Uchaguzi 2020 Rais Magufuli amepania kurejesha kwa nguvu mfumo wa chama kimoja nchini

Uchaguzi 2020 Rais Magufuli amepania kurejesha kwa nguvu mfumo wa chama kimoja nchini

THE SEAL,
Hakika inaumiza sana kwa mtu tuliyempa madaraka na kuamini kuwa ataiongoza nchi yetu kwa kufuata Katiba ya nchi yetu, ndiyo huyo huyo anatawsla kwa kutumia utashi wake binafsi na kwa kutumia upanga, huku tukiwaona hao tunaowaita watumishi wa Mungu wakijiunga na ile "Praise and worship team for Magufuli"

Hakika kama ulivyosema, siyo kwamba Mungu aliyetuumba, na ndiye aliyemuumba na yeye huyo anayetamba kwa hivi sasa, akiiamini kuwa Mungu aliye hai kuwa amelala fofofo........

La hasha, tumuhakikishie kuwa Mungu wetu tunayemwanini kuwa hiivi sasa ana-monitor kila kitu kinachoendea ndani ya nchi hii kwa ukaribu sana kwa vitendo vya watawala wetu kuamrisha majeshi yetu, ambayo tunayahudumia kwa kodi zetu wananchi wote bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kwa kuyaamrisha "yaue" raia yeyote anayepinga udhalimu wao!

Lakini wanachokisahau hao watawaka wetu.kuwa Mungu wetu ni mkuu kuliko kitu chochote na halinganishwi na kitu chochote hapa duniani na kazi yake hufanya kwa wakati anaoamini yeye kuwa ni muafaka, kwa hiyo tuwaamche hao watawala wetu na upofu wao na ulevi wa madaraka uliopitiliza na kuamini kuwa wao ndiyo "Miungu" wapya ambao wanastahili kuimbiwa mapambio ya kusifiwa na kuabudiwa kwa kila walitendalo!

Wacha kulia nyau, wewe ndiye ulimpa madaraka? Kwanza pengine hata kura hukupiga then unakuja kulialia hapa kama nyau. Leta facts usiandike majungu. Ningekubali hoja yako kwamba mambo anayofanya JPM yaani kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo itauwa upinzani ningekuelewa.
 
FUSO,
Wewe unadhani, nini kitaendelea baada ya uchaguzi huu wa serikali za mitaa??

Jibu langu ni kuwa anataka ashinde kwa asilimia 100, ili aihadae dunia kuwa hapa nchini hakuna upinzani dhabiti, bali kuna wapinzani dhaifu sana!

Ili atimize ajenda yake ya siri, ya kurejea kwenye mfumo wa chama kimoja na kumfanya yeye kuwa Life President wetu
Naomba kuuliza tu,hivi daktari na mlinzi wa magufuli nao ni watanzania ?any way sijui kwa nini nauliza hili swali
 
Wacha kulia nyau, wewe ndiye ulimpa madaraka? Kwanza pengine hata kura hukupiga then unakuja kulialia hapa kama nyau. Leta facts usiandike majungu. Ningekubali hoja yako kwamba mambo anayofanya JPM yaani kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo itauwa upinzani ningekuelewa.

Ole ,
Wewe ni Nyang'au tu!
Tunajua Policcm,NEC na UWT ndio waliompa madaraka JPM! Hili unalijua ma JPM anajua hivo. Mstahafu Mkapa katika kitabu chake:My LIfe, My Purpose ameweka wazi kuwa FEDHA YA EPA ILIMWINGIZA KWENYE URAIS Mgombea wa CCM…! Sasa unataka FACTS gani we nyang`au?
 
THE SEAL,
Wazungu hawakutaka kabisa Marekani ipate rais mweusi lakini Mungu aliposema ndiyo hakuna aliyeweza kumzuia Obama.

