Rais kuitwa mtukufu na kuabudiwa hadharani bila kukemea inaashiria nini?

Rais kuitwa mtukufu na kuabudiwa hadharani bila kukemea inaashiria nini?

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Hili jambo limenistua na kunipa hisia hasi. Sikuamini macho na masikio yangu kwa Rais huyu huyu wa wanyonge na mcha Mungu.

Akitoa maelezo ya kutaka Maendeleo jimboni kwake Kibamba, Mbunge Issa Mtemvu alimwita Rais Magufuli MTUKUFU tena akimsujudu hadi ardhini.

Nilijua Rais atakapoamka kutoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa Stendi ya mabasi huko Mbezi Louis basi angekemea kuitwa MTUKUFU Rais lakini akapiga kimya!

Nijuavyo mimi hata kama si mjuzi sana wa mambo ya dini lakini mwenye cheo cha utukufu ni Mungu pekee si binadamu mwenye nyama, damu na mifupa. Hii tabia ya kujipendekeza hadi kumwabudu binadamu mwenzio ni kumkufuru Allah.

Au nasema uongo ndugu zangu!
 
Aliyemwita hivyo alikua na maana yake anayoijua yeye mwenyewe

Screenshot_20210225-110322.jpg


Na anaweza kuwa na maana tofauti na inavyofikiriwa
 
Upo Sahihi kabisa
Mtukufu ni mwenyezi Mungu pekee kwa upande wa Dini zote.
Ipo siku magufuli ataitwa Jehova na atachekelea tu.
Kwa hili tuwe fair..Marais Nyerere na Mwinyi waliitwa hivi pia bila kuzuia. Ni Rais Mkapa ndiye aliyekuja kukataa kuitwa hivyo. Naandika hivi kwa lengo la kuweka historia sawa tu.
 
Ila mi nimefurahi sana pengine neno hili la mtukutu limemfanya rais akubali maombi yake.

Sisi wananchi wa kibamba tunataka maji na barabara. Sasa tunahesabu miezi miradi itaanza na kukamilika.

Kongole kwa Mtemvu!
 
Hujwahi kuwa na hisia chanya kwake hata siku moja. Majaji wanaitwa 'Your Lordship' hujawahi kulalamika. Malkia wa Uingereza anaitwa 'Her Majesty', 'Her Royal Highness', 'Your Royal Highness' hujawahi kuhoji. Kusujudu hiyo ni tafsiri yako yenye fikra hasi siku zote.

Hata huyo aliyemwita mtukufu analikuwa na lake jambo namna bora ya kuliwasilisha ijapokuwa hadhi yake aliikweza sana hata hivyo haikuwa lazima amkemee mbunge kwa kuwa ni mwakilishi wa wananchi hata huyo aliyeitwa mtukufu hivyo isikuume kiasi cha kukukosesha hata usingizi ewe mwanasiasa wa kudandia unayeandika ukiwa nje ya mipaka ya nchi.
 
Ndio maana Magufuli alimsifu sana huyu mbunge kwa kumuita handsome...na hata angekuwa na binti angempa!
 
Back
Top Bottom