QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: FINAL SEASON
SEHEMU YA 9

Baada ya kuachiwa na
Daniel,Agatha Mkasa alijitahidi
kuendesha gari lakini kadiri alivyozidi
kwenda ndivyo damu nyingi katika
mguu aliopigwa risasi iliendelea
kutoka.Akasimamisha gari na kuupiga
usukani kwa hasira
“Silva amepigwa risasi na wale
jamaa.Nilimsikia akitoa ukelele wakati
nikiruka nje nina imani atakuwa
ameuawa.Amenisaidia sana kwani
wangeweza kutuua sote wale jamaa.Ni
akina nani wale waliotuvamia?
Walijuaje kama tuko pale? Yule binti
Irene ni mtu hatari sana kwani
anashirikiana na watu hatari kama
wale”akawaza Agatha
“Ninachotakiwa kufanya kwa
haraka ni kutafuta namna ya kujitibu
hili jeraha.Sina namna nyingine ya
kufanya zaidi ya kurejea
ikulu.Akajipapasa na kuikuta simu yake
iko katika mfuko wa suruali aliyokuwa
ameivaa ndani ya gauni lake
pana.Akaiwasha na kutafuta namba za
mumewe Ernest na simu ikapokelewa.
“Agatha.Where are you? Akauliza
Ernest
“Ernest nahitaji msaada wako wa
haraka sana.Niko sehemu nimejruhiwa
kwa risasi nahitaji matibabu.Tafadhali
naomba msaada wa haraka sana kwa
maneno haya nilipo nikikutwa
ninaweza kudhurika zaidi” akasema
Agatha
“Agatha nielekeze tafadhali
mahala ulipo ili niwatame sasa hivi
walinzi waje wakuchue.Just stay where
you are” akasema rais.Agatha
akamuelekeza mahala alipokuwa na
rais akamuahidi kumtumia walinzi
haraka sana.
“Maisha yangu yanakumbwa na
mitihani mikubwa.Kila ninalolifanya
haliendi ninavyotaka.Nimepambana
kufa na kupona hadi Alberto’s
tukaotesha mizizi yake hapa Tanzania
lakini tulipoanza tu kuelekea katika
mafanikio yakatokea ya kutokea na
toka Ernest alipotusaliti ninaona kama
maisha yangu hayaendi
sawa.Nimenusurika kufa katika
shambulio lile baya la bomu na leo tena
kwa mara nyingine nimenusurika.Nini
hatima ya maisha yangu? Akajiuliza
Agatha
“Nimewatoa kafara watoto wangu
wote na hivi sasa sina hata mtoto
mmoja lakini mwenzangu Ernest
kumbe ana mtoto aliyezaa nje.Hili
limeniumiza sana na sijui nifanye nini
kumuangamiza huyo mtoto
wake.Lazima nifanye jambo siwezi
kukubali Ernest akawa na mtoto wakati
mimi …” Agatha akatolewa mawazoni
na simu yake iliyoita.Akatazama
mpigaji na kustuka sana akaipokea
haraka haraka
“788/26MM.” Agatha
akajitambulisha
“Tafadhali jiandae kuzungumza na
baba Alberto mkuu” ikasema sauti ya
mwanamke upande wa pili
aliyezungumza kwa lugha ya
kiitaliano.Agatha akahisi kutetemeka
mwili kwani kuzungumza na Alberto
mkuu halikuwa jambo dogo.Baada ya
dakika tano sauti nzito ikasikika katika
spika za simu.
“Agatha”
“Utukufu kwako mkuu baba
Alberto” akasema Agatha kwa uoga
“Agatha vipi hali yako?
‘ hali yangu ninaendelea vizuri”
“Agatha nimekupigia kukutaarifu
kwamba tumeamua kukuchagua wewe
kuwa mkuu wa Alberto’s nchini
Tanzania na unatakiwa kuhakikisha
kwamba unaanza kuotesha tena mizizi
upya .Maafa yaliyotokea yasikukatishe
tamaa kwani ni moja kati ya sadaka ya
damu ambayo inatakiwa kutolewa kila
baada ya miaka mitatu na safari hii
imekuwa ni zamu ya Tanzania kutoa
sadaka hiyo.Hili ni suala ambalo lipo
katika kanuni zetu na kwa kuwa
umeingia katika ngazi ya juu ya uongozi
basi utafahamu mambo mengi
kuhusiana na Alberto’s.Unachotakiwa
kufanya kuanzia sasa ni kujenga
mahusiano mazuri na
Ernest.Usipingane naye au kuanzisha
naye vita.Bado tunamtumia kufanikisha
mambo yetu na hata shambulio hili
lililotokea tumemtumia sisi bila yeye
kufahamu kama anatekeleza mipango
yetu kwa hiyo unatakiwa kuwa karibu
naye na nitakujaza nguvu ya kuweza
kumshawishi akubali kila
utakachomwambia.Alberto’s itaanza
upya na itakuwa na nguvu kubwa.Uko
tayari kulibeba jukumu hilo? Akauliza
Alberto
“Siwezi kusema hapana baba
.Nitalibeba jukumu hilo ulilonipa na
nitafanya kama ulivyonielekeza”
“Vizuri sana.Kabla ya kuanza
rasmi kulibeba jukumu hili kubwa
ulilopewa utakuja makao makuu
kusimikwa rasmi na kupewa
daraja.Sasa weka mkono wako wa
kushoto katika paji la uso wako ili
nikubariki na kukuongezea nguvu”
akasema Alberto na Agatha akaweka
mkono katika paji la uso wake na
Alberto akaongea maneno ambayo
Agatha hakuweza kuyafahamu na
baada ya dakika mbili akamaliza
wakaagana na simu ikakatwa.Agatha
akavuta pumzi ndefu
“Mwili wote unatetemeka.Kumbe
haya yote yaliyotokea ni mipango ya
Alberto’s? akajiuliza Agatha baada ya
kumaliza maongezi na Alberto mkuu
“Sadaka ya damu !!! akasema kwa
mshangao na mara kwa mbali akaziona
taa za gari zikija kwa kasi.Mawazo yake
yote yalikuwa katika yale aliyokuwa
amezungumza na Alberto
“Sasa nimepata picha kamili kwa
nini makao makuu hawakuonyesha
kustushwa kwanza na kitendo cha
usaliti alioufanya Ernest,pili hata
tulipoomba kibali cha kutaka kuonana
na Ernest walitoa Baraka zao bila
kusita na tatu nilipowataarifu
kuhusiana na vifo vya watu wetu
hawakuonyesha kustuka kabisa na
wakaniambia nitulie nisifanye lolote
nisubiri maelekezo.Nimeogopa sana.”
Akawaza Agatha na gari tatu zikafunga
breki mbele ya gari lake wakashuka
watu kadhaa na kumfuata.Aliwatambua
watu wale walikuwa ni walinzi
waliotumwa na rais.Haraka haraka
walimtoa katika gari alilokuwamo
wakampandisha katika mojawapo ya
gari waliokuja nalo na kuondoka eneo
lile haraka.Ndani ya gari alilopanda
kulikuwa na madaktari wawili ambao
walianza kulishughulikia jeraha lake la
mguu.
Moja kwa moja wakaelekea
Kobwe hospital ambako ndiko viongozi
wa juu wa serikali hutibiwa.
Rais Ernest Mkasa alifahamishwa
hali ya mke wake na kuondoka haraka
ikulu akaelekea Kobwe
hospitali.Alimkuta Agatha tayari
amekwisha hudumiwa na alikuwa
amelazwa katika chumba
maalum.Wakatazama kwa muda wa
sekunde kadhaa kisha Ernest akasema
“Pole sana Agatha.Unajisikiaje hivi
sasa?
“Ahsante sana.Ninaendelea
vyema.Vipi wewe unaendeleje
“Hata mimi ninaendelea
vizuri.Nini hasa kilichotokea.Ulikuwa
wapi? Ernest akauliza
“Ernest tutazungumza nikitoka
hapa.Kuna mambo makubwa na mazito
ambayo nataka tuzungumze ” akasema
Agatha
“Ukiruhusiwa kutoka hospitali
,are you coming back home? Akauliza
Ernest.Macho ya Agatha yakajaa
machozi kwa swali lile alilouliza Ernest
“Ernest nafahamu nimekufanyia
mambo mengi mabaya na sistahili hata
kuwa mke wako lakini I have no where
to go so I’ll be coming back home.I’m so
sorry Ernest for everything” akasema
Agatha huku akilia.Ernest naye akahisi
kitu Fulani cha tofauti akaguswa na
machozi yale ya mke wake
akamsogelea pale kitandani akamfuta
machozi
“Usilie Agatha.Huu si wakati wa
kulia.Ni kweli mambo yaliyotutokea ni
mengi na haupaswi kuendeleza
magomvi.Huu ni wakati wa kuungana
tena na kuendeleza nchi yetu” akasema
Ernest kwa sauti ya upole
“Ahsante sana Ernest” akasema
Agatha.Wakaagana na Ernest
akaondoka.
“Haya ni maajabu
makubwa.Mbona Ernest amebadilika
namna ile? Si Ernest Yule ambaye
nilikuwa nalumbana naye siku mbili
tatu zilizopita.Amekuwa mpole na
mwenye huruma.Inawezekana hizi
zikawa ni nguvu alizonipa baba Alberto
mkuu zinafanya kazi yake” akawaza
Agatha
“Agatha alikuwa wapi?Alisalimika
vipi katika tukio lile?Nani
kamshambulia?Haya yalikuwa ni
maswali yaliyojirudia kichwani kwa
Ernest Mkasa akiwa njiani kurejea
ikulu baada ya kutoka kumtazama mke
wake Agatha aliyelazwa katika
hospitali ya Kobwe.
“Imenilazimu niwe mpole ili
nifahamu kitu anachokifahamu
kuhusiana na shambulio lile.Hata yeye
kuna jambo anataka kunieleza.Nitajua
nini cha kumfanya baada ya
kumsikiliza lakini lazima naye
nimuondoe.Ni mdudu hatari sana Yule
ambaye hatakiwi kupewa nafasi
kabisa” akawaza Ernest
“Sasa mambo yangu yanaanza
kwenda vizuri.Agatha amepatikana na
ninaamini kule Congo hivi sasa akina
Austin watakuwa wamekwisha zuiliwa
kwa hiyo uhakika wa kuipata hati ya
muungano ni mkubwa
sana.Kitakachofuata baada ya kuipata
tena hati ya muungano nitafanya
makubaliano mapya na Alshabaab na
nitawalipa kitu kingine lakini si Yasmin
wala hati ya muungano kama
walivyotaka awali.Yasmin anatakiwa
kurejeshwa katika lile
gereza.Halikadhalika Austin na kundi
lake kama hawatauawa basi nao
wanapaswa kuingia katika gereza lile
na kuishi humo kwa maisha yao yote
yaliyobaki.Kidogo sasa ninaweza
kupumua kwani nchi iko
salama.Hakuna Alberto’s tena na sina
hakika kama watathubutu tena kutaka
kupenyeza mizizi yao Tanzania kwa
hiki nilichowafanyia.Japokuwa kwa
sasa amegeuka adui yangu lakini
napaswa kushukuru Austin kwa kunipa
ujasiri wa kuweza kupambana na
Alberto’s.Kwa muda mrefu nilikuwa
natamani sana kupambana na Alberto’s
lakini sikuwa na ujasiri wa kufanya
hivyo hadi alipotokea yeye na kunipa
ujasiri na nimefanikiwa kuwasafisha
wote.Mimi na yeye tulianza vizuri sana
na sijui kitu gani kimetokea kati kati ya
safari yetu na kutufanya maadui
wakubwa.Amenisaidia kufahamu kama
Monica ni mwanangu na nitamshukuru
kwa hayo lakini siwezi kumpa nafasi ya
kuniharibia mipango yangu.Pamoja na
hayo yote aliyonifanyia lakini lazima
safari yake ikaishie kwenye lile
gereza.Ni mtu hatari sana kumuacha
huru yeye na wenzake na hasa Yule
Job.Akigundua kwamba mimi ndiye
mwenye uhusiano na mke wake
Monalisa atanitafuna nyama Yule jamaa
kwani hata sura yake inaonyesha
ukatili mkubwa.” Mara rais
akakumbuka kuhusu Monalisa
“Monalisa anataka kuja Dar es
salaam kuhudhuria msiba wa Bill.Hili ni
jambo la hatari anataka kulifanya lakini
siwezi kumzuia kwani amekwisha
dhamiria.Ninachopaswa kufanya ni
kutuma ndege kesho asubuhi kwenda
kumchukua kule Arusha na kumpa
ulinzi wa kutosha.Hakuna mtu yeyote
kumsogelea na kesho jioni anatakiwa
kurejea haraka sana Arusha.Sitaki akae
hapa dar kwa muda mrefu kwani
anaweza akakutana na yule jamaa.Hili
suala natakiwa kulipa uzito mkubwa
pia kwani nikilipuuzia linaweza kuwa
na madhara makubwa huko
mbeleni.Nampenda mno Monalisa na
nina mpango wa kuishi naye pindi
nikimaliza uongozi.Yule shetani Agatha
siku zake zinahesabika” akawaza
Ernest
 
QUEEN MONICA: FINAL SEASON

SEHEMU YA 10

Job alifika eneo ambalo
alielekezwa na Mukasha waonane.Gari
kadhaa zilikuwa zimeegeshwa nje ya
kiwanda kikubwa cha mikate.Job
akaichukua tena simu ya silva
akamuandikia ujumbe Mukasha
“Tayari nimefika hapa naziona
gari kadhaa zimeegeshwa .Uko sehemu
gani? Akautuma ujumbe ule na baada
ya muda ujumbe wa majibu ukarejea
“Kuna Toyota harrier rangi nyeusi
imeegeshwa karibu na duka la madawa
niko humo”
Job akaendesha gari taratibu
akaliona gari lile aliloelekezwa na
Mukasha akasimamisha gari nyuma
yake halafu akashuka na bastora yake
ikiwa mkononi akaliendea lile gari la
Mukasha.Alikuwa amevaa kofia
kichwani iliyoufunika uso
wake.Akaufungua mlango wa mbele wa
gari akaingia ndani na kuufunga na bila
kumtazama usoni Mukasha akawasha
gari na kuondoka eneo lile
“Mambo yanakwendaje Silva?
Akauliza Mukasha.
“It’s good to see you again Wilson
Mukasha”
Laiti kama gari lile lingekuwa wazi
Mukasha angeweza kuruka baada ya
kusikia sauti ile.Alitetemeka mikono na
gari likayumba.
“Usiogope Mukasha mimi na wewe
ni marafiki na hatuwezi
kukimbiana.Wanasema milima
haikutani na binadamu hukutana,na
sisi baada ya kupotezana kwa siku
kadhaa hatimaye tumekutana tena”
Akasema Job huku akicheka
kidogo.Mukasha akasimamisha gari
alishindwa kuendesha kwa mstuko
alioupata
“Unahitaji nini toka kwangu wewe
kijana? Lini utaniacha huru na maisha
yangu? Akauliza Mukasha.Job
akatabasamu na kusema
“Geuza gari turudi tulikotoka,
mimi na wewe tuna maongezi ya
muhimu sana leo” akasema
Job.Mukasha akabaki ameduwaa
akimtazama job
“Mukasha endesha gari.!!
Akasema Job na Mukasha akageuza gari
na kurudi walikotopka.Walikwenda
hadi mahala Job alikoacha gari lake
wakashuka na kuingia katika gari la Job
wakaondoka
“What do you want from me ?
Mukasha akauliza
“Usihofu Mukasha sintakuondoa
tena sikio la pili.Safari hii nimekuja
kirafiki.Nahitaji sana kuzungumza na
wewe.Kuna mambo mimi na wewe
tunaweza kukubaliana bila kutumia
nguvu kwa hiyo usiogope” akasema Job
na baada ya mwendo wa kama dakika
kumi hivi akaegesha gari katika klabu
moja ya usiku akamtaka Mukasha
washuke wakaingia klabuni wakatafuta
meza wakakaa.
“Mukasha nafahamu mimi na
wewe hatupikwi chungu kimoja lakini
safari hii sijaja kwa shari.Nahitaji
msaada wako na mimi pia nikusaidie”
akasema Job na kumstua Mukasha
“Unahitaji msaada wangu? Msaada
gani unahitaji? Akauliza
“Nimepata taarifa kwamba dogo
Bill amefariki dunia.Yule pekee ndiye
aliyekuwa anafahamu mahala alipo
mke wangu Monalisa na mwanangu
Millen.Kwa sasa nimekwama na sina
mwanga wowote wa kufahamu familia
yangu ilipo.Nataka unisaidie niweze
kuwafahamu walipo” akasema Job
“Job nilikwisha kueleza toka awali
kwamba sifahamu mahala familia yako
ilipo.Aliyekuwa akifahamu mahala
walipo ni Bill pekee na kama amefariki
hakuna anayejua.Ninachofahamu mimi
ni kwamba Bill alikuwa anatumwa na
mtu mmoja anaitwa Don ambaye sisi
sote hatumfahamu.Aliyekuwa
akimfahamu ni Bill peke yake.”
Akasema Mukasha
“Sikiliza Mukasha,nataka
nikusaidie.Nafahamu sasa hivi
mahusiano yako na rais si mazuri na
uko mafichoni.Nitakusaidia kwanza
kwa makazi ili wewe na familia yako
muwe salama na pili wewe na sisi
tunaweza kuwa shirika moja na
tukafanikiwa kumuondoa Ernest Mkasa
madarakani na wewe ukawa huru.Bila
Ernest kuondoka madarakani na
kushtakiwa kwa mambo maovu
aliyoyafanya utaendelea kuwa
mkimbizi .Kwa hiyo kama una chochote
unachokifahamu kuhusiana na familia
yangu nieleze tafadhali” akasema Job
Maneno yale yakaonekana
kumwingia Mukasha akainama kwa
muda akatafakari kisha akasema
“Una hakika na hayo maneno
unayoyasema? Akauliza Mukasha
‘”Nina uhakika mukasha na ndiyo
maana nikakwambia kwamba safari hii
sijakutafuta kwa ugomvi ila nataka
mimi na wewe tushirikiane” akasema
Job
“Kabla hatujaendelea mbele
nataka kufahamu kuhusiana na Daniel
Swai.Umetumia simu yake kuwasiliana
nami .Where is he? Akauliza
“He’s dead”
“What ?!! he’s dead?
“yes.He’s dead.I killed him”
akasema Job
“He was a traitor na kwangu
msaliti yeyote hana nafasi hivyo
nikamuua.Forget about him.Tujadili
kilichopo mbele yetu sasa hivi”
akasema Job
“Taarifa ambayo Daniel alitaka
kukuuzia ameitoa kwangu kwa hiyo
hakijaharibika kitu ukihitaji taarifa
hiyo utaipata” akasema Job.Mukasha
alionyesha woga mkubwa
“Tell me Mukasha are you going to
help me or not? Akauliza Job.Mukasha
akafikiri kidogo na kusema
“Kuna mtu mmoja anaitwa Abdu
Chizo.Huyu ni rafiki na mtu wa karibu
sana wa Bill.Tukimpata huyu anaweza
akafahamu chochote kuhusiana na mke
wako”
“Anapatikana wapi huyo Abdu
Chizo?
“Huyu kumpata kwa usiku huu si
rahisi kwani ana ulinzi mkali
sana.Nafahamu nyumbani kwake na
tunaweza kwenda asubuhi ila
nitaonana naye mimi peke yangu kwani
hataki watu asiowafahamu nyumbani
kwake” akasema Mukasha
“Hatuwezi kusubiri hadi
asubuhi.Tunakwenda usiku huu”
akasema Job
“Job unapaswa
kunisikiliza.Unahitaji msaada wangu so
let me help you my way.Ukitaka tufanye
unavyotaka wewe katu hatutafanikiwa”
akasema Mukasha.Job akamtazama
kwa muda halafu akasema
“ Fine.We’ll do it your way !! but
tonight”akasema Job
“Haoana Job.Kesho asubuhi.Usiku
huu hakuna anayeruhsiwa kulikaribia
jumba lake” akasema Mukasha.Baada
ya muda Mukasha akasema
“Nitakusaidia kupata taarifa
unazozitaka lakini na mimi lazima
unitimizie kwanza mambo ninayotaka.”
Akasema Mukasha
“Unahitaji nini Mukasha? Akauliza
Job
“Usalama wa famila yangu.Rais
ananitafuta sana hivi sasa na japokuwa
nimejificha lakini siko salama.Nahitaji
familia yangu iende nje ya nchi
kujificha hadi hapo mambo
yatakapokuwa shwari.Nataka unisaidie
kwa hilo tafadhali”akasema Mukasha
“Hilo nitakusaidia lakini si jambo
la haraka kwani linahitaji
mipango.Ninachoweza kukusaidia kwa
sasa ni hifadhi ya familia yako.Wewe na
familia yako mtahamia katika nyumba
yangu na mtakuwa salama pale wakati
mipango mingine ikiendelea.Suala la
kuipeleka familia yako nje ya nchi kwa
wakati huu si suala jepesi na linahitaji
mchakato mrefu na itanilazimu
kuwashirikisha pia wenzangu ili
tulifanye kwa pamoja lakini ili
wenzangu wakubali kukusaidia
unatakiwa utusaidie kitu kimoja”
“Unahitaji niwasaidie kitu
gani?Mukasha akauliza
“Tunataka kukusanya ushahidi wa
kutosha kuhusiana na
Ernest.Tumegundua kwamba ana
mahusiano na haya mashambulio
yaliyotokea jana kwa hiyo tunafanya
uchunguzi ili kupata taarifa na ushahidi
wa kutosha na tumuondoe
madarakani.Wewe umekuwa ni mtu
wake wa karibu,mambo yake mengi
unayafahamu,siri zake nyingi unazijua
unaweza ukatusaidia kufahamu mambo
yake mengi yaliyojificha na sisi
tutakusaidia kwa hilo unalohitaji.Wewe
na familia yako mtakuwa salama na
tukifanikiwa kumuondoa Ernest na
kumfikisha mbele ya sheria wewe
utakuwa ni sehemu ya mchango huo na
hatutakugusa na tutakufanyia mpango
uende kuishi nchi nyingine
ukapumzike.” Akasema Job.
