Raila Odinga ana hoja,Tume imeteleza. Fomu 34A na 34B zipo kisheria

Raila Odinga ana hoja,Tume imeteleza. Fomu 34A na 34B zipo kisheria

Tume imedai imeshtushwa na tuhuma zinazotolewa hivi sasa kwa sababu vyama vyote viliwakilishwa na vikakubaliana hivyo.
Tatizo la vyama vinavyoshindwa vinapenda kubadili magoli kila mara.. Wanaomba hivi, wakiona weshindwa wanageuka
 
Pamoja na kwamba huwa tunatofautina mambo mengi, kwa hili nakuunga mkono kwa 100%. Sipunguzi wala kuongeza neno bali napigia majibu mstari.
Hivyo inakubidi uwaambie kina Mbowe hata kama watam support Uhuru yatawakuta ya Odinga pamoja ba urafiki na Sir Magu hakuna cha msaada. Nilijiuliza sana kwanini Lowasa kapoteza muda wake kwenda kushiriki kukandamiza demokrasia nchi nyingine?
 
leo umeongea kama binadamu aliyekamilika with all 5 senses of organ
Kila siku ninaongea/ninaandika kama binadamu aliyekamilika mwenye fikra zinazoangaza katika mlengo wa 3D Thinking.

Ninafahamu ukweli ni mchungu na kile ambacho hukubaliani nacho lazima utadhani sio ukweli
 
That's why I will not vote again in any upcoming elections...... Wa Africa democracy haituhusu....
True, most of thirdworld country election is to halalisha tu waliopo madarakani. Heri kuwa dog in true democratic countries, than human in countries which is primitive in election democras. BONGO BADLACK.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawana Mamlaka ya kudukua Kanzi Data ya IEBC! Kwa kifupi ni kwamba Jubilee na NASA wote wamedukua Kanzi Data ya IEBC ila Nasa wamewakuta JP, wakawaacha. Ilipofika asubuhi NASA wakakimbilia kwa Wananchi ooh JP, ooh Jubilee! Upuuzi mtupu

Bora umeniwahi mkuu.manake nami nilikuwa najiuliza kwa nia ya kutaka kujuzwa kwamba inakuwaje NASA wanasema JP wamedukua mfumo.wao walijuaje hilo. Au wao wana access privilege?
 
Sipendi kuminywa kwa demokrasia ya nchi yoyote ile,ila kwakua alimsaidia mfalme wa kuropoka na ukandamizaji wa wananchi,acha nayeye aluone ! Mshale kwa panya kwa chura unauma.atulie tu !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Africa bado tunatumia tumbo kwa kila kitu tukiweza kufikia uwezo wa kutumia vichwa ndio tutaanza kufanya mambo sahihi. Kwa sasa acha tumbo lifanye kazi.

Boss Dorrlyn Umeua na Kumaliza zote kabisa. Mimi nafikiri Ngozi nyeusi tumelaaniwa na kulogwa. Na aliyetuloga na kutulaani alishafariki.
 
Siku alipouwawa yule mkuu wa kitengo cha teknologia ya habari na mawasiliano kwenye tume ya Uchaguzi, Chris Msando ndio siku ambayo uchaguzi Mkuu ulihitimisha mwanzo wa vurugu za Uchaguzi Mkuu.
Watu wa IT wa Odinga wamegundua kuwa marehemu ame log in!inaonekana kuna watu wameingia kwa akaunti ya marehemu wakafanya figisu
 
Katika watu wanaonifanya niione fani ya sheria ni ya wababaishaji ni huyu Petro E. Mselewa lakini ninapowafikiria Tundu Lissu, Kibatala na Fatma Karume then naacha kuilaumu sheria kama fani badala yake nalaumu kila mwanasheria kivyake.
 
Niliwahi kuanzisha uzi kuhusu 'u-huru' wa tume huru ya uchaguzi ambayo wapinzani wamekuwa wakiililia.

Nadhani sasa labda ambao hawakunielewa wataweza kunielewa.

Kuna dhana potofu kwamba uwepo wa tume 'huru' basi ndo utakuwa mwarobaini wa matatizo wayapatayo wapinzani.

