepelekea IS
wakitwae kisiwa cha pemba ni
kwanza kuuvunja muungano
kati ya Tanganyika na Zanzibar
halafu visiwa vya Unguja na
Pemba kila kimoja kiwe
huru.Wakati nakamatwa
tulikuwa katika kutafuta namna
ya kulifanikisha hilo yaani
kuuvunja muungano wa
Tanganyika na Zanzibar na
mpaka sasa bado mawazo yangu
wanaendelea kuyafanyia kazi
kwa kutumia mbinu mbali mbali
za kutaka kuuvunja muungano
huu lakini bado hawajafanikiwa
na ilipojitokeza fursa kama hii
wameamua kuitumia vyema
.Kujibu swali lako IS wanaitaka
hatiya muungano wa
Tanganyikan a Zanzibar kwa
lengo la kuuvunja muungano ili
wakitwae kisiwa cha Pemba..”
Akasema Yasmin na kukawa
kimya.
Yasmin aliendelea kunywa
mvinyo huku Tariq akiendelea
kuvuta sigara kwa fujo huku
akimtazama Yasmin halafu
akatabasamu.
“ Yasmin sikuwa
nikikufahamu na wala sijawahi
kukusikia hadi nilipokutana
nawe jana katika ile nyumba
tuliyolala.Nilipokuona mwanzo
nilikuona kama mwanamke wa
kawaida lakini kwa haya
uliyonieleza na kwa mambo
niliyoshuhudia ukiyafanya leo
hadi tukafanikiwa kutoka
salama katika uwanja ule wa
ndege nimekuogopa.Mimi
nilikuwa mratibu mkuu wa
mashambulio yote ya Alshabaab
lakini nakiri mbele yako kuwa
sina akili za haraka haraka
kama ulizonazo .Ningekuwa
peke yangu nisingeweza kutoka
ndani ya ule uwanja” akatulia
akavuta sigara yake na kusema
“ Kuna jambo ambalo
sikuwa nimekueleza.Nikiwa na
Alshabab niliratibu
mashambulio mengi tu ambayo
yalipelekea vifo vya watu wengi
na kwa taarifa yako ninatafutwa
sana na serikali za Kenya na
Somalia kutokana na kuratibu
mashambulio mengi
yaliyopoteza maisha ya watu
wengi.Toka jana nilipoambiwa
kwamba tumeandaliwa ndege ya
kutupeleka Mogadishu nilikuwa
na mawazo mengi sana ni jinsi
gani nitakavyoweza kushuka
Mogadishu bila kukamatwa?
Japokuwa ni miaka mingi
imepita lakini uhakika wa
kuvuka salama pale uwanjani
ulikuwa mdogo sana. Mawazo
niliyokuwa nayo yalikuwa ni
kuiteka ndege ile kabla ya
kufika Mogadishu na kuibadili
muelekeo ili tupelekwe sehemu
nyingine jambo ambalo
ulilifanya wewe na ninashukuru
na wewe kuwa na wazo kama
langu.Sijui lengo la Habib ni nini
aliposema kwamba tupelekwe
Mogadishu wakati anafahamu
fika kwamba serikali ya Somalia
wananitafuta .Kwa hiyo kitendo
ulichokifanya cha kubadili
uelekeo wa ndege kimenisaidia
sana ni kama vile ulikuwa
katika akiliyangu.Napenda
kukuhakikishia kwamba niko
tayari kufanya kazi nawe
.Maneno uliyonieleza tukiwa
ndegeni kuhusiana na
kuendelea na ushirika na
mitandao yetu ya zamani
nimeyatafakari sana na
nimefanya maamuzi hata mimi
ya kuachana na maisha kama
yale na kuanza maisha
mapya.Kwa hiyo Yasmin kama
una mpango wowote ulionao wa
kuanza maisha mapya naomba
unishirikishe na mimi tafadhali”
akasema Tariq.Yasmin akageuka
akamtazama Tariq usoni kisha
akauliza
“ Una hakika na maamuzi
yako?