“Nitalifikiria hilo lakini kwa sasa
tuhakikishe kwanza familia yangu
inakuwa salama.Kitu kingine ni
kwamba ili kupata taarifa yoyote toka
kwa Abdu ni lazima niwe na
pesa.Nitakwenda kwake kwa kigezo
kwamba nataka tuzungumze biashara
na nikiwa na fedha ataniamini na
anaweza akanipa taarifa tunayoihitaji”
akasema Mukasha
“Ni kiasi gani unahitaji? Akauliza
Job
“Milioni thelathini zinaweza
kutosha” akasema Mukasha
“Thirty millions?!! Job akashangaa
“Ndiyo si fedha nyingi.Abdu ni
mfanya biashara mkubwa na huwezi
kumwendea ukasema kwamba anataka
mzigo wa laki mbili au tatu.Biashara
zake ni za mamilioni ya fedha.Lengo
hapa ni ili asiwe na mashaka yoyote
kwamba ninachimba taarifa”
“Ni vipi endapo hatakua
anafahamu chochote kuhusiana na mke
wangu? Pesa zetu zitakuwa zimepotea
bure? Akauliza Job
“Job hii ni pata potea.Lazima uwe
tayari kupata au kupoteza.Endapo
anaweza kufahamu chochote itakuwa
sawa kwetu lakini lazima tujiandae
kwamba yawezekana akawa hafahamu
chochote na hapo tutakuwa
tumepoteza.Unatakiwa utafakari na
ufanye maamuzi” akasema Mukasha
“15 millions.Sina zaidi ya hapo”
akasema Job
“Good.So whats next? Mukasha
akauliza
“Kinachofuata kwa sasa mimi na
wewe tunaogozana hadi nyumbani
kwangu,utalala pale na kesho tutaanza
mikakati yetu.Endapo tutafanikiwa
hiyo asubuhi kupata taarifa
ninazohitaji familia yako itahamia
nyumbani kwangu lakini kama
hutafanya juhudi nipate taarifa hizo
you’ll get nothing” akasema Job na
kumtaka Mukasha wainuke
waondoke.Wakaingia garini na
kuondoka
“Ulimwambia Irene adukue simu
ya rais.Nini ulikuwa unahitaji?Job
akamuuliza Mukasha na kumstua sana.
“Umemfahamuje Irene? Akauliza
Mukasha
“Usitake kujua nimemfahamuje
Irene.Just answer my question.Kwa nini
ulimtaka Irene adukue simu ya rais?
Ulikuwa unatafuta nini? Akauliza Job
“Niligundua mpango wa siri wa
kutaka kuniua.Siku ile usiku
uliponikata sikio nilipelekwa hospitali
nikalazwa.Baadae nikafuatwa na Bill
akanieleza kwamba rais amemtuma
anitafute na animalize.Kwa kuwa Bill
alikuwa kijana anayeniheshimu sana
akanisaidia nikatoka haraka pale
hospitali na kwenda
mafichoni,akamueleza Ernest kwamba
nimetoroka.Baada ya kugundua
kwamba rais ananitafuta aniue
nikataka kufahamu mipango yake na
njia pekee ya kufahamau
anachokipanga dhidi yangu ni kwa
kudukua simu yake kujua anaongea na
akina nani na ana mipango
gani.Umefahamuje jambo hili? Akauliza
Mukasha
“Irene aliniambia”
“Amekuambia?Ilikuaje
akakuambia mambo yale ya siri? Do
you know each other? Akauliza
Mukasha .Alishangaa sana
“Ilinimlazimu anieleze ukweli
wote wa kile alichokifanya kwani
ulichomuambia akifanye
kimemsababishia matatizo
makubwa.Hivi sasa hana makazi
anaishi nyumbani kwangu.Usiku huu
nimetoka kuwakomboa wazazi wake
waliokuwa wanashikiliwa mateka.Kuna
jambo aliligundua baada ya kuidukua
simu ya rais na hilo ndilo limemletea
matatizo makubwa ‘
“Oh my God ! what happened to
her? Amegundua jambo gani?Akauliza
Mukasha
“Jambo aliloligundua ni kubwa na
alifanya makosa akamtaarifu Agatha
mke wa rais na hapo ndipo matatizo
yalipoanzia.Agatha na Silvanus
Kiwembe wakawatuma vijana kwenda
kuwateka wazazi wa Irene wakamuua
mtumishi wa ndani na aliyemuokoa
Irene alikuwa Daniel.Ilikuwa bahati
Daniel akamleta kwangu na akanieleza
kilichomsibu.Usiku huu mimi na Daniel
tukaenda kuikoa familia yake na sasa
wako sehemu salama” akasema Job
“Kwa nini ukamuua Daniel wakati
mlikuwa wote katika kuiokoa familia
ya Irene? Akauliza Mukasha
“Daniel alikuwa msaliti na alitaka
kuuza siri zetu kwako na endapo
nisingemuua angeniua mimi.Wasaliti
wote hawana nafasi kwangu” akasema
Job na safari ikaendelea.
KINSHASA – DRC
“Thank you Austin.Sijawahi kuhisi
raha ya kufanya mapenzi kama usiku
wa leo.Sijui nikupe zawadi gani kwa
furaha niliyonayo ya kukutana na
mwanaume kama wewe
unayeyafahamu mapenzi kiasi
hiki.Maria alikosea sana alipotaka
kukuua.Mwanaume kama wewe
unapaswa kulindwa kwa gharama
yoyote” akasema Amarachi wakiwa
wamelala katika zuria baada ya
kuanguka toka kitandani kutokana na
kipute kuwa kikali sana.Austin
akamtazama Amarachi aliyekuwa
mtupu akahisi mwili bado
unamsisimka.Akatabasamu na kusema
“Amarachi kilichotokea hapa
chumbani kitabaki hapa hapa
chiumbani.Hatakiwi kufahamu mtu
mwingine yeyote na wala hatupaswi
kuendelea” akasema Austin
“Austin vyovyote utakavyoamua
ila ukweli utabaki pale pale kwamba
sijawahi kukutana na mwanaume kama
wewe.Nilitekwa na Boko haramu
nikiwa bado mwanafunzi na
kilichokuwa kinafanyika kule msituni
si mapenzi bali ni ubakaji ila leo
nimefanikiwa kufanya mapenzi ila
Austin nina ombi moja kwako”
Akasema Amarachi
“Unataka nini Amarachi?
“Kama mambo haya yatamalizika
na wote tukawa salama naomba
tutafute nafasi walau siku kadhaa mimi
na wewe tuende mahala
tukapumzike.Please dont say no”
akasema Amarachi na Austin
akatabasamu akamvuta Amarachi
kifuani pake akambusu na kusema
“Amarachi sitaki nikuahidi kitu
ambacho siwezi kukitekeleza.Pindi
masuala haya yakimalizika nitapotea
na kwenda kuanza maisha yangu
mapya mbali.I want to try again but far
from here kwa hiyo siwezi kukuahidi
kwamba ninaweza kupata nafasi ya
kupumzika na wewe”akasema Austin
“Austin you’ll go with me!!.Kokote
utakakokwenda I’ll be with you.You
cant live me behind.Ninahisi
amani,salama na furaha nikiwa karibu
nawe kwa hiyo ulipo nami nipo.Potelea
mbali utakavyofikiri kuhusu mimi
lakini siwezi kukubali ukaniacha.Take
me wherever you go.I’ll be your
maid,your slave your
everything”akasema Amarachi.
“Sijawahi kukutana na mwanamke
aliyenitamkia maneno mazito kama
haya.Amarachi nashindwa nikujibu nini
lakini ukweli ni huo kwamba you’ll
never be happy with me,you’ll never
have a normal life and you’ll never be
safe kwa hiyo nakuomba Amarachi
jitahidi kuendelea na maisha yako
nchini Tanzania .You are very happy
there” akasema Austin
“Ndiyo nina furaha lakini
nitakuwa na furaha zaidi endapo
nitakuwa karibu yako.Austin hakuna
neno unaloweza kulitamka likanibadili
mawazo.Tayari nimekwisha fanya
maamuzi.Niko tayari kwa chochote iwe
ni shida iwe ni raha niko tayari kwa
yote lakini lengo langu ni moja tu kuwa
karibu nawe” akasema Amarachi
.Wakatazama kwa muda Amarachi
akauliza
“Do you still love her? Akauliza
Amarachi
“Nani?
“Maria”
“I loved her with all my heart na
siwezi kusema kwamba tayari
nimekwisha mtoa moyoni mwangu
kabisa kwani hili jambo litachukua
muda.Mimi na yeye tulifikia hatua
kubwa sana but I have to let her
go.Hata kama bado ninampenda lakini
mimi na yeye hatuwezi kuwa pamoja
tena.It’s over” akasema Austin
“Amarachi tulale sasa na tujiandae
kwa siku ya kesho.” Akasema Austin
“Austin japo kwa usiku wa leo
naomba nikilaze kichwa changu katika
kifua chako” akasema Amarachi.Austin
akambusu Amarachi ambaye alikilaza
kichwa chake katika kifua cha Austin
taratibu machozi ya moto yakaanza
kukiloanisha kifua cha Austin
“Amarachi unalia nini? Akauliza
Austin
“It’s nothing.Let’s sleep” akasema
Amarachi
“kwa miaka mingi nimekuwa na
ndoto ya kumpata mwanaume mwenye
kunifaa na sasa nimempata Austin
lakini hayuko tayari kuwa na mimi
kwani ameumizwa sana na mahusiano
yake yaliyopita.What am I going to do?
akajiuliza
“Siwezi kumkosa Austin.Huyu ni
mwanaume wangu na ninaamini
kukutana kwetu hakukuwa kwa
makosa.Lazima nihakikishe ninafanya
kila juhudi kumpata.He must be
mine.I’m a fighter na sijawahi kukata
tamaa katika jambo lolote lile na siwezi
kushindwa kupambana kwa ajili ya
Austin.Sintojali kama kuna hatari au
vipi lakini lazima nihakikishe mwisho
wa sakata hili niwe nimempata Austin”
Akawaza Amarachi
“Monica aliwahi kuniambia siku
moja kwamba kuna kitu anakiona kati
yangu na Amarachi.Alinisistiza kwamba
nifanye kila ninaloweza kuwa na
Amarachi kwani ndiye mwanamke
anayenifaa.Naweza kukiri kwamba
alikuwa sahihi.Kweli kuna kitu kipo
kati yetu na leo hii nimethibitisha
hilo.Tulipofanya mapenzi kuna kitu
nimekiona.Nimejisikia hali ya tofauti
ambayo haijawahi kunitokea hapo
kabla.Ninatamani hiki ninachokihisi
kingekuwa kweli lakini siwezi kuingia
katika mahusiano na Amarachi
japokuwa ni mwanamke mwenye sifa
zote na anaonekana tayari ananipenda
japokuwa hajaniambia ila vitendo tu
vinanipa picha kwamba
ananipenda.Sitaki kumuingiza mtoto
mzuri kama huyu katika dunia yangu
na kumfanya aishi maisha ya taabu
yasiyo na furaha.Watu kama mimi
hatuna maisha ya kawaida yenye
furaha.Nimejaribu hilo nikashindwa na
sitaki kumuingiza Amarachi katika
matatizo.Ameteseka sana msituni na
anastahili mwanaume ambaye atampa
furaha anayoitaka na si mimi.Nitajaribu
kuendelea kumuelewesha”akawaza
Austin huku akizichezea nywele za
Amarachi
“Laiti ningekuwa na maisha ya
kawaida naamini Amarachi angenifaa
sana lakini sina maisha ya kawaida
kama wenzangu.Maisha yangu
yamekuwa hivi hivi kutwa kucha mikiki
mikiki.Kama ilishindikana kwa Maria
haitawezekana kwa mwanamke
mwingine tena” Austin akajawa na
mawazo mengi sana kuhusiana na
mustakabali mzima wa maisha yake
.Alikumbuka maisha yake ya nyuma
yalivyokuwa na alipo sasa na taratibu
akahisi kijiusingizi kikimnyemelea
akaanza kusinzia
DAR ES SALAAM - TANZANIA
Kumepambazuka tena
Tanzania.Tayari mitaa na barabara
zilijaa watu alfajiri hii wakiwahi katika
majukumu ya kujitafutia mkate wa kila
siku.Bendera bado ziliendelea kupepea
nusu mlingoti kutokana na siba mzito
uliolIkikumba taifa.Ikulu Dar es salaam
Ernest mkasa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania alidamka
mapema sana akijiandaa kwa ajili ya
safari yakuelekEa Dodoma ambako
miili ya viongozi wote waliopoteza
maisha katika mashambulio
yaliyotokea katika miji ya Dar es
salama na Dodoma itaagwa kitaifa na
kuzikwa.Kitu cha kwanza alichoamua
kukifanya rais asubuhi na mapema ni
kwenda hospitali kutazama hali ya
Agatha mke wake.
“Nashangaa asubuhi hii ninajikuta
nina hamu ya kwenda kumuona
Agatha.That woman is a
witch.Sikupanga kabisa kwena
kumtazama hospitali shetani yule
lakini ngoja nikamtazame nijue
maendeleo yake.Ngoja nijiweke karibu
yake na pengine anaweza kuwa na
jambo la muhimu la kunieleza.Nataka
nifahamu ni namna gani alinusurika
katika shambulio lile? Nitapata taarifa
hizo endapo nitajiweka karibu naye na
kuonyesha kumjali” akawaza Ernest.
Akiwa njiani kuelekea hospitali
akapata taarifa toka kwa mkuu wa
polisi kwamba imeokotwa maiti ya
mkuu wa idara ya usalama wa taifa
Silvanus Kiwembe katika bustani ya
wanyama iliyoko nje kidogo ya jiji la
Dar es salaam.Taarifa hiyo ilisema
kwamba Silvanus aliuwa kwa kupigwa
risasi zaidi ya nane.Sambamba naye
walikuwepo watu wengine kadhaa
waliokutwa wamekufa kwa kupigwa
risasi na mmoja kati ya watu
waliokwisha tambulika ni Daniel Swai
mtoto wa mfanyabiashara
mkubwa.Rais alitaarifiwa kwamba mtu
mmoja aliyejitambulisha kama daktari
anashikiliwa na jeshi la polisi kwa
mahojiano baada ya kukutwa eneo la
tukio akiwa amefungwa miguu na
mikono na kujazwa matambara
mdomoni.Jeshi la polisi pia
linawashikilia walinzi wa bustani hiyo
kwa ajili ya kusaidia katika uchunguzi.
Hizi zilikuwa ni taarifa mbaya kwa
rais Ernest asubuhi hii ambazo
zilimstua mno
“Nani kamuua Silva? Alikwenda
kufanya nini katika bustani ya
wanyama usiku ? akajiuliza.
“Japokuwa alikuwa ni mfuasi wa
Alberto’s lakini alikuwa ni mtu
niliyemuhitaji sana hasa kwa kipindi
hiki ili kusafisha hali ya mambo.Nani
nitampata ambaye atakuwa upande
wangu na kutii maelekezo yangu?
Akajiuliza
“Nimeumizwa sana na taarifa hizi
za kumpoteza Silva.Sijui nani nitampata
anayeweza kuziba nafasi yake kwa
haraka.Laiti nisingekuwa nimemuweka
Austin katika orodha ya maadui zangu
ningemteua awe mkuu wa idara ya
usalama wa taifa kwani anafaa sana
lakini mambo yamekwisha
haribika.Ngoja nimpigie simu David
Zumo nijue kama alifanikiwa
kuwakamata na kuwaweka kizuizini
Austin na wenzake” akawaza Ernest na
kuchukua simu akampigia David Zumo
“Habari za asubuhi mheshimiwa
rais Ernest” akasema David Zumo
baada ya kupokea simu
“Huku kwema kabisa sijui huko
kwenu” akasema Ernest
“Huku kwema tumeamka salama.”
“David samahani kwa usumbufu
asubuhi hii.Nimekupigia simu
kufahamu kuhusu ule msaada
niliokuomba jana.Je ulifanikiwa
kuwatia kizuizini wale watu? Akauliza
Ernest
“Ernest naomba suala hilo
tulizingumze baadae kidogo kwani kwa
sasa niko katika maandalizi ya mazishi
ya mke wangu .Nitafute baadae jioni ili
tuzungume kwa kirefu zaidi suala hili”
akasema David
“Mheshimiwa rais nafahamu leo ni
siku ngumu sana kwako na hata
kwangu pia kuna mazishi ya kitaifa kwa
wale watu waliouawa katika
mashambulio yale mawili.Ninataka tu
kufahamu kama tayari umewatia
ngvuni ili niwe na cha kuwaambia
watanzania hapo baadae
nitakapohutubia katika mazishi ya
kitaifa.” Akasema Ernest.David Zumo
akabaki kimya.
“David tafadhali nahitaji
kufahamu hilo tu halafu tutazungumza
jioni sote tutakapokuwa
tumetulia.Tafadhali ni muhimu sana
“akasema Ernest
“Wale watu hawako kizuizini”
akasema David
“ What ?!! hawako kizuizini? Kwa
nini David wakati nilikutaarifu kwamba
watu wale ni hatari na wanahusika
katika mashambulizi yaliyotokea
katika miji ya Dar es salaam na
Dodoma?Kwa nini umewaachia huru?
Akauliza Ernest kwa sauti ya ukali
“Sikiliza Ernest.Watu wale
nimewashikilia kama ulivyoniomba
lakini nililazimika kuwahoji mimi
mwenyewe na baadae nikajiridhisha
kwamba watu wale hawakuwa hatari
na wala hawakuhusika katika
mashambulio yale ya Dar es salaam
wala Dodoma.Ninadhani taarifa
ulizopewa na watu wako wa usalama
hazikuwa sahihi.Wasisitize watafute
watu sahihi na si wale hawahusiki
kabisa “
“My God!! Akasema Ernest
“Wako wapi hivi sasa?akauliza
“Kwa hivi sasa siwezi kufahamu
wako wapi kwani waliomba ruhusa ya
kuendelea na sfari na nikawaruhusu
waendelee na safari yao na sijui
wameelekea wapi ” akasema David
Zumo
“David umefanya kosa kubwa sana
kuwaachia wale jamaa ambao sisi
tunafahamu na tunamini kwamba ni
watu hatari sana kwa usalama wa nchi
yetu na wanahusika katika
mashambulizi yale ya mabomu.Naomba
nikuache kwa sasa ila nitakupigia simu
baadae jioni tuongee zaidi.Naomba
ufahamu kwamba sijafurahishwa na
kitendo ulichokifanya kwani
umeshindwa kumsaidia rafiki yako
wakati ana shida.Kwa heri kwa sasa”
akasema Ernest na kukata simu kwa
hasira
“Oh my God !! mambo gani haya
yananitokea? Mbona siku imeanza
vibaya namna hii? Kwa nini David
anifanyie hivi wakati nilimuomba na
tukakubaliana vizuri kabisa na
akaahidi kuwakamata akina Austin.I’m
confused.Sielewi nitafanya nini
kuwapata tena.They are gone.Hati ya
muungano imekwenda na Tanzania
imekwenda.!! Akawaza
“Zote hizi ni jitihada za
Austin.Anamtumia sana Monica na
ndiyo maana wamefanikiwa hadi
kumrubuni David Zumo.Je ni kweli
amewafanyia mahojiano kama
anavyodai? Kama amewafanyia
mahojiano ni wazi lazima watamueleza
ukweli na David akiufahamau ukweli
itakuwa mbaya sana kwa upande
wangu.Nitafanya nini kuliweka sawa
jambo hili? Akawaza
“Hakuna nman ninatavyoweza
kuliweka sawa suala hili bila kuipata
hati ya mungano.Suala hili tayari
limevuka mipaka na linahitaji hatua za
haraka sana kabla halijasambaa na
kuniletea mimi matatizo
makubwa.Ninaheshimika na marais wa
nchi zote za Afrika na endapo
watagundua kwamba nimehusika
katika kupanga mashambulizi yale sijui
nitaiweka wapi sura yangu.Lazima
nichukue hatua za haraka sana kwani
nikiliacha suala hili litanishinda na kila
nilichokifanya kitakuwa hakina
maana.” Akaendelea kuwaza rais
“Nilimlaumu bure Jenerali Lameck
kwa mpango wake wa kutaka kuilipua
ndege ile kabla haijavuka mpaka wa
Tanzania lakini ulikuwa ni mpango
mzuri.Ni bora ndege ile ingelipuliwa
angani na kuwaua wote waliokuwamo
mle ndani .Sioni tena faida ya Monica
kwani ni kwa sababu yake haya yote
yametokea.Austin amegundua udhaifu
wangu uko kwa Monica na anamtumia
kama fimbo ya kunichapia.Nikiendelea
na udhaifu huu nitajikuta pabaya
sana.Kuanzia sasa Monica naye
ninamjumuisha katika orodha ya wale
watu wangu wa hatari kwa kuwa
amechagua mwenyewe kujiunga na
akina Austin.Hali ilikofika si kuzuri na
siwezi tena kukubali Monica atumike
kunibomoa.Nitambomoa yeye kabla
lengo lake na wenzake halijatimia”
“Mzee tumefika” ilikuwa ni sauti
ya mlinzi wake aliyemtaarifu rais
kwamba tayari wamefika
hospitali.Kutokana na mwazo mengi
aliyokuwa nayo hakukumbuka kama
walikuwa wamewasili
hospitali.Alishuka na kuingia katika
chumba alicholazwa mke wake.
