Rais Dkt. Mwinyi amteua Maalim Seif kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Rais Dkt. Mwinyi amteua Maalim Seif kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Matakwa ya Katiba Yanakitaka Chama kilichoshika Nafasi ya Pili baada ya Uchaguzi ndani ya Siku 7 iwasilishe Jina La Atakae Kuwa Makamo wa kwanza wa Rais Lakini kwa bahati mbaya Chama cha ACT wazalendo kimevuka hizo siku kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar hivyo kwa kuwa jambo hapa ni Maslah Mapana ya Taifa inabidi hekma itumike ktk utekelezaji wake

Mh Rais wa Zanzibar atumie Busara ya kuitisha Baraza la wawakilishi na Kufanya mabadiliko ya Kifungu 39A(1) kuondosha siku 7 na kuweka maelezo kuwa chama kitakapo wasilisha vyenginevyo atakwendanda kinyume na matakwa ya Katiba

Kuhu wawakilishi haina Pingamizi na kuhusu Mawaziri Anapaswa kukipitia kifungu cha Katiba Na 66 Katiba ya Zanzibar hii Hata Uteuzi wa Juma Ali hatibu ikiwa kwa lengo la kuwa ametoka chama cha Upizani basi haikupaswa iwe vile hadi pale atapo vikusanya vyama vyote na kuchukuwa ushauri

Kila la Kheri Zanzibar Yenye Neema ni kwa wazanzinar na watanzania kwa ujumla
Inawezekana tukianza na sisi wote
Who are you?
 
Mzee Sasa hivi maisha safii[emoji16][emoji16].
ulinzi nini,nyumba nini.acha ale MAISHA.
Ila mzed usije ukajisahau wakumbuke WANANCHI wako wa Zanzibar.
Piga kazi kweli kweli.
Akitoka mwinyi UNAINGIA wewe.
 
Uchaguzi wa Zanzibar ulibidi ufanyike March 20/2021 ndio mwisho wa Miaka 5 ya Dr. Shein.Hili nalo vipi limekiuka katiba Sura ya 4. kifungu cha 2?
Kiukweli Dr. Shein Hakuwahi kabisa kujiuzulu rasmi, na muda wake ulikuwa bado kuisha ,kwa mujibu wa katiba, ni miaka 5,sasa uchaguzi ulifanyika mapema ,lakini raisi aliyepo bado hajamaliza muda wake na hakujiuzulu, Hii imekaaje?
Dr Sheni abadilishe na hii sehemu basi
 
Movements za kweli za kudai haki huanzia kwa wananchi wenyewe na si hizi za kuitishwa na wanasiasa.
 
soon taarifa itakuwa "kamati kuu chadema yawasamehe Mdee na wenzake, waendelea na Ubunge wao kama kawaida,
Halafu kati ya makosa makubwa sana kwenye muundo wa CHADEMA ni kwenye hiyo nafasi ya Katibu Mkuu; yule jamaa anaongoza kwa makelele kuliko kuongoza kwa busara. Ni mwepesi kukimbilia kwenye maikrofoni badala ya kushughulika mambo kiutawala. Utadhani kuwa Katibu mkuu ndiye katibu mwenezi; yaani Tumani Makene yupo kama hana kazi tena kwa vile Mnyika ndiye kila kitu, halafu maamuzi yake mengi ni ya pupa sana.
 
Halafu mlitaka kina halima wasusie, hakuna mwenye uwezo wa kususia..hata Mbowe, Lissu na wenzake wangepata nafasi wasingesusa.
 
Ukiamua kujitoa kupambania course fulani hutakiwi kuwa na excuses, unapambana huku ukiijua vizuri jamii yako ikoje. Siyo unapambana halafu usipofanikiwa unaanza kulaumu wananchi ni ujnga. Maana kwanza ulipoanza kutangaza sera za chama chako kwa wananchi, ulianza wewe kama wewe kuwafuata wananchi na kuwaaminisha kuwa wewe ndiye wa kuwatoa point moja kwenda ya pili iliyobora zaidi, siyo wananchi waliokufuata na kukwambia kuwa njoo utupiganie, yalikuwa ni maono yako binafsi. Sasa upo katikati ya struggle na huku tukiwa tunaenda vizuri isipokuwa inahitajika kuweka vitu fulani sawasawa unaanza kukata tamaa na kulaumu wananchi, kufanya hivyo ni kusaliti course yako mwenyewe!

Wananchi wameshawaamini wapinzani na ndiyo maana wanawapa kura nyingi tu ila wale majambazi wa kisiasa wanapora!

Sasa hapa Wapinzani wenye akili wanapaswa wajipongeze kuwa kwenye uwanja wa kisiasa tumeshaeleweka kwa wananchi, sasa tufanye nini twende hatua ya pili. Huo ndo uongozi!

