Rais Kikwete akanusha kumuokoa Ridhiwani katika kesi ya dawa za kulevya China

Rais Kikwete akanusha kumuokoa Ridhiwani katika kesi ya dawa za kulevya China

Tunaendelea kuweka rekodi ..... Rais ambaye yuko madarakani huku mwanaye anafanya biashara haramu ya madawa ya kulevya.
 
Rais Kikwete akiwa Marekani ameongea na watanzania na kukanusha madai kuwa alimuokoa mwanae Ridhiwani nchimi China baada ya kukutwa na dawa za kulevya.

Rais amesema huo ni upuuzi na hawezi kuongelea upuuzi wa aina hiyo ambao ni uzushi usio na maana.

JK pia amewaambia watanzania waishio marekani kuwa sio kweli kwamba kusainiwa mikataba 12 kati ya Tanzania na China ilikuwa ni sehemu ya masharti yaliyotolewa na China wakati wa kumuachia Ridhiwani.

Jakaya-Kikwete.jpg


=======================================
Hapa naona ukosefu wa elimu ya lugha ya mawasiliano kwa umma. Kama rais hakupaswa kutumia lugha hii. Anaonesha kuwa na hasira na kupanic ambapo kisaikolojia ni njia mojawapo ya kumnasa mhalifu kwani mara nyingi hutumia lugha ya ukali ili kujilinda. Alipaswa kuwa makini katika kujibu hili. Vinginevyo atatufanya tumuone hajui uzito wa nafasi anayoishikilia. Mara nyingi nimemsikiliza tatizo lake ni hilo. hata kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi amejichanganya sana. Anakanusha wakati huo huo anajifunga mwenyewe na kukubali kosa. awaone wataalamu wa lugha ya mawasiliano kwa umma wamsaidie
 
Kama raisi hasingekanusha ingebidi apelekwe hospitali ya magonjwa ya akili!
 
Habari inaweza kuwa ya kweli au ya uongo vyote vinawezekana.
Unamkumbuka aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nchi za nje na pia aliyeisha wahi kuwa balozi wa TZ nchi za nje "Hassan Diria alikamatwa ujerumani akiwa na mzigo wa madawa ya kulevya?
Hawa jamaa huwa hawasachiwi kisheria, hivyo hutumia nafasi hiyo. Diria siku hiyo walimsachi ingawa ilikuwa ni kinyume cha sheria kumsachi, na wakamkuta na madawa ya kulevya.

Kumbuka Ridhiwani hakuwa na hiyo haki enzi hizo zaidi alikuwa na diplomatic pass sababu ya baba yake ila alikuwa anasachiwa sababu mizigo yake haikuwa na sticker za presidential, au diplomat
Muulize Matonya wa bongo flava anajua kila kitu

Tanzania tumezoea mambo ya uswahili sana
 
Akanushe pia kuwa yeye siyo Rais dhaifu.......
 
Khaa!! Kumbe hata wewe uliamini???!!! Basi kuna kundi kubwa sana la watu hawa

Hembu tuambie ni kitu gani serikali ya ccm iliwahi kukubali kuanzia epa, meremeta, meno ya tembo, unga, kusafirisha wanyama hai, na wizi wa ascrow, na meeengi tusiyoyajua ni kiongozi gani ndani ya ccm aliyesimama na kukiri kuhusika nyie subirini siku chama cha ccm kitakaopowekwa makumbusho ndio mtajua kama mkaa hauwezi kupakwa rangi.
 
well, hakuwa na diplomatic passport by then... ila alikuwa na nyenzo (fedha) za kuwaajiri vinaja wengi atakavyo kama kweli alikuwa anajihusisha na hayo madawa ya kulevya! BTW Rais huwa anapewa information nyingi za kujua hatari zinazomkabili yeye na familia yake! Msisahau kuwa Mengi aliwahi kupambana na Maharamia waliokuwa wanamtumia mwanae !!! Kwanini tusiamini kuwa ulikuwa ni mtego wa kumuingiza mwanae kwenye kashfa kama kweli ilitokea bali tunaingia kwenye conclusion kuwa Rizwan anahusika na biashara ya Sembe?... Bado sija shawishika kuwa Rizwan ni Duwanzi kiasi cha kushindwa kupima Risk ya yeye kujihusisha na madawa ya kulevya... I stand to be corrected!!!

