Rais Magufuli amkaanga vikali Waziri Kamwelwe, atishia kumuweka ndani kwa Uhujumu Uchumi

Rais Magufuli amkaanga vikali Waziri Kamwelwe, atishia kumuweka ndani kwa Uhujumu Uchumi

March 16, 2020

Kilosa, Morogoro



Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli akiwa wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro akifanya ukaguzi wa daraja muhimu kwa taifa la Kiyegeya lililobomoka Machi 2, 2020 kufuatia mvua nyingi alionesha kutoridhishwa na utendaji wa safu za wateule wake hasa Waziri wa Uchukuzi, Ujenzi na Mawasiliano injinia Isack Kamwelwe (Mbunge wa jimbo la Katavi) kupitia CCM. Injinia Kamwelwe alipata kuwa meneja mkoa wa TANROAD na pia ofisa ngazi za juu TANROAD makao makuu kabla ya kujiingiza ktk siasa kupitia CCM.

Mh. Rais kuonesha mapungufu ya watendaji wake hakusita kumungunya maneno kiasi cha kusema ana hisia kuwa wateule wake wanahujumu juhudi na kufananisha kadhia hiyo na "Economic Sabotage" uhujumu wa uchumi wa nchi, maana daraja hilo si tu linaunganisha Tanzania bali pia na nchi za maziwa makuu za Burundi, Rwanda, DR Congo zinazotumia bandari ya Dar es Salaam.

Rais Magufuli akawaomba msamaha wananchi wa Kilosa na Tanzania kwa madhila makubwa yanayowakabili ikiwemo daraja lingine la wilaya hiyo kubomoka na hivyo wananchi kupata changamoto nyingi ikiwemo jinsi ya kufika ktk hospitali kubwa kutokana na daraja lao kutofanyiwa matengenezo baada ya daraja lao pia kusombwa na mafuriko.

Katika safari yake toka Dar es Salaam mpaka Kilosa alisimama mara kadhaa na kusikia vilio vingi vya wananchi wa mikoa ya Pwani na Morogoro juu ya utendaji hafifu wa wateule wake ktk sekta za afya, elimu na miundo mbinu ya barabara. Wananchi walionesha matamanio yao kuhusu sekta mbalimbali hayapewi vipaumbele na watendaji wa serikali waliopo maeneo yao.

Wasaidizi wa Rais wengi wao wanamuangusha sana,kila jambo hadi Rais aseme asiposema wanabakia wanarumbana tu hakuna kinachoendelea. Wananchi wa kule Mwanza wanaoishi maeneo ya barabara kutoka Mkuyuni-Mahina-Kanyerere-Nyangulugulu hadi Mwatex ni kama wanaishi uhamishoni maana barabara wanayotumia si barabara bali ni maandaki. Mbunge wa Nyamagana yupo, DC wa Nyamagana yupo, RC wa Mwanza yupo, Meneja wa Tanroads Mkoa wa Mwanza yupo, Waziri yupo lakini watendaji hao walifikia hatua ya kuwatishia wananchi waliotaka kumwambia Mheshimiwa Rais kuhusu kero ya barabara hiyo alipokuwa maeneo ya Iseni pale Butimba Mwanza wasiseme. Rais unayajua hayo? Unahujumiwa
 
Daaah! Yaani hadi huruma, ingawa nimependa nchi yetu sasa watu wanasemwa kwa ishu kama hizi ingekuwa zamani ungeskia mafuriko kaleta Mungu mimi waziri nifanyeje
Zamani ipi? AU unasema ile ya wakati wa tetemeko la Kagera? Ambayo hata michango ya kuwasaidia wakailamba?
 