“Vipi Agatha unaendeleaje? Ernest
akamsalimu mkewe
“Ninaeendelea vizuri.Vipi wewe
unaendeleaje?Mbona naona kama
hauko katika hali yako ya kawaida?
Akauliza Agatha lakini Ernest
hakumjibu kitu
“Una tatizo gani Ernest? Tafadhali
nieleze nifahamu pengine ninaweza
kukusaidia hata kimawazo” akasema
Agatha.Ernest akawatoa nje walinzi
akabaki peke yake na Agatha.
“Silva na watu wengine kadhaa
wamekutwa wamekufa katika bustani
ya wanyama nje ya jiji” Ernest
akamwambia Agatha
“Umapata wapi taarifa hizo?
Akauliza Agatha
“Nimepigiwa simu asubuhi hii na
mkuu wa polisi.Hizi nitaarifa mbaya
sana ambazo sikuwa
nimezitegemea.Ninajiuliza Silva
alikwenda kutafuta nini kule katika
bustani ya wanyama usiku? Nani
kamuua? Nimechanganyikiwa Agatha”
akasema Ernest
“Ernest nimeambiwa na
madaktari kwamba jioni ya leo
ninaweza kuruhusiwa kurejea
nyumbani.Nikitoka nitakuja kukusaidia
katika wakati huu mgumu ulio
nao.Unahitaji mtu wa kukusaidia na
ninakuomba unipe nafasi
nikusaidie.Nafahamu mimi na wewe
tuna tofauti zetu lakini naomba
tuziweke tofauti pembeni kwa sasa na
tuunganishe nguvu.Ernest mimi ni mke
wako na unapaswa kuniamini kuliko
mtu mwingine yeyote.Kuna mambo
mengi yanayoendelea hivi sasa ambayo
huyajui.Kuna mambo ninayafahamu
ambayo ni ya hatari kwako.Nipe nafasi
nikusaidie na kwa pamoja tuweze
kulimaliza suala hili linaloendelea”
akasema Agatha
“Agatha nashukuru kwa kujali
matatizo niliyonayo lakini its hard to
trust you again.Mambo uliyonifanyia
yananifanya nishindwe kukuamini
tena. Usijali ninao watu wa kutosha wa
kulishughulia suala hili.Wewe
unapaswa upumzike” Akasema rais
Ernest na kumtazama Agatha aliyetaka
kusema kitu lakini kabla hajatamka
akamuwahi
“Leo ni mazishiya kitaifa ya wale
wote waliouawa katika mashambulio
yale kwa hiyo muda mfupi ujao
nitaelekea Dodoma na baada ya
shughuli ya kuaga miili ya wabunge na
viongozi mbali mbali nitaelekea
Zanzibar kwa ajili ya kuongoza mazishi
ya makamu wa rais.Nitakuwa na siku
ndefu sana.Utakapo ruhusiwa kutoka
hospitali utaenda moja kwa moja ikulu
na utanisubiri hadi nirudi” akasema
Ernest
“ Ahsnate sana Ernest kwa kuja
kunitembelea.Kuna jambo moja nataka
nikuombe.Kuwa makini sana na watu
unaofanya nao kazi.Kuna watu
wanakuzunguka” akasema Agatha na
kumstua Ernest
“ Kwa nini unasema hivyo Agatha?
“Kuna jambo kubwa
tutazungumza jioni ukirejea”akasema
Agatha na Ernest akaondoka kurejea
ikulu
“Kuna kitu kikubwa Agatha
anakifahamu na ili kukijua natakiwa
kuendelea kujiweka karibu
yake.Ameniomba nimuamini na
kumshirikisha katika mambo yangu
lakini siwezi kufaya hivyo hata
kidogo.Yule mwanamke ni shetani na
hafai kabisa kuwa na ushirika naye
wowote.Ninajifanya kuwa karibu naye
na kumjali ili nifahamu kile ambacho
anakifahamu kuhusiana na shambulio
lile na alinusurika vipi? Nikifahamu
hayo nitamuondoa haraka
sana.Hatakiwi kuendelea kuwa hai yule
mwanamke” akawaza Ernest
“Ernest kabadilika
sana.Nitajiweka karibu nami kujifanya
nimebadilika ili aweze kuniamini tena
na baada ya kuniamini nitaanza awamu
ya pili ya kuotesha upya mbegu ya
Alberto’s hapa Tanzania kwani mimi
ndiye niliyepewa jukumu hilo” akawaza
Agatha na kuyakumbuka maneno ya
Alberto mkuu aliyomwambia
alipompigia simu usiku wa jana.
“Usiku kucha nimekuwa
ninalifikiria jambo lile alilonieleza baba
Alberto mkuu jana.Kuwa kiongozi wa
Alberto’s si jambo dogo na hasa kwa
nchi yenye changamoto nyingi kama hii
lakini sina namna ya kufanya kwani
tayari nimekwisha muhakikishia
Alberto mkuu kwamba nitaifanya kazi
aliyonipa.Kwa sasa ngoja njiweke
karibu na Ernest ili kulifanikisha jambo
hili” akaendelea kuwaza
Ernest Mkasa alifika ikulu na mtu
wa kwanza kuonana naye alikuwa
Jenerali Lameck Msuba ambaye aliwahi
sana kufika.Kama kawaida yao
wakaenda katika chumba cha maongezi
ya faragha
“Lameck kuna habari yoyote mpya
umeipata? Akauliza rais
“ Hakuna habari yoyte mpya .Sijui
kwako”
“Ninazo habari kadhaa .Kwanza
Agatha amepatikana”
“ Amepatikana ? Alikuwa wapi?
“ Bado hatujazungumza ila
amejeruhiwa mguu kwa risasi na
amelazwa hospitali.Nimetoka
kumtazama asubuhi hii anaendelea
vyema.Baadae jioni nitapata nafasi ya
kuzungumza naye ili nifahamu
alinusurikaje katika shambulo
lile,alikuwa wapi na ani kamshambulia
jana”akasema Rais Ernest
“Do you trust her mr President?
Akauliza Lameck
“I don’t.Nimejiweka karibu naye
kwa sasa ili kufahamu hadithi yake
aliokoka vipi katika shambulio
lile?Baada ya kuisikia hadithi yake
tutatafuta namna ya kummaliza kwani
ni mtu hatari sana kwetu.Jioni ya leo
naamini atanieleza kila kitu na mimi
nitakujulisha atakachoniambia.”
Akanyamaza kidogo halafu akaendelea
“Jambo la pili ni kifo cha Silvanusi
Kiwembe.”
“Nimezipata taarifa hizi za kifocha
Silva nimestuka sana” akasema Lameck
“Hata mimi nimestuka
sana.Najiuliza imetokeaje? Alikwenda
kutafuta nini kule katika bustani ya
wanyama usiku? Nani kamuua na kwa
nini? Ninajiuliza maswali mfululizo
toka nilipopata taarifa hizi na sijapata
jibu.Kuna watu kadhaa tayari
wanashikiliwa na pengine
watakapohojiwa kuna kitu
kitapatikana.Lakini hili ni pigo kubwa
kwetu kwani alikuwa ni kiungo
muhimu sana .Alifanya kila kazi
aliyopewa bila kuhoji.Sijui tutampata
wapi mtu kama yule wa kushika nafasi
yake” Akasema Ernest
“Kweli ni pigo kubwa mheshimiwa
rais.Waliofanya jambo hilo la kinyama
lazima wapatikane haraka sana”
akasema Lameck
“Tukiachana na suala hilo la Silva
ambalo jeshi la polisi
wanalishughulikia ,kuna jambo lingine
ambalo limeifanya siku hii ianze vibaya
sana.”akasema rais na kunyamaza
akamtazama Lameck
“Ulikuwa sahihi kutaka kuilipua
ile ndege ya David Zumo.Ni afadhali
ndege ingelipuliwa na wote wakauawa
kuliko hiki kilichtokea.”
“Nini kimetokea mheshimiwa
rais?
“ David Zumo amewaachia akina
Austin na Yasmin wameenda zao”
“That’s not true!! Akasema
Lameck kwa mshangao
“Its true.Nimezungumza naye
asubuhi na amenieleza kwamba eti
aliwahoji na akaona hawana kosa lolote
akaamua kuwaachia wakaondoka zao
na hajui wameelekea wapi.Lameck hili
ni pigo lingine kubwa kwetu.Nilikuwa
na mategemeo makubwa kwa David
Zumo atawazuia akina Yasmin na
nilitegemea labda leo tungeweza
kuirejesha hati ya muungano lakini
imekuwa tofauti.Matumaini hayo
hayapo tena na sina hakika kama
tutafanikiwa kuipata tena hiyo hati
kwani hatujui sehemu ya kumtafutia
Yasmin.Ametuzidi akili.Ninajilaumu
sana kwa kupuuza ushauri wako na
kuziondoa zile ndege jana na yote haya
yamesababishwa na mapenzi makubwa
niliyonayo kwa Monica.Austin
ameugundua udhaifu wangu kuwa ni
Monica na anamtumia kufanikisha
mipango yake”akasema rais
“Hata mimi nimechanganyikiwa
mheshimiwa rais na sielewi tutafanya
nini kuwapata tena kama tayari
wamevuka Congo.Lakini kama
ulivyosema kwamba haya yote
yamesababishwa na Monica na
inawezakena hata Monica ndiye
aliyemshawishi David Zumo awaachie
huru akina Yasmin.Amefanya jambo
baya sana”
“Kwa hapa tulipofika imenilazimu
kufanya maamuzi magumu.Kushindwa
kwetu kumesababishwa na Monica kwa
hiyo naye anaingia katika orodha ya
watu hatari kwetu.Sintojali kama ni
mwanangu ama vipi lakini kuanzia sasa
hataonewa huruma hata kidogo na
kama tutalazimika kuua na yeye akiwa
miongoni mwa watu tunaotaka kuwaua
hakuna huruma ni kumuondoa
tu.Siwezi kujiharibia mwenyewe
sababu ya kumtetea mwanangu ambaye
hata hafahamu kama mimi ni baba yake
” akasema Ernest
“Lakini mheshimiwa rais
nilikutaarifu jambo hili mapema sana
na laiti kama ungelipa uzito unaostahili
tusingefika hapa tuipofika.”akasema
Lameck
“Uko sahihi Lameck.Ninajilaumu
sana kwa ujinga nilioufanya.Kwa sasa
inabid tuje na mikakati mipya namna
ya kufanya ila kuna jambo ninataka
kulifanya”akasema
“Ni jambo gani mzee?
“David Zumo anadai kwamba
amewahoji akina Yasmin na akagundua
kwamba hawana kosa na wala
hawahusiki kwa namna yoyote katika
mashambulio yale kwa hiyo
akawaachia huru.Nina wasi wasi
watakuwa wamemueleza David kila
kitu wanachokifahamu na hii itakuwa
mbaya zaidi kwetu.Nina wasi wasi sana
kwa namna David alivyokuwa
akizungumza kuna jambo tayari
amekwisha ambiwa kwa hiyo kuna kitu
kimoja tu ninakifikiria kifanyike”
“Ni kitu gani mzee? akauliza
Jenerali Lameck
“ Nataka kumuondoa David
madarakani”
Chumbani kukawa kimya
wakabaki wanatazamana.Baada ya
muda Lameck akauliza
“Utamuondoa madarakani kwa
kivpi mzee?
“Tutaiangusha serikali yake”
Jenerali Lameck akafikiri kwa
muda halafu akasema
“Mheshimiwa rais jambo hilo
ulilolitamka ni jambo zito sana na
utekelezaji wake si rahisi.David Zumo
ni rais mwenye ulinzi mkali mno.Licha
ya………….”
“Lameck bado tunao muda wa
kulijadili suala hili.Nimeona nikueleze
mapema ili kwa siku nzima ya leo
ufikirie njia mbali mbali tunazoweza
kufanya ili kumuondoa David
madarakani na jioni ya leo
tutakapokutana basi tutalijadili kwa
kirefu zaidi” akasema Ernest
‘Mheshimiwa rais lakini
ninakushauri jambo moja.Usifikirie
tafadhali kuanzisha mgogoro mwingine
mkubwa kwa kuiangusha serikali ya
David Zumo.Utaiingiza nchi katika
matatizo makubwa kuzidi hata haya
tuliyonayo sasa.Tutafute njia nyingine
ya kuweka sawa mambo yetu na kama
nchi inakwenda kugawanyika let it be
lakini si kuingia katika mgogoro na
David Zumo.Nakuomba sana mzee
lifikirie hilo jambo” akasema Jenerali
Lameck
“Lameck ushauri wako ni mzurio
lakini kwa hapa ilipofika hakuna
namna zaidi ya kumuondoa David
Zumo madarakani.Tutajadili baadae
jioni.Kwa sasa tujiandae na safari ya
kuelekea Dodoma” akasema rais na
wakatoka katika kile chumba.
“David Zumo lazima nimuondoe
madarakani.Pamoja na hili alilolifanya
la kuwaachia huru akina Yasmin lakini
sitaki kabisa awe na ukaribu na
mwanangu Monica ambaye tayari
amempa mimba kwa hiyo lazima
nihakikishe ninampoteza.Sitaki damu
yangu ichanganyike na ya David
Zumo….” Akawaza rais Ernest na
kusimama kidogo baada ya simu yake
kuita.Akatazama mpigaji akastuka na
kuipokea.
‘Hallow naomba unipe dakika tatu
nitakupigia” akasema rais na kuikata
ile simu
“Mambo yameanza.Habib anataka
kunieleza nini? akawaza
Alistuka sana kwa simu ile ya
Habib asubuhi ile.Haraka haraka
akaelekea chumbani kwake
“Habib Amenistua sana.Najua
atauliza kuhusu akina Yasmin na mimi
sina jibu la kumpa” akawaza na kuvuta
pumzi ndefu
“Ngoja nimpigie nisikie
anachokitaka” akawaza na kumpigia
Habib
“Mheshmiwa rais habari za
asubuhi”akasema habib
“Habari za asubuhi nzuri ”akajibu
rais
“Mheshimiwa rais nimekupigia si
kwa kutaka taarifa za Yasmin au hati ya
muungano kwani najua ni uhuni
umenifanyia na hauko tayari kuitoa
hati hiyo.Nimekubali kushindwa katika
hilo lakini kuna jambo nataka
nikueleze.Kuna mtu anakuja Tanzania
leo hii anaitwa Bashar bin
Abdulsalaam.Anakuja na ujumbe
mzito.Mpokee na uupokee ujumbe
anaokuja nao uufanyie kazi.Endapo
utaupuuza nchi ya Tanzania itaingia
katika vilio visivyokwisha.Kila nyumba
Tanzania italia machozi kwani
tutafanya mashambulio karibu kila siku
katika sehemu mbali mbali.Uwezo huo
tunao na wewe unalifahamu hilo na
tayari tumekwisha anza maandalizi na
hadi hivi nikwambiavyo Alshabaab
wako Tanzania na wanasubiri amri
yangu tu ili kutekeleza mashambulizi
kwa hiyo usitake tuiharibu
Tanzania.Fuata maelekezo katika
ujumbe utakaopewa na Bashar ili nchi
yako iwe salama” akasema Habib
“Habib tafadhali usijaribu
kunitisha.Unafahamu kabisa mimi
sipendi vitisho na jeshi langu linaweza
likawashambulia na kuwasambaratisha
kabisa kwa hiyo msithubutu kufanya
shambulio lolote katika ardhi ya
Tanzania!!
“Mheshimiwa rais nadhani
unatusikia tu na bado haujatufahamu
vyema.Ngoja nikuonyeshe kidogo tu
nguvu yetu.Nitakupigia tena baada ya
dakika kumi” akasema Habib
“Habib!! Habib !! akaita Ernest
lakini tayari simu ilikwisha katwa.
“Huyo mtu anayetumwa kwangu
anataka nini? Ni vipi endapo atakuwa
ametumwa kuja kuchukua hati ya
muungano? Ni vipi kama vitisho vya
Habib vikawa vya kweli na wakafanya
mashambulio mfululizo hapa Tanzania
na kuharibu hali ya amani na utulivu?
Akajiuliza
“Ninajuta kuwashirikisha watu
kama hawa katika mipango
yangu.Sikujua kama mambo yangefika
hapa yalipofika.Niliupuuza ushauri wa
Lameck aliyenisihi nisithubutu
kuwashirikisha Alshabaab kwani
madhara yake ni makubwa…”
Ghafla kikasikika kishindo
kikubwa cha mlipuko.Mlango wa
chumba cha rais ukapigwa na
makomando wanaomlinda rais
wakaingia na kumchukua rais
wakamkimbiza katika nyumba ya siri
inayotumika endapo kutatokea
mashambulizi yoyote katika jengo la
ikulu.Ernest Mkasa alikuwa
anatetemeka kutoka na ukubwa wa
kishindo kile
“Nini kimetokea? Akauliza.walinzi
wake hawakumjibu kitu kwani hata
wao pia hawakufahamu nini hasa
kilichotokea.
“Jamani niambieni nini
kimetokea? Akauliza tena lakini
hakujibiwa hadi alipofikishwa katika
nyumba ya siri iliyo chini ya jengo la
ikulu mahala ambako panaaminika ni
salama zaidi.Ernest
alichanganyikiwa.Baada ya dakika tano
akafahamishwa kwamba kumetokea
mlipuko unaosadikiwa ni bomu katika
soko la samaki la kimataifa lililo karibu
na ikulu.Taarifa hiyo ilisema kwamba
mlipuko huo ulioua watu kadhaa
ulitokea baada ya watu moja lililobeba
mlipuko kulikaribia gari lililokuwa
limebeba samaki na kuzingirwa na
watu wengi waliokuwa wananunua
samai hao.
“Oh my God !!! akasema rais
akajiinamia na kushika kichwa na mara
simu yake ikaita.Akatazama mpigaji
alikuwa Habib.Akawaomba watu wote
watoke mle katika chumba na
wamuache peke yake aongee na
simu.Aliitazama simu ile ikiita na
kukatika ikaanza kuita tena akaipokea
“Mheshimiwa rais nadhani tayari
umepata salamu zangu.Nimetaka
nikuonyeshe uwezo wetu .Kama
tumeweza kufanya shambulio karibu
kabisa na ikulu yako hatuwezi
kushindwa kushambulia sehemu
nyingine yoyote kwa hiyo tafadhali
sana usicheze na sisi.Mashambulio
kama haya yataendelea kutokea
sehemu mbalimbali za nchi yako na
mamia kwa mamia ya watanzania
watapoteza maisha kila uchao endapo
hautakuwa tayari kufanya kile
tunachokuamuru .Tafadhali mpokee
mjumbe anayetumwa kwako na
umsikie alichotumwa” akasema Habib
na kukata simu.Uso wa Ernest mkasa
uliloa jasho.
KINSHASA - DRC
Mlango wa chumba walimolala
akina Austin ukagongwa na
kuwastua.Tayari kumekucha.Austin
akajiinua kitandani na kwenda
kuufungua mlango akakutana na sura
iliyojaa tabasamu pana ya Monica
“Goodmorning .can I come in?
akasema Monica huku akicheka
kidogo.Austin akamkaribisha ndani.
“Mhh !! kulikuwa na shughuli pevu
humu ndani jana usiku” Akawaza
Monica baada ya kuona namna vitu
vilivyokuwa vimeparaganyika mle
chumbani .Amarachi akaamka baada ya
kusikia sauti ya Monica
“Monica;’akasema Amarachi
akionekana kuwa bado na usingizi
mzito.
“Goodmorning
Amarachi.Umelalaje?Are you
comfortable? Akauliza Monica
‘We’re fine.Ahsante sana kwa kila
kitu Monica” Akasema Austin
“Nimekuja kuwajulisha kuwa leo
ni mazishi ya Pauline Zumo mke wa
David Zumo kwa hiyo
nitahudhuria.Litakuja gari kunichukua
baadae saa tatu za asubuhi kuelekea
mahala shughuli za mazishi
zitakapofanyika.Nadhani ninyi
mtaendelea kupumzika hapa .Jioni
David atakuja na tutalizungmza lile
suala letu.Hapa kuna wahudmu wengi
watawahudumia kila kitu
mnachokihitaji na ninawaomba
mjisikie nyumbani.You guys have been
through a lot so its your time to enjoy”
akasema Monica
“Monica ahsante sana na
tunakuombea kwa Mungu azidi
kukubariki.Hili ulilolianya ni jambo
kubwa kwa nchi yako” Akasema Austin
“Ahsante.Uliwasiliana na Job?
Akauliza Monica
“Hapana ninataka kuwasiliana
naye asubuhi hii kujua kama
wamefanikiwa kuwakomboa wazazi wa
Irene.” Akasema Austin.Monica akatoka
huku akimkonyeza Amarachi
aliyekuwa amekaa kitandani na wote
wawili wakatabasamu.
“Good morning Amarachi”
akasema Austin baada ya Monica
kutoka
“Goodmorning
Austin.Unajisikiaje?