Mkuu hilo ndo linalo tuduwaza wengi, lakini basi kwanini yeye? yeye tuuuuu?? kwani muheshimiwa nasikia nyota ya kijani kwake haikumtembelea, sasa mbona Riz1 tuuu?? hii haijatulia mkuu na huyu 'muheshimiwa mupya'
 
Rais Jakaya Kikwete aiweka nchi rehani kumuokoa mwanae asinyongwe China.

September 7, 2012


Ningumu kuamini lakini ni UKWELI

Maswali yangu yatakuwa katika wino mwekundu

Taarifa za upelelezi makosa ya jinai nchini China zinasema tarehe 01/7/2012, vijana wawili wenye asili ya kiafrika walikamatwa katika uwanja wa ndege wa Hong Kong usiku, wakiwa na madawa ya kulevya yenye thamani ya shilingi za Tanzania Bilioni nne, mkuu wa kitengo chakuzuia mihadarati cha uwanja wa Hong Kong Yiu-Kwong anawataja kuwa ni Ridhiwani Jakaya Kikwete na Abdalah Aman Mohamed

1. Swali: Huyu Abdalah Aman Mohamed, (a) Yuko wapi sasa hivi. (b) Je ni raia wa Tanzania?

Mnamo tarehe 2/7/2012 majira ya saa nne (4:13) za usiku hapa Tanzania, rais Jakaya Kikwete alipokea simu kutoka kwa mtanzania mmoja aitwae Philip Malmo ambae ni balozi wa Tanzania nchini China, Taarifa muhimu baada ya salamu ilikuwa ni Ridhiwani amekamatwa uwanja wa ndege wa Hong Kong na madawa ya KULEVYA,

Maoni/Swali: Bila shaka mtoa taarifa utakuwa mlinzi wa Rais je ulisahau kiapo cha kazi yako kuhusu kutunza siri? Maana saa 4:13 usiku wengi wamelala.

Kwa haraka, rais akamuuliza vipi suala hili limeshafika hapo ubalozini? Akajibiwa hapana ni mimi na kaimu wangu tu ndie tumepata taarifa hii mda huu, bado hatujaliifanya lakiofisi, tunasubiri ushauri wako mheshimiwa.

Swali: inaelekea uliaminiwa sana na Mh Rais, ulisikiliza mazungumzo ya siri na Philip Marmo, je leo hii uko hai?

Rais alikata simu huku hali yake usoni ikibadilika gafla, ilichukua kama dakika 20 hivi rais akiwa kimya hata kutikisa macho tu hatikisi, baadae akainua simu na kumpigia rais Hu Jintao wa China, Waliongea kwa mda mrefu yapata dakika 40 hivi, na walikonekana kama hawakubaliana kitu fulani katika mazungumzo yao. Baadae simu ikakatwa,



Akampigia simu Malmo nakumwambia suala hili walifanye kwa siri kubwa asijue mtu yeyote, naaweke maandalizi yawe tayari yeye anajiandaa kuja kulimaliza, kasha akampigia tena simu Hu Jintao na walitumia dakika 16 tu akainuka nakusema, vijana, mwambie SD53 aandae ndege haraka kwa safari ya China,

Swali: Huyu SD63 (Sargent Detective 63) Je ndiye yule Chrisopher Kyendesya?