Hapana, that was a correct approach by mr President, nchi hii ina watu wamepewa mamlaka lkn wanafanya vitu na maamuzi ya hovyo huwezi amini, na unakuta ni wasomi kweli. binafsi nadhani hamna namna nyingine zaidi ya kuwakosoa hadharani ili na wengine wabadilike, nb: nilikuwa muhanga wa daraja hilo kama msafiri.
Mkuu jambo la kusikitisha vigogo wa Tanroad walionekana kupwaya katika kujibu swali jepesi, swali ni wafanyakazi gani kimkoa wanahusika na ukaguzi wa madaraja katika mkoa huo.
Jambo jingine nimegundua kuwa Raisi Magufuli ametambua kuwa Key Perfomace Indicator yao sio kubwa kivile,alipitiliza kuwapamba hao vigogo lakini ni kama anajuta kuwafagilia,hadi akasema yeye Raisi ni layman lakini hawa Engineers hawajui hata sehemu rahisi kujenga barabara ya kupitishia daraja la muda.Kwangu naona Tanroad reshuffle and restructuring inakuja.
 
Mkuu jambo la kusikitisha vigogo wa Tanroad walionekana kupwaya katika kujibu swali jepesi, swali ni wafanyakazi gani kimkoa wanahusika na ukaguzi wa madaraja katika mkoa huo.
Jambo jingine nimegundua kuwa Raisi Magufuli ametambua kuwa Key Perfomace Indicator yao sio kubwa kivile,alipitiliza kuwapamba hao vigogo lakini ni kama anajuta kuwafagilia,hadi akasema yeye Raisi ni layman lakini hawa Engineers hawajui hata sehemu rahisi kujenga barabara ya kupitishia daraja la muda.Kwangu naona Tanroad reshuffle and restructuring inakuja.
Uko sahihi, hasa aliposema achague wanajeshi kuanzia waziri hadi mfagiaji. kwa aliesikia na aelewe akiwemo waziri husika! ni swala la muda tu.
 
Inajulikana.Kamwelwe hampendi Majaliwa,sijui walipishana wapi
Ndio.maana Majaliwa alipotoa.amri.meneja aondoke,Kamwelwe akamchuuza Mfugale nae bila adabu akamdhalilisha CeO wa seikali mbele ya hadhara
Huko nyuma huyo.kamwelwe aliwahi kumpinga majaliwa alipotoa maelezo na yeye kupinga hadharani kwa kusema Majaliwa ni.nani
 
March 16, 2020

Kilosa, Morogoro



Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli akiwa wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro akifanya ukaguzi wa daraja muhimu kwa taifa la Kiyegeya lililobomoka Machi 2, 2020 kufuatia mvua nyingi alionesha kutoridhishwa na utendaji wa safu za wateule wake hasa Waziri wa Uchukuzi, Ujenzi na Mawasiliano injinia Isack Kamwelwe (Mbunge wa jimbo la Katavi) kupitia CCM. Injinia Kamwelwe alipata kuwa meneja mkoa wa TANROAD na pia ofisa ngazi za juu TANROAD makao makuu kabla ya kujiingiza ktk siasa kupitia CCM.

Mh. Rais kuonesha mapungufu ya watendaji wake hakusita kumungunya maneno kiasi cha kusema ana hisia kuwa wateule wake wanahujumu juhudi na kufananisha kadhia hiyo na "Economic Sabotage" uhujumu wa uchumi wa nchi, maana daraja hilo si tu linaunganisha Tanzania bali pia na nchi za maziwa makuu za Burundi, Rwanda, DR Congo zinazotumia bandari ya Dar es Salaam.

Rais Magufuli akawaomba msamaha wananchi wa Kilosa na Tanzania kwa madhila makubwa yanayowakabili ikiwemo daraja lingine la wilaya hiyo kubomoka na hivyo wananchi kupata changamoto nyingi ikiwemo jinsi ya kufika ktk hospitali kubwa kutokana na daraja lao kutofanyiwa matengenezo baada ya daraja lao pia kusombwa na mafuriko.

Katika safari yake toka Dar es Salaam mpaka Kilosa alisimama mara kadhaa na kusikia vilio vingi vya wananchi wa mikoa ya Pwani na Morogoro juu ya utendaji hafifu wa wateule wake ktk sekta za afya, elimu na miundo mbinu ya barabara. Wananchi walionesha matamanio yao kuhusu sekta mbalimbali hayapewi vipaumbele na watendaji wa serikali waliopo maeneo yao.