Kuna siku ambayo CCM itaishiwa mbinu zote na upinzani kuingia madarakani. Ninamuomba Mungu aniweke hai nilishuhudie hili.
That day is not far, 2020 will not end with a ccm president, take that to the bank my sister, you cant kill people, ruin the economy, pump 37 bullets on an opposition mp and you think you will live long, NO WAY,
 
kama mwenyekiti wa CCM Hilo ni jukumu lake muhimu
 
Pascal Mayalla,
Kama kweli tumemkubali watanzania wote, ni kwanini basi anaogopa uchaguzi ulio huru na wa haki, ili wananchi ndiyo wachague viongozi wao wanaowataka katika uchaguzi ulio huru na haki??

Utasemaje kuwa watanzania ndiyo tulioamua kurudi kwenye mfumo wa chama kulimoja, wakati figisu figisu zikionekana dhahiri kwa wagombea wa upinzani zaidi ya asilimia 95, fomu zao zikikataliwa na hao wasimamizi wa uchaguzi, ambao ni makada kindakindaki wa CCM, kuwa eti zimejazwa vibaya, wakati wenzao viongozi wa CCM wakiwa wamejaza kwa usahihi wa asilimia 100??

Hivi figisu figisu zote hizo, unataka kuniambia Mkuu Pascal, umetiwa upofu na umeamua kutoziona??

Mystery,
Achana na huyo mnafiki mkubwa Bw. Pascal Njaa…!Naona anajitahidi kutetea upuuzi wa CCM ili JPM amkumbuke angalau hata u~DC!
 
Huyu jamaa Siasa kwake ni mtihani mkubwa kwake hasa siasa za ushindani ndiyo hazitaki kabisa.Nikirejea yale aliyo mfanyia mshindani wake kwenye chama kipindi cha kugombea uteuzi wa kuwania Ubunge huko kwao .
 
Ole ,
Wewe ni Nyang'au tu!
Tunajua Policcm,NEC na UWT ndio waliompa madaraka JPM! Hili unalijua ma JPM anajua hivo. Mstahafu Mkapa katika kitabu chake:My LIfe, My Purpose ameweka wazi kuwa FEDHA YA EPA ILIMWINGIZA KWENYE URAIS Mgombea wa CCM…! Sasa unataka FACTS gani we nyang`au?
Mzalendo 2015
Tatizo lako wewe ulikuwa mfaidika mkubwa wa awamu ya BWM na JK hivyo ule mlo wako umekatwa kwa sababu Chuma kiko Ikulu. Endelea kuwewesekaweweseka tu lakini unafahamu kifo cha mende unacho. Unaongelea BMW aliyeuza viwanda vyote alivyoanzisha Mchonga na mashirika yote ambayo mchonga aliyaacha. JPM Jembe na mtakoma ubishi, hakitoki kitu hapa. Hapa kazi tu!
 
Eeenh, napinga mlinganisho huo.
Yule ,Mama' wa 'Nobel' mbona siku hizi hasikiki, au kwa vile mlimpa ulaji kajisahau?
Yupi huyo? Tanzania haijawahi kuchaguliwa kwa Nobel prize najua ni Prof. Mathai tu RIP.
 
Wacha kulia nyau, wewe ndiye ulimpa madaraka? Kwanza pengine hata kura hukupiga then unakuja kulialia hapa kama nyau. Leta facts usiandike majungu. Ningekubali hoja yako kwamba mambo anayofanya JPM yaani kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo itauwa upinzani ningekuelewa.
Kama JPM anatekeleza ipasavyo ilani ya CCM, ambapo kama unavyodai wewe kila mtu anaona, ni kwanini basi anaogopa mno kupambanishwa na vyama vya upinzani??

Angeruhusu uchaguzi ulio huru na hao wananchi unaosema wanaona hayo maendeleo, wapige kura kwa kumpa ushindi wa kishindo

Siyo kuihadaa dunia kuwa tunafanya chaguzi, wakati in real sense, tunachofanya ni UCHAFUZI!
 
Pascal Mayalla,
Kama kweli tumemkubali watanzania wote, ni kwanini basi anaogopa uchaguzi ulio huru na wa haki, ili wananchi ndiyo wachague viongozi wao wanaowataka katika uchaguzi ulio huru na haki??