Gari ya kirai namba T 435 CDR aina ya Landcruiser nyeusi iliingia nakuwabeba watu watatu akiwemo rais Jakaya kuelekea airport, kama dakika 13 ikafika airport, tayari ndege ilishaandaliwa na palikuwa na maafisa watatu, wote tuliingia katika ndege ile isipokuwa yule dereva wa gari ambae aligeza mjini, hiyo ilikwa sasa ni saa 7:43 za usiku.

Swali: OK sasa unaanza kueleweka kutoka Ikulu ukiacha dereva mliingia maofisa wawili Mzee wa tatu , airport wakaongezeka wengine watatu jumla mkiwa sita mkaondoka kwen China, je njiani Rais alikaa kimya tuuuu hadi China alikuwaje na alisemaje.

Tarehe 3, majira ya saa nane za usiku kwa china, tulifika China, hakukuwa na aina ya mapokezi yoyote ya kiserikali, na baada ya kushuka tulimkuta Malmo na msaidizi wake wakitusubiri, Malmo alikuwa tayari ameshaandaa hoteli lakini kulingana na tukio lilivyo tulikubaliana tusilale na tukammwambia mheshimiwa rais amwambie Hu Jintao kuwa ameshafika. Rais alitekeleza hilo na baada ya dakika 15 maafisa watatu wa china walifika nakujitambulisha kuwa wenyeji wetu, wakatuchukua hadi alipo Hu Jintao katika moja ya ikulu ya Hong Kong,



Kikao chao kilichukua masaa manne, na jambo kuu walilokuwa wanakubaliana ni mashariti ya kumuachia, Hu Jintao alihitaji jambo moja tu, kwamba nini serikali ya china itapata kwakumwachia huru Ridhiwani? Kilichomvutia Hu Jintao naakamua muachia Ridhwani ni ahadi ya makubaliano ya Rais Kikwete kuwa ataipa China fursa ya uwekezaji wakudumu kusini mwa Tanzania ambako kumegunduliwa mafuta, gesi, na makaa ya mawe.

Swali: Ujio wa Hu Jintao ulikuwa ni kuja kuangalia ardhi yake? Kama eneo hilo ni kudumu inamaana China imepanua mipaka hadi Mtwara?

Kwakuwa sera ya china kwa sasa ni “Now we are going to Africa”, ilisaidia sana kukubali ombi hilo la jk.



Majira ya saa 11 alfajiri kwa saa za china, Ridhiwani aliletwa akiwa katika gari dogo, nakupokelewa na jk huku wakikumbatiana wote WAKILIA. Jk na Jintao wote kwapamoja wakamuonya sana nakumwambia ameliaibisha taifa la Tanzania, lakini kwakujitetea akasema sio yeye, ila inawezekana yule kijana waliyesafiri wote kutoka Ethiopia ndie mwenye mzigo huo.

Swalii: Ikiwa mawasiliano na Mh Philip Marmo alimsihi kuwa iwe ni siri, je kwenu ninyi hakuwa na neno?

Majira ya saa 12 za asubuhi tukaondoka kurudi Tz.



Taarifa hii ni yakweli mimi nilikuwemo kwenye msafara huo,



Hutaki unaacha, hulazimishwi kuamini.

Swali: Naomba kujua wote mlambatana na Rais mpo hai mkifanya idara ile ile?
 
Watanzania tubadilike tuache uzushi wa kijinga , hakuna raisi au kiongozi duniani anyetaka ujinga kama huu, hata China kwenyewe Waziri kafungwa na wengine wamenyongwa kwa ajili ya madawa ya kulevya hata na rushwa sembuse Ridhiwani nani anayemjua hata kama ni mtoto wa Rais
 
huu unaonekana uzushi kwa sababu hata kama Riz anajihusisha na dawa za kulevya (1) unadhani yeye angebeba mwenyewe mpaka China? tumboni au kwenye mkoba (2) je kuna kaushahidi wowote wa picha nk kama hao wengine wanaokamatwa. (3) ????????? bila hivyo tunaazia wapi ku justfy hizo tuhuma
 
Back
Top Bottom