Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Pale tunaposhangilia Kutokuwa na bandari badala ya kuwa na Bandari!

Serikali ya awamu ya Tano inanikumbusha msemo maarufu wa Waziri Njonjo wa Kenya aliyeipiga vijembe serikali ya Nyerere baada ya Nyerere kutoa kauli ya kuiikejeli Kenya kwa kusema "Kenya is a man eat man society", Njonjo akasema “Tanzania is a man eat nothing society"!
Kwa hiyo Njonjo alikuwa anakubali uhalali wa "Man eat man society"? Sote tunajua hakuwezekani kuwepo "Man eat nothing society."
 
Shamba la bibi, kuna mambo lazima tukubali Rais wetu anajitahidi sana kuyaweka vizuri na tumpe heko. Katika kulinda uridhi wetu kwa kweli nampa heko, anajitahidi sana.

Mikataba ya hovyo kama hii ni wizi wa mchana kabisa. Hamna maslahi kwetu kama watanzania. Hii mikataba kama ya mangungo ifutiliwe mbali.

Natamani aingilie mikataba ya gasi pia, kule nako sijui kama tupo salama.

Kama watakubaliana na mkataba ambao ni win win wajenge ila mkataba ambao hatufaidi chochote, hatuhoji chochote yaani tumeuza uridhi wetu kwa miaka 99 bila chochote watu wanachuma tu, tena bado turejeshe gharama na hatuna uwezo wa kufanya chochote mbadala, hapana kwa kweli..khaaa

Heko Rais, tuliendie urithi wetu tutakukumbuka kwa hilo.
Kwenye makinikia mliletewa porojo kama hizi kumbe ikaja kujulikana ni uongo mwingi na ukweli kidogo
Usiamini kila unachoambiwa,soma mkataba kwanza
 
Ni Tanzania tu ambapo kiongozi aliyekuwa kimya mpaka mkataba wa kinyonyaji ukapita anakuja kusema huo mkataba ulikuwa mbovu! Wakati huo huo hata yeye huo Mkataba hataki kuonyesha nini kiko ndani ya huo mkataba alipokubali upite, kisha akaukataa. Kichekesho ni pale rais huyo huyo anapogomea katiba mpya ili mambo yaendeshwe kwa uwazi zaidi na watu wanashangilia na kusema ni kiongozi sahihi!
Umeona unafiki wa viongozi wa ccm .
 
Ila hujiulizi nani alikuwa waziri wako wa ujenzi wakati president kikwete anaweka jiwe hili la msingi,why hawaku rise hizi issue?,uoga wao na njaa ya matumbo yao wakawa kimya kulinda vibarua vyao na sasa wanataka kujifanya ni mashujaa,politics za kinafiki zitatuumiza sana nchi hii ,na tukitukanwa kwa kuitwa pithole country tunachukia wakati ndio ukweli wenyewe.
Limbukeni kwa kudanganya ni kiboko aisee utafikiri hakuwa anagonga meza kuupitisha mkataba kwa mbwembwe nyingi .
 
Jana kwa Bahati tu bilious natafuta channel kwenye Luninga , nikakuta channel moja mwisho mwisho wanazungumzia uwekezaji wa waWachina na mokopo Yake ya kifisadiya Uwanja wa Ndege mkubwa zaidi huko ASIA.

Kifupi hawa Jamaa ni wajanja sana.
 
Si alikuwa Mbunge huyu na Waziri wa Ujenzi? Hakuyaona masharti hayo kabla ili kupinga mradi huo kama Mbunge na Waziri wa Ujenzi? Mtu mzima HOVYOOOO!


View attachment 1123438

RAIS John Magufuli amesema sababu kubwa ya kusitishwa kwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ni masharti magumu yaliyomo katika mkataba wa utekelezaji wa kazi hiyo.

Jiwe la msingi la ujenzi wa bandari hiyo liliwekwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete mwaka 2015 na ulitarajiwa kugharimu dola za Marekani bilioni 10. Bandari hiyo endapo ingejengwa ingekuwa kubwa zaidi Afrika Mashariki ikiwa na ukubwa wa ekari 3,000 na viwanda 190 vingejengwa.

Akizungumza jana kwenye mkutano wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliowashirikisha wafanyabishara kutoka wilaya 139 nchini, Rais Magufuli aliweka wazi sababu za kusitishwa kwa ujenzi wa bandari hiyo. Rais Magufuli alisema “kwenye mkataba wa ujenzi wa bandari hiyo kulikuwa na vipengele vya ovyo”. Rais Magufuli alisema mojawapo ya masharti ni kutojengwa wala kuendelezwa kwa bandari yoyote kuanzia eneo la Tanga hadi Mtwara.

"Yaani kwenye eneo lote kuanzia Tanga hadi Mtwara kusijengwe bandari yoyote. Bandari ya Kilwa tusiiendeleze, Bandari ya Mtwara ambayo itawezesha mikoa ya kusini kupokea mafuta badala yake Dar es Salaam kisha yarudi huko, hatutakiwi kuiendeleza, Barabara kutoka Mtwara hadi Bamba Bay ambayo itatuwezesha kusafirisha mizigo hadi Msumbiji tusiijenge," alisema Rais Magufuli

Pia alisema wawekezaji hao wangeweza kumiliki ardhi kwa hati ya miaka 99 pamoja na kutoruhusiwa kuuliza nani anamiliki eneo hilo. Rais Magufuli alisema sharti lingine ni gharama zitakazotumiwa na mwekezaji huyo katika ujenzi wa bandari hiyo kutakiwa kurejeshwa.
 