“ Ndiyo Yasmin.Nahitaji
kupotea na kwenda kuanza
maisha mapya mbali kabisa na
Alshabaab.Kauli yako
imenifanya nitafakari sana
maisha yangu ndani ya
Alshabaab na faida
nilizozipata.Mpaka sasa sijaona
faida yoyote niliyopata kwa
kulitumikia kundi hili .Nimeua
watu wengi lakini hakuna kitu
cha maana nilichopata sina mke
,sina mtoto sina familia .Nataka
nianze upya. Usiniache tafadhali
kama una mipango yoyote
mizuri ya kuanza maisha mapya
mbali na hapa.” Akasema Tariq
“ Sawa nimekusikia
.Nitakusaidia kama kweli una
nia ya dhati” akasema Yasmin
na kuendelea kunywa mvinyo.
“Ninatakiwa kuwa makini
sana na huyu
jamaa.Ninafahamu namna ya
kuwasoma watu huyu si mtu
mzuri hata kidogo.Nikimtazama
machoni hamaanishi kile
anachokisema.Najua ana lengo
lake lingine lakini hapa kwangu
hawezi kufanya lolote.” Akawaza
Yasmin
“ Yasmin”akaita Tariq na
Yasmin akageuka akamtazama.
“ Habib alikuwa na
mategemeo leo saa kumi na
moja tungefika Mogadishu lakini
mpaka sasa hatujatokea na
hatuna mawasiliano naye
yoyote.Nini kitatokea iwapo
mpaka kesho asubuhi hatakuwa
ametuona ?
“ Ni wazi atafanya
mawasiliano na rais wa
Tanzania kumuuliza nini
kimetokea na hapo ndipo msako
wa kututafuta
utakapoanza.Kesho asubuhi
tunarejea Dar es salaam.”
“ Dar es salaam? !! akauliza
Tariq kwa mshangao
“ Ndiyo tunarejea Dar es
slaam” akajibu Yasmin bila wasi
wasi wowote
“ Tunakwenda kutafuta nini
Dar es salaam? Kule ni hatari
sana kwetu.Kama ulivyosema
mwenyewe kwamba lazima
Habib atawasiliana na rais wa
Tanzania na atamfahamisha
kwamba hatujafika Mogadishu
na tutaanza kutafutwa kila
kona.Kwa sasa tuko mbali na
Dar es salaam kwa nini tusianze
safari yetu na kutokomea mbali
bila kwenda kutafuta hatari
tena? Yasmin maisha ya mateso
niliyokaa gerezani yananitosha
sitaki tena maisha kama yale na
ndiyo maana nimeanua kuanza
maisha mapya.Tafadhali
nakuomba ufikirie upya mpango
wako huo wa kurejea tena Dar
es salaam” akasema
Tariq.Yasmin akanywa mvinyo
kidogo na kusema
“ Kesho tunarejea Dar es
salaam.Kuna kazi ambayo
sijaikamilisha .Natakiwa kwenda
kumchukua mwanangu ambaye
yuko Dar es alaam na safari ya
kuelekea katika maisha mapya
itaanzia hapo.Siwezi kuondoka
bila mwanangu Shamim.kama
uko kitu kimoja na mimi
tutaongozana wote kurejea Dar
es salaam.Tuko pamoja?
Akauliza.Tariq akatumia muda
kidogo kutafakari na kusema
“ Sawa tutaenda huko Dar
es salaam” akasema Tariq huku
akiwasha sigara nyingine.
