Rais Dkt. John Pombe Magufuli, tunaendelea kukuomba Mkoa mpya wa Nyakanazi

Rais Dkt. John Pombe Magufuli, tunaendelea kukuomba Mkoa mpya wa Nyakanazi

Kabende Msakila

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2020
Posts
1,809
Reaction score
1,692
Dkt. John Pombe Magufuli, hongera sana kwa kutekeleza vema majukumu yako ya urais

Naomba kukukumbusha juu ya maombi ya kutengewa mkoa mpya wa Nyakanazi. Mkoa huu ilipendekezwa uundwe na wilaya za Kakonko na Kibondo (Kigoma), na Ngara na Biharamulo (Kagera). Mkoa huu uwe na jumla ya wilaya nne.

Sababu za kutenga mkoa:-

(i). Kutoka Ngara - Bukoba (300kms), Biharamulo - Bukoba (200kms), Kakonko - Kigoma (300kms), na Kibondo - Kigoma (250kms). Kwa haraka ni kuwa mzazi akihitaji kuhamisha mtoto wa shule tu gharama zinakuwa kubwa, watendaji wa Serikali wanaposafiri hutumia mafuta mengi, muda mwingi nk

Kutoka wilaya hizo kuja Nyakanazi:-
Kibondo - Nyakanazi (90kms), Kakonko - Nyakanazi (51kms), Ngara - Nyakanazi (90kms), na Biharamulo - Nyakanazi (45kms). Sifa za eneo hili kuunda mkoa zinatosha sana. Wakuu wa wilaya wanabaki hivyo hivyo, majimbo ya uchaguzi yanabaki hivyo hivyo kitakachoongezeka ni Ofisi ya Mkuu wa mkoa na mamlaka zake.

Dkt. John Pombe Magufuli (Rais), naleta kwako maombi haya mahususi nikiamini kuwa utatenda lkn niseme tulikuomba, tunakuomba na tutakuomba.

Mungu akubariki wewe na wananchi unaowaongoza,
Mungu ibariki Tanzania

Msakila M Kabende
Kigoma
13 Januari, 2021
 
Vipi mtayaweza makusanyo ya halmashauri Au mtaanza na 32%, maana hali sio poa
 
Kutoka Chato hadi Nyakanazi ni km ngapi? Kama ni double digits kama ilivyo kwa wilaya zingine ulizotaja, bandiko lako lingepewa heshima kama ungeiweka Chato kwenye list na Makao makuu ya mkoa yawe Chato.
Hili nalo ni wazo zuri
 
Ye anawaza mkoa wa Rubondo wewe unawaza mkoa wa Nyakanazi?
 
Kidanganye, mkoa tunauunda huku Chato na utaita mkoa Rubondo makao makuu yatakuwa Chato! Huko unakotaka Kuna hospital ya rufaa? Kuna uwanja wa ndege? Kuna vyuo vya Vetsidg
Sidhani iwapo hiyo ndiyo dhamira ya Rais JPM, tuliomba, tunaomba, na tutamwomba mkoa wa Nyakanazi kama nilivyofafanua hapo juu.
 
Hizi wilaya zote nne nimezitembelea, kiufupi zimechoka sana kimapato. Haziwezi ku sustain gharama za uendeshaji. Kibondo na Kakonko wakiondoka wakimbizi hazitakuwa na utofauti na vijiji vilivyochangamka. Somehow Ngara. Mzigo wa kuhudumia sekretarieti ya mkoa sio ndogo.
Mkoa upi Tanzania unaoendeshwa kwa mapato yake ya ndani? Fedha zote hupelekwa kwenye mfuko Mkuu (central govt) kisha huwa allocated ktk bajeti kulingana na vipaumbele vya kila mkoa

Fafanua unataka mkoa ujisasteini vipi vinginevyo huenda una uelewa mdogo na masuala ya sekretarieti za mikoa.
 
Mtoa mada anahoja za msingi sana, ushauri wangu wabunge na wadau eneo husika wapaze sauti.
Fikra za mkoa wa Rubondo hazina mashiko ukilinganisha na uhitaji halisia.
 
Omba yote,Lakini usije kuongilia contents zinazoiathiri Chato kama mbuga za wanyama,misitu
Mkoa upi Tanzania unaoendeshwa kwa mapato yake ya ndani? Fedha zote hupelekwa kwenye mfuko Mkuu (central govt) kisha huwa allocated ktk bajeti kulingana na vipaumbele vya kila mkoa

Fafanua unataka mkoa ujisasteini vipi vinginevyo huenda una uelewa mdogo na masuala ya sekretarieti za mikoa.
Sasa wewe kama una uelewa mzee si angeshakupachika kwenye ka-cheo.Maana umesota zamani sana.
 
Back
Top Bottom