Rais Hussein Mwinyi wa Zanzibar, naomba nikukosoe kwa staha; usingilie Mahakama

Rais Hussein Mwinyi wa Zanzibar, naomba nikukosoe kwa staha; usingilie Mahakama

Natilia mkazo kweli wasipewe dhamana...hasa hao wabakaji...na nyie kueni mnaojidai rais kalewa madaraka hamjielewi. Kwan ikitokea habar mtu kabaka kitoto cha miaka 2 mnaanza toa povu hapa...hakuna kutetea ujinga waache wasipate dhamana..
Hakuna anayetetea wabakaji, wafungwe hata milele ila taratibu za kisheria zitumike, kama sheria ni dhaifu taratibu za kuzirekebisha zifuatwe ili ziwe bora.
Hatari za sheria za mdomoni na papo kwa papo ni kwamba hujui kesho sheria ipi itafuata. Ukiacha kichwa kimoja kitunge sheria kuna hatari ya kuwepo sheria isiyotekelezeka.
 
Hivi na bangi inahesabika kwenye kundi la dawa za kulevya ?🙄
 
Natilia mkazo kweli wasipewe dhamana...hasa hao wabakaji...na nyie kueni mnaojidai rais kalewa madaraka hamjielewi. Kwan ikitokea habar mtu kabaka kitoto cha miaka 2 mnaanza toa povu hapa...hakuna kutetea ujinga waache wasipate dhamana..
subiri siku mama ako asingiziwe kubaka ndio utaelewa nini maan ya matamko ya hovyo. Uwepo wa mahakama ni kuthibitisha bila shaka na kuhukumu
 
Natilia mkazo kweli wasipewe dhamana...hasa hao wabakaji...na nyie kueni mnaojidai rais kalewa madaraka hamjielewi. Kwan ikitokea habar mtu kabaka kitoto cha miaka 2 mnaanza toa povu hapa...hakuna kutetea ujinga waache wasipate dhamana..
Unaandika kama wewe hauishi kwenye hii dunia.angalia sio hadi yakukute ya walimwengu ndo ujue wenzako wanaposisitiza umuhimu wakuheshimu sheria za nchi na vyombo vyake ni muhimu.Aliye salama duniani ni marehemu peke yake.
 
Ni mwendawazimu peke yake ndiye anaweza kutegemea hawa viongozi ambao hawana kibali cha wananchi kama Mwinyi kuacha kuingilia na kuiweka mfukoni mihimili mingine.

Hata kama mimi ningekuwa Mwinyi as long as sina kibali cha wananchi katika urais wangu lazima ningevuruga mihimili mingine kwa maslahi yangu binafsi ya kuweza kutawala uma bila bugudha kutoka kwa niliowapora mamlaka.
 
Udhalilishaji na Madawa ya kulevya ni tatizo kubwa katika nchi yetu, sote tunawajibu wa kuwafichua wadhalilishaji. Natoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini yoyote atakae kamatwa kwa kosa la madawa ya kulevya au udhalilishaji nasisitiza asipewe dhamana.
Mie sikubaliani na hoja ya kuondoa dhamana, naamini kosa likiwa halina dhamana linatumika mara nyingi kinyume na malengo. Kama ulivyosema ulinzi uimarishwe na wote walio na hatia iachwe mahakama ifanye kazi yake.

Ukiondoa dhamana basi itakuwa sawa na iyo ya uhujumu uchumi na ugaidi, wanasiasa watakuwa wanabambikizia kesi mahasimu wao wanasota magereza.
 
Natilia mkazo kweli wasipewe dhamana...hasa hao wabakaji...na nyie kueni mnaojidai rais kalewa madaraka hamjielewi. Kwan ikitokea habar mtu kabaka kitoto cha miaka 2 mnaanza toa povu hapa...hakuna kutetea ujinga waache wasipate dhamana..
Halafu wanawekewa dhamana wanarudi mitaani kurejea makosa yale yale. Na hasa wabakaji watoto wanafichwa na kutetewa na ndugu wa karibu.

Kwa kweli inauma sana kuona mtoto mdogo wa miaka labda 6 au 8 amebakwa, mbakaji anatembea mtaani kwa kujitapa kabisa halafu kesi inaishia hivi hivi.
 
Rais Dk. Mwinyi yuko sahihi. Tusichezee na wauza dawa za kulevya. Hawa ni watu hatari. Wanaua nguvu kazi ya Taifa, wanazunguusha fedha haramu na mtandao wao ni hatari. Pili, udhalilishaji huacha makovu makubwa ya kisaikolojia kwa waliotendewa.

