Rais kuwekewa zuria barabarani wananchi hawana barabara!

Rais kuwekewa zuria barabarani wananchi hawana barabara!

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Nilishauliza je utamaduni wetu ni tatizo?

Kwa wenzetu Maraisi wanajaribu kufanana na watu wao lakini Tanzania Raisi ni kama mfalme au malikia!

Raisi Samia kutandukiwa zulia kila mahali wakati wananchi wake hawana barabara, maji, kazi na wana maisha duni ni kitu cha kutafakari sana.

Nitoe tu mfano mimi naishi maeneo ya Dallas na Fortworth Taxas mashuhuri kama DFW metro kuna watu 7.5 M na GDP ya $600B . Tanzania yote GDP yake ni kama $100B tu lakini jiulize tuna viongozi wangapi wanahudumiwa kwa vitu ambavyo haviongezi thamani yaani mtu ana ajiribu kuweka zulia tu chini kwa raisi kukanyaga. Misafara mikubwa mikubwa bila ulazima. Hatutengenezi magari wenzetu mfano hapa tunatengeneza Toyota wenyewe, hatuna mafuta wenzetu hapa tuna chimba mafuta lakini serikali ya Tanzania inatumia pesa nyingi sehemu ambazo sio za lazima na viongozi wanajali ufalme kuliko wananchi.

Lakini tulaumu utamaduni wetu. Ni sawa tu Raisi kutembelea msafara mdogo na magari ya kawaida tu badala ya magari 30 ya milioni 400 kwa gari. Pili sio lazima kila kiongozi awepo kwenye shughuli za Raisi mikoani maana inapunguza ufanisi kazini. Mambo kama haya ndiyo yanafanya katiba mpya isifanikiwe maana Raisi anaona atakosa ufalme au umalikia tubadilike. Serikali wafanyakazi ni waajiriwa wa wananchi nchi hii sio ya kifalme
 
Trump "Viongozi wa Afrika ndio sababu kubwa ya umaskini wa nchi zao , hawana mtazamo wa maendeleo kwa nchi zao ndio maana huchezea rasilimali zao na kutegemea misaada kutoka kwa walipakodi wa nchi zetu zilizoendelea"
 
Fidel Castro " kiongozi mbinafsi wa fikra na maono huchukua kingi na kutapanya katika starehe zake na marafiki zake wakati wananchi wakiteseka, ndio maana nimeamua Kutokua mbinafsi na nitaifia Cuba"
 
Macron" Wanapigana vita wao , ufisadi wanafanya wao, wizi wa rasilimali wanafanya wao , mikataba mibovu wanafanya wao, lakini mwisho wanatulaumu sisi bila kukumbuka tulishaondoka kwenye nchi zao na kuwapa Uhuru wao wajiongoze lakini lawama kila siku zinarudi kwetu hawa watu wa ajabu Sana"
 
Mwafrika ni ishara ya udumavu wa akili na fikra.Kutaka jambo hili kuwa katika ithibati sahihi angalia matendo yetu,Tanzania kutumia 34b kujenga makubusho ya maraisi nk
 
Back
Top Bottom