Rais Kikwete amteua Prof. Mussa Assad kuwa CAG mpya akimrithi Ludovic Utoh

Rais Kikwete amteua Prof. Mussa Assad kuwa CAG mpya akimrithi Ludovic Utoh

Leo tena Professor mwingine kaula kama CAG mbali na Professor Benno Ndulu na Muhongo

Anawaamini sana ingawa watendaji wadogo chini yao huenda wabovu.

Professor Assaid apewe ushirikiano
 
Leo tena Professor mwingine kaula kama CAG mbali na Professor Benno Ndulu na Muhongo

Anawaamini sana ingawa watendaji wadogo chini yao huenda wabovu.

Professor Assaid apewe ushirikiano
Taja Professor aliyeteuliwa Na JK ambaye amefanya kazi Nzuri
Kumbuka Profesa maji marefu alisema yeye ni sawa na Prof Muhongo na tumepata majibu sasa
 
Leo tena Professor mwingine kaula kama CAG mbali na Professor Benno Ndulu na Muhongo

Anawaamini sana ingawa watendaji wadogo chini yao huenda wabovu.

Professor Assaid apewe ushirikiano

Tatizo pia ni sisi.Kwa mfano huu mtazamo kuwa kuteuliwa kwake maana yake "Kaula" ni lini utatutoka?
 
Jamani huyu rais kachemka issue urgent ilikuwa ni kumteua AG,Waziri wa Nishati, Katubu mkuu na Waziri wa ardhi na makazi sasa yeye kaanza na kulipisa kisasi kwa kaimu AG alitoa taarifa ya escrow kwa kumteuwa mwingine jamani sasa hayo ndiyo maazimio ya Bunge? ajabu sana.
 
Tatizo pia ni sisi.Kwa mfano huu mtazamo kuwa kuteuliwa kwake maana yake "Kaula" ni lini utatutoka?

Ben neno "kaula" in real sense ni sahihi ni level tofauti katika rank of employee compared to supervision of dissertation and thesis

Haimaanishi ready for corruption

Soma Maslow's theory of hierarchy
 
Samahani nilikuwa na maana kamteuwa CAG mwingine badala ya huyo anayekaimu aliyetoa ripoti ya escrow.
 
Jamani huyu rais kachemka issue urgent ilikuwa ni kumteua AG,Waziri wa Nishati, Katubu mkuu na Waziri wa ardhi na makazi sasa yeye kaanza na kulipisa kisasi kwa kaimu AG alitoa taarifa ya escrow kwa kumteuwa mwingine jamani sasa hayo ndiyo maazimio ya Bunge? ajabu sana.
Huyo kaimu alishashindwa kazi.
yaani mwanamahesabu mkuu wa nchi unajibu eti,''pesa za escrow zaweza kuwa sehemu nyingine za serikali ama sehemu nyingine za iptl''.

mtu tuliemtegemea apige mahesabu na atwambia jibu moja kwamba ni pesa za umma ama za iptl.
au za umma ni ngapi za iptl ni ngapi.
 
Tatizo pia ni sisi.Kwa mfano huu mtazamo kuwa kuteuliwa kwake maana yake "Kaula" ni lini utatutoka?

Tuna kazi kubwa kubadili fikra zetu. Mtu akistaafu baada ya kushikilia nyadhifa kubwa na akawa na hali ya kawaida :si tajiri wala maskini, jamii inamwona kama mjinga mbaya zaidi kama mpumbav.u
 
ni vizuri rais apunguziwe madaraka.....huyo lazima kamchagua kwa kujuana tu
 
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


PRESIDENT'S OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.

Kabla ya uteuzi wake, Bwana Assad alikuwa Profesa Mshiriki, Idara ya Uhasibu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Bwana Ludovick Utouh ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.

Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991.

Profesa Assad pia ana Stashahada ya Kitaaluma ya Uhasibu (Professional Diploma in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City mwaka 1990 na Shahada ya Biashara (Bachelor of Commerce) ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam mwaka 1988.

Pamoja na uzoefu wa kitaaluma, Profesa Assad anao uzoefu mkubwa katika eneo la uhasibu na ukaguzi. Alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwa miaka saba (2007 - 2014); ni Rais na Mjumbe wa Chama cha Wahasibu Afrika (Pan African Federation of Accountants) tangu mwaka 2012; na ni mjumbe wa Bodi kadhaa za Wakurugenzi nchini Tanzania.