Kama tunavyoona huko Kenya, uwepo wa tume 'huru' si mwisho wa figisu.

Ni dhahiri kabisa kuwa Odinga kafanyiwa figisu na ambaye hakuliona hilo kuwa litatokea atakuwa mbumbumbu wa mwisho kabisa.

Na ndo maana nikasema [kwenye ule uzi wa updates za matokeo ya uchaguzi wa Kenya] kuwa ningeshangaa sana endapo Uhuru Kenyata angeshindwa!

Anayedhani kuwa hiyo IEBC ni huru namwonea huruma😀
Naomba niende kinyume na wewe tume huru ni dhana, ila uhalisia wake haupo katika maana/dhana/definition ila upo katika utendaji kazi wake kwa maana uhuru/kutoingiliwa, uwazi, effeciecy ya kumudu majukumu ya kichaguzi, usawa/fairness na mwisho kabisa uundwaji wake/upatikanaji wake na udhibiti wake kwa maana ya vyombo kama mahakama huru au kamati zibiti za ambazo zitakuwa shirikishi za wanufaika wa chaguzi. Tume ikitimiziwa haya inaweza kuwa huru.
 
Kujazwa kwa Fomu nilizozitaja,ni sharti la kisheria. Lazima kuzijaza na kuziwasilisha. Inataarifiwa kuwa Tume ya Uchaguzi ilitangaza matokeo bila Fomu 34A na 34B. Kwasasa,Tume inakusanya Fomu wakati matokeo yameshatangazwa na kubishiwa.

Hivyo,Odinga ana hoja ya kisheria kuyabishia matokeo hayo. Je,atayapinga matokeo ya Urais kisheria au kisiasa? Matokeo yaliyotangazwa bila fomu husika yanabakije kama halali? Raila Odinga ataamua muda ukifika.Kwa mujibu wa Katiba ya Kenya,Tume ya Uchaguzi ina siku 7 kumtangaza mshindi wa Urais.

Mkuu umepigilia msumari.
TUME ya uchaguzi imesalimu amri na imekubaliana na hoja zako na za RAILA


 
Hizi ndizo tume zetu ''huru'' za Uchaguzi!

Tume ''huru'' ya Uchaguzi inatangaza matokeo ya Uchaguzi ''huru'' halafu baadaye inatuambia hayo sio matokeo rasmi ya Uchaguzi!

Kwa kifupi, kwenye siasa za nchi ''zinazoendelea'' ni vigumu sana kumshinda Rais ambaye anatetea kiti chake cha Urais. Huu ndio ukweli pamoja na kwamba ni vigumu kuukubali.

Siku alipouwawa yule mkuu wa kitengo cha teknologia ya habari na mawasiliano kwenye tume ya Uchaguzi, Chris Msando ndio siku ambayo uchaguzi Mkuu ulihitimisha mwanzo wa vurugu za Uchaguzi Mkuu.

Tume ya Tanzania ndio most corrupt kabisa
 
Hizi ndizo tume zetu ''huru'' za Uchaguzi!

Tume ''huru'' ya Uchaguzi inatangaza matokeo ya Uchaguzi ''huru'' halafu baadaye inatuambia hayo sio matokeo rasmi ya Uchaguzi!

Kwa kifupi, kwenye siasa za nchi ''zinazoendelea'' ni vigumu sana kumshinda Rais ambaye anatetea kiti chake cha Urais. Huu ndio ukweli pamoja na kwamba ni vigumu kuukubali.

Siku alipouwawa yule mkuu wa kitengo cha teknologia ya habari na mawasiliano kwenye tume ya Uchaguzi, Chris Msando ndio siku ambayo uchaguzi Mkuu ulihitimisha mwanzo wa vurugu za Uchaguzi Mkuu.
So you mean wao ndo walimyonğelea mbali? Kisa madaraka ya kulevya? La Mungu atusaidie sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mgombea wa Urais wa Kenya kupitia NASA,Raila Odinga amejitokeza na kupinga matokeo ya awali ya Urais ya Kenya yanayotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya yakimweka mbele Rais Uhuru Kenyatta.