“Ninajisikia vizuri sijui wewe”
“Hata mimi najisikia vizuri
mno.Sijawahi kuamka nikiwa najisikia
vizuri kiasi hiki.Thank you for the last
night.Ni wewe uliyesababisha niwe na
usiku mzuri ambao sijawahi kuupata
katika maisha yangu’ akasema
Amarachi.Austin akatabasamu na
kusema
“Wake up Amarachi.Ni muda wa
kujiandaa kuikabili siku”
“Austin bado ni mapema
mno.Please come to bed.Hatuendi
kokote leo hii.Let’s enjoy the morning”
akasema Amarachi
“Nahitaji kuwasiliana na Job kujua
kinachoendelea Dar es salaam”
Akasema Austin na kwenda katika
meza ya simu akaziandika namba za
simu za Job akapiga.
“Hallow” akasema Job baada ya
kupokea simu
“Hallow Job ,Austin hapa
ninaongea”
“Austin. Mambo yanakwendaje
huko ? Mko salama kabisa? Akauliza
Job
‘Tuko salama Job .Tulifika salama
japokuwa tulipata misuko suko
njiani.Jamaa waligundua kwamba
tumepanda ndege ya David Zumo na
zikatumwa ndege vita kutufuata na
zilikuwa tayari kutushambulia
ikamlazimu Monica ampigie simu rais
na kumfahamisha kwamba tunataka
kushambuliwa na ndipo ndege zile
zikaondoka.Kama haitoshi rais
akawasiliana na David Zumo
akamuomba atuweke kizuizini pindi
tukiwasili Kinshasa.Ndege ilitua katika
uwanja wa kijeshi na tukachukuliwa
tukapelekwa kizuizini katika kambi ya
jeshi.Tunamshukuru Monica kwani
alitusaidia na tukafanikiwa kutolewa
tukazungumza na David Zumo
tukamueleza ukweli wote,ametuelewa
na ameahidi kutusaidia.Hapa tulipo
tupo katika jengo moja kubwa lenye
ulinzi mkali na siku ya leo tutashinda
hapa hadi jioni kusubiri kuongea na
David Zumo.Tutakutaarifu kila
kitakachokuwa kinajiri huku.Vipi huko
Dar es salaam kuna habari gani?
akauliza Austin
“Huku tumepiga hatua.Jana
tumefanikiwa kuwakomboa wazazi wa
Irene na nimewaleta hapa nyumbani
kwa ajili ya usalama wao.”
“Safi sana.Mlifanikiwa
kuwafahamu ni akina nani waliokuwa
wamewateka wazazi wa Irene? Austin
akauliza
“Alikuwa ni Agatha mke wa rais
pamoja na Silvanus Kiwembe mkuu wa
idara ya usalama wa taifa.Walihitaji
kufahamu Irene alifahamuje kuhusu
lile shambulio? Tulifanikiwa
kuwakomboa wazazi wa Irene lakini
kuna mambo yalitokea.Silvanus
Kiwembe mkuu wa idara ya usalama
wa taifa alifariki,Agatha akafanikiwa
kutoroka.Daniel pia amefariki dunia.I
killed him!!
‘You killed him? Austin
akashangaa
“ Yes I did.Daniel ni mtu mbaya
sana na sikupata nafasi ya kukueleza
sifa zake.Ni wakala wa mashirika ya
kijasusi na amekuwa akijipatia fedha
nyingi kwa kuuza taarifa mbali mbali za
siri na nilimgundua akiwasiliana na
Mukasha akimueleza kwamba anazo
taarifa nyeti anataka kumuuzia”
“dah ! akasema Austin
“One more thing” akasema Job
‘Jana usiku nimefanikiwa
kumnasa tena Mukasha kwa kutumia
simu ya Daniel.Yuko tayari kutusaidia
kupata taarifa na ushahidi wa kuweza
kumuondoa Ernest madarakani lakini
ameomba ulinzi kwa familia yake.Yuko
hapa kwangu na ninawasubiri ninyi
mrejee kutoka Kinshasa ili tujadili kwa
upana zaidi hili suala lake na tuona
atatusaidia vipi”
“Mukasha again? Austin akauliza
‘Ndiyo Austin.Kwa sasa yeye na
Ernest si marafiki tena na amekuwa
kama mkimbizi na tunaweza kutumia
fursa hiyo kupata taarifa muhimu
kuhusu Ernest zinazoweza
kutusaidia.Kumbuka huyu ni mtu wake
wa karibu na anafahamu mambo yake
mengi” akasema Job
“Job una hakika umemchukua
tena Mukasha kwa sababu hiyo
uliyoieleza au kuna sababu nyingine
binafsi? Akauliza Austin
“Both.Austin katika yale
mashambulio ya juzi,Yule jamaa dogo
Bill ambaye alikuwa na taarifa za
kuhusu mahala aliko mke wangu ni
miongoni mwa waliofariki kwa hiyo ni
Mukasha pekee anayeweza kunisaidia
kupata walau mwanga mahala aliko
mke wangu.Asubuhi ya leo atanipeleka
kwa mtu mmoja ambaye ni rafiki
mkubwa wa Bill na tunategemea
tunaweza kupata taarifa kuhusu
mahala aliko mke wangu.Utanisamehe
kwa kuongeza kazi nyingine lakini sina
namna lazima niitumie fursa hii
kumtafuta mwanangu Millen”Akasema
Job.Austin akafikiri kidogo na kusema
“Sawa Job.Endelea na hiyo
operesheni na endapo kutakuwa na
tatizo lolote usisite kunijulisha kupitia
namba hii ya simu niliyotumia
kukupigia.Chukua tahadhari kubwa”
akasema Austin halafu wakaagana.
“Akina Job walifanikiwa
kuwakomba wazazi wa Irene jana
usiku” Austin akamwambia Amarachi
“Austin uliniahidi kuniweka wazi
kuhusiana na suala la Irene.Ana
matatizo gani? Amarachi
akauliza.Austin akaketi karibu yake
akamsimulia kila kitu kuhusu Irene.
“Siamini kama rais amefika
mahala hapa.Kumbe mashambulio yale
yote ni mipango yake!!!Austin damu za
watu wasio na hati zimepotea na
tunapaswa kufanya kila tuwezalo
kuhakikisha rais Ernest anafikishwa
mbele ya sheria.!!
“Ni kweli Amarachi.Lazima yeye
na washirika wake wafike mbele ya
sheria” akasema Austin
“Lakini kwa nini aamue kuua watu
wengi kiasi hiki? Akauliza Amarachi
“Swali kama hilo hata mimi
nimekuwa nikijiuliza mara nyingi na
kuna kitu ninakihisi.Endapo yeye ndiye
kweli anahusika katika mashambulio
yale basi dhumuni lake kubwa ni
kuwaangamiza Alberto’s kwani
ukitazama kwa haraka haraka
utagundua kwamba waliokuwamo
ndani ya hoteli ile iliyoshambuliwa Dar
es salaam wengi ni Alberto’s.Ukiacha
Dar kule Dodoma bungeni kuna idadi
kubwa ya Alberto’s na ninahisi aliamua
kulilipua jengo la bunge ili kuwaondoa
kabisa Alberto’s.Yawezekana lengo lake
llikuwa jema na zuri la kuwaondoa
Alberto’s Tanzania lakini hakupaswa
kutumia njia hii ya kufanya
mashambulio kwani miongoni mwa
waliofariki walikuwemo pia watu
wema wasio na hatia yoyote.Tukubali
njia aliyotumia haikuwa sahihi na hivyo
anahesabika kama ni muuaji na
anapaswa ashtakiwe kwa kosa hilo.”
Austin akakatishwa na muhudumu
aliyegonga kengele ya mlangoni
.Austina akaenda kuufungua na
muhudumu alitaka kufahamu kila
mmoja angependa kutumia kitu gani
katika mlo wa asubuhi.
“kweli hapa tumefika katika
himaya ya kifalme.Sijawahi
kuhudumiwa na wahudumu
wachangamfu na wenye adabu kubwa
kama hawa” akasema Austin halafu
akaelekea bafuni kuoga.Akiwa bafuni
mlango ukafunguliwa akaingia
Amarachi.Bila aibu akaliachia taulo
likaanguka chini akabaki mtupu na
kuyaamsha upya mashetani ya
Austin.Ikulu kukakasirika ghafla.
“This is the good way to start a
day” akasema Amarachi na kumfuata
Austin akaikamata ikulu kwa mikono
yake laini akaanza kuichezea na kuzidi
kuipandisha hasira.Austin hakupoteza
muda akaanzisha mtanange wa asubuhi
humo humo bafuni.Ilikuwa ni asubuhi
njema sana kwao.Baada ya kipute kile
cha kuanzia siku kumalizika wakaoga
pamoja
“Ni heri nikakosa kila kitu lakini si
kumkosa Austin.This man is my
world.Nadhani nilipangiwa nipitie
mateso makali na baadae nije nianze
maisha ya furaha na kusahau magumu
yote niliyopitia na Austin ndiye furaha
yangu.Huyu pekee ndiye anayeweza
kunisahaulisha machungu yote
niliyopitia.I’ll figt for him.Nitapambana
na yeyote hadi nihakikishe nimepata
nafasi ndaniya moyo wake.Upatapo
bahati ya kumpata mwanaume kama
huyu usikubali akakuponyoka na
ndivyo nitakavyofanya” akawaza
Amarachi wakati wakioga
Kisha oga wakaenda kuungana na
akina Yasmin kwa ajili ya chakula cha
asubuhi
“Wote mmeamka salama? Austin
akawauliza akina Yasmin
“Tuko salama.” Akajibu Yasmin.
Walipata kifungua kinywa na
baada ya kumaliza Austin akasema
“Yasmin suala lenu
linashughulikiwa.Tayari rais David
Zumo amekubali kuwasaidia na kama
mnavyofahamu huyu ni mtu tajiri sana
na nchi nyingi zinamuheshimu kwa
hiyo ni rahisi kwake kupata mahala
ambako mnaweza kwenda kuishi na
kuanza maisha yenu mapya.Pindi
mambo yakikaa tayari nitakujulisha ila
naendelea kusisitiza kwamba uwe na
uhakika kwamba hati ile ipo na si
kunidanganya.Kwa juhudi zote hizi
tunazozifanya halafu nigundue kwamba
ulikuwa unanidanganya nakuapia
nitakuteketeza wewe na familia yako
bila huruma” akasema Austin huku
Maria na Boaz wakimtazama kwa woga
“Usiwe na hofu Austin.Ninafahamu
nini maana ya makubaliano na katu
siwezi kukudanganya katika jambo
kubwa kama hili.Uwe na amani na
endelea kukamlisha mambo .Kila kitu
kikiwa tayari nitakuelekeza mahala
hati ilipo” akasema Yasmin na Austin
akainuka
“Austin ninaweza kuzungumza
nawe kwa dakika chache? Akauliza
Boaz na Austin akakubali wakasogea
karibu na bwawa la kuogelea.
“Austin my son” akasema Boaz na
Austin akamkatisha
“Don’t call me your son” akasema
Austin kwa ukali
“Sawa Austin hata kama ukikataa
nisikuite hivyo lakini kwangu utabaki
kuwa mwanangu kwani nimepata
nafasi ya kuishi nawe na kukulea kama
mwanangu.Tuachane na hayo nataka
kuzungumza nawe jambo dogo la
muhimu” akasema Boaz na kumtazama
Austin kwa makini halafu akaendelea
“Nafahamu mimi na wewe kwa
sasa hatuna mahusiano mazuri.Kama
binadamu ninakiri nimekukosea sana
na haya yote yanayonikuta sasa hivi
ninayastahili.Kwa muda ulionifunga
katika kile chumba nimejitafakari sana
kuhusu maisha yangu na nimegundua
namna nilivyokuwa naenenda katika
njia mbaya.Nimewakosea watu wengi si
wewe peke yako lakini kwa niaba yao
wote nataka nikuombe samahani
wewe.Nafahamu ni vigumu kwako
kunisamehe lakini nakuhakikishia
kabisa kwamba toka ndani ya moyo
wangu nimeyajutia makosa
yangu.Ninashukuru kwa kunipa tena
nafasi nyingine kuanza maisha
mapya.Sikuwa nimetegemea kabisa
kama ningeipata nafasi hii.Endapo
tutafanikiwa katika mpango huu na
tukaenda nchi za mbali nataka nibadili
maisha yangu na kuishi maisha ya
kawaida na ya halali kwa hiyo
nimefanya maamuzi.” Akanyamaza
kidogo na kuendelea
“Nataka uuze mali zangu zote na
fedha itakayopatikana tutaigawa katika
mafungu matatu.Moja lako,lingine
langu na lingine ni kwa ajili ya mdogo
wako.Nilimpotezea dira na mwelekeo
kwa hiyo nataka kuyabadili maisha
yake.Nataka awe na maisha mazuri.Ni
hilo tu ninalotaka kukueleza” Akasema
Boaz
“Boaz ninashukuru umenisaidia
sana na nimefika hapa nilipo kwa
msaada wako.Siwezi kulisahau hilo na
ndiyo maana nimekupa nafasi nyingine
japokuwa uwezo wa kukupoteza kabisa
nilikuwa nao.Hata hivyo ahsante kwa
hilo uliloliamua lakini kama utauza
mali zako ni kwa ajili yako na familia
yako.Mimi na mdogo wangu hatuhitaji
hata senti moja kutoka katika mali
zako.We need honest money and not
drug money.Nenda ukautumie utajiri
wako kuanzisha biashara za halali na
uishi maisha ya halali” akasema Austin
“Austin nakuomba tafadhali jipe
muda na ulitafakari suala hili,usifanye
maamuzi kwa haraka.Hili ni jambo
lenye manufaa makubwa kwako.Nina
mali nyingi na endapo zitauzwa zote
pesa itakayopatikana ni nyingi sana na
utaweza kuishi maisha mazuri wewe na
mdogo wako.Nataka niwasaidie na wala
sina lengo baya nanyi” akasema Boaz
“Boaz nimekwisha kuambia
kwamba mimi na mdogo wangu
hatuhitaji pesa zako.Bado nina nguvu
za kufanya kazi na nitafanya kazi kwa
bidii nitapata pesa za kutuwezesha
mimi na mdogo wangu kuishi maisha
mazuri.” Akasema Austin na kuondoka
akamfuata Amarachi aliyekuwa
amekaa katika kiti pembeni ya bwawa
la kuogelea
“Alikuwa anasemaje Boaz?
Akauliza
“ he’s crazy.Anataka kuuza mali
zake zote halafu atugawie nusu ya
fedha mimi na mdogo wangu Linda”
“Umemkubalia? Amarachi
akauliza
“Hapana.Siwezi kukubali fedha
yake haramu yenye laana,inayotokana
kuuza dawa za kulevya.Bado nina
nguvu na nitapambana kuhakikisha
ninapata mali za kuniwezesha mimi na
mdogo wangu kuishi maisha mazuri”
akasema Austin.
DAR ES SALAAM - TANZANIA
Hali ya mzee maboko baba yake
Irene iliendelea vyema.Marcelo
alikesha macho usiku mzima
kuhakikisha kwamba hali yake
inaimarika na hadi ilipofika asubuhi
hali yake ilikuwa nzuri.
“Marcelo ninaondoka na Mukasha
kuna sehemu tunakwenda kwa hiyo
utasimamia kila kitu hapa.Hakuna mtu
yeyote kutoka wala kuingia humu
ndani” akasema Job
“Sawa Job lakini baadae
nitalazimika kutoka kidogo kwenda
hospitali kuchukua baadhi ya dawa na
kulirudisha lile gari la wagonjwa
nililoondoka nalo siku ile kwani
linahitajika hospitali. Vile vile ninataka
nikafanye mpango ili ikiwezekana mzee
huyu apelekwe nje ya nchi haraka kwa
gharama za hospitali yangu kwani kwa
hali yake anahitaji huduma kwa haraka
sana” akasema Marcelo
“Ok fanya hivyo.Mimi sifahamu
nitarejea saa ngapi ila ikitokea nikipata
tatizo nitakutaarifu” akasema Job kisha
akaongozana na Mukasha wakaelekea
garini
“ Nahitaji kuonana na Irene”
akasema Mukasha
“Hapana huwezi kuonana naye
kwa sasa,amepumzika” akasema
Job.Wakaingia garini na kumkabidhi
Mukasha mkoba uliojaa pesa.
“milioni kumi na tano ziko humo.”
Akasema Job
“Tutakapofika kwa Abdul,utabaki
ndani ya gari na nitakutambulisha
kama dereva wangu.Usithubutu kutoka
ndani ya gari” akasema Mukasha.
Job akachukua kisanduku Fulani
kidogo akakifungua na kutoa kidude
kidogo na kumtaka Mukasha akiweke
sikioni.
“Hiki ni kifaa kwa ajili ya
mawasiliano kati uangu nawe.Nitasikia
kila utakachokiongea kwa hiyo
usijaribu kufanya ujinga wowote na
wala usithubutu kukitoa sikioni”
akasema Job wakaondoka
Walikaribia kufika katika jumba
la kifahari analoishi Abdul Chizo
ambaye ni mtu wa karibu sana na dogo
Bill.
“Nyumbani kwake ni pale kwenye
lile jumba la rangi ya bluu bahari”
akasema Mukasha.Jumba la Abdul
lilikuwa juu ya kilima kidogo na toka
ukiwa mbali uliweza kuuona uzuri
wake.
“Watu hawa wanaishi maisha
mazuri kama wako peponi.Yote hii kwa
sababu ya biashara ya dawa za
kulevya.Maisha haya ndiyo
yaliyomshawishi mke wangu Mona
kuniacha na kuolewa na wauza
madawa.Sijui nitamfanya nini siku
nikionana naye uso kwa uso” akawaza
Job
Walikaribia kufika getini
wakakutana na taa ikawamulika
“Hiyo taa ni kifaa cha kukagua
magari na kutambua kama gari lako
limembeba mlipuko au kama kuna
hatari yoyote na kutoa taarifa.Ulinzi wa
hapa ni mkali sana” akasema
Mukasha.Walisimamishwa getini na
walinzi wawili wenye silaha .Mukasha
akajitambulisha na wakaombwa
wasubiri ,Abdul akapigiwa simu na
baada ya muda wakaruhusiwa kuingia
ndani.Walielekezwa sehemu ya
kuegesha na Mukasha akashuka akiwa
na ule mkoba wenye fedha Job akabaki
ndani ya gari
“Ee Mungu nisaidie niweze kupata
taarifa zitakazonisaidia kumpata
mwanangu” akaomba Job
Mukasha akaongozwa ndani na
kutakiwa asubiri katika sebule ndogo
yenye samani za kuvutia.Ilichukua
dakika kumi kwa Abdul
kuwasili.Alikuwa amevaa kaptura na
fulana nyepesi na alionekana kutoka
katika mazoezi.Abdu alikuwa ni mrefu
mwenye umbo lililojaa
“Mzee Mukasha.Shikamoo mzee
wangu”
“Marahaba Abdu.habari yako?
“Habari yangu nzuri.Nimestushwa
kwa ujio wako wa ghafla asubuhi hii.Ni
muda refu sana umepita toka ulipokuja
hapa kwangu.Halafu nilisikia ulipatwa
na matatizo.Vipi maendeleo yako?
akasema Abdul
“Kwa sasa ninaendelea vyema na
jeraha la sikioni nililolipata linaendelea
kupona.Baada ya kupata nafuu
nimeona nije kumsalimia kijana wangu
mara moja’
“Karibu sana”akasema Abdul
“Abdul nafahamu una shughuli
nyingi kwa hiyo sitaki kuchukua muda
mrefu.Nimekuja kwa mambo
mawili.Kwanza kabisa ningependa
ufahamu kuwa kwa sasa mimi niko
mafichoni.Nimeingia katika mgogoro
mkubwa na rais Ernest.Ni mgogoro
binafsi kwa hiyo ninafanya mambo
yangu kwa kujificha ficha wakati
nikishughulikia taratibu za kwenda nje
ya nchi na kutulia uko.Hili si jambo
kubwa sana kwani liko ndani ya uwezo
wangu kulimaliza ila siku nikija kwako
kukuomba msaada tafadhali usiache
kunisaidia.Jambo la pili nimesikia
taarifa za kuhusu Bill ila bado
sijaamini.je ni kweli Bill kafariki?
“Ni kweli Bill kafariki.Naye
alikuwemo katika ile hoteli
iliyolipuliwa.Mimi na yeye kuna mahala
tulitakiwa kwenda lakini tukaahirisha
kwani alitakiwa kuonana na rais katika
hoteli ile.Akiwa pale hotelini alinipigia
simu tukaongea akanifahamisha
kwamba bado anamsubiri rais na
baadae ukatokea mlipuko.Nilikwenda
kuthibitisha kama kweli ni yeye na
ndipo nilipoanza kusambaza taarifa
kwa watu mbali mbali utanisamehe
kwa kutokufikishia taarifa kwani
mambo yalikuwa mengi na sikuweza
kuwataarifu watu wote.Kwa kuwa
mwili wake umeharibika sana
tumeamua kwamba hatutaweza
kuuweka kwa muda mrefu kwa hiyo
leo atazikwa.Taratibu zote
zimeandaliwa na shuguli za kuuaga
mwili wa marehemu zitafanyika
katikaule uwanja wa mpira ulio karibu
na nyumbani kwake ambao
aliutengeneza kwa gharama zake”
Akasema Bill
“Nimesikitika sana.Bill alikuwa ni
kijana jasiri mno na mpambanaji
mkubwa kama ulivyo wewe.Pole sana
Abdul” akasema Mukasha huku sura
yake ikionyesha simanzi kubwa
“Ahsante sana mzee” akasema
Abdul.
