Rais Dkt. Hussein Mwinyi kumuwakilisha Rais Samia Suluhu kwenye mkutano wa Wakuu wa nchi SADC

Mwinyi hana kazi za kufanya huko Znz? au ndio wameanza kufanya kazi kishkaji hawa waswahili?

Kwani Dr. Mpango ana kazi gani? naona hii nchi sasa inaanza kujiendea tu kama gari bovu mtaroni.
Cha ajabu nini hapo? Mwinyi anawakilisha JMT, kipi hujaelewa? Mnapenda Sana kulalamika
 
Muungano gani huu hauna manufaa yoyote kwa yoyote. Ni kama tumejimilikisha jini lisilozalisha,linanyonya. Kwetu Watanganyika mpaka sasa huo muungano hauna maana yoyote. Nao kwao wazanzibar hauna maana pia. Tena nahisi tumerudisha nyuma sana. Wangekuwa mwenyewe wangekuwa mbali sana hao,maana hawana hizi janja janja za bara
 
KUNA HAJA KUBWA SANA WATANZANIA KUELIMISHWA KUHUU MUUNGANO SIKUTARAJIA HATA KIDOGO KWAMBA KUNA WATU WATASHANGAA RAIS WA ZANZIBAR KUMUWAKILISHA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. YAONESHA WAZI WATANZANIA WENGI HAWAELEWI KUHUSU MUUNGANO!!!

HIVI LEO BAADHI YA WATU TENA WENGINE NI WASOMI WANASHANGAA JAMBO HILO!! KAZI KWELI KWELI!!!
 
Mama yupo smart Ipo agenda muhimu kutoa ushauri waasi magaidi pia Mpango afya bado kutengemaa vizuri.
 
Zanzibar ni sehemu ya JMT, tumia akili basi.
Sawa, lakini Mwinyi ni mkuu wa serikali ya Zanzibar ambayo si mwanachama wa SADCC. Kama alitaka kumtuma mzanzibari wapo wengi tu kwenye serikali ya muungano.

Kamba kaachiwa ndefu sana naona akienda kujinyonga mwenyewe.
 
Nafikri JPM alishawahi kumtuma DK Shein pia
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanzania ambayo iko SADC
Sawa, lakini Mwinyi ni mkuu wa serikali ya Zanzibar ambayo si mwanachama wa SADCC. Kama alitaka kumtuma mzanzibari wapo wengi tu kwenye serikali ya muungano.

Kamba kaachiwa ndefu sana naona akienda kujinyonga mwenyewe.
 
Makamu wa rais hayupo, au sarakasi ndo zimeanza mapema..
Kwani Rais wa Zanzibar ana cheo/wadhifa gani katika serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kama isemavyo katiba...???
Na kama katiba inamtambua katika serikali ya Muungano basi ni haki yake kuagizwa kwenda huko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…