For sure kabisa, hapa kwa mara ya pili au ya kwanza nakubaliana na Magufuli....

Ni ngumu sana kuamini kuwa daraja kama hili limekatika two weeks ago lakini halijajengwa na sisi ni nchi....!!

Kwa kiongozi makini alitakiwa kujua kuwa daraja hilo ni kiungo muhimu zaidi ya 98% ya eneo lote la nchi yetu achilia mbali nchi jirani hizi; DRC, Zambia, Rwanda, Burundi, Kenya na Uganda....

Lakini cha ajabu siku 14 nothing has been serious done...!!

Tatizo ni nini? Fedha hakuna? Kuogopa kufanya maamuzi? Kukwamisha tu mambo or what??

USHAURI KWA MZEE KAMWELWE;

Nimekutazama na kukuona jinsi ulivyokuwa mnajibizana na mwanaCCM mwenzako. Nikakuona umekuwa mdogo kama piriton na sijui kama hukumwaga maji chini.....

Binafsi nimekuhurumia sana na kwa hakika kuna kitu kinakusumbua lakini ulishindwa kukisema mbele ya Rais wako....

Sasa basi, kama msamaha wako ulikubaliwa, nakushauri ukirudi ofisini ama nyumbani kwako, kaa chini kwa utulivu, andika barua ya kujiuzuru kwa heshima.....

Wewe ni Mzee, umeshakua, inatosha. Tawala za kiimla huwa zinapiga kotekote. Dikteta huweza hata kugeukia hata wenzake na "kuwala vichwa vyao" iwapo akiona unamharibia kufikia matamanio yake....

Usisubiri ufukuzwe ama "uliwe kichwa" na jamaa yenu huyo. Unaweza kupotelea kusikojulikana, shauri lako.....

Lakini kikubwa zaidi, nadhani, you are not fit for that job no matter whether you're an engineer or whatever. Kipimo cha ukomo wa uwezo wako, kilikuwa ni daraja hilo. You have failed Mzee.....!!

Waachie wengine kazi hiyo, pumzika kula pesheni yako kwa Amani.....!!!
 
Ningekuwa mimi ni huyo Waziri kwa kweli ningeandika barua tu ya kushukuru na kupumzika!! Aisee!!
 
Hisia zangu zilinituma kuwaza hiyo ekonomik sabotage.
 
March 19, 2020
Waziri Kamwelwe : Yapi Merkezi mkandarasi wa ujenzi wa reli mpya SGR atua na vifaa daraja la Kiyegeya barabara ya Morogoro - Dodoma

Futuatia chagizo la Rais na wadau wengine wanaotumia barabara kuu ya Dodoma Morogoro, wizara ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano imeomba msaada wa kampuni ya Turkey ya Yapi Merkezi na serikali itanunua makalavati toka kampuni hiyo ya Yapi Merkezi.



Kampuni hiyo ya Yapi Merkezi itatoa makalavati 120 ya sege wanayotumia kujengea reli mpya ya SGR ili yatumike kukarabati njia hiyo kuu ya barabara ya Morogoro Dodoma sehemu ya makalavati ya daraja la Kiyegeya.

Source : millard ayo

Yapi Merkezi: YM is ranked as 78th in 2017 in the Top International Contractor’s List prepared by monthly magazine Engineering News Record (ENR). Besides it is ranked as 9th in 2017 in Mass Transportation / Light Rail Category of Top International Contractor’s List.
 
March 20, 2020
Kidatu , Morogoro

Kamwelwe atinga Daraja la mto Ruaha Mkuu

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano akiri taasisi ya TANROAD ilizembea ktk kuhakikisha barabara zote muhimu na madaraja yanayounganisha nchi yawe yanapitika na pale inapohitajika matengenezo basi yafanyike kwa uharaka.


Waziri Kamwelwe alifika katika daraja hilo kuona ukarabati wa kingo za mto na daraja zilizoliwa na kasi kubwa ya maji mengi ya mto Ruaha Mkuu.

