Rais Dkt. John Pombe Magufuli, tunaendelea kukuomba Mkoa mpya wa Nyakanazi

Rais Dkt. John Pombe Magufuli, tunaendelea kukuomba Mkoa mpya wa Nyakanazi

Omba yote,Lakini usije kuongilia contents zinazoiathiri Chato kama mbuga za wanyama,misitu

Sasa wewe kama una uelewa mzee si angeshakupachika kwenye ka-cheo.Maana umesota zamani sana.
Ungesema nimesotaje!
Na hili linahusiana vipi na mada yangu jmn? Mada inahusu kuwa na mkoa mpya wa Nyakanazi, mambo ya vyeo yafungulie mada nyingine inayojitegemea
 
Sema unatafuta uteuzi wewe
Ni bahati nzuri kuwa kinywani mwangu hayatoki maneno ya kushusha staha ya mtu, kutukana, wala dharau (nielekeze nilitakiwa kuleta uzi gani wa kukufurahisha?)

Hivi mtu unaweza kutafuta uteuzi kwa kuomba mkoa mpya wa Nyakanazi? Njoo na tusi jingine Mkuu
 
Nyakanazi gani Tena na wakati tulishasema mkoa uitwe Chato..[emoji849]
 
Ni bahati nzuri kuwa kinywani mwangu hayatoki maneno ya kushusha staha ya mtu, kutukana, wala dharau (nielekeze nilitakiwa kuleta uzi gani wa kukufurahisha?)

Hivi mtu unaweza kutafuta uteuzi kwa kuomba mkoa mpya wa Nyakanazi? Njoo na tusi jingine Mkuu
Kwa hiyo Kigoma wewe ndiyo bonge la mjanja unaweza kuomba mkoa kuliko RCC?
 
Kwa hiyo Kigoma wewe ndiyo bonge la mjanja unaweza kuomba mkoa kuliko RCC?
Kuna kitu hukijui kwa faida ya wengine elewa yafuatayo:-
(i). Mwaka 2014 agenda ya kugawa maeneo ya kiutawala kwa kutenga mkoa wa Nyakanazi ilijadiliwa na kupitishwa na RCC Kigoma (kikao kilikubali wilaya ya Kakonko na Kibondo ziunde mkoa mpya wa Nyakanazi)

Mwaka huo huo mkoani Kagera chini ya RC Kanali Fabian Massawe alielekeza kikao cha RCC kiwe na agenda ya kuichukuwa Biharamulo na Ngara ili ziunde mkoa wa Nyakanazi. Kikao kikiwa kwenye hatua za mwisho kufanyika ndipo yalifanyika mabadiriko ya kiuongozi ambapo Kanali Fabian Massawe alitenguliwa na nafasi hiyo kuwekwa RC wa sasa wa Mwanza Mongella. Siku ya kikao agenda hii iliwasilishwa kisha akaagiza kwa kuwa ni mgeni iahirishwe itajadiliwa baadae.

So, muda ulienda ndipo 2015 tuliingia ktk uchaguzi mkuu na baada ya uchaguzi alihamishiwa Mwanza. Lkn pia kama unakumbuka baada ya Rais kuchaguliwa aliagiza kuwa ktk kipindi hicho maeneo mapya ya kiutawala si kipaumbele kwake. Ndiyo maana niliandika "tulikuomba, tunakuomba, na tutamwomba"

Kama hujaelewa niambie nikupe zaidi
 
Bogus kabisa kufikiria kuwa mikoa mingi ndio maendeleo kumbe ni mzigo kwa walipa kodi.

Marekani enzi na enzi wana mikoa 50 tu lkn hadi neti za mbu wanawapa. Kweli sisi waafrika tuna akili ndogo sana.
 
Kuna kitu hukijui kwa faida ya wengine elewa yafuatayo:-
(i). Mwaka 2014 agenda ya kugawa maeneo ya kiutawala kwa kutenga mkoa wa Nyakanazi ilijadiliwa na kupitishwa na RCC Kigoma (kikao kilikubali wilaya ya Kakonko na Kibondo ziunde mkoa mpya wa Nyakanazi)

Mwaka huo huo mkoani Kagera chini ya RC Kanali Fabian Massawe alielekeza kikao cha RCC kiwe na agenda ya kuichukuwa Biharamulo na Ngara ili ziunde mkoa wa Nyakanazi. Kikao kikiwa kwenye hatua za mwisho kufanyika ndipo yalifanyika mabadiriko ya kiuongozi ambapo Kanali Fabian Massawe alitenguliwa na nafasi hiyo kuwekwa RC wa sasa wa Mwanza Mongella. Siku ya kikao agenda hii iliwasilishwa kisha akaagiza kwa kuwa ni mgeni iahirishwe itajadiliwa baadae.

So, muda ulienda ndipo 2015 tuliingia ktk uchaguzi mkuu na baada ya uchaguzi alihamishiwa Mwanza. Lkn pia kama unakumbuka baada ya Rais kuchaguliwa aliagiza kuwa ktk kipindi hicho maeneo mapya ya kiutawala si kipaumbele kwake. Ndiyo maana niliandika "tulikuomba, tunakuomba, na tutamwomba"

Kama hujaelewa niambie nikupe zaidi
Peleka kwenye vikao rasmi na usome vigezo vya kuanzisha mkoa mkuu, huyo Rais wako yupo humu?
 
Peleka kwenye vikao rasmi na usome vigezo vya kuanzisha mkoa mkuu, huyo Rais wako yupo humu?
Si wajibu wangu kujua yumo au hayumo humu - hili ni jukwaa huru la kisiasa. Jenga tabia ya kuskip hoja unapokuwa huna cha kuchangia.
 
Vipi mtayaweza makusanyo ya halmashauri Au mtaanza na 32%, maana hali sio poa
Nilishatoa ufafanuzi kabla, nirudie tena kukujuza kuwa hakuna halmashauri nchini isiyokuwa na vyanzo vya mapato ingawa haimanishi kwamba vyanzo hivyo hulingana (mfano ktk mkoa wa Kagera halmashauri ya Bukoba hailingani na Karagwe)

Suala la pili ni kuwa mfumo wa kodi zetu hukusanya kodi na kuziweka Serikali kuu, kisha fedha hizo hutekeleza majukumu kadhaa (mishahara = salaries, miradi ya maendeleo = development projects, na matumizi mengineyo = other charges) ktk mikoa kulingana na vipaumbele.

Kwa ufupi ni kuwa hakuna mkoa unaoendeshwa kwa makusanyo yake yenyewe.
 
Jiji la Mwanza soon litakuwa na Wilaya tatu. Baada ya kuwa na idadi ya Wilaya hizo wilaya zilizo nje na Jiji hilo zitaundiwa mkoa wake ambazo ni Magu, Kwimba, Misungwi na Sengerema. Stay tuned.
 
Back
Top Bottom