Adhabu hutolewa kutokana na aina, mazingira ya uhalifu na trend . Kama wanapewa dhamana halafu trend inaonyesha kuongezeka kwa kasi kwa matukio yeye akiwa Rais anayeongoza serikali, lazima akumbushe umuhimu wa kusimamia sheria.
 
hivi unajua maumivu ya kutuhumiwa, ukakosa dhamana miaka 2 halafu ukashinda kesi au mashtaka wakajitoa kwenye kesi???
Nadhani ame over-react kwasababu amewahurumia wanaoharibika kuwa mateja na wanaobakwa. Tuangalie nia yake zaidi.
 
Natilia mkazo kweli wasipewe dhamana...hasa hao wabakaji...na nyie kueni mnaojidai rais kalewa madaraka hamjielewi. Kwan ikitokea habar mtu kabaka kitoto cha miaka 2 mnaanza toa povu hapa...hakuna kutetea ujinga waache wasipate dhamana..
NANI SASA, UNAWAJUA WATUHUMIWA?.. MAANA YA MTUHUMIWA UNAIJUA?
 
Rais Dk. Mwinyi yuko sahihi. Tusichezee na wauza dawa za kulevya. Hawa ni watu hatari. Wanaua nguvu kazi ya Taifa, wanazunguusha fedha haramu na mtandao wao ni hatari. Pili, udhalilishaji huacha makovu makubwa ya kisaikolojia kwa waliotendewa.

Adhabu hutolewa kutokana na aina, mazingira ya uhalifu na trend . Kama wanapewa dhamana halafu trend inaonyesha kuongezeka kwa kasi kwa matukio yeye akiwa Rais anayeongoza serikali, lazima akumbushe umuhimu wa kusimamia sheria.
SHERIA INARUHUSU DHAMANA KWA MTU.... AU UNAONGELEA SHERIA IP?

PUMBA HII MZEE
 
"Udhalilishaji na Madawa ya kulevya ni tatizo kubwa katika nchi yetu, sote tunawajibu wa kuwafichua wadhalilishaji. Natoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini yoyote atakae kamatwa kwa kosa la madawa ya kulevya au udhalilishaji nasisitiza asipewe dhamana. " -Mh. Rais Dk Hussein Mwinyi ziarani Donge.

My Take:
Sishabikii unyanyasaji wa kingono Wala mawa ya kulevya. Lakini kupewa dhamana na kitopewa dhamana vipo kwenye kanuni zetu. Sasa wewe unasema kama nani? Hakimu au Jaji? Ndio maana tunahitaji Katiba itakayofuatwa na kuheshimiwa kudhibiti Mamlaka ya Rais.

Kigwangala amesema katiba inaweza kuwa na statement nzuri lakini utekelezwaji ukawa sifuri.

Dk Mwinyi atambue kuwa kauli ya Rais ni kama amri. Ukitamka hovyo ni hatari sana. Tutegemee haki za watuhumiwa kuminywa sasa!
Nchi ngumu hii mnalalamika asubuhi hadi jioni hata kwa jambo jema
 
Siasa nyingi kwenye issues za madawa ya kulevya zinaangamiza taifa letu, tuendelee tu kujidanganya na eti sheria; unadhani kuna madoni wa UNGA anaweza KUFUNGWA na mahakama zetu? Kujidanganya tu. Binafsi nimeupenda msimamo wa Dr. Mwinyi
 
Nadhani ame over-react kwasababu amewahurumia wanaoharibika kuwa mateja na wanaobakwa. Tuangalie nia yake zaidi.
Inshu sio nia ya dhati, haya madaraka ndio yametuumiza sana awamu ya tano, yaani rais akitamka tu tayari inakuwa ni sheria hata kama inakinzana na katiba!!!kama amechukizwa sana basi waifanye iwe sheria tu,
 
Udhalilishaji na Madawa ya kulevya ni tatizo kubwa katika nchi yetu, sote tunawajibu wa kuwafichua wadhalilishaji. Natoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini yoyote atakae kamatwa kwa kosa la madawa ya kulevya au udhalilishaji nasisitiza asipewe dhamana.

Ziara: Donge Chechewe

Huu ni ujumbe katika account ya twitter ya Mhe. Hussein Mwinyi, tumekatazwa kumkosoa Rais na baba yetu ila kwa hapa naomba nitimize wajibu wa Kikatiba.

1. Rais Hana mamlaka ya yakuingilia utendaji wa mahakama, dhamana ni haki ya kisheria si haki ya tamko la Rais

2. Zanzibar awazalishi dawa za kulevya, zinaingizwa na wakina nani? Je, wanaoingiza hawafahamiki?

3. Kwa kauli hii Tunaenda kujaza mateja magereza, je hii ndiyo suluhu ya dawa za kulevya? Kwanini asiongeze nguvu kwenye vyombo vya ulinzi wakabaini mtandao nakuufyeka?