“ Sipati picha Habib
atakuwa katika hali gani muda
huu .Atakuwa na hasira
zisizomithilika.Ninamfahamu
Yule jamaa ni mkatili sana na
ana roho ya kinyama .Endapo
atagundua kwamba
tumemzunguka na kumfanyia
mchezo huu sijui nini kitatokea
.Atatusaka kwa maisha yake
yote yaliyobaki na akitupata
kitakachofuata ni kutuua.Siwezi
kumsaliti Habib kiasi hiki,lazima
nitafute namna ya kufanya na
kuichukua hii hati
nikamkabidhi Habib.Huyu
mwanamke hawezi kunishinda
kwani tayari nimekwisha
muweka upande wangu na
tayari ananiamini
.Ninachotakiwa kabla ya kesho
asubuhi niwe nimemmaliza
kisha niondoke na hati hii.Kabla
ya yote natakiwa kutafuta nafasi
ya kuzungumza na Habib au
mtu mwingine yeyote katika
Alshabaab nimfahamishe kile
kinachoendelea.pamoja na
kukaa gerezani muda mrefu
lakini siwezi kulisaliti kundi
langu hata kidogo.Nimejiunga
na Alshabaab nikiwa kijana
mdogo sana wa miaka kumi na
nne na nitakufa mtiifu kwa
Alshabaab.”akawaza Tariq na
kukohoa kidogo kisha akaita
“Yasmin”
Yasmin akageuka
akamtazama
“Kwa miaka kadhaa
tumekuwa kifungoni lakini
baada ya kutoka kifungoni bado
tunaendelea kujificha
ndani.Japo kwa mara moja kwa
nini tusitoke tukaenda sehemu
kupoteza mawazo na kutuliza
akili zetu.Tumepitia mambo
mengi sana hadi tumefika hapa
kwa hiyo si vibaya endapo
tukatoka kidogo.Hakuna
anayetufahamu hapa Zanzibar
kwa hiyo tuko huru kwenda
sehemu mbali mbali za
burudani.Ninahisi kuboreka
sana hapa ndani” akasema
Tariq.Yasmin akatabasamu na
kusema
“ Mimi si mwendaji wa
sehemu za burudani na zaidi ya
yote sijaboreka hapa ndani na
ninajisikia furaha
sana.Niliyakosa sana maisha
haya nilipokuwa gerezani.”
Akasema Yasmin na kuinuka
akamfuata Tariq akaketi
pembeni yake.
“ Kitu gani hasa
ulichokikosa ulipokuwa
gerezani? Akauliza Yasmin.Tariq
akatabasamu na kusema
“ Nilikosa vingi lakini
kikubwa nilichokikosa ni
kushuhudia milipuko ya
mabomu niliyoyatega.Mimi ndiye
niliyekuwa mratibu wa
mashambulio yote ya Alshabaab
na nilisikia raha sana kuona
shambulio nililoliratibu
linafanikiwa” akasema Tariq
“ Hicho peke ndicho
kinachokupa furaha katika
maisha yako? Ukiacha milipuko
ya mabomu hakuna kingine
ambacho kinakupa furaha
katika maisha ? Hakuna
wanawake huko katika kambi
zenu wa kuwastarehesha?
“ Wanawake? Akauliza Tariq
“ Ndiyo”
“ Wanawake wapo lakini
mimi starehe yangu si
wanawake bali ni milipuko kama
nilivyokueleza.Wanawake nakaa
nao mbali kabisa na ndiyo
maana mpaka sasa sina mke
wala mtoto” akasema Tariq na
kuwasha sigara nyingine.Yasmin
akamshika bega na kusema
“ Ni vipi endapo
nitakwambia kwamba kitu
nilichokikosa sana nikiwa
gerezani ni mwanaume wa
kufanya naye mapenzi?
Akasema Yasmin huku
akitabasamu.Tariq akastuka.
‘”Mbona umestuka Tariq?
Hicho ndicho kitu nilichokikosa
mno nikiwa gerezani.Ninapenda
sana kufanya mapenzi.Ni
starehe yangu kubwa na kwa
usiku wa leo kwa kuwa niko
nawe humu chumbani utanikata
kiu yangu ya miaka mingi.Kwa
hiyo hatutakwenda kokote
nataka tufanye mapenzi usiku
kucha kufidia miaka yote
ambayo nilikuwa gerezani.”
Akasema Yasmin huku
akimshika shika Tariq maeneo
nyeti.