Utasemaje kuwa watanzania ndiyo tulioamua kurudi kwenye mfumo wa chama kulimoja, wakati figisu figisu zikionekana dhahiri kwa wagombea wa upinzani zaidi ya asilimia 95, fomu zao zikikataliwa na hao wasimamizi wa uchaguzi, ambao ni makada kindakindaki wa CCM, kuwa eti zimejazwa vibaya, wakati wenzao viongozi wa CCM wakiwa wamejaza kwa usahihi wa asilimia 100??

Hivi figisu figisu zote hizo, unataka kuniambia Mkuu Pascal, umetiwa upofu na umeamua kutoziona??
Ulimpima kwa meter gauge gani kuona hiyo hofu?
Jamaa hana hofu, yeye ni kazi tu 24/7.
Mwenye hofu ni Chadema
 
Ulimpima kwa meter gauge gani kuona hiyo hofu?
Jamaa hana hofu, yeye ni kazi tu 24/7.
Mwenye hofu ni Chadema
Hivi ni kwanini nyinyi maccm tunapousema ukweli kuwa Magu anauogopa sana upinzani, mnakana kuwa siyo kweli??

Sasa mbona tunapowauliza maswali ya msingi, kuwa iweje aendeshe uchaguzi huu wa serikali za mitaa kwa uhuni wa kiwango hiki, mnakosa majibu!
 
Wacha kulia nyau, wewe ndiye ulimpa madaraka? Kwanza pengine hata kura hukupiga then unakuja kulialia hapa kama nyau. Leta facts usiandike majungu. Ningekubali hoja yako kwamba mambo anayofanya JPM yaani kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo itauwa upinzani ningekuelewa.
Hakuna jambo hata moja analofanya JPM linaloweza kuua upinzani isipokuwa ukandamizaji wa demokrasia. Hivi umejiuliza kwa nini atoe maagizo kwa watendaji wa kata ambao ni wasimamizi wa uchaguzi waharibu uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kuwaengua wagombea wote wa upinzani!!?
Anatambua nguvu ya upinzani. Hapo alipo yeye ni zao la upinzani. Sema tu mtu mwenyewe inawezekana hata maana ya neno "demokrasia" atakuwa haelewi. Sababu kubwa ni kuwa vyuo vya uongozi wa umma nchini ni kizungumkuti.
Anaweza kuwa anaamini 'demokrasia' ni barabara ya lami, flyover, ndege, sgr au stiegler's gorge!!! Kwamba demokrasia ni pamoja na Uhuru na haki za kiraia, kwake ni kiza kinene.
Nasema hivi kwa sababu sioni ni kwa sababu zipi za msingi kwamba Rais mwenye PhD katika karne ya 21 atamani kutawala kwa mfumo wa Chama kimoja!!! Yalipofanywa na akina Idd Amin au Bokasa, tulielewa ni 'inferiority complex', maana wale walikuwa ni darasa la nne la zamani!!!
 
Naomba kuuliza tu,hivi daktari na mlinzi wa magufuli nao ni watanzania ?any way sijui kwa nini nauliza hili swali
Hao ni wa kutoka nchi jirani, kwa yule Best friend wake, anayefahamika kwa initials za PK

Huyu jamaa amefikia hatua ya kutowaamini kabisa watanzania!
 
Tokea mwaka 1992, nchi yetu iliamua kuirejesha nchi hii kwenye mfumo wa vyama vingi na mfumo huo ukaingizwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 3(1) ambayo inatamka wazi kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia na ni nchi ya vyama vingi" mwisho wa kunukuu

Ingekuwa Rais Magufuli anaurejesha mfumo wa chama kimoja, kutokana na ridhaa ya wananchi wake, kutokana na wananchi hao kupiga kura katika uchaguzi ulio huru na wa haki, mimi nisingekuwa na hoja ya kupinga

Lakini kwa njia hii tunayoiona tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, ambapo Rais huyu "analazimisha" ionekane wananchi ndiyo wameupokea mfumo huo wa chama kimoja, ndipo ninapokataa na kuiona njia hiyo ni uhuni wa hali ya juu na uvunjifu wa waziwazi wa Katiba yetu ya nchi!

Dunia nzima imeshuhudia namna ambavyo utawala huu wa awamu ya tano ulivyovunja Katiba ya nchi, kupitia kwa wasimamizi wa uchaguzi, ambao ni makada wa kindakindaki wa CCM, wakionekana kupewa "maagizo" maalum, kutoka juu, kuanzia zoezi la uandikishaji wapiga kura, uchukuaji fomu na urudishaji wa fomu hizo na namna walivyowa-disqualify, wagombea wa vyama vya upinzani, ambapo zaidi ya asilimia 95, wakakatwa majina yao, kwa kile wasimamizi hao wamekiita ni ujazaji mbaya wa fomu hizo za kuomba uongozi wa serikali hizo za mitaa

Wakati hayo yakifanyika kwa upande wa vyama vya upinzani nchini, hali imekuwa tofauti kabisa kwa upande wa Chama tawala cha CCM, ambapo wagombea wake wote wameonekana kama "malaika" kwa asilimia 100 ya wagombea wake kuzijaza kwa usahihi mkubwa na hivyo kuwa- qualify kuwa wagombea waliopita bila kupingwa!

Kutokana na hali hiyo, vyama vinane, vikiongozwa na chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, kutangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro hicho katika huo "uchafuzi" unaotarajiwa kufanyika hapa nchini, tarehe 24 ya mwezi huu

Kumetolewa miito kadhaa na vyama hivyo vya upinzani, pamoja na viongozi wa dini mbalimbali, kuomba uchaguzi huo ufutwe na upangwe katika tarehe nyingine, chini ya Tume mpya ya uchaguzi iliyo huru, lakini miito yote hiyo, imekuta masikio ya watawala wetu yakiwa yamewekwa "pamba" masikioni na kuamua kuendelea na uchaguzi huo.

Ndipo hapo ninapoona kuwa Rais Magufuli ameamua kuivunja Katiba ya nchi hii waziwazi kabisa kwa kutaka kuurejesja mfumo wa chama kimoja kwa nguvu, bila ridhaa ya wananchi hao.

Je Rais Magufuli aendelee kuchekewa na aendelee kuimbiwa mapambio na wananchi wote wa nchi hii kwa kuungana na kujiunga na "praise and worship team for Magufuli" kwa huu uvunjifu wa Katiba ya nchi wa waziwazi kabisa?

Tunajua kuwa watawala wetu wanakuwa na kiburi na kulewa madaraka kwa kiasi cha kutisha, kwa kuamini kuwa wao ndiyo "wanaolimiliki" Jeshi la Polisi nchini na ndiyo sababu kuu, inayowafanya watishie wananchi wote kuwa atakayeupinga huo UCHAFUZI wao atashughulikiwa ipasavyo!

Nakaribisha maoni katika kuirekebisha hali hiyo ambayo inanyemelea Taifa letu ambapo zoezi muhimu sana la kidomokrasia la kutoa Uhuru kwa wananchi wa nchi hii, kuchagua viongozi wanaowataka wenyewe katika uchaguzi ulio huru na haki, ukiwa umenyongwa.

Nitoe wito kwa watawala wetu walioamua kuweka pamba masikioni, kuwa zoezi la wananchi kuchagua viongozi wao katika uchaguzi ulio huru na haki, kupitia sanduku la kura, ndiyo njia pekee, inayoweza dumisha AMANI na UTULIVU hapa nchini.

Watawala wetu watakuwa wanajidanganya kupita kiasi kwa kuamini kuwa risasi, magari ya washawasha na mabomu ya machozi ya Jeshi letu la Polisi, ndiyo yatakayowadumisha wao CCM madarakani.

========
Mawazo ya wachangiaji
Kwanza nakupa hongera kwa kupenda kuchukuwa mawazo ya upande mmoja nakuyafanya ndio sahihi bila ya kuyabalance.Pili ningependa kukuweka sawa hakuna Rais ameeonekana au kusikika akiwapa maelekezo watendaji wake kuhusiana na uchaguzi, ninavyojua ni pale Rais anapokuwa ziarani na kutaka kujua kero za wananchi halafu mhusika hayupo hapo utakuta lipo chini ya vyama pinzani sasa huoni hizo ni dharau Rais atawezaje kuwasaidia wananchi wakati wawakilishi wao hawapo na ndio maana anakuwa anatoa kauli za kuwataka wananchi kuchagua viongozi wanaofaa sasa hapo ni kosa. Kuhusu fomu kumbuka vyama pinzani vilishasusia kabla hata ujazaji fomu kuanza huoni kuwa walikuwa na lengo la kususa kabla ya kujaza fomu?hapo walishaona mambo mazuri yanayofanyika wakaona watumie mbinu hizo ili ionekane wanaonewa kwa kuwaweka wagombea wasiowapa maelekezo ya jinsi ya kujaza fomu na pia kila chama kina mwanasheria wake na ilikuwa unavyojaza fomu unatakiwa ugongewe mhuri na katubu wake hilo nalo utalizungumziaje. Wagombea wa ccm waliweza kujaza fomu vizuri ni kutoka na kupewa maelekezo mazuri na wanasheria wao. Pia kumbuka vyombo vya ulinzi na usala vipo kwa ajili ya usalama wa wananchi wake na sio ccm pekee, hao wengine wanavunja sheria na ndio maana unaona kama wanaonewa. Hivyo nakushauri uwe unajitahidi kutafuta taarifa vizuri na kuzilinganisha la sivyo baadae utakuja kujilaumu na muda utakuwa umeshapita.
 
Hao ni wa kutoka nchi jirani, kwa yule Best friend wake, anayefahamika kwa initials za PK

Huyu jamaa amefikia hatua ya kutowaamini kabisa watanzania!
Sasa siku akimkorofisha PK ndo maisha yake yameishia hapo
 
Kwanza nakupa hongera kwa kupenda kuchukuwa mawazo ya upande mmoja nakuyafanya ndio sahihi bila ya kuyabalance.Pili ningependa kukuweka sawa hakuna Rais ameeonekana au kusikika akiwapa maelekezo watendaji wake kuhusiana na uchaguzi, ninavyojua ni pale Rais anapokuwa ziarani na kutaka kujua kero za wananchi halafu mhusika hayupo hapo utakuta lipo chini ya vyama pinzani sasa huoni hizo ni dharau Rais atawezaje kuwasaidia wananchi wakati wawakilishi wao hawapo na ndio maana anakuwa anatoa kauli za kuwataka wananchi kuchagua viongozi wanaofaa sasa hapo ni kosa. Kuhusu fomu kumbuka vyama pinzani vilishasusia kabla hata ujazaji fomu kuanza huoni kuwa walikuwa na lengo la kususa kabla ya kujaza fomu?hapo walishaona mambo mazuri yanayofanyika wakaona watumie mbinu hizo ili ionekane wanaonewa kwa kuwaweka wagombea wasiowapa maelekezo ya jinsi ya kujaza fomu na pia kila chama kina mwanasheria wake na ilikuwa unavyojaza fomu unatakiwa ugongewe mhuri na katubu wake hilo nalo utalizungumziaje. Wagombea wa ccm waliweza kujaza fomu vizuri ni kutoka na kupewa maelekezo mazuri na wanasheria wao. Pia kumbuka vyombo vya ulinzi na usala vipo kwa ajili ya usalama wa wananchi wake na sio ccm pekee, hao wengine wanavunja sheria na ndio maana unaona kama wanaonewa. Hivyo nakushauri uwe unajitahidi kutafuta taarifa vizuri na kuzilinganisha la sivyo baadae utakuja kujilaumu na muda utakuwa umeshapita.
Kwa rais kujua shida za wananchi wake lazima afanye ziara,sasa hiyo representation tunayoambiwa niya nini na tunawakilishwa kwa nani?Je hiyo ya wapinzani kutokujumuika kwenye ziara za rais imeanza tangu 1992 au wakati huu wa Magufuli?
 
Back
Top Bottom