Zitto ndo kasaini huo mkataba?
Zitto hatetei huo mkataba Bali kusitishwa kujengwa hyo BANDARI.
mikataba MIBOVU WALIINGIA CCM NA MWENYEKITI WENU WA MSOGA.
Niliwashangaa sana Chadema kutetea huu mradi, isijekuwa wabunge wa hiki chama walirubuniwa. Nina mashaka sana na Zito kwa sasa. Maana aliutetea sana huu mradi.
 
Ameongea kwa uchungu mwingi hadi nimemhurumia mzee wa watu, sio kwa wawekezaji, sio kwa Watanzania, kila mtu mpigaji. Makajanja wa Dar walikwenda Bagamoyo wakatia kapuni mabilioni ya hela na kuwaacha wazawa na wakazi wa Bagamoyo mikono mitupu, nao wawekezaji wanaonekana kuja na masharti ya kiajabu ajabu.

Lakini tatizo hamsemi kimoja mueleweke nini sababu haswa za kusitishaa huo mradi, maana hapa rais amesema mengi ambayo hayajawahi kutajwa kati ya yote ambayo huwa mnayasema, halafu kama kweli hajaongeza chumvi, then ina maana rais Kikwete alikua anairubuni nchi yenu, kama kweli Kikwete alikubaliana na yote hayo yaliyotajwa humo, aisei nitamshangaa sana huyo rais wenu wa zamani, alikua ameipokeza nchi kwa watu mchana peupe.
Japo pia ni vigumu kuamini ukweli bila kuskliza upande wa pili, maana kila siku tunaskia ya nyie, hatujaskia naye muwekezaji kama kweli alikua na masharti kama hayo ya kuikoloni na kuifilisi nchi ya Tanzania.
 
Mikatabba ya Kiwanja cha ndege cha Chato, ya Stiegler's Gorge, ya ununuzi wa ndege pia viwekwe hadharani, ili watanzania wafanye comparisons!!!
Kwanini hukufanya comparison masharti ya hiyo bandari???? Tatizo hamtaki kumuamini kiongozi na kumuacha afanye kazi, mmempa jukumu na kuongoza nchi basi muaminini
 
Mimi naamini hayo mawazo yako ni mazuri ila siyo kwamba hayaja fikirika na wenye dhamana ya uongozi tuliowapa, isitoshe miaka 99 ni mingi sana kutokuendelezwa kwa bandari nyingine yoyote alafu tutegemee bandari Mona kwa nchi kubwa(geographically) kuleta maendeleo ya haraka. Kitu cha msingi na ili mambo yaende sawa katika taifa hili ni TUMUAMINI RAISI,anania njema na Tanzania.
 
Hiyi ilikuwa kazi kuu ya serikali ya awamu ya nne na watendaji wake wakuu!! Halafu unaona watu wanakenua!! Hata mababu zetu ambao hawakuwa wamepata elimu ya hata kindergarten ya Kimangaribi(Western education) hawakuwa na akili finyo kama za wasomi wa vyuo vikuu wenye Masters na PhDs!!!! Kudos Rais Dr Magufuli.
Hivi hiyo mkataba ilikua inatoka China na moja kwa moja adi ikulu? yaani haipiti wizarani? make naona sign inatiwa chini ya wizara husika na mawaziri husika wakiwepo.
Hapa tunamlaumu Mawaziri wa sheria; biashara na wengine kuhusu ishu ya korosho..ila cha kushangaza unaweza kuta huo mkataba inayomkono wa waziri wa ujenzi wa wakati huo JPM.

Na kama rais alisign bila wizara kushirikishwa natambua kuna loophole iliyompa mh Rais mamlaka hayo na kilimkera sana waziri wakati huo akiwa Jpm lakini bado yupo hapo hataki kubadilisha hizo sheria wala kikatiba zikabadilika anasubiri mwenye nia mbaya aje aingie azitumie; mimi nasema na yeye hana nia njema kama walewale.

Kuna ishu ya Rais kugawa vipande vya rasilimali apendavyo kama utalii kule Loliondo kwa Wadubei; cha kushangaza awamu hii wameingia na hawataki kuzibadilisha ata kama katiba inasema wazilete mezani wasibaki kutaka sifaza muda mfupi tu.
 
Ameongea kwa uchungu mwingi hadi nimemhurumia mzee wa watu, sio kwa wawekezaji, sio kwa Watanzania, kila mtu mpigaji. Makajanja wa Dar walikwenda Bagamoyo wakatia kapuni mabilioni ya hela na kuwaacha wazawa na wakazi wa Bagamoyo mikono mitupu, nao wawekezaji wanaonekana kuja na masharti ya kiajabu ajabu.

Lakini tatizo hamsemi kimoja mueleweke nini sababu haswa za kusitishaa huo mradi, maana hapa rais amesema mengi ambayo hayajawahi kutajwa kati ya yote ambayo huwa mnayasema, halafu kama kweli hajaongeza chumvi, then ina maana rais Kikwete alikua anairubuni nchi yenu, kama kweli Kikwete alikubaliana na yote hayo yaliyotajwa humo, aisei nitamshangaa sana huyo rais wenu wa zamani, alikua ameipokeza nchi kwa watu mchana peupe.
Japo pia ni vigumu kuamini ukweli bila kuskliza upande wa pili, maana kila siku tunaskia ya nyie, hatujaskia naye muwekezaji kama kweli alikua na masharti kama hayo ya kuikoloni na kuifilisi nchi ya Tanzania.

Rais Akisema hatuhitaji kusikia upande wa pili,
Besides, Kikwete was not Different from Uhuru Kenyatta and William Ruto.
 
Back
Top Bottom