Tetesi: Rais Kabila kuwa Waziri Mkuu Congo DRC baada ya uchaguzi.

Tetesi: Rais Kabila kuwa Waziri Mkuu Congo DRC baada ya uchaguzi.

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Habari zimezagaa jijini Kinshasa kuwa Kabila atakuwa waziri mkuu nchini Congo huku Emmanuel Shadari akiwa Rais. Nafuatilia habari hizi kwa kina.

Tetesi hizi zinajiri huku chama chake cha PPRD kikiwa kimehakikisha Kabila atakuwa mwenyekiti wa kudumu wa chama hicho. Pia atakuwa mwenyekiti na mratibu mkuu wa muungano wa vyama vya siasa vinavyounga chama chake maarufu kama Common Front for Congo (CFC).

Mchakato wa kumpata mgombea ndani ya chama cha PPRD na muungano wake pacha wa CFC uliwekwa chini ya mikono ya Rais Kabila bila kujua ni kwanini watu wote hao walikubali hali hii.

Wagombea 26 wameshachukua Fomu za kuwania urais Congo na kila moja akilipa dola laki moja. Hizi ni hela nyingi ktk nchi masikini huku mtu akiwa na ari ya kugombea ili awatumikie wananchi wenzie.

Hivyo kwa unyonyaji huu tume ya uchaguzi CENI imeingiza dola za Marekani 2600,000. Hata hivyo wachambuzi wa mambo wameendelea kuwashangaa wakongomani kwa wengi kujitokeza kuchukua Fomu licha ya gharama za fomu kuwa juu.

UPDATES: Wakati wa kipindi cha Maoni cha radio DW kiswahili ya ujerumani jumamosi tarehe 11/08/2018 saa saba mchana kwa saa za Africa Masahariki na saa sita mchana kwa saa za Congo DRC limeibuka jambo. Mbunge wa PPRD Franswaa Nzekuye kakiri wazi Kabila anaweza kuwa waziri mkuu na baada ya miaka mitano kama wananchi wamemchoka Emmanuel Shadari, Kabila anaweza kugombea urais tena bila kizuizi chochote. Kipindi hicho cha maoni kilizungumzia siasa za Congo DRC na walioshiriki ni Wakongomani tupu.
 
Ataheshimika kama atakaa pembeni, atafute kitu cha kusaidia jamii nnje ya serikali. Vinginevyo atajipalia mkaa......
 
Mtu Chake njoo huku utuambie huko Lubumbashi ulipo habari hizi zimeenea kama ambavyo zimeenea huku Kinshasa.
Habari zimezagaa jijini Kinshasa kuwa Kabila atakuwa waziri mkuu nchini Congo huku Emmanuel Shadari akiwa Rais. Nafuatilia habari hizi kwa kina.

Tetesi hizi zinajiri huku chama chake cha PPRD kikiwa kimehakikisha Kabila atakuwa mwenyekiti wa kudumu wa chama hicho. Pia atakuwa mwenyekiti na mratibu mkuu wa muungano wa vyama vya siasa vinavyounga chama chake maarufu kama Common Front for Congo (CFC).

Mchakato wa kumpata mgombea ndani ya chama cha PPRD na muungano wake pacha wa CFC uliwekwa chini ya mikono ya Rais Kabila bila kujua ni kwanini watu wote hao walikubali hali hii.
Mkuu nilikuambia yajao hapa Congo yanafurahisha zaidi ,hii Mimi nililijua mapema tu na nikawa nasema humu JK Jr hatoki ktk system

Tuendelee kuchunga Mkuu ,na Bemba hana sifa za kua mgombea, kifupi jina lake halirudi,na kumbe alikuja km kanya boya tu ,kuzuga watu
 
Mkuu nilikuambia yajao hapa Congo yanafurahisha zaidi ,hii Mimi nililijua mapema tu na nikawa nasema humu JK Jr hatoki ktk system

Tuendelee kuchunga Mkuu ,na Bemba hana sifa za kua mgombea, kifupi jina lake halirudi,na kumbe alikuja km kanya boya tu ,kuzuga watu
Sasa wakimtoa Bemba si kura zitahamia kwa Tshekedi na upinzani kushinda kwa urahisi?
 
hahaaa mamaee dola laki 1 .. ml.200s na upuuzi hiyo " hao kweli wabakaji " wa democracy
 
Back
Top Bottom