“ Yasmin subiri
kwanza.Mimi si mpenzi wa
mambo hayo.Japokuwa nimekaa
gerezani kwa miaka mingi lakini
bado sina hamu ya kufanya
mapenzi.” Akasema Tariq lakini
Yasmin hakusikia chochote
kwani tayari mashetani
yalikwisha mpanda.Akavua
gauni alilolivaa na kubakiwa na
nguo za ndani.Pamoja na kukaa
miaka mingi gerezani lakini
bado mwili wa Yasmin ulikuwa
mwororo na wenye
kung’aa.Tariq akahisi mwili
unamchemka baada ya
kuushuhudia mwili ule mwororo
.Yasmin akaendelea na utundu
wake akaifungua suruali ya
Tariq na kwa kutumia mdomo
na ulimi wake akafanya utundu
mkubwa pale ikulu kiasi cha
kumfanya Tariq atoe
miguno.Ghafla kama mbogo
majeruhi Tariq akavua fulana
aliyoivaa akaitupa chini
akamuinua Yasmin na kumbeba
mikononi.Tariq alikuwa ni pande
la mtu mwenye nguvu
nyingi.Hakuwa na subira
akakianzisha kipute.Yasmin
alitoa ukele kufurahia kipute
kile na gwaride alilochezeshwa
na Tariq.Kilikuwa ni kipute hasa
kilichochukua dakika arobain
.Hadi wote wanamaliza vitu
vilikuwa vimetawanyika hovyo
mle chumbani kwani kutokana
na ugumu wa mpangano ule
mechi ilichezwa kila mahali .
Wote wawili walikuwa
wanahema kama wakimbiaji wa
mbio ndefu.
“ Sikutegemea kama una
uwezo mkubwa kiasi
hiki.Ahsante kwa kunikata kiu
japo bado nitahitaji zaidi na
zaidi usiku wa leo” akasema
Yasmin
“ Mapenzi si starehe yangu
lakini nikiamua kufanya nina
uwezo mkubwa sana na
ninaweza kufanya kwa muda
mrefu” akasema Tariq.
Yasmin akainuka
akachukua taulo akaingia
bafuni kujimwagia maji
“ Hii ndiyo nafasi niliyokuwa
naitafuta” akawaza Tariq
akainuka kitandani akajifunga
taulo halafu akanyata hadi
katika begi la Yasmin
akalifungua na kuitafuta simu
.Alipoipata akanyata hadi katika
mlango wa bafu akasikia maji
yakimwagia,Yasmin aliendelea
kuoga.Haraka haraka akaiwasha
halafu akaziandika namba
Fulani katika simu ile akapiga
na kuiweka sikioni ili kusikia
kama inaita taratibu
akaufungua mlango akatoka nje
.Akazungumza na mtu fulani
haraka haraka kwa kiarabu
halafu akakata simu na
kufungua mlango taratibu
kurejea ndani.Alipata mstuko
mkubwa pale alipojikuta
akitazamana na Yasmin
aliyekuwa mtupu akichuruzika
maji mwili huku akiwa
amemnyooshea bastora.
“ Ingia ndani taratibu kama
ulivyotoka” akasema
Yasmin.Tariq akaingia ndani na
kuufunga mlango akaamriwa
apige magoti .Ghafla kikatokea
kitu ambacho Yasmin hakuwa
amekitegemea.Tariq aliruka
mzima mzima na kumvaa
Yasmin wote wakaanguka
chini.Bastora ya Yasmin
ikamponyoka na kuanguka
pembeni.Tariq akampiga Yasmin
ngumi nzito sana na kunyoosha
mkono ili kuichukua bastora ile
lakini Yasmin tarai alikwisha
msoma na hakutawa tayari
kumpa nafasi hiyo.Akamchoma
kidole cha jicho.Tariq
akapandisha hasira na kuanza
kumvurumishia Yasmin
makonde mazito.Yasmin
akaishika stuli iliyokuwa
pembeni na kumpiga nayo Tariq
kichwani akaanguka
chini.Akainuka haraka haraka
na kumpiga teke zito maeneo ya
korodani na kumfanya Tariq
agugumie kwa maumivu makali
aliyoyapata.Kama hiyo haitoshi
akauchukua stuli ile na
kumbamiza nayo mara mbili
kichwani.Tariq akaanza kutokwa
na damu kichwani.Yasmin
akaiokota bastora yake na
kumuelekezea
“ Nani ulikuwa unaongea
naye? Nieleze ukweli ama sivyo
sintakuacha hai” akasema
Yasmin
Tariq hakusema chchote
aliendelea kugugumia maumivu
“ Tariq hii ni mara ya
mwisho nieleze nani uliyempigia
simu? Akauliza lakini Tariq
hakumjbu.Akaiokota simu
akatazama namba aliyopiga
Tariq lakini tayari ilikuwa
imefutwa.