Source : Azam TV
 
Ifakara, Morogoro

RAS wa Mkoa wa Morogoro awahimiza makandarasi Reynolds Construction kukamilisha ujenzi wa barabara na makalavati katika wilaya ya Ifakara kutokana na umuhimu wake kwa uchumi wa mkoa na taifa zima la Tanzania




27 Jan 2020
Na.Vedasto George. Serikali Mkoani Morogoro imesema hairidhiki na kasi ya Ujenzi wa Barabara ya Kidatu hadi Ifakara inayojengwa kwa kiwango cha lami na Kampuni ya ujenzi ya ReynoldConstruction (RCC) ya kutoka nchini Nigeria baada ya muda uliopangwa kukaribia kuisha huku mradi umefikia asilimia 10 pekee.


Source: RS Morogoro / SUA Media
 
ZIARA YA KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO KUKAGUA UJENZI WA BARABARA IFAKARA- KIDATU

Premiered on 27 Jan 2020
Na.Vedasto George. Serikali Mkoani Morogoro imesema hairidhiki na kasi ya Ujenzi wa Barabara ya Kidatu hadi Ifakara inayojengwa kwa kiwango cha lami na Kampuni ya ujenzi ya ReynoldConsrtraction (RCC) ya kutoka nchini Nigeria baada ya muda uliopangwa kukaribia kuisha huku mradi umefikia asilimia 10 pekee.

Kauli hiyo ya kutoridhishwa na ujenzi huo imetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo Januari 25 alipotembelea ujenzi wa Mradi na kupokea taarifa ya ujenzi huo kwa kifupi ambayo ilionekana kumsikitisha kutokana na kasi ndogo ya ujenzi inayoendelea.

“Mradi uko asilimia kumi ya utekelezaji wakati muda umekwisha kwa asilimia tisini, hii haisubiri mtu aambiwe kuwa kazi hairidhishi, kazi hii hairidhishi. Na hairidhishi kwa sababu kutoka Mikumi mpaka Ifakara ni barabara hii moja tu hakuna barabara nyingine inayotegemewa”. Alisema Mhandisi Kalobelo.

Aidha, Mhandisi kalobelo amesema matumaini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye mwezi May 2018 alizindua ujenzi wa Barabara hiyo anategemea mradi huo kukamilika kwa wakati ambao ni ndani ya miezi 36 ili kuwaondolea wananchi wake kero yausafiri, lakini kazi bado iko asilimia 10.

Kwa sababu hiyo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ambaye amesema kuwa amekuwa haridhishwi na ujenzi wa mradi huo hivyo amemwaagiza Mkandarasi Mshauri na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Morogoro kumsimamia kwa ukaribu mkandarasi huyo na pale ambapo atakwenda ndivyo sivyo wachukue hatua mara moja.

Lakini pili, Katibu Tawala Kalobelo, amesema kama kasi ya Ujenzi haitobadilika, Mkoa utachukua hatua za haraka kutoa taarifa ngazi zinazohusika ili kumchukulia hatua zinazostahili juu kwa lengo la kukamilisha azma ya Mhe. Rais ya kujenga barabara hiyo kwa kiwangocha lami kwa kuwa eneo la Kilombero linachangia kwa kiasi kikubwa katika kutoa chakula kwa watanzania walio wengi hapa nchini.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo alimweleza Katibu Tawala wa Mkoa waMorogoro namna ambavyo barabara hiyo imekuwa kero kwa wasafiri na wenyeji wa Wilaya hiyo hususan katika kipindi cha mvua, ambapo usiku wa kuamkia Januari 25 karavati moja eneo la Kanolo Kata ya Kisawasawa lilichukuliwa na maji na kusababisha mawasiliano kukatika kwa zaidi ya saa saba.

Pamoja na Mkuu huyo wa Wilaya kutoa pongezi kwa ushirikiano aliouonesha Mkandarasi katika kurejesha haraka mawasiliano hayo bado amezungumzia ujenzi wa barabara hiyo kuwa sio wakuridhisha huku akitoa wito kwa Mkandarasi kufanya utafiti kwa makaravati yanayojengwa kwani inaonekana kuwa ni madogo ukilinganisha na wingi wa maji ya mvua yanayopita katika maeneo hayo wakati wa Mvua.

