Marekani kuna vyama vingi vya siasa mbali na Democrat na Republicans.
Uchaguzi wa marekani mwaka 2020 una wagombea zaidi ya kumi toka vyama tofauti na hivyo viwili lakini pia marekani inaruhusu mgombea binafsi.
Hawa baadhi wagombea wa USA mwaka huu ukitoa Trump na Biden.
- Howie Hawkins wa chama cha Green Socialist
- Jo Jorgensen wa chama cha Libertarian
- Don Blankenship wa chama cha Constitution
- Brian T. Carroll wa chama cha American Solidarity.
- Roque De La Fuente wa chama cha American Delta Party
Kuhitimisha kuna wgombea 21 kwenye nafasi ya uraisi wa marekani, lakini sio majimbo yote hao wagombea watatokea kwenye ballots. Majimbo yatakayokuwa na wagombea wote ni
Vermont na
Colorado. Pitia hii linki
Presidential candidates, 2020 - Ballotpedia kuelewa jinsi uchaguzi wa US unavyofanyika na pia kuwafahamu wagombea wengine.
Tunawajuwa Trump na Biden kwa sababu wanatoka kwenye vyama vikubwa na vikongwe nchini Marekani ila vyama vya siasa vipo vingi.