Hoja ya Odinga ni kukosekana kwa Fomu 34A na 34B zinazopaswa kujazwa na kusainiwa,ikiwa ni pamoja na mawakala, kisheria kabla ya kutangazwa matokeo. Fomu 34A hujazwa na kusainiwa katika Kituo cha Kupigia kura. Kimsingi,Fomu 34A hubeba taarifa za kura za kituo kimoja.

Fomu 34A huwasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo. Taarifa zote za vituo vya Jimbo husika hujazwa kwenye Fomu 34B. Hatimaye,Fomu 34B huwasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi kwa ajili ya kutangazwa matokeo rasmi.

Kujazwa kwa Fomu nilizozitaja,ni sharti la kisheria. Lazima kuzijaza na kuziwasilisha. Inataarifiwa kuwa Tume ya Uchaguzi ilitangaza matokeo bila Fomu 34A na 34B. Kwasasa,Tume inakusanya Fomu wakati matokeo yameshatangazwa na kubishiwa.

Hivyo,Odinga ana hoja ya kisheria kuyabishia matokeo hayo. Je,atayapinga matokeo ya Urais kisheria au kisiasa? Matokeo yaliyotangazwa bila fomu husika yanabakije kama halali? Raila Odinga ataamua muda ukifika.Kwa mujibu wa Katiba ya Kenya,Tume ya Uchaguzi ina siku 7 kumtangaza mshindi wa Urais.
mheshimiwa mkubwa wakat mwingine uwe unafatilia habari kabla ya kuleta uzi...... walichofanya tume ni matakwa ya kisheria baada ya NASA kwenda mahakamani.......

awali sheria ya tume ni kutangaza matokeo sambamba na hizo forms, lkn NASA wakaenda mahakamani kupinga wakidai huenda matokeo yakachakachuliwa in btn...... hivyo wakaiomba mahakama iamure tume itangaze matokeo ya moja kwa moja toka mtandaoni kabla ya forms.......

na kwa kulijua hilo tume waliendelea kutangaza matokeo hata baada ya malalamiko ya NASA, na ndio maana NASA hawajaenda mahakamani kuzuia IEBC isitangaze matokeo mpk hizo forms kw vile wangekua wanapingana na ombi lao la awali.......



Sent using Jamii Forums mobile app
 
mheshimiwa mkubwa wakat mwingine uwe unafatilia habari kabla ya kuleta uzi...... walichofanya tume ni matakwa ya kisheria baada ya NASA kwenda mahakamani.......

awali sheria ya tume ni kutangaza matokeo sambamba na hizo forms, lkn NASA wakaenda mahakamani kupinga wakidai huenda matokeo yakachakachuliwa in btn...... hivyo wakaiomba mahakama iamure tume itangaze matokeo ya moja kwa moja toka mtandaoni kabla ya forms.......

na kwa kulijua hilo tume waliendelea kutangaza matokeo hata baada ya malalamiko ya NASA, na ndio maana NASA hawajaenda mahakamani kuzuia IEBC isitangaze matokeo mpk hizo forms kw vile wangekua wanapingana na ombi lao la awali.......



Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ndivyo, kwanini sasa Tume inatangaza tena matokeo kwa kutumia hizo Fomu?
 
Kama ndivyo, kwanini sasa Tume inatangaza tena matokeo kwa kutumia hizo Fomu?
mbona nimeeleza hapo kwenye hio post, ni kwamba baada ya matokeo yote kujumlishwa ndipo hizo forms zitatumika kuhakiki hayo yaliyotangazwa......

huo sio uamuzi wa tume ni makubaliano kati ya vyama vyote shiriki, pia ndio takwa la kisheria kuhusu uchaguzi....... yaani hawatangazi matokeo RASMI bila kupitia hatua zote izo ili haki sio tu itendeke bali ionekane imetendeka.....

wakitoka hapo, ndipo watatangaza, kisha watatoa siku 7 kwa ambae hajaridhika na mchakato kwenda mahakamani kusema shida yake!..... infact wana utaratibu ambao hata mtoto mdogo ataelewa kama kuna udanganyifu au la

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom