Rais Magufuli amkaanga vikali Waziri Kamwelwe, atishia kumuweka ndani kwa Uhujumu Uchumi

Rais Magufuli amkaanga vikali Waziri Kamwelwe, atishia kumuweka ndani kwa Uhujumu Uchumi

Udhalilishaji tu ,unamfanya waziri kama muhudumu wa baa.This is character assassination. Just respect them ,you don't have to shout public.
Hata wahudumu wa bar ni binadamu. Waheshimiwe pia.
 
Udhalilishaji tu ,unamfanya waziri kama muhudumu wa baa.This is character assassination. Just respect them ,you don't have to shout public.
Hapana, that was a correct approach by mr President, nchi hii ina watu wamepewa mamlaka lkn wanafanya vitu na maamuzi ya hovyo huwezi amini, na unakuta ni wasomi kweli. binafsi nadhani hamna namna nyingine zaidi ya kuwakosoa hadharani ili na wengine wabadilike, nb: nilikuwa muhanga wa daraja hilo kama msafiri.
 
Kosa lake nini?
Hii iliyompata Engineer Isack Kamwelwe leo inapaswa aandike barua ya kujiuzulu ili kuwajibika kama waziri bila kusuburi alazimishwe kama Kangi Lugola.

Itakuwa jambo la kiungwana akikubali kama kiongozi kuwajibika kwa kujiuzulu kuliko kuendelea kukaa ofisini aking'ang'ania nafasi hiyo ya kisiasa iliyomletea mtafaruku mkubwa na bosi wake leo hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
March 16, 2020

Kilosa, Morogoro



Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli akiwa wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro akifanya ukaguzi wa daraja muhimu kwa taifa la Kiyegeya lililobomoka Machi 2, 2020 kufuatia mvua nyingi alionesha kutoridhishwa na utendaji wa safu za wateule wake hasa Waziri wa Uchukuzi, Ujenzi na Mawasiliano injinia Isack Kamwelwe (Mbunge wa jimbo la Katavi) kupitia CCM. Injinia Kamwelwe alipata kuwa meneja mkoa wa TANROAD na pia ofisa ngazi za juu TANROAD makao makuu kabla ya kujiingiza ktk siasa kupitia CCM.

Mh. Rais kuonesha mapungufu ya watendaji wake hakusita kumungunya maneno kiasi cha kusema ana hisia kuwa wateule wake wanahujumu juhudi na kufananisha kadhia hiyo na "Economic Sabotage" uhujumu wa uchumi wa nchi, maana daraja hilo si tu linaunganisha Tanzania bali pia na nchi za maziwa makuu za Burundi, Rwanda, DR Congo zinazotumia bandari ya Dar es Salaam.

Rais Magufuli akawaomba msamaha wananchi wa Kilosa na Tanzania kwa madhila makubwa yanayowakabili ikiwemo daraja lingine la wilaya hiyo kubomoka na hivyo wananchi kupata changamoto nyingi ikiwemo jinsi ya kufika ktk hospitali kubwa kutokana na daraja lao kutofanyiwa matengenezo baada ya daraja lao pia kusombwa na mafuriko.

Katika safari yake toka Dar es Salaam mpaka Kilosa alisimama mara kadhaa na kusikia vilio vingi vya wananchi wa mikoa ya Pwani na Morogoro juu ya utendaji hafifu wa wateule wake ktk sekta za afya, elimu na miundo mbinu ya barabara. Wananchi walionesha matamanio yao kuhusu sekta mbalimbali hayapewi vipaumbele na watendaji wa serikali waliopo maeneo yao.

Hawa viongozi wetu nao wakati mwingine kuna mambo mengine wanajitakia, hawajui kuwasoma viongozi wao. Mimi ningekuwa waziri kwenye Serikali ya JPM, ningekuwa mwangalifu sana na PM, kuliko hata Rais mwenyewe. Mimi ninaona kam PM ni mkali pengine kumzidi hata Mkuu wa Kaya, lakini sidhani kama wote wameshaliona hilo. Ningesikitika mno kumkosa Kamwele, kazi nzuri anayofanya. Mara nyingi mimi maamuzi ya JPM huwa yananipa amani sana isipokuwa tu pale anapokuwa ametumbua watu kama akina Kamwele. Kwa sababu kuna mtu mwingine kweli sababu ya kutumbuliwa inakuwa ipo na ipo valid lakini bado mnamumiss, case kama ilivyokuwa ya Simbachawene kabla hajarudi tena kwa mara ya pili. From my heart, Kamwele angetoka ningekosa amani kabisa
 
