Radi yaua watoto wawili wa familia moja Handeni

Radi yaua watoto wawili wa familia moja Handeni

Bravo snr

Senior Member
Joined
Aug 16, 2020
Posts
182
Reaction score
477

Saturday May 01 2021

In summary

Waliofariki ni Jafari Amiri (12) mwanafunzi wa darasa la nne na Hamidu Amiri (9) mwanafunzi wa darasa tatu.

Handeni. Watoto wawili wa familia moja wakazi wa kata ya Malezi wilayani Handeni Mkoa wa Tanga wamefariki baada ya kupigwa na radi.
Diwani wa Malezi, Shabani Kitombo leo Jumamosi Mei Mosi, 2021 amethibitisha kutokea kwa tukio hilo leo jioni wakati watoto hao wakiwa nyumbani kwao.

“Wakiwa ndani radi iliwapiga na kufariki dunia hapohapo kabla ya kupatiwa huduma ya kwanza.

Walioshuhudia tukio hilo wamesema watoto walikuwa nyumbani kwao wakati mvua inanyesha na punde ilipiga radi ambayo imesababisha vifo vyao,” amesema.
 
Mungu akawe faraja kwa familia yao ...
 

Saturday May 01 2021

In summary

Waliofariki ni Jafari Amiri (12) mwanafunzi wa darasa la nne na Hamidu Amiri (9) mwanafunzi wa darasa tatu.

Handeni. Watoto wawili wa familia moja wakazi wa kata ya Malezi wilayani Handeni Mkoa wa Tanga wamefariki baada ya kupigwa na radi.
Diwani wa Malezi, Shabani Kitombo leo Jumamosi Mei Mosi, 2021 amethibitisha kutokea kwa tukio hilo leo jioni wakati watoto hao wakiwa nyumbani kwao.

“Wakiwa ndani radi iliwapiga na kufariki dunia hapohapo kabla ya kupatiwa huduma ya kwanza.

Walioshuhudia tukio hilo wamesema watoto walikuwa nyumbani kwao wakati mvua inanyesha na punde ilipiga radi ambayo imesababisha vifo vyao,” amesema.

Bahati mbaya sana kwao.

Ndani ya nyumba. Watoto wadogo. Watu wachukue tahadhari ipi?

Hiiiiii bagosha.

Wapumzike kwa amani watoto hawa.
 
Unataka kusema walikua ndani na nyumba ni nzima kabisa aijabomoka sehemu !!!????
 
So sad! R.I.P watoto,😒

ila mechanism ya radi sijawahi kuielewa kabisa, mara iangukie na ikaushe miti, pia wanasema inaweza ikaanguka na kuondoka bila kuleta madhara yeyote hapo.mara inaweza ikaingia hadi ndani🤔 Mungu atuepushie tu.
Radi ni umeme wenye nguvu sana , ikija inatafuta conductor ( kupitisha umeme ) ,ili ipitie hapo , ndio maana nyumba nyingi uwekwe steel rod kulichojitokeza juu ya Bati ili iweze kupitia humo , wanyama na miti mibichi upitisha umeme ndio maana ufuatwa na radi iwapo chenyewe kirefu kwenye maeneo hayo, radi nyingine uwa za kishirikiana lakini ( Kama wasemavyo baadhi ya watu )
 
Radi ni umeme wenye nguvu sana , ikija inatafuta conductor ( kupitisha umeme ) ,ili ipitie hapo , ndio maana nyumba nyingi uwekwe steel rod kulichojitokeza juu ya Bati ili iweze kupitia humo , wanyama na miti mibichi upitisha umeme ndio maana ufuatwa na radi iwapo chenyewe kirefu kwenye maeneo hayo, radi nyingine uwa za kishirikiana lakini ( Kama wasemavyo baadhi ya watu )
Ok nimekuelewa mkuu! Ila hizo steel rod zinasaidia kweli? Na sidhani kama watu wanapewa elimu hii wanapojenga nyumba zao hasa humo vijijini🤔 dah hizo radi za kichawi nazo mmh ni hatari na watu ni fundi basi tu
 
Ok nimekuelewa mkuu! Ila hizo steel rod zinasaidia kweli? Na sidhani kama watu wanapewa elimu hii wanapojenga nyumba zao hasa humo vijijini🤔 dah hizo radi za kichawi nazo mmh ni hatari na watu ni fundi basi tu
Zinasaidia sana , Ila mara nyingi uwekwe ghorofani , kwenye nyumba za kawaida kuwekwa sio sana ( hasa vijijini) kwa kuwa watu wengi hawana elimu husika , kingine vijijini miti mibichi mirefu ni mingi yaani nyumba ni fupi kuliko miti , hivyo radi ikija ufika Kwanza kwenye miti kabla ya nyumba
 
Ok nimekuelewa mkuu! Ila hizo steel rod zinasaidia kweli? Na sidhani kama watu wanapewa elimu hii wanapojenga nyumba zao hasa humo vijijini🤔 dah hizo radi za kichawi nazo mmh ni hatari na watu ni fundi basi tu
Kingine radi uwambatana na sauti , yaani mwanga na sauti , kwa kuwa mwanga ( light) Una speed kubwa kuliko sauti , mwanga uunza kutokea kabla ya sauti ( radi) , huu mwanga ( lighting) ndio hatari zaidi kuliko hiyo sauti , lighting ndio usababisha madhara , Ila watu wengi uogopa sauti
 
Back
Top Bottom