Rais Magufuli amekosea sana kuagiza magari ya kesi za Uhujumu Uchumi yapewe Taasisi za Serikali

Rais Magufuli amekosea sana kuagiza magari ya kesi za Uhujumu Uchumi yapewe Taasisi za Serikali

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Raisi Magufuli amefanya kosa kubwa sana kuagiza kwamba magari yaliyotaifishwa kuhusiana na kesi za uhujumu uchumi yagaiwe kwa taasisi za Serikali kwa sababu mbili kubwa zifuatazo;
  1. Haya magari mengi ni ya zamani sana, zaidi ya miaka 10, na mengi yalinunuliwa kama used vehicles. Wamiliki binafsi huwa wana namna yao ya kuya-maintain kwa gharama za chini, na kuyaingiza serikali kutasababisha gharama kubwa za matengenezo na maintanance ambayo mwisho wa siku itakuwa ni hasara kwa taifa. Watu wa uhasibu wakipiga hesabu za "depreciation" za haya magari wanaweza kukuta ni scrap tu. Gharama ya ku-maintain gari "scrap" ni kubwa sana afadhali kununua gari jipya
  2. Kuna sera ya serikali ya manunuzi kwamba taasisi za serikali hazipaswi "kununua" (acquisition) magari au vitu ambavo ni second hand. Kwa hiyo japo magari haya yanatolewa bure kwa hizi taasisi za serikali, kimsingi hili linakiuka sera ya taasisi za serikali kutoingiza kwenye leja zao za umiliki wa mali vitu magari ambayo ni "used".
Nini kifanyike basi?

Ningemshauri Rais Magufuli kwamba haya magari yapigwe mnada na fedha zitakazopatikana ziingizwe kwenye shughuli zinazohusiana na kupambana na uhujumu uchumi nchini, ili wakamate magari mengi hata zaidi!
 
Ni kweli una mawazo mazuri ila najiuliza Range Rover ukiipeleka kwenye taasisi kila Boss atataka iwe yake aitumie yeye. Lakini pia mnada nao nyie hao hao mngesema ooh wameuziana magari !!!! yaani Uongozi ni shidaaa.
 
1598428283441.png
1598428504600.png

1598429465792.png
 
Ni kweli una mawazo mazuri ila najiuliza Range Rover ukiipeleka kwenye taasisi kila mtu atataka iwe yake ambae ni boss...Lakini pia mnada nao wangesema ooh wameuziana magari yaani Uongozi ni shidaaa..
Ngoja siku waipeleke hiyo Range Rover service waone bili itakayokuja, wataiacha garage!
 
Kuna maeneo hayana magari kabisa ya huduma kwa wananchi, sasa bora nini? Wapate magali yaliyotumika na kuyatumia au wawe bila magari watumie baiskeli?
Kama serikali inaona umuhimu mkubwa wa hizo sehemu kuwa na gari basi iwanunulie, lakini sio kuwapa gari ambazo watu wengine walikuwa wanazifanyia service chini ya miti na sasa zinaingizwa katika taasisi za serikali.

Ni kuingia gharama zisizo na msingi, na utakuta hizo gharama ya kuhudumia hizi gari zitakuwa kubwa sana kiasi ni bora hizo taasisi zingenunua gari mpya.
 
Hizo screpa watumishi wa serikali watakuja kuuziana tu.

Haya TEMESA kaeni mkao wa kula.
 
Kama serikali inaona umuhimu mkubwa wa hizo sehemu kuwa na gari basi iwanunulie, lakini sio kuwapa gari ambazo watu wengine walikuwa wanazifanyia service chini ya miti na sasa zinaingizwa katika taasisi za serikali. Ni kuingia gharama zisizo na msingi, na utakuta hizo gharama ya kuhudumia hizi gari zitakuwa kubwa sana kiasi ni bora hizo taasisi zingenunua gari mpya

Iwanununulie kwa bajeti ipi mkuu. Why huoni jema kwenye kitu direct hivyo. Kasema kule ambako Kuna Shida hasa wananchi kupata huduma. Watu kama nyie sijui Ni Perfect kiasi gani. Lakini kisaikologia the opposite is true.
 
Back
Top Bottom