“ Nilifahamu toka awali
lengo lako na nilikuwa
nakusubiri ufanye
ulivyofanya.Ulisema hutaki tena
kushirikiana na Alshabaab ili
nikuamini na mwisho wa siku
uweze kuchukua hati hii na
uondoke nayo.Mimi ni mtu
mwingine Tariq huwezi
kunizunguka hata mara moja na
kwa hili ulilolifanya
sintakusamehe.” Akasema
Yasmin
“ Unadhani utafanikiwa
malengo yako? Usijidanganye
Yasmin hakuna chochote
utakachofanikiwa.Hutafanikiwa
kundoka salama hapa Zanzibar
na hautakwenda
kokote.Jisalimishe kwa Habib
na umrejeshee kilicho mali
yake.Usipofanya hivyo hata
mwanao hautamuona tena .Hivi
tunavyoongea vikosi vyote vya
ulinzi tayari vina taarifa zako
muda wowote toka sasa
utakamatwa” akasema Tariq na
kuzidi kumpandisha hasira
Yasmn na kwa kutumia bastora
ile iliyofungwa kiwambo cha
sauti akammiminia Tariq risasi
kichwani.
“ Yasmin Esfahani huwa
hazungukwi hata mara
moja.Hukujua unacheza na mtu
wa aina gani” akasema Yasmin
kwa hasira.Tariq hakuwa na
uhai.Akamvuta na kumpeleka
bafuni na kuufunga
mlango.Akavaa haraka na
kujitazama katika kioo.
“Lazima niondoke hapa
haraka iwezekanavyo.Natakiwa
kwenda Dar es salaam
kumchukua Shamin ” Akawaza.
SEASON 6: SEHEMU YA 5
Imetimu saa tatu na dakika
ishirini katika makao makuu ya
Alshabaab hali ikiwa ya
ukimya.Ulinzi ulikuwa mkali
kama ilivyo kawaida yake.Mpaka
mida hii hakukuwa na taarifa
zozote kuhusiana na walipo
Tariq na Yasmin ambao
walitegemewa wangewasili
Mogadishu mida ya jioni baada
ya ndege yao kusemekana
kupata hitilafu angani na
kulazimika kutua kwa dharura
kisiwani Unguja.
Habib Alzaraq alirejea
kutoka kuswali,akauliza kama
kuna taarifa zozote kuhusiana
na akina Tariq lakini hadi muda
huo hakukuwa na taarifa zozote
zilizopatikana .Akamuagiza mtu
wake anayehusika na masuala
ya mawasiliano afanye
mawasiliano na uwanja wa
ndege wa Zanzibar kufahamu
kama ndege ile waliyokuwa
wanasafiria akina Tariq iliyotua
kwa dharura pale Zanzibar
kama imekwishaondoka pale
uwanjani au bado inaendelea na
matengenezo.Mawasiliano
yalifanyika na taarifa
iliyopatikana ni kwamba baada
ya kufanyiwa uchunguzi katika
injini yake ndege ile ilifanikiwa
kuruka na kurejea Dare s
salaam.Habib akapewa taarifa
hizo na zikamstua
“ Dar es salaam ? akauliza
Habib kwa mshangao.
“ Ndiyo mkuu.Nimetaarifiwa
kwamba ndege ilifanyiwa
uchunguzi na kisha
ikaruhusiwa kuondoka na
ikarejea Dar es salaam.”
“Yasmin na Tariq
walikuwemo ndani ya hiyo ndege
iliporejea Dar es salaam?
Akauliza Habib
“ Nimepewa jibu la jumla
kwamba ndege hiyo imerejea
Dar es salaam,hawakufafanua
kama akina Tariq nao
walikuwemo ndani yake”
akasema Yule msaidizi wake wa
masuala ya mawasiliano.Habib
akajaribu kupiga zile namba za
simu ambazo Yasmin alimpigia
mara ya mwisho akiwa hospitali
lakini hazikuwa zikipatikana.
“ Naanza kuingiwa na wasi
wasi kwamba yawezekana kuna
mchezo unataka kuchezwa
hapa.Kwa nini ndege irejee Dar
es salaam wakati ilitakiwa
iendelee na safari kuelekea
Mogadishu? Watu wa kutoka IS
watawasili usiku huu kwa ajili
ya kufanya makabidhiano ya ile
hati ya muungano ambayo
tayari Yasmin na tariq
wamekwishakabidhiwa.Nitawael
eza nini? Akajiuliza Habib kisha
akazitafuta namba za simu za
rais akapiga.Sura yake ilikuwa
imejikunja kwa hasira.Simu
iliita bila kupokewa akapiga tena
na safari hii ikapokewa.
“ Hallo Habib niko kwenye
kikao kizito sana kuhusiana na
mambo yaliyotokea hapa nchini
leo.Naomba niwasiliane nawe
baada ya kama saa moja hivi”
akasema rais kwa sauti ndogo.
“Sina muda wa kusubiri rais
nataka tuongee sasa hivi.Kama
ni muhimu wewe kuwepo katika
kikao hicho simamisha kikao
uzungumze nami kwanza.”
Akasema Habib kwa ukali.Rais
akatazama pande zote kama
kuna mtu karibu kisha akauliza
“ Unasemaje Habib?
“ Sikiliza rais,sihitaji ugomvi
na wewe wala vita na nchi
yako.Tulikubaliana vizuri na
nimeifanya kazi yako kama
ulivyotaka.Nataka unipatie
Tariq,Yasmin na ile hati kama
tulivyokubaliana kama si hivyo
utatufahamu sisi ni nani !!
akasema Habib kwa ukali
“ Mbona sikuelewi Habib?
Nilitoa ndege kwa ajili ya
kuwapeleka Tariq na Yasmin
Mogadishu.Hawapo hapa
nchini,tayari wamekwisha
ondoka.”
“Hawajafika
Mogadishu.Niliwasiliana na
Yasmin jioni ya leo walitua kwa
dharura katika uwanja wa ndege
wa Zanzibar kutokana na
hitilafu katika ndege .Mpaka
usiku huu hakuna taarifa zozote
kuwahusu wao.Tumefuatilia
uwanja wa ndege wa Zanzibar
tumetaarifiwa kwamba ndege ile
baada ya kufanyiwa uchunguzi
imepaa na kurejea Dar es
salaa.Mheshimiwa rais naamini
huu ni mchezo
unatuchezea.Nilikuonya hapo
awali kwamba usijaribu kufanya
mchezo wowote wa kihuni na
sisi lakini unaonekana
kulipuuza onyo hilo na unataka
kutuzunguka.Tumeifanya kazi
yako na sisi tunahitaji haki
yetu” akasema habib.
“ Habib naomba unisikilize
vizuri.Mimi sifahamu chochote
kuhusiana na suala hilo.Nilitoa
ndege ambayo ni nzima kabisa
na haina hitilafu yoyote
nashangaa kusikia kwamba
walitua Zanzibar kwa
matengenezo.Kinachonishangaz
a sijataarifiwa chochote
kuhusiana na jambo hilo
nikiamini kwamba mpaka muda
huu tayari Yasmin na Tariq
watakua wamekwisha fika
hapo.Hizi unazonipa ni taarifa
ngeni kabisa.Naomba unipe
muda nilifuatilie suala hili.”
Akasema rais
“ Ninakupa mpaka kesho
saa mbili asubuhi tuwe
tumepata kila kile tulichokuwa
tumekubaliana .Kama
hatutakuwa tumepata haki yetu
nakuhakikishia damu hii
iliyomwagika leo itaendelea
kumwagika kila uchao hapo
Tanzania.” akasema Habib na
kukata simu.Ernest Mkasa
akahisi mwili kuloa jasho.
“ Nini kimetokea? Ni kweli
ndege waliyopanda akina Tariq
ilipata hitilafu na kutua
Zanzibar kwa dharura? Mbona
sijataarifiwa jambo hili?
Akajiuliza.
“ Hili sasa ni suala jipya
ambalo natakiwa
kulishughulikia kwa haraka.
Tariq na Yasmin wako wapi?
Akajiuliza rais.
“ Au huu ni mpango wa
Yasmin ili anirudishie hati ile ya
muungano kwa lengo la
kumpata mwanae? Nahisi hivyo
kwani aliniahidi kufanya kila
atakachoweza ili kumpata
mwanae.Kama huu ni mpango
wake kwa nini basi hajanitaarifu
chochote? Hata hivyo natakiwa
kuanza maandalizi ya
kuhakikisha ninampata Maria
haraka iwezekanavyo ili ikitokea
Yasmin akamuhitaji basi tayari
niwe naye.” Akawaza rais na
kumpigia simu mmoja wa vijana
wake aliyempa jukumu la
kuhakikisha kwamba Yasmin na
Tariq wanaondoka nchini
akamtaka afuatilie suala lile
kama lina ukweli wowote na
amjulishe ndani ya muda
mfupi,halafu akarejea katika
ukumbi wa mikutano
Baada ya kuongea na
rais,Habib akawakusanya
makamanda wake kwa ajili ya
kikao cha dharura kujadili
kilichotokea.Kabla ya kikao
kuanza,Aziz mmoja wa wasaidizi
wake anayemuamini sana
akatokea akiwa anahema na
ilionekana alikuwa anakimbia
“ Samahani nimechelewa
mkuu nilikwenda kuswali lakini
hata hivyo nimekuja na habari
ya muhimu sana”
“ Habari gani Aziz? Akauliza
Habib
“ Nimezungumza na Tariq.”
“ Tariq? Amekupigia simu?
“ Ndiyo mzee.Tariq
amenipigia simu nikiwa njiani
kuja hapa.”
“ Yuko wapi? Nini kimetokea
hadi wakashindwa kufika hapa
kama tulivyokuwa tumepanga?
Akauliza Habib
“Kuna tatizo
limetokea.Amenieleza kwa ufupi
sana kwani alitumia simu ya
Yasmin bila yeye
kufahamu.Tariq anasema
kwamba ndege waliyokuwa
wanaitumia haikupata hitilafu
yoyote bali Yasmin
aliwalazimisha marubani
kubadili muelekeo na kutua
Zanzibar kwa kisingizo cha
hitilafu katika injini.Anasema
kwamba Yasmin amebadilika na
ana mpango wa kutokomea
kusikojulikana na hati ya
muungano.Ameniambia kwamba
tufanye haraka tumuwahi
Yasmin wako Hotel Lepatido”
akasema Aziz na wote
wakamtazama Habib kusikia
atasema nini
“ Niliwakatalia IS kwamba
siwezi kumpa nyaraka kubwa ile
ya hati ya muuungano mtu
nisiyemfahamu vizuri lakini
wakakataa na kudai kwamba
Yasmin hana matatizo ni mtu
wao lakini kumbe hisia zangu
zilikuwa za kweli.Huu ni
mgogoro mwingine kati yetu na
IS.Nilifanya kosa kubwa sana
kumuamini Yasmin badala ya
mtu wangu Tariq.” Akawaza
Habib na kuchukua simu
akampigia rais Ernest ambaye
licha ya kuwa katika kikao kizito
na wakuu wa vyombo vyote vya
usalam wakijadili mashambulio
yale yaliyotokea alilazimika
kutoka nje ya ukumbi wa
mikutano baada ya kuiona
namba ya Habib
“ Habib nilikuomba unipe
muda nilifuatilie suala
lako.Vijana wangu bado
hawajanipa taarifa zozote mpaka
sasa.Nitakujulisha nikipata
taarifa zozote toka kwao”
akasema Ernest
“ Mheshimiwa rais
nimepata taarifa sasa hivi nini
kimetokea.Tariq amemmpigia
simu mmoja wa wasaidizi wangu
na akamweleza kwamba ndege
waliyopanda haikuwa na hitilafu
yoyote bali ni Yasmin ndiye
aliyewatishia marubani kwa
bastora na kuwataka wabadili
uelekeo waelekee
Zanzibar.Yasmn amefanya
usaliti mkubwa na sasa anataka
kutoroka na hati ile
uliyompatia.Kwa mujibu wa
Tariq mpaka sasa bado wako
Hotel Lepatido
walikofikia.Mheshimiwa rais
nakuomba fanya kila unaloweza
uweze kumdhibiti Yasmin na
niweze kuipata hiyo hati usiku
wa leo na umkabidhi
Tariq.Tuma vikosi vya polisi sasa
hivi vilizingire jengo la hoteli
hiyo walimo na Yasmini
akamatwe haraka sana.Tayari
nimekupa taarifa zote na
ukishindwa kufanikisha
kukamatwa Yasmin nitaamini
kwamba wewe na Yasmin mko
kitu kimoja.Nitakupigia tena
baada ya robo saa kujua
maendeleo” akasema Habib na
kukata simu.Rais
akachanganyikiwa.
