Raha ya kuwa na tume huru ya uchaguzi hakuna mwenye uhakika wa kushinda watu wanamenyana kweli kweli

Huku NEC inajua mshindi wa 2025 ni nani inasubiri tu kumtangaza
 
Hii nchi imekuwa ni takataka kabisa, kila kitu ni hovyo kuanzia serikali feki iliyoingia ikulu kwa mtutu wa bunduki, bunge ni halmashauri kuu ya chama tawala, mahakama ni ya kangaroo, yani kila kitu ni hovyo tu.

Leo hii ili uwe jaji sifa kubwa kabisa lazima uwe mwanachama wa chama tawala na weledi sio muhimu na hiyo inahusu hadi wataalamu katika nyanja mbalimbali.

Miaka kadhaa ijayo hiki chama kiking'ang'ania madarakani huenda hata madaktari pia watatakiwa kuwa wanachama wa chama hicho.
 
Una uhakika Kenya Wana tume huru ya uchaguzi?🤔
 
Kwani sisi huwa tunachinjana kila baada ya uchaguzi?
Kwani Tanzania kuna uchaguzi. Uliona wapi chama kinachoshiriki kwenye uchaguzi eti ndicho kina andaa na kusimamia utaratibu wote katika huo uchaguzi halafu eti unakuta RPC ana orodha ya watakaoshinda ubunge/udiwani kwenye mkoa hata kabla ya tarehe ya uchaguzi.

Tanzania inapofika kwenye maswala ya uchaguzi muwe na aibu na mkae kimya kabisa kwani kwenye nchi yenu waga hamna uchaguzi ni uhuni tu mnafanya. Bure kabisa.
 
Kama hatuna uchaguzi basi hoja yako inakosa mashiko. Inabidi uanzishe hoja ya kutaka tuanze kufanya uchaguzi kwanza, then yatokanayo na huo uchagzi ndo yatafuata.
 
Kumbuka akiwa madarakani uchaguzi uliopita ilibidi urudiwe .tume ya uchaguzi Kenya ilimtoa jasho uhuru alishindwa Cha kuwafanya
mkuu kwa hapa bongo kama samia akionyesha upande wake kwa wagombea ni kibega tayari na kelele mngetoa sana,ila ni kenya na kusifu mnasifu.
 
Hapo ndipo utakapoona THAMANI ya kura yako sio hapa kwetu haswa 2020 kwenye Uchafuzi Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…