Raia Mwema: Tozo kufutwa, Mwigulu kuwasilisha Mapendekezo mapya Bungeni

Raia Mwema: Tozo kufutwa, Mwigulu kuwasilisha Mapendekezo mapya Bungeni

Hii ndiyo Taarifa mpya inayosambaa kwa kasi kwa muda huu, kwamba serikali imekubali kufuta Tozo zote ili kuitikia kilio cha wananchi.

Chanzo: Raia Mwema

Swali: Zile hela zetu walizotukata tangu Tozo zianze tutarudishiwaje?
Itakua safi sana
 
Nina wasiwasi tozo zitarudi kwa jina jipya la kodi, yaani tutapandishiwa kodi mpaka tujute.

Mwl Nyerere aliwahi kusema, mtu akila nyama ya binadamu ni ngumu kuacha, washazoea utamu wa pesa sidhani kama wataacha hivi hivi lazima watukamue tuu
hapa umesema ukweli.lazima watafute chanzo kingine cha kutukamua kwa jina jingine sababu kwenye walikuwa wanapata fedha nyingi na lazima mapato hayo yatafutiwe chanzo kingine.
 
Hizi siasa tozo zitabadilishwa njia ya kuzipata lakini haziwezi kufutwa. Ni matakea ya mabeberu tukusanye hela zaidi ndani tulipe mikopo

Sent from my Infinix X605 using JamiiForums mobile app
Mikopo itaziba pengo.

Lakini wakiwa na dhamira njema, wanaweza kupunguza matumizi mabaya ya fedha kwa Serikali.

Kuna matumizi mengi ya hovyo ya Serikali:

1) Iwe marufuku Serikali kununua V8. Badala ya V8, inunue prado na landcruiser mikonga.

2) Misafara ya viongozi wakuu, isizidi magari 25.

3) Posho za safari zishushwe toka 250,000 mpaka150,000 kwa siku.
 
Hii ndiyo Taarifa mpya inayosambaa kwa kasi kwa muda huu, kwamba serikali imekubali kufuta Tozo zote ili kuitikia kilio cha wananchi.

Chanzo: Raia Mwema

Swali: Zile hela zetu walizotukata tangu Tozo zianze tutarudishiwaje?
Sahau kuhusu kurudisha.Zimeenda kujemga shule,zahanati nk htkusikia?
 
Hii ndiyo Taarifa mpya inayosambaa kwa kasi kwa muda huu, kwamba serikali imekubali kufuta Tozo zote ili kuitikia kilio cha wananchi.

Chanzo: Raia Mwema

Swali: Zile hela zetu walizotukata Yaa

Hii ndiyo Taarifa mpya inayosambaa kwa kasi kwa muda huu, kwamba serikali imekubali kufuta Tozo zote ili kuitikia kilio cha wananchi.

Chanzo: Raia Mwema

Swali: Zile hela zetu walizotukata tangu Tozo zianze tutarudishiwaje?
Yaani penalty wasababishe wao,halafu penalty wapige wao na points 3 wachukue wao 😂😂😂
 
Waturudishie hela hizo!
Ndugu yangu TUJITEGEMEE, kweli uvumilvu una mwisho...sikutegemea kabisa hata wewe kuna siku utaonesha kuishangaa serikali ya CCM na kukiri uovu kama huu dhidi ya Watanzania wenzako.

Anayedai kuwa na PhD ya heshima katika uchumi katu hawezi kubuni wizi kama huu dhidi ya wananchi ambao amebahatika kuwa kiongozi wao.

La pili hizo pesa zilizopatikana kwa njia hii ambayo hata yeye baada ya kuzidiwa hoja kakiri pengine haikuwa halali, je tulioibiwa tutarudishiwa?

Mtaalamu wa uchumi mwenye PHD hawezi kukata eti tozo kwenye akiba iliyo benki. Benki ndiyo inatakiwa imlipe faida kwa kutumia pesa zake kama mtaji.

Mtaalamu wa uchumi mwenye PhD hawezi kukata tozo kwenye hela iliyokatwa kodi zaidi ya mara moja, huo ni wizi na hata sheria za kodi haziruhusu kamwe.

Mtaalamu wa uchumi mwenye PhD hawezi kukosa uzalendo kwa taifa lake na kuwatishia wananchi ambao ndio walipa kodi wahamie Burundi kama wanahoji tozo.

Mtaalamu wa uchumi mwenye PhD, anayethubutu kubuni mbinu chafu kama alivyofanya Mwigulu, ni kuvuliwa hiyo PhD yake ya heshima na kuchunguzwa aliipataje?
 
Ndugu yangu TUJITEGEMEE, kweli uvumilvu una mwisho...sikutegemea kabisa hata wewe kuna siku utaonesha kuishangaa serikali ya CCM na kukiri uovu kama huu dhidi ya Watanzania wenzako.

Anayedai kuwa na PhD ya heshima katika uchumi katu hawezi kubuni wizi kama huu dhidi ya wananchi ambao amebahatika kuwa kiongozi wao.

La pili hizo pesa zilizopatikana kwa njia hii ambayo hata yeye baada ya kuzidiwa hoja kakiri pengine haikuwa halali, je tulioibiwa tutarudishiwa?

Mtaalamu wa uchumi mwenye PHD hawezi kukata eti tozo kwenye akiba iliyo benki. Benki ndiyo inatakiwa imlipe faida kwa kutumia pesa zake kama mtaji.

Mtaalamu wa uchumi mwenye PhD hawezi kukata tozo kwenye hela iliyokatwa kodi zaidi ya mara moja, huo ni wizi na hata sheria za kodi haziruhusu kamwe.

Mtaalamu wa uchumi mwenye PhD hawezi kukosa uzalendo kwa taifa lake na kuwatishia wananchi ambao ndio walipa kodi wahamie Burundi kama wanahoji tozo.

Mtaalamu wa uchumi mwenye PhD, anayethubutu kubuni mbinu chafu kama alivyofanya Mwigulu, ni kuvuliwa hiyo PhD yake ya heshima na kuchunguzwa aliipataje?
Siku ya mwisho kila goti litapigwa
 
AxVmM9o.gif

Ngoja tuone.
 
Ndugu yangu @TUJITEGEMEE, kweli uvumilvu una mwisho...sikutegemea kabisa hata wewe kuna siku utaonesha kuishangaa
Mkuu, kwa kurejea msemo wa wananzengo, saa yako mbovu kuna wakati saa hiyo hiyo huwa inakuonyesha muda sahihi. Ha ha hahahaha AA!

Asante, Mkuu. Ninafurahi mnapotoa maoni.
 
CCM na wabunge wao walikurupuka, huwezi kujenga uchumi wa nchi kwa TOZO, nchi inajengwa kwa kuuza bidhaa ndani na nje ya nchi kwa wingi.
Kilimo kimewashinda
Viwanda vimewashinda
Mkakimbilia njia ya mkato ya Tozo, haya wenye nchi yao wamewagomea!!
 
Hii ndiyo Taarifa mpya inayosambaa kwa kasi kwa muda huu, kwamba serikali imekubali kufuta Tozo zote ili kuitikia kilio cha wananchi.

Chanzo: Raia Mwema

Swali: Zile hela zetu walizotukata tangu Tozo zianze tutarudishiwaje?
Na zikifutwa kweli bado Kuna watu watalaumu Tena, hii Nchi ngumu sana
 
Back
Top Bottom