Naye Mhandisi wa Miradi kutoka Wakala wa Barabara nchini - TANROADS Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Salehe Juma amekiri kuwa hakuna kiongozi yoyote katika Ofisi yao anayeridhika na kasi ya ujenzi wa barabara hiyo na kwamba mpaka sasa Mkandarasi yuko nyuma ya muda kwa wiki 79 huku akifafanua kuwa taarifa zote na ushauri mbalimbali ulishafikishwa ngazi za juu.

Kwa niaba ya Mhandisi Mshauri wa Mradi huo wa Barabara, Mhandisi Maburuge Mapambano amekiri mradi kuwa nyuma ya wakati hata hivyo alijitetea kuhusu ucheleweshwaji wa kazi hiyokuwa unatokana na ushuru bandarini ambapo vifaa vyake vilikwama bandarini kwa kipindi kirefu.

Kwa upande wao Shaban Likulike na Ally Miginga kutoka kijiji cha Kanolo Kata ya Kisawasawa Wilayani Kilombero miongoni mwa wakazi wanavyotakiwa kunufaika na barabara hiyo wametoa maoni yao kwa Serikali kutaka kumbadilisha Mkandarasi huyo kwa kuwa ameonesha hana uwezo wa kukamilisha kazi hiyo kwa muda uliopangwa. Barabara ya Kidatu – Ifakara inajengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi za kitanzania Bil. 101 Ujenzi wake umeanza tarehe 2 Oktoba 2017 na kutegemea kukamilika mwezi Aprili tarehe 20 mwaka huu.
 
March 18, 2020
Iringa, Tanzania

Barabara ya Ipogolo Iringa kufuatia mvua nyingi na maporomoko ya udongo



Source : DARMPYA TV
 
March 16, 2020

Kilosa, Morogoro



Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli akiwa wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro akifanya ukaguzi wa daraja muhimu kwa taifa la Kiyegeya lililobomoka Machi 2, 2020 kufuatia mvua nyingi alionesha kutoridhishwa na utendaji wa safu za wateule wake hasa Waziri wa Uchukuzi, Ujenzi na Mawasiliano injinia Isack Kamwelwe (Mbunge wa jimbo la Katavi) kupitia CCM. Injinia Kamwelwe alipata kuwa meneja mkoa wa TANROAD na pia ofisa ngazi za juu TANROAD makao makuu kabla ya kujiingiza ktk siasa kupitia CCM.

Mh. Rais kuonesha mapungufu ya watendaji wake hakusita kumungunya maneno kiasi cha kusema ana hisia kuwa wateule wake wanahujumu juhudi na kufananisha kadhia hiyo na "Economic Sabotage" uhujumu wa uchumi wa nchi, maana daraja hilo si tu linaunganisha Tanzania bali pia na nchi za maziwa makuu za Burundi, Rwanda, DR Congo zinazotumia bandari ya Dar es Salaam.

Rais Magufuli akawaomba msamaha wananchi wa Kilosa na Tanzania kwa madhila makubwa yanayowakabili ikiwemo daraja lingine la wilaya hiyo kubomoka na hivyo wananchi kupata changamoto nyingi ikiwemo jinsi ya kufika ktk hospitali kubwa kutokana na daraja lao kutofanyiwa matengenezo baada ya daraja lao pia kusombwa na mafuriko.

Katika safari yake toka Dar es Salaam mpaka Kilosa alisimama mara kadhaa na kusikia vilio vingi vya wananchi wa mikoa ya Pwani na Morogoro juu ya utendaji hafifu wa wateule wake ktk sekta za afya, elimu na miundo mbinu ya barabara. Wananchi walionesha matamanio yao kuhusu sekta mbalimbali hayapewi vipaumbele na watendaji wa serikali waliopo maeneo yao.

Ajatajaa kumweka.NDAN BANA loh
 
Back
Top Bottom