‘By the way unaweza
kumkumbuka mwanamke mmoja Bill
aliwahi kuwa naye Yule mweupe mrefu
ana nywele ndefu nimemsahau jina”
“Monalisa? Akauliza Abdul
“Exactly !! Monalisa.Yuko wapi
sasa hivi? Sijamuona naye kwa muda
mrefu”
“Monalisa kwa sasa anaishi
Arusha.Yule hakuwa mtu wa Bill bali
alitumwa na Don ila yeye na Bill
walikuwa watu wa karibu sana na mara
nyingi walikuwa wakiwasiliana.Tayari
nimekwishamjulisha kuhusu msiba huu
toka jana na amesema kwamba leo saa
nne asubuhi atakuja na ndege ili
kushiriki mazishi.Mona mambo yake ni
mazuri sana siku hizi.Si Mona Yule
aliyekuwa akiishi na yule bwana wake
aliyepata kichaa.Alikuwa anamchakaza
bure.Hivi sasa wewe mwenyewe
ukimuona utampotea.Atakuwepo
msibani leo kama utapata nafasi ya
kuja utamuona” akasema Abdul.
“Abdul nataka nikuulize
swali.Umewahi kumuona Don? Who is
he? Tumekuwa katika mtandao huu
kwa muda mrefu mara zote tumekuwa
tukimsikia” akasema Mukasha
“Don sijawahi kumuona hata mimi
ninamsikia tu.Hii ilikuwa ni siri kubwa
ya Bill na amekufa nayo.Sijui kama
kuna mtu mwingine atakayemfahamu
huyo Don ni nani”akasema Abdul
“Abdul naomba nisiendelee
kuchukua muda mrefu,nina jambo la
mwisho lililonileta hapa
kwako.Nimeishiwa mzigo hivyo
nimekuja kutafuta kama una kiasi
chochote unisaidie.Nataka mzigo wa
milioni kumi na tato tu” akasema
Mukasha
“Oh Mukasha mbona umekuja kwa
wakati mbaya sana.Kwa hivi sasa mzigo
umekuwa adimu mno kutokana na hali
kubadilika ghafla.Nimemaliza kabisa na
sina akiba.Ninategemea kupokea mzigo
wiki ijayo na nikipokea nitakujulisha”
Akasema Abdul
Mukasha hakuwa na cha kufanya
tena hapo nyumbani kwa Abdul
wakaagana akarejea katika gari
alimokuwamo Job wakaondoka.
“Natumai umesikia mazungumzo
yangu na Abdul.Pesa zako zote hizi
hapa zimesalimika ” akasema Mukasha
“Abdul hakuweza kukutilia shaka
yoyote? Akauliza Job
“ Hapana ni vijana wangu wale
nimekua nao katika mtandao wetu kwa
miaka mingi kwa hiyo hana shaka
yoyote na mimi.Nadhani sasa kazi yako
nimeifanya vizuri na umekwisha
fahamu kila kitu.Mkeo anaishi Arusha
na huyo mtu anayeitwa Don ndiye yuko
naye.Leo hii atakuja kwa ajili ya
mazishi ya Bill na endapo kutakuwa na
uwezekano basi utaonana naye”
akasema Mukasha
“Mukasha mimi ni mtu jasiri lakini
leo nimeumizwa sana.Nilimpatia Mona
kila alichokuwa anakihitaji.Nilimpa
maisha mazuri lakini bado hakuridhika
na akataka maisha ya starehe
zaidi.Kinachoniumzia zaidi kama
alitaka maisha yale ya starehe
angeenda yeye pekee kuliko kuondoka
na mwanangu.Sijawahi kumuona
mwanangu wa pekee kwa miaka
kadhaa sasa.Lazima nimtafute Mona na
anieleze alipo mwanangu.Sina shida na
yeye ila ninachokitaka ni mwanangu
tu” akasema Job
“Job mimi kazi yangu uliyotaka
nikusaidie imekwisha na kilichobaki ni
upande wako.Ninahitaji na mimi
unitekelezee mambo yangu kama
tulivyokubaliana”
“Usihofu Mukasha.Twende
tukaichukue familia yako na
tutaipeleka nyumbani kwangu .Akina
Austin watakaporejea basi tutaangalia
namna ya kufanya kuwaondoa hapa
nchini.Nimezungumza na Austin
asubuhi ya leo na amekubali
kukusaidia lakini endapo utatusaidia
kupata taarufa za muhimu kuhusu
Ernest kwani wewe umekuwa ni
mshirika wake wa karibu sana”
akasema Job
“Msihofu kuhusu hilo mimi
nitawasaidia na kwa pamoja
tutafanikiwa kumuondoa Ernest kwani
mimi na yeye kwa sasa ni maadui
wakubwa” akasema Mukasha
Walikwenda hadi katika nyumba
walimokuwa wakiishi familia ya
Mukasha wakawachukua na kuelekea
moja kwa moja nyumbani kwa Job.
 
QUEEN MONICA : FINAL SEASON
SEHEMU YA 11
Mlango wa ndege ndogo iliyotua
katika uwanja wa ndege wa kimataifa
wa Julus Nyerere ulifunguliwa na toka
ndani ya ndege ile akashuka
mwanamke mmoja mrembo
sana.Alikuwa mweupe mrefu aliyevalia
koti refu jeusi lililomfika
mogotini.Kichwani alivaa kofia pana
nyeusi ya mviringo iliyokuwa na nakshi
za kupendeza.Mikononi alivaa glovu
zilizoendana na rangi ya koti na
kofia.Ndani alivaa gauni jeusi lililoishia
magotini.Itoshe tu kusema kwamba
alikuwa ni mrembo na mavazi yale
aliyokuwa amevaa yalimpendeza
vilivyo.Alishuka ngazi taratibu.Watu
sita waliovalia suti nadhifu walikuwa
wakimsubiri.Wakampokea na kutoka
naye nje ya uwanja wakaenda katika
gari la kifahari aina ya Marcedece benz
lililokuwa limeandaliwa kwa ajili yake
wakaondoka pale uwanjani.
“Hatimaye nimerejea tena Dar es
salaam.Ni miaka mingi imepita toka
nilipoondoka.Kumekuwa na
mabadiliko makubwa sana .Jiji linazidi
kupendeza mno.Nalipenda jiji hili na
ninatamani kama ningerudi tena kuishi
ndani ya jiji hili lililojaa starehe za kila
aina lakini haiwezekani.Acha tu
niendelee kuishi kwa amani
Arusha.Yule kichaa yuko ndani ya jiji
hili na sijui hali yake ikoje hivi
sasa.Ningefurahi sana kama ningepata
taarifa kwamba amekwisha fariki.Kama
ningeendelea kukaa kwake asingeweza
kunipa maisha kama haya ninayoishi
hivi sasa.Tazama ulinzi nilio nao.Ni
kama vile binti mfalme.Ninaishi maisha
ya kifahari sana ambayo yule bwege
asingeweza kunipa .Japokuwa watu
wataniona mimi sina akili nzuri na
mkatili kwa kumuacha Job lakini kwa
upande wangu sijutii maamuzi
niliyoyafanya.Kama ningeendelea
kung’ang’ania maisha yale mpaka sasa
ningekwisha zeeka.Kwa sasa kwa
matunzo ninayopata ninaoekana kama
binti wa miaka ishirini.Japokuwa yule
mzee simpati mara kwa mara lakini
ninachokitaka mimi ni maisha
mazuri.Mambo ya kimwili hapo
siangalii sana.” Akawaza Monalisa
akiwa garini na uso wake ukiwa na
tabasamu baada ya kuliona tena jiji hili
ambalo alizaliwa na kukulia.
Walifika katika hoteli moja kubwa
ya nyota tano inayomilikiwa na rais
Ernest Mkasa.Monalisa akapelekwa
katika chumba maalum alichoandaliwa
chenye hadhi ya rais au presidential
suit.
“This is life.Yule kichaa katu
asigeweza kunipa maisha kama
haya.Pesa ya kunileta katika hoteli
kama hii angepata wapi? Nitamshukuru
siku zote Bill kwa kunikutanisha na rais
ndiyo maana pamoja na rais kunizuia
nisije Dar lakini nimemkatalia.Siwezi
katu kushindwa kuhudhuria msiba wa
mtumu himukama yule ambaye
alifanya juhudi tukakutana.” Akawaza
halafu akachukua simu na kumpigia
rafiki yake mmoja anaitwa Maimuna
akamtaka afike pale hotelini kwa lengo
la kumsindikiza msibani.
********************
Umati mkubwa wa watu ulijaa
katika uwanja mkubwa zinamofanyika
sherehe za kumuaga bilionea
aliyefahamika kama dogo Bill.Kutokana
na umaarufu wake ililazimu shughuli za
kuuaga mwili wake zikafanyike katika
uwanja wa mpira ulio jirani na
nyumbani kwake uwanja ambao
aliutengeneza kwa gharama zake kwa
kuweka nyasi bandia na kuufanya uwe
wa kisasa.Msiba huu ulikusanya
mabilionea wengi waliofika kumuaga
mwenzao aliyefariki katika mlipuko
uliotokea katika hoteli jijini Dar
Job akiwa amependeza kwa suti
kali nyeus aliyoivaa pamoja na miwani
mikubwa myeusi kiasi cha kumfanya
iwe vigumu kutambulika aliwasili
uwanjani pale akiwa ameongozana na
Julieth mdogo wake Marcelo.Job na
Julieth walitafuta nafasi katika eneo
ambalo lingemuwezesha Job kuona kila
anayeingia pale uwanjani.
Saa tano na dakika ishirini na saba
gari mbili,moja aina ya mercedece benz
likiwa limetanguliwa na gari lingine
aina ya BMW rangi nyeusi zikawasili
pale uwanjani.Toka katika gari la
mbele wakashuka watu wanne
waliokuwa wamevalia nadhifu
kabisa.Kutoka katika ile mercedece
benz mlango wa mbele ukafunguliwa
akashuka mwanadada mmoja aliyevalia
suti nyeusi akafungua mlango wa
nyuma na akina dada wawili
wakashuka toka katika gari
lile.Wakiwa wameongozana na wale
watu wenye suti wadada wale
wakapokewa na wahudumu
waliowekwa kwa ajili ya kuwapokea
wageni maalum na kuwaongoza katika
sehemu iliyotengwa kwa ajili yao.Kila
mtu alikuwa anajiuliza mwanadada
yule aliyeonekana kunuka utajiri ni
nani?Alitembea akiwa ametazama chini
na kofia yake aliyovaa ilimsaidia
kutoweza kutambulika kirahisi
“Monalisa !! akasema Job kwa
sauti ndogo baada ya kumtambua
mwanake yule aliyeingia pale
msibani.Mwili wote ukamsisimka.
“Amebadilika sana na anaonekana
kama anatoka familia ya kifalme.Ana
walinzi sita wanaomlinda.Haya ndiyo
maisha yaliyomfanya anikimbie.Hata
hivyo mimi sina shida naye nahitaji
kufahamu alipo mwanangu tu”
Akawaza Job
Shughuli za kuaga mwili wa Bill
zilianza na baadae ukafika wakati wa
kwenda makaburini.Msafara wa magari
kuelekea makaburini ulikuwa mrefu
sana na eneo la kuegesha magari katika
makaburi likaonekana kuwa dogo.Job
naye ni miongoni mwa watu waliofika
makaburini pale lakini yeye akiwa na
lengo tofauti.Alikuwa anamfuatilia
Monalisa.Hakutaka kumpoteza.Baada
ya mazishi watu wakaanza
kutawanyika.Monalisa akapanda gari
lake na kuongozana na magari mengine
kuondoka pale makaburini.Job akiwa
na Julieth garini alikuwa makini sana
asiweze kulipoteza gari alilopanda
Monalisa.Baada ya kuiacha njia ya
makaburini gari zile mbili zikakamata
barabara kuu ya uzaramo.Hii ni
barabara yenye njia nne kila upande.
“Julieth jiweke tayari kazi
inakaribia kuanza.” Akasema Job na
kumpa maelekezo Julieth.Akakanyaga
mafuta gari likaongeza mwendo
akalipita gari alilopanda Monalisa na
alipofika usawa wa lile gari la mbele
walilopanda walinzi wa
Monalisa,akampa maelekezo asilipite
bali aende nalo sambamba.Job akatoa
bomu la kutupa kwa mkono akauma
kifuniko halafu akashusha kioo cha
dirisha na kulirusha bomu lile chini ya
uvungu wa gari na mara mlipuko
mkubwa ukatokea.Gari alilopanda
Monalisa lililokuwa nyuma ya gari lile
lililotupiwa bomu,likapoteza uelekeo
na kwenda kugonga nguzo ya taa ya
barabarani.Ulitokea mtafaruku
mkubwa kwa magari kugongana kwani
mengi yalikuwa yakienda kwa mwendo
mkali .Gari la akina Job lkikafunga
breki ya ghafla na Job akaruka nje na
moja kwa moja akaenda katika gari lile
alimopanda Monalisa lililokuwa
limegonga nguzo ya taa akakipiga kioo
cha dirisha la mlango wa nyuma
akaufungua mlango.Monalisa alikuwa
amepoteza fahamu kutokana na
mstuko alioupata.Job akambeba
akachukua na mkoba wake na
kumkimbiza katika gari lao
wakaondoka kwa kasi eneo
lile.Kilikuwa ni kitendo ambacho
kilichukua muda mfupi sana
Safari iliendelea kwa kasi huku
Job akimpepea Monalisa aliyekuwa na
majeraha usoni
“Ameumia sana? Akauliza Julieth
“Ameumia lakini si sana.She’ll be
ok” akasema Job
“Nimeogopa sana.Sijawahi
kushuhudia kwa macho yangu tukio
kama lile.Ni kama nilikuwa natazama
filamu fulani Dah ! akawaza Julieth
akiwa makini katika usukani
“Kumbe matukio kama yale
tuyaonayo katka filamu yanaweza
kutokea kweli katika maisha halisi
kama nilivyoshuhudia Job akifanya
leo.Hawa jamaa nimewaogopa ni watu
hatari sana” akaendelea kuwaza Julieth
“Leo utanieleza aliko mwanangu
Millen shetani mkubwa we.Pone pone
yako usiamke tena lakini endapo
utazinduka tena nitakupa mateso
ambayo hujawahi kuyapata toka
umezaliwa na utasema kwa nini
ulinitoroka na utaonyesha aliko
mwanangu Millen” akawaza Job huku
akiendelea kumpepea Monalisa
Walifika nyumbani kwa Job
,Monalisa akashushwa na kupelekwa
katika chumba kile maalum cha
mahojiano Job akamtaka Marcelo
amuhudumie na ahakikishe
anazinduka
 
Mbududa tuendelee mkuu

sent from Sanduku la Posta using JamiiForums mobile app
 
mbududa tupia mkuu

sent from Sanduku la Posta using JamiiForums mobile app
 
QUEEN MONICA : FINAL SEASON
SEHEMU YA 12

Siku ilikuwa ndefu sana kwa
Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania.Aliwaongoza
watanzania kuaga miili ya watu
waliopoteza maisha kwenye shambulio
lililofanyika katika ukumbi wa bunge
na Dar es salaam.Baada ya shughuli za
kuaga miili kumalizika mjini Dodoma
rais akaelekea kisiwani Zanzibar
kuhudhuria mazishi ya makamu wa
rais aliyepoteza maisha katika mlipuko
jijini Dar es salaam.
Saa kumi na mbili za jioni rais
akarejea Dar es salaam.Katika uwanja
wa ndege akapokewa na viongozi mbali
mbali na kisha akelekea ikulu.Mara tu
alipofika ikulu akapewa taarifa
kuhusiana na hali ya usalama.Kikundi
cha kigaidi cha Alshabaab kilijitangza
kuhusika na mlipuko uliotokea katika
soko la kimataifa la samaki
asubuhi.Alipewa taarifa ya tukio
liliotokea na walinzi watatu kuuawa
baada ya gari lao kutupiwa bomu na
Monalisa akachukuliwa na watu
wasiojulikana.Taarifa hii ilimstua mno
rais.Hakupewa nafasi ya kupumzika
akataarifiwa kwamba mke wake Agatha
tayari amerejea nyumbani akitokea
hospitali na mwisho akataarifiwa
kwamba mgeni wake Bashar bin
Abdulsalaam tayari amekwisha wasili
na alikuwa anamsubiri.Ernest
akachanganyikiwa.Hakujua aanzie
wapi.Akaamua kwanza akaonane na
Bashar ndipo aendelee na mambo
mengine.Moja kwa moja akaelekeza
Bashar apelekwe katika chumba cha
maongezi ya faragha.
“Habari yako Bashar” rais Ernest
akamsalimu Bashar wakiwa katika
chumba cha maongezi ya faragha
“Habari nzuri sana mheshimiwa
rais”
“Karibu sana” Akasema rais
“Ahsante mheshimiwa rais.Poleni
sana kwa mambo yanayoendelea nchini
kwenu.Naamini baada ya muda si
mrefu mambo yatakaa sawa” Akasema
Bashar
‘Tunaomba iwe hivyo kwani
watanzania hawajazoea kuishi katika
hali ya mashaka mashaka kama
sasa.Hali hii itatulia si muda mrefu.”
“Mheshimiwa rais nafahamu una
majukumu mengine kwa hiyo nataka
nisikupotezee muda.Naomba
nijielekeze moja kwa moja katika kile
nilichotumwa kwako” akasema Basher
na kufungua mkoba wake akatoa
bahasha nyeupe akamkabidhi rais
ambaye aliifungua na kusoma barua
iliyokuwamo ndani yake.Kadiri
alivyozidi kuisoma ndivyo sura yake
ilivyozidi kubadilika na kujikunja.
Alipomaliza akaitupa barua ile mezani
na kumtazama Bashar kwa hasira
“Huu ni upuuzi mkubwa.Siwezi
katu kukubali ujinga kama huu”
akafoka rais huku akigonga meza kwa
hasira.Akaichukua tena barua ile na
kuanza kuisoma halafu akasimama
“Huu ni ujinga mkubwa sana.Watu
hawa waliokutuma ni wapuuzi
wakubwa.Siwezi mimi kutelekeza haya
wanayonitaka niyatekeleze.Katu siwezi
kukubali.” Akasema rais na kuketi
kitini akaichukua barua ile na kuisoma
tena kwa mara ya tatu
“kwako mheshimiwa rais wa
Tanzania
Tunamtuma mjumbe wetu maalum
kwako kufikisha ujumne huu wa
muhimu sana.Rejea makubaliano yetu
ya awali ambayo kwa makusudi kabisa
umemua kuyapuuza.Umetufanyia
kitendo cha kihuni na sisi tumefadhaika
sana kwa kitendo
ulichokifanya.Tumekaa kikao kujadili
suala hili na tumeamua yafuatayo.
Utabaki na hati ya muungano
wenu wa Tanganyika na Zanzibar
ambayo umekataa kwa makusudi
kutupatia,lakini sisi tunakitaka kisiwa
cha Pemba.Siku si nyingi kuanzia sasa
litatolewa tamko la kisiwa cha pemba
kutaka kujiondoa katika jamhuri ya
muungano wa Tanzania na kuwa nchi
huru.Wewe kama rais wa Tanzania
utaliunga mkono jambo hilo na
kuhakikisha linafanikiwa.Tunafahamu
ni suala gumu lakini tunakutaka
usimame imara kuhakikisha kwamba
linafanikiwa na kisiwa cha Pemba
kinajitoa kutoka jamhuri ya muungano
wa Tanzania na kuwa nchi
huru.Muungano utabaki wa Tanganyika
na kisiwa cha unguja pekee.
Mheshimiwa rais hii ni nafasi ya
pili tunakupa na kitendo chochote cha
kujaribu kulizuia suala hili litakuwa ni
tangazo la vita kati ya nchi yako na
mtandao wetu na ninakuhakikishia
kwamba Tanzania haitakuwa tena
kisiwa cha amani.Damu itamwagika kila
uchao.mamia ya watanzania
watapoteza maisha kila
siku.Tutasambaza watu wetu katika kila
mkoa na mashambulio yatatokea
sehemu mbali mbali za Tanzania.Hii
itakuwa ni vita ya vizazi na vizazi
haitakuwa na kikomo.Usitake
kulitumbukiza taifa lako katika vita hii
mheshimiwa rais.Tekeleza maagizo
tuliyokupa na Tanzania itakuwa
salama.
Tunakutakia utekelezaji mwema
Habib
Hivi ndivo barua ile
ilivyoandikwa.
Ndani ya kile chumba cha
maongezi ya faragha kulikuwa
kimya.Rais Ernest alizama katika
mawazo mazito.Bashar akatazama saa
yake na kumstua rais
“Mheshimiwa rais naona muda
unasonga kwa kasi natakiwa kuondoka
nchini ndani ya nusu saa ijayo.Ahsante
kwa mapokezi mazuri na kuupokea
ujumbe wangu.Kabla sijaondoka kuna
chochote unanituma nikawaambie
walionituma kwako?akauliza Bashar
“Ahsante sana kwa kufika na
kuufikisha ujumbe.Nimeupokea ila
wanipe muda niutafakari na nitawapa
majibu”akasema rais.Wakaagana na
Bashar akaondoka
“Kwa mara ya kwanza ninajutia
maamuzi yangu ya kutaka kupambana
na Alberto’s.Haya yote yasingetokea
endapo nisingeamua kupambana
nao.Kila likitoka hili linaingia lingine.”
akawaza rais na kuvua koti kwani
alihisi joto
“Nafahamu hizi ni njama za IS
kukipata kisiwa cha Pemba ili
waanzishe kundi lao kule.Yasmin
alinieleza kuhusu mipango ya
IS.Nitafanya nini ? Nikubaliane na
matakwa yao au niingie nao vitani ?
Akajuliza rais
“Endapo nitaamua kuingia katika
vita na hawa jamaa nchi hii amani
itatoweka kabisa, kwani hawa jama
wanafanya mashambulizi ya kustukiza
na kuua raia.Wangekuwa ni Alshabaab
peke yao ningeingia nao vitani kwani
ningetuma majeshi yetu yangewasaka
ndani ya Somalia na kuwamaliza kabisa
lakini katika hili suala naamini
Alashabaab wanashirikiana na IS na
hawa ni kundi kubwa la kigaidi
linaloitikisa dunia.I don’t know what to
do” akawaza na kumuta Jenerali lameck
ambaye alifika mara moja
“Lameck nimepokea ujumbe muda
mfupi kutoka kwa Habib lakini naamini
ni ujumbe wa IS ila wameupitisha kwa
habib.” Akasema rais na kumpa Lameck
ujumbe ule ausome.
“Mheshimiwa rais huu ni upuuzi
mkubwa sana.Umewapa jibu gani?
“Nimewaambia ujumbe
nimeupokea na nitautafakari ”
“Sikiliza mheshimwa rais jambo
hili haliwezekani kabisa.Hawa watu si
wa kuwapa nafasi na hawawezi
kutulazimisha tufanye wanavyotaka
wao”akasema Lameck
“Unashauri nini Lameck?
“Kataa ombi lao na waweke wazi
kwamba hilo haliwezekani” akasema
Lameck
“Hilo litakuwa ni tamko la vita kati
yetu na wao”akasema rais
“Then let’s go to war!! Hatuwezi
kukubali upuuzi wa namna
hii.Mheshimiwa rais tayari
tumetengeneza matatizo makubwa
ambayo tunakabiliana nayo hapa nchini
hatuwezi kukubali tena kuongeza
matatizo mengine.Ukilikubali ombi lao
hili litakuwa ni tatizo lingine kubwa na
ambalo hatutaweza kulitatua.Nchi hii
ambayo tunaipigania kuisafisha
itagawanyika na juhudi zetu zote
zitakuwa kazi bure.Damu yote
iliyomwagika itakuwa imekwenda
bure” Akasema Lameck
“Lameck unachokisema ni sahihi
na hata mimi sipendi kufanya vile
wanavyotaka lakini hawa jamaa ni
wabaya sana na sasa wanaungana na
IS.Unafahamu hawa jamaa namna
wanavyofaya mashambuluo yao kimya
kimya.Bado mfumo wa kutambua
mashambulio ya kigaidi katika nchi
yetu ni mdogo kwa hiyo wataitumia
nafasi hiyo kufanya mashambulio kila
uchao.Damu nyingi ya watanzania
itamwagika.Lameck sitaki tena
kuiingiza nchi hii katika majanga
mengine.Damu tuliyoimwaga damu
inatosah.No more blood” akasema rais
“Mheshimiwa rais,uliponiapisha
niwe mkuu wa majeshi ya ulinzi wa
nchi ya Tanzania niliapa kuwalinda raia
wa Tanzania dhidi ya wale wote
wanaotishia amani na ustawi wa taifa
hili.Hawa Alshabaab na IS wanatishia
amani yetu kwa hiyo siwezi kukaa
kimya lazima nisimame imara
kuhakikisha kwamba ninayaongoza
mapambano dhidi yao.Tukikubali leo
kisiwa cha Pemba kichukuliwe na IS
itakuwani hatari zaidi kwa usalama wa
nchi.Watajiimarisha na watakichukua
kisiwa cha Unguja pia na mwisho
watataka kuingia Tanzania
bara.Hulioni hilo mheshmwia rais?!!
Akauliza Lameck kwa sauti ya juu
kidogo.Ernest akainamisha kichwa
akatafakari baada ya muda akasema
“Asubuhi ya leo nilipigiwa simu na
Habib tukabishana kidogo na akasema
anataka kunionyesha nguvu yao.Baada
tu ya kukata simu ukatokea ule
mlipuko katika soko la samaki.Lameck
hawa jamaa wamejipanga vilivyo.Si
watu wa kufanyia mchezo.Tazama
mambo yanayotokea katika nchi za
jirani ambao wameingia katika
mapambano nao.Damu ya watu
wasiona hati ainamwagika.kama
wameweza kufanya shambulio jirani
kabis ana ikulu basi ni watu
waliojiandaa vizuri na wanachiokisema
wanawza wakakitekeleza.”
“Mheshimiwa rais walichokifanya
Alshabaab ni kukuogopesha na
kwuaogopesha watanzania lakini
usiingie katika mtego wao.Wanaweza
kuendelea kufanya mashambulio
mfululizo katika sehemu mbalimbali za
nchi kwa lengo la kuleta hofu lakini
nakuomba mzee usikate tamaa na
kuwapa wanachokitaka.Let’s fight.Tuna
jeshi imara na tukiamua kupamba nao
hawataweza kutushinda.Hiki ni kikundi
kidogo tu” akasema Lameck
“Alshabaab ni kikundi kidogo
lakini hatari na hasa wakiungana na
IS.Ni rahisi kupigana vita na adui
mkubwa kama nchi ambaye unajua
nguvu yake na unafahamu utampiga
wapi lakini hawa jamaa ni vigumu
kupigana nao kwa sababu hawajulikani
wako wapi,wako wangapi,uwapige
wapi na mashambulio yao ni ya
kuvizia”akasema rais
‘kwa hiyo umeamua nini
mheshimiwa rais?
“Niachie suala hilo nilitafakari
halafu nitakupa jibu nimeamua kitu
gani” akasema rais.Baada ya muda
kidogo akasema
“Lamec hatimaye zoezi letu
tumelimaliza rasmi leo.Japo
tumekutana na changamoto nyingi na
nyingine bado tunaendelea kukutana
nazo lakini tunastahili kujipongeza
kwani tumefanikiwa kukipata
tulichokihitaji.Alberto’s karibu wote
ninaowafahamu isipokuwa Agatha
pekee wameteketea.Huu ni ushindi
mkubwa japo tunaofahamu ni sisi
wawili pekee.Kinachofuata sasa ni
awamu ya pili ya zoezi letu ambayo ni
kukabiliana na athari zile zilizojitokeza
na zinazoendelea kujitokeza kutokana
na shambulio lile.Tunaendelea
kupambana ili nchi ibaki salama.Kwa
usiku huu nataka tujadili kuhusiana na
David Zumo” Akanyamaza kidogo kisha
akasema
“ Asubuhi kabla ya kwenda
Dodoma nilikueleza azma yangu ya
kutaka kuhitimisha utawala wa David
Zumo.”
“Ndiyo ulinieleza mheshimiwa rais
lakini nina swali dogo kwa nini
umefikiria jambo kama hilo? Kuna
sababu yoyote kubwa ya kukupelekea
ukafikiria kufanya hivyo?
‘Sababu kubwa ni kitendo chake
cha dharau alichokifanya.Nilimuomba
awakamate akina Yasmin lakini kwa
jeuri ameamua kuwaachia huru.Siwezi
katu kuvumilia kitu kama hiki.Endapo
taifa letu litabomoka basi na yeye
atakuwa na mchango mkubwa kwani
mtu ambaye anatembea na hati ya
muungano wetu alimtia mikononi na
akaamua kumuachia.Kingine ni
kwamba hawa jamaa akina Austin
naamini watakuwa wamemueleza kila
kitu kilichotokea kwa hiyo huyu ni mtu
hatari sana kwangu.Sababu ya tatu ni
ya kibinafsi zaidi lakini kwa kuwa
wewe ni mtu wangu wa karibu
nitakueleza.Ni kwamba David Zumo
tayari amempa mimba Monica.Sitaki
mbegu ya msaliti Yule ichanganyike na
damu yangu.Kwa sababu hizo kubwa
nataka nimuondoe
madarakani”akasema rais.Jenerali
Lameck akavuta pumzi ndefu.Alihisi
kuchoka mwili na akili
“Mheshimiwa rais sitaki
kupingana na maamuzi yako lakini
sababu ulizozitoa naona kama hazina
mashiko makubwa kukufanya ufikirie
kuuondoa utawala wa David
Zumo.Tunaweza kutengeneza tatizo
kubwa sana baina ya nchi zetu
hizi.Mimi ushauri wangu ni kutafuta
njia mbadala kupambana na David na si
kumuondoa madarakani”
“Lameck hakuna njia
mbadala.Nimekwisha amua
kumuondoa David Zumo madarakani
na lazima nifanye hivyo.Siwezi kubadili
msimamo wangu kwa hiyo nataka
unipe plani tutalifankishaje sualah
hilo?Nilikupa nafasi ya kutafakari njia
mbalimbali tunazoweza kutumia
kumuondoa David nadhani mpaka sasa
una jibu zuri la kunipa” akasema rais
“Mzee nimetafakari sana suala hili
kama ulivyonitaka na nimefikiria
jambo moja”
“tell me” akasema rais
“Davd Zumo aliwakusanya waasi
wote waliokuwa wakipigana kwa miaka
mingi na serikali ya Congo
akawajumuisha katika jeshi la Congo
ambalo kwa sasa linajulikana kama
jeshi la pamoja.Wale makanda wakuu
wa vikosi vya waasi amewapa nyadhifa
kubwa katika jeshi na uasi umekoma
kabisa Congo.Tunachoweza kukifanya
ili kumondoa David Zumo madarakani
ni kuzungumza na mmoja wa aliyekuwa
kiongozi wa waasi ili awakusanye
wanajeshi wake na kumpindua rais
David” akasema Lameck
“Hili linaonekana ni wazo
zuri.Hebu nifafanulie namna
tunavyoweza kufanya” akasema rais
“Tutazungumza na kiongozi huyo
wa zamani wa waasi ambaye ninamini
lazima atakubali kwani hivi majuzi
alipohojiwa hakuonekana kupendezwa
na kitendo cha nchi ya Congo kutaka
kugeuzwa kuwa nchi ya kifalme kwani
hakutakuwa na uchaguzi wa rais na
badala yake familia moja ndiyo
itakayoongoza Congo kwa vizazi na
vizazi.Siku zote lengo la kuanzisha uasi
huwa ni kukamata madaraka makubwa
na huyu jamaa endapo tutamuahidi
kumsaidia kukamata madara ya
kuiongoza Congo lazima
atakakubali.Sisi tutamsaidia mbinu za
kijeshi na silaha au hata vikosi vya jeshi
endapo vitahitajika.Mchezo mzima
utakakuwa hivi.Tanzania kwa sasa ni
mwenyekiti wa jumuiya ya afrika
mashariki ambayo nchi ya Congo DRC
ni mwanachama aliyejiunga hivi
karibuni.Kama mwenyekiti utaitisha
kikao cha dharura chenye lengo la
kujadili hali ya usalama katika ukanda
wa afrika mashariki.Wakati kikao
kikiendelea vikosi vya wanajeshi
walioasi wataivamia ikulu ya Congo na
kutangaza kuipindua serikali ya David
Zumo.Unaonaje kuhusu mpango huo?
Akauliza lameck
“Ni mpango mzuri sana
lameck.Ninayakubali mawazo yako
asilimia mia moja na kwa kuongezea tu
ni kwamba baada ya mapinduzi
kufanyika David nitampa hifadhi hapa
Tanzania na haraka sana nitafanya
mpango wa kumuondoa.Nataka
auawe”akasema Ernest
Baada ya majadiliano marefu
Lameck akapewa jukumu la kufanya
mazungumzo na meja Jenerali Paul
Ntamanywa mmoja wa viongozi wa
kundi la waasi waliopigana na serikali
ya Congo kwa miaka zaidi ya ishirini na
sasa yeye na kundi lake
wamejumuishwa katika jeshi la Congo.
Baada ya kikao kirefu rais
akaachana na Jenerali Lameck halafu
akazungumza na mkuu wa jeshi la
polisi akamtaka mpaka kufikia kesho
saa sita mchana Monalisa awe
amepatikan kisha akaelekea chumbani
kwake.Agatha mke wake alikwisha
ruhusiwa kutoka hospitali na alikuwa
amejipumzisha chumbani .
“Welcome home darling” akasema
Agatha
“Vipi maendeleo yako? Akauliza
Ernest
“Ninaendelea vyema.Hali yangu
imeboreka sana.Ahsante kwa kunijali”
akasema Agatha
“Pole sana kwa siku ngumu ya
leo.Unahitaji mapumziko” akasema
Agatha
‘Ni kweli nimechoka sana lakini
mimi na wewe bado tuna maongezi
mengi.Nataka kufahamu ulikuwa wapi
na nani aliyekupiga risasi
mguuni?akasema Ernest
“Relax Ernest.Nitakujulisha kila
kitu lakini kwa sasa unapaswa
upumzike.Tutazungumza pale
utakapokuwa umetulia.Kuna mambo
mengi ya muhimu sana ambayo nataka
tuzungumze”akasema Agatha
“Agatha kichwa changu kina
mambo mengi sana kwa sasa na
sifahamu kama nitaweza kupata nafasi
ya kutulia.Nina majukumu mazito ya
kuhakikisha nchi inatulia baada ya
mashambulio yale mawili kutokea.Nchi
haina serikali ,natakiwa kufikira nama
nitakavyoweza kuiongoza nchi kwa
hiyo usitegemee kuwa nitapata naafsi
nzuri ya kutulia.Lets talk now.Siku ile
ulikuwa katika lile jengo tulimopanga
nikutane nanyi Alberto’s wote lakini
baada ya shambulio kutoea
haukuwepo.Nini kilitokea? Ulinusurika
vipi? Akauliza rais.Baada ya muda
kidogo Agatha akasema
“Nilipokea simu toka kwa Irene
Maboko Yule mfanyakazi wa ikulu
anayeshughulikia masualaya mtandao”
“Irene!! Ernest akashanga
‘Ndiyo.Nilipokea simu toka kwake
akanitaka nitoke haraka ndani ya jengo
lile kwani kuna jambo baya linataka
kutokea.Kwa namna alivyonisisitiza
nikaamua kutoka haraka bila kumuaga
mtu yeyote ili kuona kama kweli kuna
jambo litatokea na kweli baada ya
muda jengo likalipuliwa.Irene alikuwa
na taarifa za kuhusiana na shambulio
lile na ndiye aliyenikoa” akasema
Agatha.Ernest akazidi
kuchanganyikiwa
“I cant believe this!!Irene
alifahamuje kama kuna shambulio
linakwenda kutokea? Akauliza rais
“Hata mimi sifahamu
alifahamuje.Baada ya kunusurika
katika shambulio lile nilienda kujificha
mahala salama na mtu pekee
niliyemueleza mahala nilipokuwa ni
Silvanus Kiwembe.”
“Ulimtaarifu Silva?!!Mbona
hakunijulisha wakati nilimpa jukumu la
kukutafuta na kufahamu mahala ulipo?
Akauliza
“Nilimwambia asikujulishe kwani
nilifahamu kuwa miongoni mwa watu
wanaokuzunguka wapo wasaliti kwa
hiyo sikutaka kujulikana nilikuwa
wapi.Nilitaka kwanza nifanye
uchunguzi kujua Irene alipataje taarifa
zile za kuwapo kwa lile
shambulio.Nilimshirikisha Silva suala
hili naye akapanga vijana wake
kumtafuta Irene lakini tukagundua
alikuwa anashirikiana na watu
tusiowafahamu ambao ni hatari.Mara
kadhaa vijana aliowapanga Silva
kumtafuta Irene walijaribu kumkamata
lakini walikutana na upinzani mkali
kutoka kwa watu anaoshirikiana nao
Irene.Hali hiyo ikatulazimu
kuwachukua mateka wazazi wa Irene ili
kulazimisha Irene ajisalimishe na
akafanya hivyo.Wakati tukiendelea
kumuhoji ili kufahamu alipata wapi
taarifa za shambulio lile,watu wake
anaoshirikiana nao wakatokea na
kutushambulia,wakawaua vijana wetu
pamoja na Silva na mimi nikajeruhiwa
mguuni ila niliokolewa na kijana
mmoja baada ya kujitambulisha kama
mke wa rais.Baada ya kufanikiwa
kutoka salama ndipo nikakupigia simu
kukuomba msaada”akasema Agatha
‘This is unbelievable.Irene?!!
Ernest akauliza tena kwa
mshangao.Hakuamini kama Irene
maboko ndiye aliyevujisha taarifa za
kuwepo kwa shambulio lile kwa mke
wake.
“Ernest suala hili si dogo na kuna
ulazima wa kulifuatilia kufahamu Irene
alitoa wapi taarifa za shambulio
lile.Inawezekana labda anashirikiana
na magaidi? Lazima atafutwe kokote
aliko na apatikane aeleze alifahamuje
kuwepo kwa shambulio katika ile
hoteli” Akasema Agatha
“Agatha umezidi kuichanganya
akili yangu.Irene maboko ni msichana
ambaye ni vigumu kuamini kama
anaweza kuwa na taarifa kama
hizo.Mimi na yeye ni sawa na baba na
mwana kwa nini hakuja kwangu moja
kwa moja na kunieleza kuhusiana na
taarifa hizo? Halafu kitu cha ajabu toka
ulipotokea mlipuko ule hajulikani yuko
wapi” akasema Ernest
“Hata mimi nina mashaka na yule
binti yawezekana anashirikiana na
watu waliofanya mashambulio yale.
Anatakiwa atafutwe kwa kila namna na
akipatikana basi tunaweza kupata
taarifa za muhimu sana.Yule binti
anafahamu kila kitu” akasema Agatha
“Swali lingine,kama alifahamu
kuhusu kuwepo kwa shambulio lile
kwa nini basi hakuweza kuripoti katika
vyombo husika ili kulizuia au hata
kuwaokoa watu waliokuwamo ndani na
badala yake akachagua kukuokoa
wewe peke yako? Akauliza Ernest.
“Muda mfupi baada ya kutoka
kwenye ile bustani ya wanyama jana
usiku nilipigiwa simu na baba Alberto
mkuu akanieleza kwamba yale
mashambulio yote mawili yaliyotokea
hapa Tanzania ni mipango yao kwani
walikuwa wanahitaji kutoa sadaka ya
damu inayopaswa kutolewa kila
mwaka.Mimi kubaki hai pia ulikuwa ni
mpango wao” akasema Agatha na
Ernest akajikuta akipandwa na hasira
kama mtu aliyerukwa na akili
akamshika shingo Agatha na kusema
kwa hasira huku akitetemeka
“That’s not true.Mimi si alberto’s I
hate them na nimefanya haya yote ili
kuwafuta kabisa katika ardhi ya
Tanzania !!
“You did that?!! Akauliza Agatha
kwa mshangao mkuwa na kuutoa
mkono wa Ernest shingoni kwake
akamsukumia pembeni.
“Answer me.Ni wewe uliyeratibu
mashambulio yale kwa ajiliya kuwaua
Alberto’s?? akauliza Agatha.Ernest
hakujibu kitu akabaki kimya ameshika
kichwa.
“What have I done? Kwa nini
nimetamka siri hii kubwa mbele ya
huyu shetani.Huyu mwanamke ni
mchawi mkubwa na ametumia nguvu
zake za kichawi mpaka nimejikuta
nikiropoka mimi mwenyewe siri hii
kubwa.Mambo yanazidi kuniharibikia”
akawaza Ernest
“Ernest umetamka kwa mdomo
wako kwamba ulifanya vile ili
kuwaondoa Alberto’s wote hapa
nchini.Ulitaka kuniua na mimi pia?!!
Akauliza Agatha kwa ukali.Ernest
hakujibu kitu.Agatha akamsogelea
“kwa nini umekuwa na roho ya
ukatili kiasi hicho? You wanted to kill
your own wife?Umesahau mambo yote
tuliyopitia na ukataka kuniua? Akauliza
na kumnasa Ernest kibao.
“Wewe una faida gani hapa
duniani hata ukifa?Umewaua watoto
wako wote kwa ujinga wako kuna faida
gani ya kukuacha hai? Ni bora ufe
upunguze idadi ya watu shetani wewe !!
akasema Ernest
“You are so wrong Ernest
.Unadhani utaweza kupambana na
Alberto’s? Ulikula kiapo kwa kunywa
damu na kiapo kile kitadumu hadi siku
yako ya mwisho hapa duniani .Wewe
bado ni Alberto’s na yote haya
uliyoyafanya bado ni kazi za
Alberto’s.Wanaendelea kukutumia na
utaendelea kuwatumikia daima”
akasema Agatha na kuzidi
kumpandisha hasira Ernest.
“Say that again and I’m going to
kill you right here !!! Ernest akasema
kwa ukali, alikuwa na hasira kali mno
hadi mwili ukimtetemeka.
“You wont kill me Ernest.Endapo
bado una mipango hiyo iondoe kabisa
katika akili yako kwani mimi nimebaki
hai peke yanu miongoni mwa Alberto’s
kwa ajili ya kazimoja ya muhimu nayo
ni kuijenga upya Alberto’s.Isitoshe
ukifikiria kunia fikiria pia kumpoteza
mwanao Monica”
Ernest mkasa akahisi kama
nyundo kubwa imetua kichwani
aliposikia Agatha akimtaja
Monica.Akamvaa na kumuangusha
kitandani. Akamkaba shingo na
purukushani ikaanza
“Nikisikia unalitaja tena jina hilo
nitakuchinja !! Umenisikia ? akauliza
kwa ukali Ernest akiwa amemkaba
Agatha kwa nguvu shingoni kiasi cha
kumfanya apumue kwa shida
“Umenisikia wewe shetani?!!
Akauliza Ernest
“Huyu mjinga ataniua kweli kama
nisipojitahidi kujiokoa” akawaza
Agatha na kunyoosha mkono akaishika
taa iliyokuwa pembeni ya kitanda na
kumpiga nayo Ernest kichwani
akaanguka chini.