WAZIRI kamwelo Na Mfugale wanapaswa wajitathimini wenyewe na kisha wachukue hatua wenyewe sio kwa kukasirika kule kwa mh Rais!! Alikereka sana sana, inaonekana walimkatisha tamaa sana Rais,
Wakati mwengine tumrahisishie kazi Rais sio lazima akutimbue bali wewe mwenyewe unaweza jitafakari na kuwajibika kwa kukiuzulu mwenyewe kwa matendo yako, ni heshima kubwa kuliko kusubiria uwajibishwe, tujenge utamaduni wa kuwajibika wenyewe kabla
Ila jiwe anadhalilisha sana watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana, that was a correct approach by mr President, nchi hii ina watu wamepewa mamlaka lkn wanafanya vitu na maamuzi ya hovyo huwezi amini, na unakuta ni wasomi kweli. binafsi nadhani hamna namna nyingine zaidi ya kuwakosoa hadharani ili na wengine wabadilike, nb: nilikuwa muhanga wa daraja hilo kama msafiri.
Yeye akikosolewa hadharani unajua ambacho huwa anafanya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana, that was a correct approach by mr President, nchi hii ina watu wamepewa mamlaka lkn wanafanya vitu na maamuzi ya hovyo huwezi amini, na unakuta ni wasomi kweli. binafsi nadhani hamna namna nyingine zaidi ya kuwakosoa hadharani ili na wengine wabadilike, nb: nilikuwa muhanga wa daraja hilo kama msafiri.
Maamuzi gani ya wasomi,nikikwambia hilo daraja liliombewa pesa tangu 2015 na likapuuzwa na huo hao wanaowafokea utasemaje.Mtu hawezi kubadilika kwa kufokewa wewe mtu anabadilika kwa kuonywa kwa kutumia mifumo imara ya uongozi na malezi ya makuzi imara.Unaweza kumfokea mtu akawa na nidhamu ya uoga tu .Tujenge culture ya uwajibikaji .Mimi nikiona mtu ananifkea mbele za watu najua asilimia 100 ajiamini hata kidogo ni mwoga au ameadhirika kisaikologia .Iwe kazini au mahusiano ni ugonjwa
 
Maigizo tu. Hivi watu hawawezi kukarabati daraja au kipande cha barabara bila hizi drama na macamera. Mbona hatusikii haya nchi nyingine na mambo yanakwenda.
 
Maamuzi gani ya wasomi,nikikwambia hilo daraja liliombewa pesa tangu 2015 na likapuuzwa na huo hao wanaowafokea utasemaje.Mtu hawezi kubadilika kwa kufokewa wewe mtu anabadilika kwa kuonywa kwa kutumia mifumo imara ya uongozi na malezi ya makuzi imara.Unaweza kumfokea mtu akawa na nidhamu ya uoga tu .Tujenge culture ya uwajibikaji .Mimi nikiona mtu ananifkea mbele za watu najua asilimia 100 ajiamini hata kidogo ni mwoga au ameadhirika kisaikologia .Iwe kazini au mahusiano ni ugonjwa
Haya mambo ndio tunaambia watu humu mara kwa mara. Waziri au kiongozi yoyote hahitaji kutoka ofisini kwenda site kufokea watu mbele ya macamera ya wandishi wa habari. Yule Prof. Ndalichako alijikuta anajiaibisha kwa English mbovu baada ya kukurupuka kwenda kufokea wachina huku kafuatana na waandishi wa habari kutafuta kiki, kiki zikamtokea puani.
'Chains of command' zinafahamika! Mifumo ya kiutawala na managementi pia inajuliakana! Mbona kama viongozi siku hizi wanatumia sana approach ya micromanagement?
 
Hii movie ya leo wote wawili, Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Kamwele wamezitendea haki nafasi walizo act.
 
Inawezekana Mheshimiwa akagoma kutukarantini watanzania dhidi ya corona kwa kisingizia cha economic sabotage, sababu ideally ni lazime tule movement ban kwa takribani siku hizo hizo 14, hakuna kitu kitatembea kwenye hizo barabara kwa kipindi hicho.
 
Asimame pia hapo Segerea azungumze na Wale waliowapiga Wanawake. Hili aslifumbie macho wala asipite hivi.Wameliaibisha taifa.
Jiwe mwenyewe kaliingiza taifa mkenge vitu kibao aanze yeye kuachia nafasi kama kweli mzalendo au makosa akifanya mwingine ila kwake sahihi?😁😁😁
 
Hapana, that was a correct approach by mr President, nchi hii ina watu wamepewa mamlaka lkn wanafanya vitu na maamuzi ya hovyo huwezi amini, na unakuta ni wasomi kweli. binafsi nadhani hamna namna nyingine zaidi ya kuwakosoa hadharani ili na wengine wabadilike, nb: nilikuwa muhanga wa daraja hilo kama msafiri.
Mwambie na yeye awe tayari kukosolewa hadharani sio kukosoa na kukemea wengine tu ebo!!😅😅😅😅😅
 
Bagamoyo,
Vilio vya wananch ni sahihi kabisa na hata mimi naamini kwamba kwa jinsi mambo yalivyo,juhudi za Rais kuwaletea Watanzania maendeleo zinahujumiwa.Hili tumelisema mara nyingi huko nyuma,na kwa vile kalishuhudia yeye mwenyewe,labda sasa atakuwa makini zaidi katika kupokea ushauri wa washauri wake katika teuzi mbali mbali,kwa kuwa inawezekana nao wanamhujumu.
 
Hii iliyompata Engineer Isack Kamwelwe leo inapaswa aandike barua ya kujiuzulu ili kuwajibika kama waziri bila kusuburi alazimishwe kama Kangi Lugola.

Itakuwa jambo la kiungwana akikubali kama kiongozi kuwajibika kwa kujiuzulu kuliko kuendelea kukaa ofisini aking'ang'ania nafasi hiyo ya kisiasa iliyomletea mtafaruku mkubwa na bosi wake leo hii.
Kile kiyoyozi cha kwenye V8 unafikir mchezo nn kupita na ving'ora kuna raha yake bwana anaanzaje kujiuzulu kirahis

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom