Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa za kishamba sana hizi. Yaani mtu unatrgeneza tatizo Kisha unakuja kulitatua ili uonekana hero!! Rais wa ajabu sana. Mpaka mswada unapita alikuwa wapi??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sasa ulijitoa muhanga kuwa kuhakikisha wastaafu wanateseka kumbuka na wewe ni mtumishi utastaafu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi alisaini kuwa sheria Mkuu ?
Alisaini aisee...Alikuwa anasikilizia kelele! Hata siku ile ya Mnyika akaishia kutoa vijembe. Kama walau tusingepiga kelele jamaa alikuwa anazunda akaendeleze miradi na viwanda! Si unaona hata swala la nyongeza ya mishahara?
 
watu wanatafuta kiki tu hapo.

wametengeneza tatizo ili waonekane wamelitatua!

si ajabu waziri mhusika akatolewa kafara.
Saa nyingine ni busara kusikiliza na kusoma kimya kimya bila kuchangia kitu.

Umeambiwa hicho kikokotoo kilipangwa na waziri na katibu wakuu wa wizara husika wakati wa awamu ya nne.
 

Ajiuzulu
 
Mimi nakubaliana na maamuzi 100% lakini swali kwani kuna serikali ndani ya serikali? maana Serikali ikiongozwa na yeye ndio walipeleka haya mabadiliko yakafanywe sheria bungeni leo tena anakuja mwenyewe kupinga mapendekezo yake, na kama suala matumizi mabaya hili ni la serikali kuchukuwa hatua wafanyakazi hawana dhambi kwanini walikuwa wabebeshwe mzigo sio wao. Sheria imepitishwa bungeni inatengeliwa ikulu na hakukuwa na haja ya kuwasikiliza kuongea maana Rais alishakuja na maamuzi tayari. Mimi naschukulia kuwa kampeni za uchaguzi zimeanza rasmi ila play ground haiko level. leo kocha kawa refa.
 
Nimeshangaa maamuzi aliyotoa ni kama wanajichanganya,
Kwani hao viongozi wa mifuko ya jamii si yupo nao kila saa na hata usikute wazo alilitoa yeye,
Sipingi ila ninavyoona serikali inafanya mambo kwa kukurupuka na kutokufikiria
Kwani hawakuona sheria hii ni mbovu na itaumiza watu wakati wakitaka kuipitisha?
Yani lililofanyika leo ni kama siasa
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Katumwa na huyo huyo jiwe!

Then jiwe huyo huyo kafanya yake!

Namshauri Irene ajiuzulu ili walao kutuma msg kwa jiwe kwamba mchezo anaofanya ni wa kitoto mno na sio vizuri kabisa!

Yaani jiwe kageuza vijakazi wake ni mapunguani!
 
BINARY NO hao wanaopewa maagizo hawana uwezo wa kufikiri? Kama wewe ni mteule na unaenda mwendo bendera hufai. Yaani huwezi kutumia hata common sense na logic kidogo na kuweza kusema hapana kwa kutoa supporting facts!
Bahati mbaya sana serikali hii ndivyo ulivyosoma.Kufuata upepo/bendera ni kigezo kwenye teuzi za awamu hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa nilishangaa alipomtimua Mwiguru akidai amechoka kutoa pole wakati yeye ndiye chanzo cha matatizo na alifanya hivyo baada ya " mtoto wake" kumzidi ujanja na kuwafanyizia hata wale wasiohusika na maelekezo yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…