“You want to fight with me?!
Akauliza Ernest kwa ukali huku
akitetemeka kwa hasira halafu
akajiinua pale chini na kuelekea katika
kabati lake.Agatha alifahamu
alichokuwa anakitafuta Ernest kabatini
na kwa haraka akauchukua mkasi
uliokuwa katika meza ndogo
akamkimbilia Ernest.
Ernest akasikia vishindo vya
Agatha akimkimbilia akageuka mara
moja akiwa na bastora mkononi
akamlenga Agatha lakini kabla
hajafanya lolote Agatha ambaye naye
alikuwa amepandwa na hasira kali
akamvaa Ernest na kumuangusha
chini.Bastora ya Ernest ikaanguka
pembeni na Agatha akamkalia
juu.Ernest akamchapa ngumi nzito
Agatha iliyomuangusha chini akataka
kuiokota bastora yake lakini Agatha
akakiona kitendo kile na kuokota
mkasi uliokuwa karibu yake
akauzamisha katika shingo ya Ernest.
“Go to hell you devil !!! akasema
kwa ukali.Ernest akaanguka pembeni
huku akitapa tapa na damu nyingi
ikaanza kumwagika.Agatha akainuka
pale chini huku damu ikimtoka
mdomoni.Ghafla Agatha akawa ni kama
mtu aliyestuka toka usingizini baada ya
kumuona Ernest akitapa tapa huku
akitokwa na damu nyingi.
“Ernest!! Akaita Agatha
“Ernest !! akaita tena kwa nguvu
na kisha akauchomoa ule mkasi
mkubwa shingoni mwa Ernest na damu
nyingi ikaruka.
“Nimeua !! akasema huku
akitetema
“Nimeua !!!
Agatha akaanza kutetemeka kwa
woga.Alishindwa afanye
nini.Akamtazama Ernest aliyekuwa
amelala katika dimbwi la damu.
“Nini kimetokea? Mbona kama
nilikuwa ndotoni? Akajiuliza Agatha
“Hapana hii si ndoto.Nimemuua
Ernest.Nimemuua rais wa nchi.!!
Akawaza na mara simu ya rais ikaita
Agatha akazidi kuogopa.Akaichukua
simu ile akatazama mpigaji alikuwa ni
Jenerali Lameck.Akaikata na kuzima
simu.Baada ya sekunde kadhaa
akasikia mlango wa chumba
ukigongwa.Agatha akazidi
kuchanganyikiwa.Mara akaiona
bastora pembeni na alipokuwa amelala
Ernest mkasa akaichukua.Mlango
ukagongwa kwa mara ya pili.
“Kila kitu
kimeharibika.Nikikamatwa hapa ni
kwenda gerezani na sintoweza kutoka
tena.Maisha yangu yameishia hapa….”
akawaza Agatha huku machozi
yakimtoka na kuuweka mdomo wa
bastora chini ya kidevu.Mlango
ukagongwa kwa mara ya tatu na mara
ukasikika mlio wa risasi.Mlango wa
chumba cha rais ukapigwa na
kufunguka wakaingia walinzi wa rais
na kuwakuita rais na mke wake wakiwa
wamelala chini katika damu.Haraka
haraka gari la wagonjwa likaletwa
wakapakiwa na kukimbizwa hospitali.
KINSHASA – DRC
Msafara wa David Zumo uliwasili
katika nyumba walimofikia Monica na
wenzake akina Austin.Tayari ni saa
tatu za usiku.Ndani ya gari David
alikuwa na Monica ambaye baada ya
shughuli za mazishi ya Pauline
hakurejea katika makazi yake
aliyoandaliwa bali aliungana na
viongozi wa mataifa na wawakilishi
wao katika chakula maalum
kilichoandaliwa na rais David kwa ajili
yao.
“Karibu ndani Monica” akasema
David huku akimfungulia Monica
mlango.Walinzi wote wakabaki
nje.Sebuleni Yasmin na maria walikuwa
wanatazama runinga.Walitaka kuondoa
walipomuona David Zumo lakini
akawataka waendelee kutazama
akamuongoza Monica kuelekea katika
sebule nyingine.Nyumba ile ilikuwa na
sebule tatu.
“Monica sipati neno zuri la
kukushukuru kwa ushirikiano ulionipa
kwa kuacha shughuli zako na kuja
kuungana nami katika mazishi ya
Pauline.Ahsante sana” akasema David
“Usijali David.Ni wajibu wangu
kufanya hivi.Hakuna ambacho
kingenizuia nisifike katika mazishi ya
Pauline.Hata kama Pauline na mmoja
wazazi wangu wangefariki katika siku
moja basi ningehudhuria kwanza
mazishi ya Pauline.Nimebahatika
kukutana na Pauline katika siku za
mwisho za uhai wake lakini nakiri
sijawahi kukutana na mwanamke
mwenye upendo wa ajabu kama yeye
katika maisha yangu. David umepoteza
kitu cha thamani kubwa sana”
“Nakubaliana nawe
Monica.Pauline alikuwa ni mtu mwenye
upendo wa aina yake.Alimpenda kila
mtu na ndiyo maana umeona maelfu ya
watu waliofurika leo kuja kumsindikiza
katika safari yake ya
mwisho.Alipendwa na kila mtu hapa
Congo lakini Mungu ana makusudi yake
,ameondoka Pauline na ameniletea
zawadi nyingine ambayo ni
wewe.Naweza kusema kwamba Mungu
ananipendelea sana mimi kwa
kuniletea wanawake ambao ni adimu
sana kuwapata katika ulimwengu wa
sasa.Monica nina bahati sana kukupata
na sijui nitamshukuruje Mungu kwa
Baraka hizi anazonijalia” akasema
David
“Monica siku imekuwa ndefu sana
na unahitaji upumzike kwa hiyo sitaki
kukuchosha sana nataka kuzungumza
na akina Austin.Nataka tulizungumze
suala lao ili nione namna ya
kuwasaidia”akasema David.Monica
akaenda katika chumba cha akina
Austin akagonga na Austin akaufungua
mlango
“Queen Monica” akasema Austin
na uso wa Monica ukachanua tabasamu
“Mmeshindaje leo? Akauliza
“ Tumeshinda salama.Pole kwa
shughuli nzito ya leo” akasema Austin
“Ahsanteni sana.Shughuli
imekwisha salama.Tutazungumza zaidi
baadae lakini nimekuja na David
anahitaji kuonana nanyi ili tuzungumze
lile suala letu.Kuna taarifa zozote toka
Dar es salam kwa Job? Akauliza Monica
‘Nimezungumza na Job asubuhi na
walifanikiwa kuwakomboa wazazi wa
Irene.They are all safe” akasema Austin
“That’s good news.Tutaongea zaidi
baadae twendeni tukaonane na rais
David” akasema Monica kisha
wakaongozana hadi sebuleni
alikokuwepo David
“Pole sana mheshimiwa rais kwa
shughuli nzito ya leo.Pamojana kuwa
katika kipindi kigumu lakini umetafua
muda na kuja kuonana nasi.Hii ni
heshima kubwa umetupa” akasema
Austin
“Usijali Austin.Suala hili pia ni la
muhimu sana kwani linahusu maslahi
ya nchi ambayo mimi naichukulia Kama
nyumbani.Tanzania ni kama nyumbani
kwetu k wani kwa miaka mingi watu wa
Congo wameishi Tanzania wakati ule
ambao nchi ilikuwa imegubiokwa na
vita vya wenyewe kwa wenyewe.Suala
lolote linalohusu maslahi ya Tanzania
linanihusu kwa sababu Tanzania ndiko
anakotoka malkia mtarajiwa wa Congo”
akasema na wote wakatabasamu
“Jana ulinieleza kwa kifupi juu ya
suala hili lakini kwa kuwa leo ninao
muda wa kutosha ninaomba unieleze
kwa kirefu nilifahamu kwa kina zaidi
suala hili ili na mimi nione nitatoa
mchango gani kutokana na uzito wa
suala lenyewe” akasema David.
Austin akaanza kumuelezea David
toka mwanzo hadi pale
walipofikia.David akabaki kinywa wazi
“Mhh ! haya ni mambo mazito
sana.Sikuwahi kufikiri kama siku moja
Tanzania ingefika hapa
ilipofika.Nimestuka sana.” Akasema
halafu baada ya muda kidogo akauliza
“Kwa hiyo ni msaada upi zaidi
mnaohitaji niwasaidie?
‘Tunahitaji kuwapatia Yasmin na
familia yake sehemu ya kwenda kuishi
mbali mahala ambako haitakuwa rahisi
kwa IS kuwafahamu.Wanahitaji majina
na pasi mpya za kusafiria.wanahitaji
mtaji au biashara yoyote ambayo
itawasaidia kuendesha maisha
yao.Endapo tukivikamilisha hivyo vitu
basi Yasmin atatuonyesha mahala
alipoificha hati ya muungano” akasema
Austin
“Nimewasikia Austin na ombi lenu
nimelipokea ila naomba mfahamu
kwamba kwa kufanya haya tayari
nimeingia katika msuguano na rais
wenu Ernest Mkasa.Asubuhi ya leo
amenipigia simu kuniuliza kama
niliwaweka kizuizini nikamweleza
ukweli kwamba sikuwaweka kizuizini
kwa sababu sikuona kosa lolote
mlilonalo hivyo nikawaachia
huru.Hakufurahishwa na jambo hili
lakini baada ya kunipa picha kamili
sasa nnafahamu kwa nini anatumia
nguvu kubwa namna hii
kuwatafuta.Hata hivyo nawahakikishia
kuwapeni ushirikiano mkubwa sana
hadi mfanikisha suala
lenu.Ninachohitaji kujua ni mipango
yenu baada ya kufanikisha kupata hati
ya mungano.Mmepanga kufanya nini?
“Kitu tulichopanga kukifanya ni
kukusanya ushahidi wa kutosha wa
kumuhusisha rais na mashambulio yale
mawili na kisha tutamfikisha
mahakamani.Hapa ninamaanisha
kwamba lazima tumuondoe
madarakani na kisha tumfikishe mbele
ya sheria”
“Nitawasadia kwa hilo.Nitawapa
ushirikiano wa kutosha na kuhakikisha
Ernest mkasa anafikishwa katika
sheria.Niachieni suala hilo nilifanyie
kazi na kesho nitakuwa na jibu la
kuwapa” akasema David wakaendelea
na maongezi hadi ilipotimu saa sita za
usiku wakaagana na Ernest akaondoka
na Monica wakaelekea chumbani.
“Ahsante sana David kwa kujitolea
kuwasaidia wenzangu hawa
walioyaweka maisha yao hatarini
wakipambana kwa ajili ya nchi
yao.Najua utaingia katika mgogoro na
rais Ernest lakini usikate tamaa
endelea kutusaidia” akasema Monica
wakiwa chumbani
“Monica mambo aliyonieleza
Austin yamenigusa sana na hasa baada
ya kuisikia rekodi ile ya mazungumzo
kati ya rais Ernest na mkuu wa majeshi
wa Tanzania wakiongelea kuhusiana na
yale mashambulizi.Nimeumia sana
kuona mtu kama rais anatumia
madaraka yake kuteketeza roho za
watu wasio na hatia yoyote.Nitatoa
msaada wa kila aina hadi nihakikishe
Yule mzee anafikishwa mbele ya
sheria.Ni wakati wa kuisaidia Tanzania
kwani wakati wa mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe hapa Congo
Tanzania walisimama kidete na hata
kutuma vikosi vya jeshi kuja
kupambana na waasi na sasa ni zamu
yetu kusimama kwa ajili ya ndugu zetu
wa Tanzania” Akasema David halafu
wakaingia kuoga na kisha wakarejea
kitandani
“Monica ulinieleza kwamba kuna
jambo unataka kunieleza siku tukipata
nafasi.Wakati ni huu ambao unaweza
ukanieleza” Akasema David.Monica
akastuka na kuingiwa na woga.
“Nieleze malaika wangu
ninakusikia” akasema David na
kumbusu
“David nina jambo zito ambalo
nataka nikueleze na sijui
utalichukuliaje lakini sina budi
kukueleza”
“Nieleze malaika wangu.Hata
kama ni jambo gumu ambalo huwezi
kumueleza mtu mwingie yeyote nieleze
mimi nitakusikiliza.Hata kama
umewahi kuua mtu niambie na itabaki
kuwa siri yangu” akasema David na
wote wakachela
“David wewe ndiye uliyekuwa
mwanaume wangu wa kwanza kuingia
naye katika mahusiano na ni wewe
uliyeniondoa usichana
wangu.”akasema Monica akamtazama
David halafu akaendelea
“Niliporejea Dar es salaam
nilikumbuka kwamba tulifanya
mapenzi katika tarehe zangu za hatari
na hata tarehe zilipofika sikuona siku
zangu.Suala hili limekuwa linanitesa
mno akili yangu.Nikamshirikisha mama
na akaniambia kwamba kuna
uwezekano labda nimeshika ujauzito
japokuwa sina uhakika bado hadi hapo
nitakapop….” Monica hakumaliza
sentesni yake David akamrukia na
kuanza kumporomoshea mabusu
mazito.
“Monica niambie kama taarifa hizi
si utani.”
“Si utani David ni taarifa za kweli
na ndiyo maana sikutaka kukueleza
katika simu nikasubiri nije nikueleze
ana kwa ana.Hilo ndilo jambo ambalo
limekuwa linaniumiza kichwa kwani
sikuwa nimepanga kupata mtoto kabla
ya ndoa” akasema Monica na
kuinamisha kichwa
“Monica malaika wangu
nakuomba tafadhali usiumize kichwa
chako kwa suala hili.Hizi ni Baraka
Mungu ametujalia.Hiki kilikuwa ni kilio
changu cha miaka mingi nikiomba
mtoto hatimaye leo hii ombi langu
limejibiwa na ninakwenda kuitwa
baba.Oh ahsante Mungu”akasema
David na kushindwa kuyazuia machozi
ya furaha kumtoka.Monica naye
akapatwa na hisia kali akamkumbatia
David na wote machozi yakawatoka
“Sijawahi katika maisha yangu
kupata taarifa ambayo imenifurahisha
hadi kunitoa machozi.Hii ni taarifa ya
kwanza kuniliza.Nimefurahi kupita
maelezo na sijui nikwambie nini
Monica malaika wangu.Nimshukuruje
Mungu kwa Baraka hizi ambazo vidole
havitoshi kuzihesabu?Itoshe kusema tu
ahsante Mungu” Akasema David
“David nimeharakisha kukueleza
suala hili lakini bado sina uhakika
kama kweli nina ujauzito ama vipi hadi
hapo tutakapofanya kipimo ndipo
tutajua”
“Monica nina uhakika mkubwa
hiyo lazima itakuwa ni mimba.Kesho
watakuja madaktari hapa watakupima
kama unavyotaka lakini nina uhakika
kabisa lazima humo tumboni mwako
umebeba kiumbe kitakachovishwa taji
la urtawala wa Congo.Umebeba mrithi
wangu.Umebeba mfalme au malkia wa
baadae wa Congo” akasema David kwa
furaha na kumkumbatia tena Monica
kwa nguvu huku akimwagia
mabusu.David alisahau kabisa kama
bado alikuwa katika majozi ya kufiwa
na mke wake kutokana furaha
aliyokuwa nayo
“Endapo kweli utakuwa mja mzito
nitafanya haraka sana ili tuweze
kufunga ndoa na mtoto wetu aanze
kulelewa katika jumba la kifalme toka
akiwa mdogo” akasema David.Ulikuwa
ni usiku wa aina yake ambao David
alihisi kama vile hayuko katika dunia
hii.waliongea na kupanga mambo
mengi kuhusiana na maisha yao ya
usoni.
DAR ES SALAAM - TANZANIA
Baada ya chakula cha usiku Job
akawataka watu wote waende
vyumbani mwao kupumzika.Sebuleni
akabaki na Marcelo na Julieth
akawataka waelekee katika chumba
alimowekwa Monalisa.Aliufungua
mlango wa chumba kile maalum kwa
ajili ya mahojiano na kuingia
ndani.Mstuko alioupata Monalisa
ulkuwa mkubwa sana na hakuamni
macho yake kwa kile alichokiona.
“My God !! akasema Monalisa kwa
mshangao
“This is unbeliavable..!! Job !!
akasema Monalisa bado akishangaa.Job
akavuta kiti na kuketi
“Halo Monalisa.habari za siku
nyingi? Habari za Arusha? Akauliza Job
na Monalisa alishindwa kuongea
midomo ilikuwa inamtetemeka.
“Relax Mona” akasema Job huku
akitabasamu kwa namna Monalisa
alivyokuwa anaweweseka baada ya
kumuona.Baada ya muda akasema
“Karibu tena Dar es salaam Mona”
Akasema na kunyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Samahani sana Monalisa kwa
kukuchukua kwa vurugu namna ile
lakini imenilazimu nifanye hivyo kwani
kukupata kwa njia ya kawaida
isingewezekana.Nimekuleta hapa kwa
ajili ya jambo moja tu ambalo
ukinisaidia nikalipata basi nitakuachia
uende zako lakini endapo utashindwa
kunipa ushirikiano basi nakuhakikishia
utakuwa ndio,mwisho wako wa kuliona
jua” akasema Job na taratibu sura yake
ikaanza kubadilika na kuonyesha
kwamba alianza kupandwa na
hasira.Monalisa akazidi kuogopa.
“Sitaki kufukua kaburi na
kukumbusha mambo yaliyopita baina
yetu kwani imebaki historia lakini
ninachokihitaji kwa sasa ni kufahamu
alipo mwanangu Millen.Nionyeshe alipo
mwanangu na nitakuachia ukaendelee
na maisha yako” akasema Job.Monalisa
akamtazama akashindwa
kuzungumza.Job akainuka
akamsogelea
“Mona huwezi kuongea? Wewe ni
bubu? Nieleze aliko
mwananguMonalisa” akasema Job
lakini bado midomo ya Monalisa
ilikuwa inamtetemeka na akashindwa
kuzungumza.
Ghafla bila kutegemea Job
akamnasa kibao kikali sana na
kumfanya apige kelele.
“Nadhani sasa unaweza
kunijibu.Ukishindwa kunipa jibu
nitakufanyia kitu kibaya sana.Tafadhali
usinilazimishe nikufanyie kitu kibaya
kwani nakuheshimu kama mama wa
mwanangu lakini endapo utaendelea
kukaa kimya utanilazimisha
nikuharibu.Nitachukua kisu na
kuukwangua uso wako na kuuondoa
huo uzuri wote ulio nao.Nakuuliza mara
ya mwisho mwanangu Millen yuko
wapi? Akauliza Job lakini Monalisa
aliendea kulia huku akitetemeka kwa
woga.
“Nadhani bado hujanifahamu
vizuri.I’m a monster!! Mimi ni mtu
mbaya sana
ukinikorofisha.Nitakuonyesha upande
wangu wa pili ambao hujawahi kuuona”
akasema Job na kulifugua sanduku lake
dogo jekundu.Marcelo akamuwahi
“Job subiri kidogo usimfanye
chochote.Let me talk to her” akasema
Marcelo
“Marcelo stay out of this” akasema
Job
“Job nakuomba tafadhali nipe
dakika mbili nizungumze naye ili aweze
kujibu swali ulilomuliza.Usimtese
tafadhali huyu ni mama wa mtoto
wako.Wewe na yeye mmewahi kuwa na
historia.Dakika mbili tu naomba”
akasema Marcelo.Job akamtazama
Marcelo na kusema
“Ok two minutes!! Akasema Job
“Naweza kubaki naye peke yake
tafadhali!! Akasema marelo.Job na
Julieth wakatoka nje
Marcelo akamuendea Monalisa
pale kitini na kumshika mabegani
“Monalisa look at me.My name is
Dr Marcelo.Tafadhali naomba
unisikilize na ufanye kile
nitakachokueleza.Take a deep breath”
akasema Marcelo na Monalisa akavuta
pumzi ndefu mara tatu akimfuatisha
Marcelo
“Good.Sasa nisikilize.Job
unamfahamu vizuri kwani aliwahi
kuwa mumeo lakini Job huyu
umuonaye sasa si yule ambaye
ulimfahamu awali.Katika kipindi
ambacho wewe na yeye mmetengana
amepitia mambo mengi sana magumu
kwa hiyo tafadhali usijaribu kumfanyia
mchezo au kiburi cha aina
yoyote.Msikilize na umjibu kila kile
atakachokuuliza.Nimemshuhudia
wakati akiwa kazini ni mkatili sana na
hana huruma hata kidogo.Amekuambia
kwamba atakuharibu uzuri wako wote
na atafanya hivyo endapo hautamjibu
kile anachokitaka.Narudia tena
kukuomba Mona Job hana shida na
wewe hata kidogo na ndiyo maana
mpaka sasa hajakutesa lakini
usimlazimishe akutese ,mueleze aliko
mwanae kwani hiyo ndiyo shida yake”
akasema Marcelo.Huku akilia Monalisa
akasema
“Ninaogopa kumueeza aliko
mwanangu atamchukua na kuja kuishi
naye katika maisha haya ya taabu.Sitaki
kumpoteza mwanangu” akasema
Monalisa
“Monalisa tafadhali nakuonea
huruma sana.Usipomuonyesha mahala
alipo mwanae sina hakika kama
utatoka salama katika hii
nyumba.Mueleze alipo mwanae na
muyamalize haya mambo.Tafadhali
nakuomba” akasema Marcelo na mara
mlango ukafunguliwa akaingia Job na
Julieth
“Dakika mbili
zimekwisha.Niachieni nafasi niifanye
kazi yangu” akasema Job
“Monalisa fanya kama
nilivyokuelekeza” akasema Marcelo
kisha yeye na Julieth wakatoka nje
akabaki Job peke yake mle ndani
“Sasa tumebaki wawili.Uko tayari
kunionyesha alipo mwanangu au
nianze kuifanya kazi yangu? Akauliza
Job.Monalisa akashindwa kuzungumza
kutokana na woga aliokuwa nao
“Fine.Hutaki kuzungumza kwa
hiari sasa utazungumza kwa lazima”
akasema Job na kuchukua baadhi ya
vifaa vya kutesea akaviweka mezani
“Job usinitese tafadhali !! akasema
Monalisa huku akilia
“Ukitaka nisikutese Mona
nionyeshe alipo mwanangu.Mimi sina
shida na wewe!! Akasema Job
“Job tafadhali usimchukue
mwanangu.Yeye ndiye kila kitu
kwangu!! Akasema Mona huku akilia
“Mona usinipotezee wakati
wangu.Nionyeshe alipo Millen ama
sivyo hatatoka salama humu ndani!!
