Rais kuteua makada UVCCM kuwa Wakurugenzi ni kuvuruga Utumishi wa Umma

Rais kuteua makada UVCCM kuwa Wakurugenzi ni kuvuruga Utumishi wa Umma

Naunga mkono hoja. Nadhani nafasi hizi ingependeza kama zingekuwa zinaombwa na watu wanafanyiwa usaili kwenye panel na TBC ccm inaonesha wazi kama Kenya.

Nafasi hizi zinahitaji mtu mwenye uzoefu na utumishi wa umma, lazima awe na utaalamu wa uhasibu au uchumi na pia usimamizi wa biashara.

Hakuna vitu vinarudisha nyuma utendaji serikalini kama kuteua makada wa ccm. Wengi wao vilaza na wanawaza kujinufaisha hawana uwajibikaji. Katiba mpya tungependa nafasi hizi ziombwe live on national tv interview. Mtu akianza ze chama ze ilani wananchi tunajua dafu hili japo kada lakini kichwani halina kitu linatoswa instantly.
 
Hii nchi jamani kweli kuna haya mambo ya kuzaliwa kwenye silver spoon hapo.

Kuna mteuliwa UDE namfahamu tokea amalize chuo ajira yake ya kwanza ni kuteuliwa uded.

Magufuli alifanya hivyo kwenye uteuzi wa Ma DAS naona mama kamuiga au kahujumiwa.

Mama embu angalia vizuri CV za hao wateule wako.

Nyingine zitakuwa zimebumbwa embu zifuatilie usibitishe ukweli
 
Naunga mkono hoja. Nadhani nafasi hizi ingependeza kama zingekuwa zinaombwa na watu wanafanyiwa usaili kwenye panel na TBC ccm inaonesha wazi kama Kenya.

Nafasi hizi zinahitaji mtu mwenye uzoefu na utumishi wa umma, lazima awe na utaalamu wa uhasibu au uchumi na pia usimamizi wa biashara.

Hakuna vitu vinarudisha nyuma utendaji serikalini kama kuteua makada wa ccm. Wengi wao vilaza na wanawaza kujinufaisha hawana uwajibikaji. Katiba mpya tungependa nafasi hizi ziombwe live on national tv interview. Mtu akianza ze chama ze ilani wananchi tunajua dafu hili japo kada lakini kichwani halina kitu linatoswa instantly.
Nadhani wamaanisha kuwa DEDs hawa wawe sawa na maofisa watendaji wakuu CEO au?

Katiba mpya haiwezi kupatikana ila marekebisho ya katiba iliyopo.

Hata hivyo Tanzania ina uhaba mkubwa wa watu wenye sifa za kuwa CEO.

Ila kwa hawa DEDs ni lazima serikali itengeneze kitu chaitwa Municipal Charter au Council Charter yaani mkataba rasmi ambao ni lazima DEDs wasaini mbali na kula viapo.

Ufanisi wa utendaji wake wa kazi utatokana na kuzingatiwa mambo yaliyomo kwenye mkataba.
 
Hivi kweli hako kadada Form four kwetu kwa wakulima wa mpunga Kwetu Malinyi kweli tumepata hasara sura ya kitoto kweli jamani anyway macho yangu Basi kari
View attachment 1877625
View attachment 1877629
View attachment 1877630

Hawa ni baadhi ya vijana wadogo kabisa toka UVCCM walioteuliwa kuwa makurugenzi.

KWA MUJIBU WA MEMORANDA YA FEDHA SERIKALI ZA MITAA(LGA) HAYA NDIO MAJUMKUMU MAZITO YA DED

1. Ensuring the existence of a formal and satisfactory system of financial administration;

2. Securing compliance with the prescribed financial procedures by operating departments;

3. Directing the work of the Internal Audit section, receiving their reports and after consultation with relevant head of departments, ensuring recommendations and acted upon and submitted to relevant authorities;

4. Overall management of Council’s expenditures, revenues, and all assets and liabilities;

5. Ensuring compliance of all statutory guidelines for the financial Management of Council affairs;

6. Responding to queries within given deadlines from the Office of the Controller and Auditor General, the Local Authority Account Committee (LAAC) and the Minister;

7. Making certain that councillors are kept regularly informed of the financial affairs of the Council;

8. Being secretary to the finance Committee;

9. Making sure that computerized system operates;

10. Keeping under good Custody all assets and property of the Council; and

11. Adhering to procurement functions stipulated in Public Procurement Act and its related

KWA TAFSIRI ISIYO RASMI

1. Kuhakikisha kunakuwa na mfumo rasmi na wakuridhisha katika usimamizi wa fedha

2. Kuhakikisha idara zinafanya matumizi kwa mujibu wa taratibu za fedha

3. Kuhakikisha kitengo cha ukaguzi wa ndani kinafanya kazi vyema, kupokea taarifa za ukaguzi wa ndani, na kwa kushirikiana na wakuu wa idara ahakikishe maoni ya mkaguzi wa ndani yanajibiwa na kutekelezwa na anawasilisha majibu hayo kwa mamlaka husika ambazo ni CAG, RAS na Chief Internal Auditor