Na mapambano siyo lazima ushinde pambano leo au mwakani au baada ya miaka 10 inaweza kuchukua hata miaka 50 lakini sharti ni. lazima usimamie misimamo ya msingi bila kuyumba na kwa kuvumilia tabu, na mateso.

Civil rights movement hawakupata mafanikio kwa struggle ya miaka 10 tu, waliendelea kupambana na kupambana mpaka wakapata nafuu kubwa. ANC haikumuangusha Kaburu kwa miaka 20, iliwachukua zaidi ya miaka 80 ya kupambana na kupambana. Wewe unafikiri ndani ya South Africa hakuna watu waliokuwa wakila bata kwa kushirikana na serikali ya Kikaburu, mfano ni Chief Mongustu Buthelezi wa chama cha Inkatha, lakini hii haikuwazuia akina Oliver Tambo kuendelea kupambana wakiwa in exile.

Kwa hiyo ukiona kingozi wa kisiasa eti anawakatia tamaa wananchi ambao kimsubgi waeshaonyesha kumuunga mkono kwenye sanduku la kura basi huy siyo kiongozi ni. mchumia tumbo!

Ukiwa kiongozi kweli utawaonyesha wananchi njia A, B, C za kuresist na uwe na subira wakati wakijiadapt kuzifuata hizo njia, usiwalazimishe maana vitu vingine vinakuwa ni vigeni kwao!

Kiongozi wa kweli hawezi kulaumu wananchi, wakati at the end of the day hata mshahara wake, au ruzuku ya chama chake, au uhalali wa uwepo wa chama chake msingi wake ni wananchi!

Umeniwahi boss nilichotaka kusema, japo ww umekisema kwa ubora zaidi ya ambavyo ningesema.
 
Halafu kati ya makosa makubwa sana kwenye muundo wa CHADEMA ni kwenye hiyo nafasi ya Katibu Mkuu; yule jamaa anaongoza kwa makelele kuliko kuongoza kwa busara. Ni mwepesi kukimbilia kwenye maikrofoni badala ya kushughulika mambo kiutawala. Utadhani kuwa Katibu mkuu ndiye katibu mwenezi; yaani Tumani Makene yupo kama hana kazi tena kwa vile Mnyika ndiye kila kitu, halafu maamuzi yake mengi ni ya pupa sana.

Uko sahihi kabisa boss, sasa fanya hivi, hebu anzisha chama chako tuje tuone utendaji bora. Au ni mambo ya motivational speaker?
 
Wanasiasa wana mahitaji yao.

Na sisi wananchi tuna mahitaji yetu.

Ila sasa sisi wananchi tumewatelekeza wanasiasa, wameamua kufanya yao.

Maana sisi pia tuko busy kufanya yetu, ukiachana kubwabwajaaaa tu hakuna jipya tunafanya.

Lissu nusra auawe, Mdude yuko Jela, Mawazo hatunaye, Mange anaogopa kuja.

Sisi tuko busy kula bata na kuwapa pesa na kuwapigania celebrities kwenye mishow ya Wasanii wasio na mchango wowote wa mageuzi.

Wabongo akili zetu tunazijua wenyewe, tunapenda kupewa vitu vizuri tukiwa tumekaa na kustarehe yaani.

Anyway,

Nadhani sasa ni kuisoma namba kikamilifu ili kila mtu sasa atoke ndani,lugha iwe moja!
Ulitaka tufanyaje sisi wananchi? Ulitaka tuandamane au? Mbona wao hawatoki wakat wa maandamo..mtu anasema tuingie road..kesho yako hata yy mwenyewe haonekani road..nenda kaandamane ww na familia yako.
 
Pongezi kwa CCM kwa ukomavu wa kisiasa, hongera ACT kwa kukubali kwamba maendeleo hayana chama
Tuliwaasa sana ndugu zetu kwamba hakuna upinzani Tanzania ila kuna wachumia tumbo na vibaraka wakatukatalia....... ila nadhani sasa wataelewa
View attachment 1643488
Mungu ibariki Tanzania
Kweli kabisa na umenena vyema. Hakuna upinzani hapa Tanzania. Hao unaowasikia ni wachumia tumbo. Mnaokataa ukweli huu ni vibaraka wa Mabeberu.
 
Kwa hiyo na wale alio wahamasisha KUANDAMANA na wakaishia KUPATA ULEMAVU/KUPOTEZA NDUGU na wengine wakafikia hatua ya KUFILISIKA.

Mzee anawaachaje kuwapunguzia machungu??? Au ndio Mzee anaenda na ile ya "INZI KUFIA KWENYE KIDONDA SIO UFALA, NI KUPENDA"???
Huo uchochezi,
Kwani wewe ulipoipigia CCM au Chadema ulipata nini zaidi ya kupigwa najua kwenye foleni?
Si tunakula rumba pamoja Kiaa.
Hii ndivyo siasa ilivyo, tuwapigania viongozi ,wafalme ili waendelee kuwa wakubwa kwa damu yetu sisi wanyonge , na wafia nchi.
 
Back
Top Bottom