Akasema Job na kuchukua kifaa kidogo
kinachojlikana kama koleo akakishika
kidole cha Monalisa na kuibana kucha
kwa lengo la kuibandua .
“Basi Job nitakueleza kila
kitu.Tafadhali usinitese!! Akasema
Monalisa.Job akamtazamana kwa
hasira
“Millen anasoma Arusha katika
shule ya kimataifa inaitwa Mama
Theresa international school.” Akasema
Monalisa
“Nitawezaje kumpata?
“Job tafadhali usimchukue mtoto
muache amalize shule!! Akasema Mona
“Mona tafadhali
usinichezee.Nahitaji kumpata
mwanangu.Siwezi kumuacha
mwanangu akasomeshwa kwa fedha
haramu” Akasema Job na kutoa simu ya
Monalisa katika mkoba na kumpatia
“Piga shuleni kwa akina Millen na
uwafahamishe walimu kwamba
umepata msiba na unamuhitaji Millen
Dar es salaam kesho.Waeleze kwamba
wewe hautaweza kufika bali utamtuma
mtu akamchukue” Akasema Job
Monalisa akaishika simu
akazitafuta namba za mkuu wa shule
anakosoma mwanae Millen akampigia
na kumtaarifu kwamba amepata
matatizo ya kifamilia na hivyo
anamuhitaji Millen kesho afike Dar es
salaam.Alimaliza kuzungumza na mkuu
wa shule akaiweka simu mezani na
kuangua kilio.
“Job tafadhali nakuomba
usimchukue mwanangu!! Akasema
Monalisa huku akilia
“Kesho nakwenda kumchukua
mwanangu Arusha na hautamuona tena
katika maisha yako” akasema Job kwa
ukali
“Job nakuomba
tafadhali.Nitafanya kila
utakachoniamuru nifanye lakini
usimchukue mwanangu” akazidi kulia
Monalisa
“Yule ni mwanangu pia na
ninakuhakikishia kwamba hautamuona
tena katika maisha yako.Wewe
mwanamke ni shetani mkubwa!!
Akafoka Job akamtazama Mona kwa
hasira na kusema
“Kwa muda wa miaka kadhaa
nimeteseka sana mateso ambayo
yamesababishwa na wewe.Nililazimika
kuishi kama kichaa nikila na kunywa
majalalani kwa ajili ya kuwakimbia
watu ambao walitaka kuniua kwa
sababu yako.Mambo niliyoyapitia ni
mazito na siwezi kukueleza kwani
ndicho hasa ulichokuwa
unakihitaji,mimi niteseke au niuawe na
wewe ubaki huru ukifurahia maisha na
huyo bwana wako” akasema Job na
kuendelea kumtazama Monalisa kwa
macho makali
“Nilipoamua kuacha wanawake
wote wa dunia hii na kukuchagua wewe
nikiamini kwamba wewe ndiye pekee
uliyeumbwa kwa ajili
yangu,sikutegemea kabisa kama siku
moja ungekuja kufanya jambo kama hili
ulilolifanya.Sikutegemea kama siku
moja ungeweza kufanya kitendo
kikubwa cha usaliti kama
ulichokifanya.Pamoja na kuyatoa
maisha yangu kukupa kila ulichokitaka
lakini bado hukutosheka.Sitaki
kuongeleza zaidi suala hilo
ninachokihitaji kukifahamu huyo Don
ambaye uliamua kuniacha ukakimbia
naye ni nani? Akauliza Job.Monalisa
hakujibu kitu
“Nijibu Monalisa.Nahitaji
kumfahamu huyo mtu
aliyekuchanganya hadi ukaamua
kuniacha ni nani? Akauliza tena lakini
Monalisa alibaki akilia hakujibu kitu.
“Nilikuonya toka awali kwamba
sipendi kupotezewa muda
wangu.Nikikuuliza nataka jibu mara
moja” Akasema Job na kuchukua koleo
akamshika mkono na kukiminya kidole
kimoja.Monalisa akapiga ukelele
mkubwa
“Hata ukipaaza sauti ya namna
gani hakuna atakayekusikia.Ni mimi na
wewe tu humu ndani.Usiponijbu
nitaanza kuziondoa kucha zako nzuri
moja baada ya nyingine.Maumivu yake
siwezi kukuelezea.Nakupa sekunde
tano unijibu Don ni nani? Akauliza Job
na kutazama saa yake.
“Sekunde tano zimekwisha.sasa
nakuonyesha nilivyo mkatili!! Akasema
Job na kuchukua tena koleo.
“Nitakueleza Job usiendelee
kunitesa” akasema Monalisa
“Nijibu haraka sana” akasema Job
“Mtu niliyenaye ambaye sifahamu
kama anaitwa Don ni rais wa Tanzania”
akasema Mona
‘What ?!!
‘hebu rudia tena!!
“Mwanaume niliyenaye ni rais wa
Tanzania”
‘Oh my God !! Ernest Mkasa
again??akasema Job .Alistuka sana
kusikia habari ile.
“Ndiyo maana ulikuwa tayari mimi
nife ili upate nafasi ya kuwa na huyo
mzee wak😵h Monalisa ulikosea sana
kukubali kuwa hawara ya Yule mzee.Ni
bora kama ungeondoka na mwanaume
mwingine ningekuelewa lakini si Yule!!
akasema Job akiendelea kumtazama
Mona kwa hasira
“Nashindwa nikufanye
nini.Natamani nikukate kate vipande
vipande ili hasira zangu zote ziishe
lakini haitasaidia.Usiku huu nitautumia
kutafakari nini nikufanye shetani wewe
!! Utakaponiona kesho asubuhi ujue
hatima yako imefika !! akasema Job na
kutoka mle chumbani akawakuta
Marcelo na Julieth nje yakile chumba
wakimsubiri.
“Pole sana Job.Make a deep breath
!! akasema Marcelo baada ya kuona
namna Job alivyokuwa amebadilika.
“Siamini nilichokisikia.Kumbe
Ernest mkasa ndiye aliyenipora mke
wangu.Ndiye aliyesabaisha miaka hii
yote mimi nimeteseka na kuishi kama
kichaa nikila na kunywa katika
majalala.Nimechanganyikiwa na sijui
nifanye nini.Sijui nitamfanya nini huyu
mwanamke !! akasema Job
“Usimfanye chochote Job.Kwa
kuwa tayari umekwisha fahamu alipo
mwanao fanya jitihada za kumpata
mwanao na huyu mwanake muache
aende akaendelee na maisha yake.Hata
ukimkata mikono yote haitasaidia
kitu.Let her go.Mungu anayaona mateso
yako na atakusaidia siku moja na wewe
utampata mwanamke mwenye mapenzi
ya kweli” Akasema Marcelo.
Job akaegemea ukuta akawaza
kwa muda halafu akasema
“Julieth nahitaji msaada
wako.Nataka kesho asubuhi upande
ndege uende Arusha ukamchukue
mwanangu Millen.Nitagharamia safari
hiyo” akasema Job
“Hakuna tatizo lolote katika
hilo.Nitakwenda Arusha kesho
kumchukua mwanao na nitahakikisha
anafika hapa salama” akasema Julieth
Job akaachana na akina Marcelo
akaenda kumpigia simu Austin
akamfahamisha kila kitu kilichotokea
naye akataarifiwa kile kinachoendelea
kule Kinshasa na baada ya zaidi ya nusu
saa za maongezi wakaagana.
 
QUEEN MONICA : FINAL SEASON
SEHEMU YA 13
Taarifa za kifo cha Ernest Mkasa
rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania na mke wake Agatha zilianza
kusambaa katika mitandao ya kijamii
kama mzaha usiku wa manane na
ilipofika asubuhi taarifa hizi zikazidi
kusambaa kwa kasi kubwa.Ikulu
kulikuwa na pilika pilika nyingi lakini
hakuna aliyetoa tamko
lolote.Mkurugenzi wa habari wa ikulu
akawaita waandishi wa habari ikulu na
hadi ilipotimu saa nne za asubuhi
ukumbi wa habari wa ikulu ulikwisha
jaa waandishi wa habari.Saa nne na
dakika ishirini rais wa Zanzibar
akajitokeza mbele ya waandishi wa
habari
“Habari za asubuhi ndugu waandishi
wa habari na watanzania wote kwa
ujumla” ndivyo alivyoanza hotuba yake
“ndugu wahandishi wa
habari,nimewaiteni hapa ikulu ili kupitia
kwenu watanzania waweze kufahamu kile
kilichotokea na kinachoendelea katika nchi
yetu
Ni jana tu tumetoka katika mazishi ya
kitaifa ya ndugu zetu waliofariki katika
mashambulio ya kigaidi yaliyotokea siku
chache zilizopita katika jiji la Dar es salaam
na mjini Dodoma.Kabla machungu ya
kuwapoteza ndugu zetu hao hayajapoa
taifa letu linajikuta tena katika giza nene
kwa kuondokewa na mtu mwingine
muhimu sana katika taifa letu”
Akanyamaza kwa sekunde kadhaa
halafu akaendelea.
“Ndugu watanzania kwa huzuni
kubwa ninatangazia kwamba usiku wa
kuamkia leo rais wetu mpendwa wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania Ernest
Mkasa,pamoja na mkewe Agatha Ernest
Mkasa wamefariki dunia.” akanyamaza
kwa muda kidogo halafu akasema
Siku ya jana rais,kipenzi chetu Ernest
Mkasa alikuwa mzima wa afya na
aliongoza mazishi ya kitaifa ya marehemu
waliofariki katika mashambulio na hadi
aliporejea ikulu alikuwa salama
salimini.Uchunguzi wa vifo vya rais na mke
wake unaendelea na ukikamilika
mtaelezwa sababu ya vifo vyao.
Ernest mkasa alikuwa ni mmoja kati
ya maraisi shupavu na jasiri sana.Mambo
aliyoyafanya katika kipindi chake kifupi
alichokaa katika uongozi ni makubwa na
yatakumbukwa daima.
Nafahamu taarifa hizi zitawastua
sana na kuwapa hofu kwamba nchi haiko
salama lakini napenda kuwatoa hofu
kwamba nchi yetu iko salama.Tuweni
watulivu katika kipindi hiki kigumu
ambacho tunapitia kama nchi .
Rais Ernest mkasa na mke wake
wataagwa na kuzikwa kwa heshima zote za
kiserikali.Mtatangaziwa hapo baadae
utaratibu wote wa kuaga na hatimaye
mazishi ya kiongozi wetu huyu mpendwa
na mke wake.
Nawaombeni tuendelee kuwa
watulivu na kumuombea mpendwa rais
wetu na mke wake ili Mwenyezi Mungu
mwingi wa rehema aweze kuwapumzisha
mahala panapostahili.
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza
Makamu wa pili wa rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
ambaye pia ni rais wa Zanzibar na
mwenyekiti wa baraza la mapinduzi
akamaliza hotuba yake.
KINSHASA - DRC
Taarifa za msiba wa rais Ernest
Mkasa zilivuka mipaka na kuwafikia
akina Austin wakiwa katika jumba la
kifahari jijini Kinshasa.Amarachi
alikuwa wa kwanza kuiona taarifa hiyo
wakati Austin akiwa bafuni
akioga.Akatoka mbio na kuufungua
mlango wa bafuni na kumstua sana
Austin
“Amarachi kuna tatizo gani ?
akauliza Austin
“Austin kuna tatizo limetokea!!
Akasema Amarachi huku akihema kwa
kasi
“Tatizo gani Amarachi ? akauliza
Austin kwa wasi wasi
“Rais wa Tanzania..’
“ Relax Amarachi.Rais wa
Tanzania amefanya nini?
“he’s dead!
Austin alipatwa na mstuko
mkubwa
‘That’s not true!! Akasema
Amarachi akamshika Austin
mkono wakatoka mle bafuni na kwenda
kutazama runinga na kumkuta
makamu wa pili wa rais ambaye ni rais
wa Zanzibar akimalizia kutangaza kifo
cha rais Ernest
‘How it happened? Nini
kimemuua? Akauliza
“Sababu ya kifo chake haijawekwa
wazi ila amefariki yeye na mke wake
Agatha” akasema Amarachi
“Agatha naye amefariki? Austin
akazidi kushangaa.Wakabaki kimya
wakitazamana.Austin akavaa haraka
haraka wakatoka mle chumbani
wakaelekea katika chumba cha
Monica.Wakagonga mlango na akatoka
daktari mmoja akawaomba wasubiri
kwa muda kwani Monica alikuwa
anafanyiwa vipimo.Wakastuka na
kurejea chumbani kwao
“Siamini bado kama kweli Ernest
amefariki dunia.” Akasema Austin na
kuamua kumpigia simu Job
“Job naomba kabla ya yote
unithibitishie kuhusu taarifa hizi za
kifo cha Ernest Mkasa kama ni za kweli”
akasema Ernest baada ya Job kupokea
simu
“Hizi ni taarifa za kweli.Hata mimi
nimestuka sana baada ya kusikia
kuhusu jambo hili.Japo kwa upande wa
pili nimefurahi lakini nilipenda sana
nionane naye ana kwa ana na apate
mateso yangu kwa kitendo
alichonifanyia.Nimefahamu kumbe
yeye ndiye sababu ya mimi kuteseka
namna ile,kuishi kama kichaa nikila na
kunywa majalalani.Yeye ndiye
aliyemchukua mke wangu” Akasema
Job kwa hasira.
“Vipi kuhusu mwanao Millen?
Tayari amefika Dar es salaam?
“Nimezungumza na Julieth muda
mfupi uliopita tayari amekwisha fika
Arusha na anaelekea shuleni
anakosoma Millen.Nadhani mida ya saa
saba hivi au nane atarejea” Akasema
Job wakaagana na Austin akakata simu
“Ni kweli adui yetu namba moja
amefariki dunia” Austin akamwambia
Amarachi halafu wakakumbatiana kwa
nguvu
“Haijazoeleka kuona watu
wakishangilia kifo cha mtu lakini kwetu
sisi kifo hiki cha Ernest Mkasa ni
ushindi mkubwa”akasema Austin
”So the war is over? Akauliza
Amarachi
“Opereheni kuu ilikuwa ni
kuwaondoa Alberto’s wote
nchini.Baadae upepo ukabadilika na
ikaanza vita baina yetu na Ernest.Ernst
amewaua Alberto’s wote na kwa kuwa
Ernest naye amefariki kwa hiyo hakuna
vita tena ila bado kuna usafi lazima
ufanyike.Ernest alikuwa na vibaraka
wake ambao wote lazima watafutwe
kokote waliko na wafikishwe katika
sheria na wa kwanza ambaye
anatakiwa apatikane kwa haraka sana
ni huyu Jenerali Lameck Msuba ambaye
amekuwa akishirikiana na Ernest
Mkasa na hata katika rekodi tuliyonayo
amesikika akiwasiliana na Ernest
kuhusiana na shambulio la Dar es
salaam.Ukiacha huyu na wengine
ambao wamekuwa wakishirikiana na
Ernest kuna hili kundi la
wafanyabiashara wa dawa za kulevya
ambao orodha yao wote tunao.Hawa
wote nao wanatakiwa wasafishwe
.Japokuwa mapambano yamekwisha
lakini bado tuna kazi kubwa inatusubiri
ya kuisafisha nchi lakini hii haitakuwa
yetu peke yatu bali tutashirikiana na
vikosi na watu wazalendo” akasema
Austin.
“Ernest amekufa bila ya Monica
kujua kama ni baba yake.What are you
going to do? Akauliza Amarachi
“Wazazi wake ndio wenye jukumu
hilo la kumwambia ukweli.” Akasema
Austin
“What about us? Akauliza
Amarachi na kabla Austin hajajibu kitu
mlango ukagongwa Amarachi
akaufungua na kukutana na Monica
“Are you ok Monica? Tumekuja
kukutazama tukaambiwa kwamba uko
na madaktari unafanyiwa vipimo.Kuna
tatizo lolote? Akauliza Austin na Monica
akatoa tabasamu kubwa na kusema
“Kuna jambo la furaha sana
ambalo nataka kuwashirikisheni ndugu
zangu” akasema Monica na kwenda
kuketi sofani
“Madaktari wale walikuja
kunipima ili kujua kama nina
ujauzito.Majibu yametoka mazuri
kwamba ni kweli nina ujauzito”
akasema Monica na Amarachi akainuka
wakakumbatia kwa furaha.Austin naye
akawafuata na wote wakakumbatiana
wakimpongeza Monica
“Hizi ni habari njema mno kwa
siku kama ya leo.Lakini pamoja na
habari hizo njema kuna habari ambazo
si nzuri pia” Akasema Austin na
kumstua Monica .
“Kuna habari gani? Akauliza
Monica kwa wasi wasi
“Tumepata habari muda mfupi
uliopita kwamba rais Ernest Mkasa
amefariki dunia”
“What ?! Amefariki dunia? How?
Akauliza Monica
“Bado haijawekwa wazi nini
kimemuua lakini kifo chake tayari
kimethibitishwa na kutangazwa na rais
wa Zanzibar ambaye ni makamu wa pili
wa rais”akasema Austin na Monica
akashusha pumzi
“Hatimaye nchi imesalimika.The
war is over” akasema Monica
“Ernest alikuwa rais shetani
kabisa na nina uhakika mkubwa
kwamba huko aliko hivi sasa atakuwa
anawaka katika moto wa
jehanamu.Ameteketeza roho za watu
wengi sana wasio na hatia.” Akasema
Monica
“Kwa sasa nchi iko salama lakini
lazima tuhakikishe tunaipata hati ya
muungano ili kuinusuru kugawanyika
vipande vipande”akasema Austin
“Uhakika wa kuipata ni mkubwa
kwani David amekwisha ahidi
kutusaidia hadi tuipate hati ya
muungano.Atakuja hapa muda si mrefu
sana” akasema Monica.
DAR ES SALAAM - TANZANIA
Saa tisa na dakika kumi ndege ya
abiria kutoka Arusha ikawasili katika
uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar
es salaam na miongoni mwa abiria
waliokuwamo katika ndege hiyo
alikuwa ni Julieth aliyekwenda
kumchukua Millen.Job alikuwepo
uwanjani akiwa na furaha
iliyochanganyika na woga.Kwa miaka
kadhaa hakuwa amemuona mwanae.
Abiria waliokuwa ndegeni
wakaanza kushuka na katika sehemu
ya kusubiria abiria akatokea Julieth
akiwa amemshika mkono Millen.Job
akapatwa na furaha ya ajabu sana
kumuona tena mwanae Millen.
“Julieth!! akaita Job na Julieth
akageuka akamuona Job na kumfuata
“Dady!! akasema Millen kwa
mshangao na kumkimbilia Job
akamkumbatia.
“Millen my soul..!! akasema Job
“Mama aliniambia kwamba
ulipotea ukiwa kazini Sudan !! akasema
Millen
“Millen my daughter,I’m still
alive.I didn’t die !! akasema Job
Wote wakaingia garini na
kuondoka kuelekea katika hoteli ya
Amarachi ambako tayari kuna chumba
kizuri kilikuwa kimeandaliwa kwa ajili
ya Millen.
“Millen utabaki hapa na aunt
Julieth.Mimi ninakuja muda si mrefu
kuja kukuchukua na kukupeleka
nyumbani” akasema Job na kuingia
garini akarejea nyumbani.Akamfunga
kitambaa Monalisa na kumpakia garini.
“Unanipeleka wapi? Akauliza
Monalisa lakini Job hakumjibu
kitu.Baada ya kama dakika ishirini
hivi,Job akasimamisha gari na
kumfungua Mona kile kitambaa usoni.
“Now its over.Nilikuahidi
sintakufanya chochote and now I’m
leting you go.Lakini kabla sijakuacha
uendelee na maisha yako kuna mambo
mawili ambayo nataka
uyafahamu.Kwanza ni kukufahamisha
kwamba tayari nimempata mwanangu
Millen yuko sehemu salama.Pili bwana
wako rais Ernest amefariki dunia usiku
wa kuamkia leo kwa hiyo umekuja kwa
wakati muafaka ili kuhudhuria msiba
wa mume wako”
“That’s not true !! akasema
Monalisa na Job akatoa tabasamu
kubwa
“Get out of my car !! akasema Job
“Job huwezi kuniacha namna hiyo
!! Huwezi kuniacha hapa !! akasema
Mona .Job akashuka akaenda
kuufungua mlango wa upande aliokaa
Mona na kumvuta nje.
“Thank you for everythig
Monalisa.Nakutakia maisha mema.”
Akasema Job na kuingia garini kisha
akaondoka kwa kasi akimuacha
Monalisa ameduwaa asijue afanye nini.
 
Back
Top Bottom