Raila Odinga anaamini Rais Magufuli hashauriwi vizuri

Raila Odinga anaamini Rais Magufuli hashauriwi vizuri

Baada ya kushindikana kukutana au kufanya mkutano kwa njia ya video call, hatimaye imefahamika nini kinaendelea chini ya zulia.

Kupitia vyombo vya habari vya kimataifa kama BBC, inaelekea viongozi wa nchi kadhaa za Afrika Mashariki wamekuwa na nia ya kukutana kama siyo kuongea na Rais wa Tanzania JPM ili kujadili issue ya covid-19 bila mafanikio wamekwama.

Kutokana na mkwamo huo, inaonekana viongozi hao kama Museven, Kenyatta na Kagame wamejitahidi kuwasiliana na mkuu lakini bila mafanikio yoyote, hali hiyo imepelekea kupata njia mbadala ya kuwasiliana naye.

Njia iliyopatikana ni kumtumia rafiki wa karibu wa Rais Magufuli ambaye ni Waziri mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga ambaye yeye mwenyewe amekili kumpigia simu mara kadhaa lakini bila mafanikio haikuweza kupokelewa.

Lengo la kutaka kufanya maongezi ni kuangalia njia mahususi inayochukuliwa au kuchukuliwa dhidi ya gonjwa hatari linaloendelea kupukutisha binaadamu hapa nchini na nchi za ukanda wa maziwa makuu.

Hata hivyo alichoweza kufanya Odinga ni kuandika ujumbe wa maandishi (sms) na kumtumia Rais Magufuri ili akiupata aweze kuwasiliana naye.
 
Wanamtafuta kwa maswala binafsi au ya kiofisi? Kama ni masuala ya kiofisi, rais ni taasisi hivyo wawasiliane na ofisi. Tatizo hao wamezichukulia nchi zao kama mali binafsi.
 
Wanamtafuta kwa maswala binafsi au ya kiofisi? Kama ni masuala ya kiofisi, rais ni taasisi hivyo wawasiliane na ofisi. Tatizo hao wamezichukulia nchi zao kama mali binafsi.
Kipindi nipo mdogo tulikuwa tunaambiwa kuwa Raisi hata simu huwa hagusi. Wala pesa. Ila huyu ananyanyua simu muda wowote anapigia shirawadu au diamond akiwa kwenye shoo alafu unasema kuna Taasisi apo.
Anabeba besa anagawa atakavyofurahishwa unasema kuna taasisi hapo?

Kumbuka kama wanamtafta kiofice, ofice yake ipo makao makuu dodoma ila anazaidi ya mwezi hajakanyaga uko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
6 May 2020
Johannesburg, RSA

COVID-19 and Africa | Majority of African countries have responded well to pandemic: Raila Odinga



Africa could emerge stronger and more united from the COVID-19 crisis as it looks for more coordinated solutions to the disease. This is according to the African Union Head of Infrastructure Development High Representative Hon.Raila Odinga.

Hon. Odinga says with African innovators now seeking homegrown solutions to some of the emerging challenges in containing the disease, the continent could be more self-reliant. Let's cross to Kenya in Nairobi where our East Africa Correspondent Sarah Kimani is having an exclusive interview with Raila Odinga.
Source: SABC Digital
 
Hiyo title umeandika kishigongo kweli kweli
Mkuu media zinazotumia magazeti na mitandao zinauza story kwa heading vinginevyo utabaki na gazeti au kabrasha lako.
 
Wanajukwaa,yule rafiki mkubwa wa Magu katika ukanda huu wa Afrika mashariki bwana Raila Odinga amekiri kwamba huenda rais Magufuli hapewi ushauri mzuri na amewaasa viongozi wengine wampe ushauri kwani ni msikivu. Hayo yamejiri wakati akihojiwa na kituo cha habari, japo haikuwekwa wazi ni katika jambo gani ndugu Raila ameona rais hashauriwi vizuri.

WanaJF vipi maoni yenu kuhusu ushauri wa Raila Odinga?

Kwahiyo hako ka tweet ndio ithibati ya kauli ya Raila ? Haki watizedi ! Nimewachoka


Mk54
 
Raila amesema viongozi wa kanda wamekua wakitaka kushauriana na rais John Pombe Magufuli, bila mafanikio.
Video: SABC
Virusi vya corona: Kiongozi wa upinzani wa Kenya Raila Odinga amesema Rais Magufuli ''anashauriwa vibaya'' - BBC News Swahili

Raila amesema
"Sijaweza kuongea na rafiki yangu, nimejaribu kumfikia kwenye simu lakini sijafanikiwa ila nimemuachia ujumbe kwamba ningependa kujadiliana nae masuala yenye tija kitaifa, kikanda, kibara na hata kimataifa. Nadhani yeye kama mzawa na mzalendo, anahitaji kupata taaria toka kwa viongozi wenzake.

Nadhani rais Uhuru pia amejaribu kuzungumza naye, rais Museven; kwasababu mara kwa mara tunashirikishana taarifa, Museveni, Kagame na wengineo kwasababu hili ni suala la kikanda kama hatutalizuia Kenya, litaathiri Tanzania, Uganda, Sudani Kusini, Ethiopia, Rwanda na Burundi kwasababu tumefungamana na nchi moja haiwezi kupata tatizo bila kuathiri nyinginezo.
 
Back
Top Bottom