4. Usimamizi wa matumizi, mapato, mali na madeni yote ya halmashauri kwa ujumla

5. Kuhakikisha sharia, sera, kanuni na miongozo yote ya usimamizi wa fedha za halamashauri inafuatwa.

6. Kuhakikisha kuwa anajibu kwa wakati hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa(LAAC) na wizara

7. Kuhakikisha waheshimiwa madiwani wanapata taarifa za fedha za halamashauri

8. Kuwa katibu wa Kamati ya fedha ya Halamshauri. Kamati hii wajumbe wake ni madiwani.

9. Kuhakikisha mifumo ya kompyuta inafanya kazi

10. Kuhakikisha utunzaji mzuri wa mali za Halmashauri

11. Kuhakisha sharia ya manunuzi ya umma na kanuni zake zinafuatwa

MAJUMKU MENGINEYO

1. Kuidhinisha malipo

2. Kuidhinisha mikataba yote ya halmashauri

3. Kuteua Bodi ya Zabuni kwa mujibu wa sharia

4. Kuteua Kamati ya Ukaguzi(Audit Committee) kwa mujibu wa sharia

5. Kuwa mkurugenzi wa uchaguzi ngazi ya wilaya pale inapotokea

6. Kuteua kamati ya upembuzi wakati wa manunuzi makubwa

MY TAKE

Hii kazi sio rahisi kama mashabiki wa mwendo kasi mnavyodhani. Huyu mtu anaenda kuwa msimamizi wa idara 19 pale halmashauri. Ikiwepo idara ya elimu na afya zenye changamoto za kufa mtu. Huyu mtu ndio anaenda kukuza uchumi wa wilaya na kuongeza pato la taifa kupitia wilaya yake. Mikataba mikubwa ya mabilioni ya fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo inaenda kuidhinishwa na yeye baada ya kujiridhisha kila kitu kiko sawa.

Anakwenda kusimamia matumizi ya mapato ya ndani ya zaidi ya bilioni 20 mfano Manispaa ya Kinondoni mpaka milioni 500 kwa halmashauri mpya. Anakwenda kusimamia ruzuku ya serikali mabilioni ya fedha.

Anakwenda kusimamia ufungaji wa hesabu na kujibu hoja ngumu za CAG kama tulivyoona hapo juu, matokeo yake unashindwa kuzuia au kujibu hoja unaanda maburungutu ya kuhonga wakaguzi

Kwa maoni yangu, serikali isione aibu, pangia hawa watu wasio na sifa majuku mengine mara moja. System inajua nani mwenye uwezo na asiye na uwezo

Mjadala
Je huku ni kunajisi utumishi wa umma?

Thanks
Hivi kweli hako katoto Kataweza hapa Malinyi kwenye mpunga wetu labda ,,, Basi karibu tyu tujipatie mke maana inaonekana hujaolewa Bint na suala inafaa kuwa mke wa maonesho,, Lakini hako ka Joanfaith hakawezi kupaisha Uchumi wetu wa Malinyi anyway nisiandike mwishowe nikakosea
 
Ila mkitumia hicho kigezo vipi wengine kujifunza na ku grow, watumishi wengi wa umma ni magoi goi flani na wamezoea kufanya kazi bora liende tu. So kuchaganya watu tofauti tofauti sio mbaya. Walio kwenye miradi ukifanya na watumishi wa umma wako lazy sana bora liende tu bora kuwe na mixture flani hivi
ni vema kujifunza..
Ila km hujawai kufanya kazi hata kuwa mkuu wa kitengo au idara aombe Mungu.
Wazoefu Wanaweza kukuyumbisha akajikut anaingiza halmashauri kwenye migogoro.
Pili inawavunja moyo watu waliotumikia kwa umakini na unyenyekevu nafasi zao na wana vigezo vya uteuzi ila hawateuliwi wakikata tamaa utaumiz wengi.hawatakuwa na moyo wa kujitoa km awali
Watu wengi tunaangalia tulipoanguka siotulipojikwaa; mfano watu wengi wapo lazy..Ila hatuangalii.kwa nn wapo lazy..
Ni Sawa na kumlaumu kwa nn baba hakumpeleka mama hospital kwa tax au bodaboda katumia baiskeli au daladala wakati hiyo baiskeli tu ya kufika hospital kaiazima Ili asevu pesa ya matibabu ya mama kutokana a mavuno haba aliyoyapata msimu ulopita na hajawai kukulalamiia japo unajua na ww mtt umefanikiwa Umeanza matanuzi na maamuzi ya kujijenga ww kwanza ukiamini muda Upo utawakumbuka.
 
Mama anawakomoa mataga na sukuma gang!
.
Alisikika mamwia toka ufipa
 
Bora wangeteuliwa hata maafisa elimu kata kwenye digiri na uzoefu wanao.Hao watoto hata kuwa maafisa utumishi hawajawahi Fanya.Hii ni dharau sana
 
Mkuu hata hawa wengine wapya hakutakuwa na tofauti. Trust me. Sababu zinazofanya hao wengine kuwa magoigoi ndiyo hizi hizo zinakwenda kufanya hao wapya wawe hivyo. Hawa watu walitakiwa wawe wanabanwa na sheria kanuni ili wasiwe magoigoi. Tubadilishe wanavyopatikana na jinsi wanavyopimwa kwa kazi. Tufumue mfumo!
Ulichoandika uko sahihi tena bora wapya damu moto majority walioko serikalini husubiria mishahara na posho basi ubinifu zero, inabidi serikali ije na system nzuri ya kumonitor miradi ya maendeleo na ufanisi wa utendaji kazi wa watumishi wa umma, bila hvo umaskini kuisha Tanzania haitakwisha wala
 
Saizi upigaji utakuwa mkubwa kwa sababu Hawa madada hawajawahi kufanya Kazi zozote za Halmashauri hawajui taratibu yaani watakuwa bypassed Sana japo watazoea baada ya kama mwaka hivi,sijui kwenye vikao vya madiwani na RCC watakuwa wanajieleza vipi
Hata huo upigaji ni vile serikali inaruhusu kwanini wasiweke mifumo inayozuia huo upigaji na hyo mianya yote huko serikalini?
Wenzetu wamewezaje kuzuia hyo Hali na sisi kwanini tushindwe
 
Back
Top Bottom