Pls Mzee usiturejeshe kwa JPM, tumeona watu wasio na hatia walivyojazwa Magereza. Usiwajaze wasio na hatia Magereza kwa kisingizio cha madawa. JPM alianza kuwahita wahujumu uchumi akawatungia na sheria kumbe lengo nikuwazoba mdomo maasimiu na wabaya wake.

Don't do that pls, iache mahakama ipambane kivyake.
Wauza ngada bwana hawataki kusikia mtu anapiga vita madawa ya kulevya
 
Udhalilishaji na Madawa ya kulevya ni tatizo kubwa katika nchi yetu, sote tunawajibu wa kuwafichua wadhalilishaji. Natoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini yoyote atakae kamatwa kwa kosa la madawa ya kulevya au udhalilishaji nasisitiza asipewe dhamana.

Ziara: Donge Chechewe

Huu ni ujumbe katika account ya twitter ya Mhe. Hussein Mwinyi, tumekatazwa kumkosoa Rais na baba yetu ila kwa hapa naomba nitimize wajibu wa Kikatiba.

1. Rais Hana mamlaka ya yakuingilia utendaji wa mahakama, dhamana ni haki ya kisheria si haki ya tamko la Rais

2. Zanzibar awazalishi dawa za kulevya, zinaingizwa na wakina nani? Je, wanaoingiza hawafahamiki?

3. Kwa kauli hii Tunaenda kujaza mateja magereza, je hii ndiyo suluhu ya dawa za kulevya? Kwanini asiongeze nguvu kwenye vyombo vya ulinzi wakabaini mtandao nakuufyeka?

Pls Mzee usiturejeshe kwa JPM, tumeona watu wasio na hatia walivyojazwa Magereza. Usiwajaze wasio na hatia Magereza kwa kisingizio cha madawa. JPM alianza kuwahita wahujumu uchumi akawatungia na sheria kumbe lengo nikuwazoba mdomo maasimiu na wabaya wake.

Don't do that pls, iache mahakama ipambane kivyake.
Inabidi sasa labda Mh. rais Mwinyi afanye utaratibu kama ule wa kipindi cha Nyerere, kwamba ilikuwa mtu akikamatwa amekula rushwa, tayari sheria ilikuwa inasema aina ya adhabu atakayopata na si hakimu aliyekuwa anaamua aina ya adhabu.

Sheria ilikuwa inasema kwanza anachapwa viboko 12 wakati wa kuingia, halafu tena 12 wakati wa kutoka ili akamwonyeshe mkewe..... Yaani waliweka adhabu tayari kwa mtu anayekula rushwa, na si hakimu aliyekuwa anaamua aina ya adhabu.

Mh. Rais inabidi sasa aanze kufikiri katika mkondo huu wa Nyerere, kwamba itungwe sheria inayosema kuwa watu wenye makosa ya aina hii hawatakuwa na dhamana!
 
Udhalilishaji na Madawa ya kulevya ni tatizo kubwa katika nchi yetu, sote tunawajibu wa kuwafichua wadhalilishaji. Natoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini yoyote atakae kamatwa kwa kosa la madawa ya kulevya au udhalilishaji nasisitiza asipewe dhamana.

Ziara: Donge Chechewe

Huu ni ujumbe katika account ya twitter ya Mhe. Hussein Mwinyi, tumekatazwa kumkosoa Rais na baba yetu ila kwa hapa naomba nitimize wajibu wa Kikatiba.

1. Rais Hana mamlaka ya yakuingilia utendaji wa mahakama, dhamana ni haki ya kisheria si haki ya tamko la Rais

2. Zanzibar awazalishi dawa za kulevya, zinaingizwa na wakina nani? Je, wanaoingiza hawafahamiki?

3. Kwa kauli hii Tunaenda kujaza mateja magereza, je hii ndiyo suluhu ya dawa za kulevya? Kwanini asiongeze nguvu kwenye vyombo vya ulinzi wakabaini mtandao nakuufyeka?

Pls Mzee usiturejeshe kwa JPM, tumeona watu wasio na hatia walivyojazwa Magereza. Usiwajaze wasio na hatia Magereza kwa kisingizio cha madawa. JPM alianza kuwahita wahujumu uchumi akawatungia na sheria kumbe lengo nikuwazoba mdomo maasimiu na wabaya wake.

Don't do that pls, iache mahakama ipambane kivyake.
Rais Mwinyi , KWA kweli binafsi nimeshangaa kauli yake , wenda na majirani zake wanashangaa kauli yake,
 
Back
Top Bottom