Katika kumteua Profesa Mussa Juma ASSAD kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Rais anayo imani kubwa kuwa elimu, weledi, ujuzi na uzoefu ambao Profesa Assad anao utamwezesha kutekeleza vema majukumu ya nafasi hiyo muhimu sana katika utawala bora wa nchi yetu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
1 Desemba,2014


-----------------------

10313732_648287681948876_6001176764329198945_n.jpg

Pamoja na Maroroso yanayotoka Magogoni...naomba wale wataalam wanaochangia kukua kwa Kiswahili watueleweshe 'mchanyato' huu ni-aje??

" Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991."


Umakini wa hawa wakuu wetu wa Press Release! Mmh!, Naomba kutoa hoja..

Swali: Huyu siye Mwenyekiti wa Bodi ya NBC Bank?? If yes, NBC inaendeleaje!....then fill the blanks!
 
utawala wa Kikwete umenyofoa Ma-Dr. na Ma-Prof wengi sana kutoka Vyuo Vikuu japo wengi wao wameishia kutenda chini ya kiwango kilichotarajiwa, kuingia kwenye kashfa na wengine kuondolewa kwa aibu.

Nafikiri imani kuwa Dr. au Prof. anafanya kazi nzuri kuliko watendaji wengine haina mashiko sana.
 
Pamoja na Maroroso yanayotoka Magogoni...naomba wale wataalam wanaochangia kukua kwa Kiswahili watueleweshe 'mchanyato' huu ni-aje??

" Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991."


Umakini wa hawa wakuu wetu wa Press Release! Mmh!, Naomba kutoa hoja..

Swali: Huyu siye Mwenyekiti wa Bodi ya NBC Bank?? If yes, NBC inaendeleaje!....then fill the blanks!

Hawajui maana ya uzamivu na umahiri na uzamili, ni lugha mpya hii. Ikulu inakosea lugha, je watoto wa sekondari itakuwaje?
 
Binafsi namfahamu vizuri sana Mussa Assad toka akiwa UDSM na hata katika maisha a kitaaluma. Ni mtu mwenye upeo na weledi mkubwa sana katika eneo la accounting na amefana kazi nyingi za kitaaluma.

Naamini inshallah atafana vizuri sana kama atapata ushirikiano katika afisi hiyo yya CAG.

Hongera sana Prof Assad na Mkeo Bi Adiya
 
utawala wa Kikwete umenyofoa Ma-Dr. na Ma-Prof wengi sana kutoka Vyuo Vikuu japo wengi wao wameishia kutenda chini ya kiwango kilichotarajiwa, kuingia kwenye kashfa na wengine kuondolewa kwa aibu.

Nafikiri imani kuwa Dr. au Prof. anafanya kazi nzuri kuliko watendaji wengine haina mashiko sana.


Ina maana unamanisha elimu si kitu na unaunga mkono hoja ya mbunge ajue kusoma na kuandika pekee?
 
Duh!!mungu ibariki Tz yetu,
mungu ibariki EAC mungu
ibariki Africa
 
Shida si uprofesa.. Shida ni UADILIFU.......

MSOMI WA KWELI ANATAKIWA AWE MWADILIFU NA ASIYUMBISHWE.. KWAMBA KAMA WAKUBWA ZAKE WANAMLAZIMISHA KUFANYA YALE YASIYOENDANA NA MAADILI YA KITAALUMA apambane nayo ikishindikana unaachia ngazi

lakn wasomi wa nchi wapo tayari kukiuka maadili ya kitaaluma kwa maslah binafs na ulev wa madaraka.. Huu ni upuuz sana

jaman nchi hii ni yetu sote tuitendee haki

mtu unalipwa maybe 5 millions per month

marupurupu kibao

gari linalojazwa mafuta kila siku

nyumba na kila kitu

LAKN BADO UNATAMANI KUIIBIA NCHI.. HAYA NI MAMBO YA AIBU NA WALA SI SIFA KUIIBIA NCHI ILIYOKULEA NA KUKUSOMESHA

KUMBUKA WAPO WANAOLIPWA SH. LAKI 2 KWA MWEZ LAKIN BADO WAMERIDHIKA NA.WANAITUMIKIA NCH

nb. Tujiulize... Wazee wetu wa zaman kama akina hayati moringe sokoine... Nyerere na wenzake wangeendekeza ufahari binafs na wizi nchi hii ingekuwa wapi?????
 
Back
Top Bottom