“ Ninaamini Yasmin
amefanya hivi alivyofanya
kutokana na yale makubaliano
yetu kwamba akinirejeshea hati
na mimi nitampatia mwanae.Ni
juu yangu sasa kuchagua
kwamba ninataka hati au
ugomvi na Alshabaab? Akawaza
na kumuita mkuu wa majeshi
Jenerali lameck Msuba
akamueleza kuhusiana na
jambo lile
“ Mheshimiwa rais hii ni
nafasi imepatikana ambayo
hatupaswi
kuichezea.Tunatakiwa kufanya
kila tunaloweza kumdhibiti
Yasmin na kuichukua hati
yetu.Usiogope vitisho kutoka
kwa Alshabaab kwani hawawezi
kufanya chochote.Tutapambana
nao” akasema lameck
“ Kwa hiyo unanishauri nini
Lameck?
“ Ushauri hapa ni kutuma
kikosi maalum toka usalama wa
taifa kwenda hotelini hapo
kuwadhibiti akina Tariq na
Yasmin.Hawatakiwi kwenda
askari au wanajeshi .Watu wale
wanapaswa kukamatwa kimya
kimya na kurejeshwa mahala
walikokuwa wamefungwa ”
akasema Lameck na rais
akamuita Silvanus Kiwembe
mkurugenzi wa idara ya
usalama wa taifa ambaye naye
alikuwemo katika kikao kile.
“ Silva nimekuita hapa kuna
jambo nataka lifanyike kwa
haraka na ambalo ni muhimu
mno.Yasmin Esfahani pamoja
na mtu mwenzake anaitwa Tariq
wako katika hoteli moja inaitwa
Lepatido kisiwani Zanzibar
.Nataka haraka sana tuma
kikosi cha vijana hodari kumi au
zaidi waende hotelini hapo usiku
huu na wahakikishe
wanawakamata watu hao wawili
na warejeshwe kule
gerezani.Kuna bahasha anayo
Yasmin ambayo nataka
ichukuliwe na isifunguliwe na
mtu yeyote kuona kilichomo
ndani bali iletwe kwangu moja
kwa moja.Kwa umuhimu wa
suala hili nataka wewe
mwenyewe uwepo katika kikosi
hicho ili kila kitu kiende
sawa.No mistake.Nawahitaji
Tariq na Yasmin wakiwa hai.”
Akasema rais na Silvanus
akaondoka kwenda kutekeleza
maagizo yale ya rais..Baada ya
Silva kuondoka ,rais
akamgeukia Jenerali Lameck
“Lameck nataka njia zote za
kuingilia na kutokea Zanzibar
zifungwe kwa muda ili kuzuia
Yasmin asiweze kupata nafasi ya
kutoroka.Viwanja vyote vya
ndege visiruhusu ndege yoyote
kutoka na hata bandari zote
zisiruhusu mtu yeyote kutoka
hadi hapo tutakapofanikiwa
kumpata Yasmin.” Akasema
Rais