Rais kuitwa mtukufu na kuabudiwa hadharani bila kukemea inaashiria nini?

Rais kuitwa mtukufu na kuabudiwa hadharani bila kukemea inaashiria nini?

Nyerere hakuitwa Mtukufu alikuwa comfortable kuitwa Mwalimu, Mwinyi na aliyopo leo madarakani tu ndo Watakatifu, kwa sababu MaCCM yanafanya kila kitu kwa mazoea, wapambe walianza kumtukuza Mkapa lakini aliwakemea mapema wakaacha. Kikwete hakuitwa Mtukufu kabisa kwa kuwa alikuwa anajiweza kwa mengi na alikuwa karibu na watu mpaka wakawa wanamwita Shemeji kwa niaba ya Walimu. Wasiojiweza ndo wanajikweza na kukwezwa na wasiojiweza!

Wasiojiweza ndio hupenda kujikweza na kukwezwa na wasiojiweza.
Barikiwa ndugu.
 
Nijuavyo mimi hata kama si mjuzi sana wa mambo ya dini lakini mwenye cheo cha utukufu ni Mungu pekee si binadamu mwenye nyama,


Siyo kweli, Utukufu ni cheo anachoweza kuitwa/ kupewa mtu pia, na siyo utukufu tu bali pia kuna vyeo vingine anavyoweza kuitwa mtu na hapo hapo Mungu akawa navyo, mfano Ukuu nk ni cheo anachoweza kupewa mtu lakini pia Mungu ila tifauti ni hii kwa upande wa Mungu vyeo vyake vinayohadhi kubwa sana isiyoisha wala kupimika kinyume na binadamu vyeo hivyo vinaweza kupungua na kuisha na vinaweza kulinganishwa/kupimwa kati ya binadamu mmoja na mwingine, hiyo ndiyo maana ya maneno; "na tuumbe mtu kwa mfano wetu" au "tujipake rangi ya Allah"--- maneno "mfano' na "rangi" katika hayo maandiko ya Mungu ni sifa za Mungu ambazo binadamu anaweza kuziiga, kujifunza na kuzitekeleza katika upeo wake wa kibinadamu.
 
Nilisoma kisa cha Mtanzania mmoja aliyekuwa anaishi na kufundisha moja kati ya technical college huko Norway na alikuwa mkuu wa department ya Metallurgy. Rais Mkapa akawa ameenda kwenye ziara huko na alikuwa anapota hapo chuo, lengo mojawapo ilikuwa ni kumshawishi jamaa arudi ili kuanzisha hiyo department hapa UD.

Bahati mbaya sana jamaa aliondoka Tanzania wakati wa Mwinyi. Wamekutana na Mkapa akamuita "mtukufu Rais". Jamaa anasema Mkapa alikasirika vibaya mno. Meeting ikavurugika, hakuna kilichoongelewa, na plan nzima za kumshawishi kurudi kwa hiyo kazi zikawa zimeishia hapo.
 
Hili jambo limenistua na kunipa hisia hasi. Sikuamini macho na masikio yangu kwa Rais huyu huyu wa wanyonge na mcha Mungu.

Akitoa maelezo ya kutaka Maendeleo jimboni kwake Kibamba, Mbunge Issa Mtemvu alimwita Rais Magufuli MTUKUFU tena akimsujudu hadi ardhini.

Nilijua Rais atakapoamka kutoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa Stendi ya mabasi huko Mbezi Louis basi angekemea kuitwa MTUKUFU Rais lakini akapiga kimya!

Nijuavyo mimi hata kama si mjuzi sana wa mambo ya dini lakini mwenye cheo cha utukufu ni Mungu pekee si binadamu mwenye nyama, damu na mifupa. Hii tabia ya kujipendekeza hadi kumwabudu binadamu mwenzio ni kumkufuru Allah.

Au nasema uongo ndugu zangu!
Maswali ya kitoto
 
Kwa hili tuwe fair..Marais Nyerere na Mwinyi waliitwa hivi pia bila kuzuia. Ni Rais Mkapa ndiye aliyekuja kukataa kuitwa hivyo. Naandika hivi kwa lengo la kuweka historia sawa tu.
Nyerere hakuwahi kuukubali ujinga huo. Ndiyo maana aliitwa "NDUGU" Rais . Neno mheshimiwa limekuja wakati wa Mwinyi na kuendelea crocodile
 
Mtoa post hujawahi ona MAJALIWA akipita huyu jamaa mbele yake huinua had mikono kuonesha utukufu wa huyu kanjanja yaaan PM huinama kama yupo altare kabsa, inaleta simanzi sana.
Simanzi ya nini kunyenyekea ndo kumemfikisha hadi kuwa PM Endelea na ujeuri
 
Kwa hili tuwe fair..Marais Nyerere na Mwinyi waliitwa hivi pia bila kuzuia. Ni Rais Mkapa ndiye aliyekuja kukataa kuitwa hivyo. Naandika hivi kwa lengo la kuweka historia sawa tu.
Nyerere hakuwai kuitwa mtukufu, alikataa kabisa na akawa anasisitiza aitwe Mwalimu, rudi kwenye historia usome vizuri
 
Hili jambo limenistua na kunipa hisia hasi. Sikuamini macho na masikio yangu kwa Rais huyu huyu wa wanyonge na mcha Mungu.

Akitoa maelezo ya kutaka Maendeleo jimboni kwake Kibamba, Mbunge Issa Mtemvu alimwita Rais Magufuli MTUKUFU tena akimsujudu hadi ardhini.

Nilijua Rais atakapoamka kutoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa Stendi ya mabasi huko Mbezi Louis basi angekemea kuitwa MTUKUFU Rais lakini akapiga kimya!

Nijuavyo mimi hata kama si mjuzi sana wa mambo ya dini lakini mwenye cheo cha utukufu ni Mungu pekee si binadamu mwenye nyama, damu na mifupa. Hii tabia ya kujipendekeza hadi kumwabudu binadamu mwenzio ni kumkufuru Allah.

Au nasema uongo ndugu zangu!
Utukufu,ni jinsi mtu atakavyo,sasa kwa jinsi jiwe anavyoobgoza nchi hii,ni mtukufu,na ili upate utakacho muite hivyo
 
Wafanye wawe masikini ili uwatawale.Kila ajaisujudiae na kukuabudu ataepuka njaa.
Ukisujudia na kuniangukia miguu pangu nitakupa fahari na miliki zote za dunia.Yesu akamwambia Shetani enenda zako imeandikwa msujudie Mola wako tu.
 
Wazee wa escrow wakianguka na kusujudu kwa unyenyekevu ndipo pilato atawarudishia uhuru wao.
 
Back
Top Bottom