kichongeochuma
JF-Expert Member
- Jan 21, 2024
- 1,669
- 2,864
Kwenye swala la mipaka ndio utajua JWTZ ni kina nani , ila nimeshangaa sana kuona hili ziwa nyasa google walisha badilisha muda mrefu sana sijui serikali yetu ilikiwa wapiKiongozi ya ndani kwetu ni magumu, kutokana na katiba yetu; mengine kuyaongelea sio salama.
Iła mipaka ya Tanzania sio swala la mzaha kabisa, hilo ndio eneo kama nchi JWTZ aicheki.
Huyu mama anaweza sema wawachwe tuu kwani ardhi ni mali ya allah!Nyerere alikuwa mbabe na jeshi imara
Kwenye swala la mipaka ya nchi ubabe upo hadi sasaNyerere alikuwa mbabe na jeshi imara
Mwalimu kwa propaganda alkua mkali sana...Banda asingemweza...idd amini aliitwa nduli...hivi nini MAANA ya nduli? Kwenye swala la mipaka hakuwa na mchezoNakumbuka miaka ile ya 70 wakati tunaimba nyimbo za kumkejeli Banda
Banda wa Malawi, atuvalia ngozi ya simba, kututishia watanzania hatujali hatujali
Hili wamemruhusu vipi huyu mama kulitekeleza? Mbona ajabu hii na viongozi wa Tanganyika wamekaa tuu?Hili linanikumbusha pia kisiawa cha ''Latham'' kati ya Tanganyika na Zanzibar
Kwa muda mrefu kimekuwa Tanganyika hadi Samia alipokirudisha Zanzibar alipokuwa Rais wa JMT
Uwezi lazimisha kuamua wengine wanavyotaka kuku-label; JWTZ inajua mipaka halisi ya Tanzania sio Google.Kwenye swala la mipaka ndio utajua JWTZ ni kina nani , ila nimeshangaa sana kuona hili ziwa nyasa google walisha badilisha muda mrefu sana sijui serikali yetu ilikiwa wapi
Sio mmalawi, utaitwa mnyassaMbeya kuwa Malawi! 🤔🤔😲 Labda huko mpakani Kasumulu, lakini kujumuisha Mbeya yote kuchukuliwa na Malawi hiyo Ni impossible. Yaani mie wa Kambikatoto Chunya mara paap nimekuwa Mmalawi. Lol!
Aliipenda sana nchi yakeMwalimu kwa propaganda alkua mkali sana...Banda asingemweza...idd amini aliitwa nduli...hivi nini MAANA ya nduli? Kwenye swala la mipaka hakuwa na mchezo
Hakuna kucheka nao haoKwenye swala la mipaka ya nchi ubabe upo hadi sasa
Kwenye suala la ardhi hawezi kwa sababu nyingi tu na wanaosimamia sio ardhi bali JeshiHuyu mama anaweza sema wawachwe tuu kwani ardhi ni mali ya allah!
Dah akomae malawi.........asee kuna nchi ni tishio ila sio malawi aisee,,,,,,labda kama watasogeza mipaka na hao waganga wao wa style za waganga wa wakingaHii kitu iliwahi ongelewa humu miaka ya nyuma ni kama ramani ilichezeshwa mahali.
Iliwahi tokea hadi hiyo mipaka ikawa inalindwa muda wote.
Hata sasa najua wapo wanajeshi wetu muda wote wanalinda huo mpaka.
Ila, nakuapia akikomaa mpaka utasogezwa, note me.
Tuna ujinga kwenye mambo mengine ila kwenye ulinzi wa mupaka sijui kama nako tumesha ingiza ujingaHakuna kucheka nao hao
Niko upande wako 100%They are stupid najua hata wakati wa uongozi wa yule mama ndio alianzisha hii chokochoko, aisee pale panalindwa kuliko wanavyodhani na hatutaachia hata hatua moja mipaka ilishakuwa settled zamani so wasitutafute ubaya sababu wanajua vema uwezo tulionao.
Africa iligawanywa na wazungu ikawekwa mipaka kila nchi ikapigania uhuru wake na kulinda mipaka yake. Haya yanayokuja kuibuka baada ya miaka zaidi ya 60 ya uhuru ni uhuni tu na hakika hakuna ardhi wataipata kama ni ziwa Nyasa tulishakubaliana miaka kibao ligawanywe katikati na hiyo imekuwa hivyo miaka yote sasa haya wanayoleta kuna kitu wanakitafuta na watakipata watanzania sio wapole kiasi hicho mbona tunawaacha tunwanakaa kwetu hatuwapi shida hata kuwasumbua kuhusu permits zao? Si tunaishi nao tu ? Hakika kwa hili diplomasia ikishindwa naamini kila mtanzania atakuwa tayari kuvaa konbati na kuingia front uzuri watanzania halisi tunajijua when it comes to national interests.
Kama mambo ni mazuri hivyo basi huku mjini wasingejazana watu wao wakifanya kazi za ndaniSisi ambao tuko mipakani karibu na Malawi ikitokea tukapiga kura ya kuwa sehemu ya Malawi hatukatai.Malawi kunamifumo mizuri ya kielimu,kiuchumi , kibiashara na,kijamii kuliko Tanzania.
Nimewahi kusoma hilo chapisho. Kesi ya Ziwa Nyasa kwa asilimia kubwa haipo upande wetu. Na kumbe mwanzoni Nyerere alitambua kwamba hatuna sehemu ya ziwa!! Alitegemea Wamalawi watakuwa reasonable na watamaliza suala mezani.Shukurani mkuu. Shukurani zaidi kwa muandishi aliyefanya kazi kubwa.
Watu wasije kufikiri Kiranga ndiye huyo muandishi sasa. 😆😆
Mimi nilikuwa natafuta andiko la wanazuoni kuhusu huu mgogoro, nikakutana nalo hili.
Nimelisoma lote, limechambua mgogoro kirefu.