Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Hivi hiyo mkataba ilikua inatoka China na moja kwa moja adi ikulu? yaani haipiti wizarani? make naona sign inatiwa chini ya wizara husika na mawaziri husika wakiwepo.
Hapa tunamlaumu Mawaziri wa sheria; biashara na wengine kuhusu ishu ya korosho..ila cha kushangaza unaweza kuta huo mkataba inayomkono wa waziri wa ujenzi wa wakati huo JPM.

Na kama rais alisign bila wizara kushirikishwa natambua kuna loophole iliyompa mh Rais mamlaka hayo na kilimkera sana waziri wakati huo akiwa Jpm lakini bado yupo hapo hataki kubadilisha hizo sheria wala kikatiba zikabadilika anasubiri mwenye nia mbaya aje aingie azitumie; mimi nasema na yeye hana nia njema kama walewale.

Kuna ishu ya Rais kugawa vipande vya rasilimali apendavyo kama utalii kule Loliondo kwa Wadubei; cha kushangaza awamu hii wameingia na hawataki kuzibadilisha ata kama katiba inasema wazilete mezani wasibaki kutaka sifaza muda mfupi tu.
'ruhi' watu wamekazana sana kutaka sote tukubali uigizaji huu kuwa ndio hali halisi.
Hawaamini kuwa wapo wanaoona na kutambua uigizaji na kuuweka pembeni na kuwaambia ukweli ulivyo.

Ni wajibu wa wanaouona ukweli na kuusema bila kuchoka.
Hawa wanaotafuta kuwalaghai watu wakidhani wote ni wajinga, mwishowe ulaghai wao utaonekana wazi. Jitihada zote za kuzima vyombo vya habari visifanye kazi bila kuingiliwa ni sehemu ya kupumbaza watu na ni njia hizo hizo walizodhani ujinga wa waTanzania utazidi kuenea ili waendelee kulaghai watakavyo.

Huu ni uongozi wa ajabu sana.
 
Na kama rais alisign bila wizara kushirikishwa natambua kuna loophole iliyompa mh Rais mamlaka hayo na kilimkera sana waziri wakati huo akiwa Jpm lakini bado yupo hapo hataki kubadilisha hizo sheria wala kikatiba zikabadilika anasubiri mwenye nia mbaya aje aingie azitumie; mimi nasema na yeye hana nia njema kama walewale.
Watu hawawezi kuyasoma haya na wakayaelewa? Tuna tatizo gani nchi hii!
 
Shamba la bibi, kuna mambo lazima tukubali Rais wetu anajitahidi sana kuyaweka vizuri na tumpe heko. Katika kulinda uridhi wetu kwa kweli nampa heko, anajitahidi sana.

Mikataba ya hovyo kama hii ni wizi wa mchana kabisa. Hamna maslahi kwetu kama watanzania. Hii mikataba kama ya mangungo ifutiliwe mbali.

Natamani aingilie mikataba ya gasi pia, kule nako sijui kama tupo salama.

Kama watakubaliana na mkataba ambao ni win win wajenge ila mkataba ambao hatufaidi chochote, hatuhoji chochote yaani tumeuza uridhi wetu kwa miaka 99 bila chochote watu wanachuma tu, tena bado turejeshe gharama na hatuna uwezo wa kufanya chochote mbadala, hapana kwa kweli..khaaa

Heko Rais, tuliendie urithi wetu tutakukumbuka kwa hilo.
Umeuona huo Mkataba? unataka kuniambia Mkwere alikuwa mwehu wakiwango hicho chakutaka kuiuza nchi yake?
 
Kwani huo wa Bagamoyo ulimeshawekwa wazi? sianaongea yeye tu bila wengine kujilidhisha kama ni kweli au ni urongo
Mikatabba ya Kiwanja cha ndege cha Chato, ya Stiegler's Gorge, ya ununuzi wa ndege pia viwekwe hadharani, ili watanzania wafanye comparisons!!!
 
Rais Akisema hatuhitaji kusikia upande wa pili,
Besides, Kikwete was not Different from Uhuru Kenyatta and William Ruto.

Haijawahi kutokea nchi yoyote ikakubali masharti kama hayo, sio Afrika wala nje, masharti ya kikoloni kabisa, nchi ilikua imeuzwa, bado nashangaa Kikwete alikua kweli ameyakubali yote hayo.

Eti msiendeleze bandari yoyote kutokea Tanga hadi Mtwara, na mengine ya kiajabu ajabu ameyataja rais wenu. Kama kweli Kikwete anatazama hizi hotuba lazima anapata aibu sana.
Hii hadi tuwasklize wawekezaji, ni ngumu kumeza kama ilivyo.
 
On this project,I think he did the right thing to terminate the contract.Listening to him explain with a lot of bitterness shows how the Chinese wanted to milk the country dry.Hongera Magufuli!
 
Haijawahi kutokea nchi yoyote ikakubali masharti kama hayo, sio Afrika wala nje, masharti ya kikoloni kabisa, nchi ilikua imeuzwa, bado nashangaa Kikwete alikua kweli ameyakubali yote hayo.

Eti msiendeleze bandari yoyote kutokea Tanga hadi Mtwara, na mengine ya kiajabu ajabu ameyataja rais wenu. Kama kweli Kikwete anatazama hizi hotuba lazima anapata aibu sana.
Hii hadi tuwasklize wawekezaji, ni ngumu kumeza kama ilivyo.
Na katika gesi alichelewa, akakuta maji yameishamwagika.

Halafu unakuta kuna mpumbavu anajisikia vibaya kisa magufuli haongei kiingereza fasaha[emoji16][emoji16][emoji16], hapa ndio utajua kila binaadam ana kipaumbele chake.
 
"Natamani aingilie mikataba ya gasi pia, kule nako sijui kama tupo salama"Hata mimi natamani aingilie huku ingawa najua huku pia lazima kuna michezo imechezwa na hakuko salama...
Bila kusahau wa Catle
 
please my no 1,kipindi cha awamu ya nne wewe si ulikuwa waziri ?why hukuliona hili na kulizungumzia?njaa yako ilikupeleka usiyaseme haya?na please my no 1 tuelezee also kuhusu mauzo ya nyumba za serikali je yalikuwa above the board???
 
Kuna pahali Magufuli ameongea kuhusu bandari ya Dar, yenye project ya Sh1.2 trillion.. Amesema ''Tumekopa fedha, tunatumia fedha yetu.''.
Leo hii nimekuja kujua kwamba 'pesa yetu' ina maana tofauti Tanzania.
 
That was the best decision if those were the terms they gave, burdening your country and enslaving your people for generations to come so that you can have a shiny new port that will not not be fully utilized unless you shut down the other port.

It's like telling me to cut my hand so that you give me food.

Africans should vigorously develop their own local capacity esp in TECH, so that we stop relying on these scam leeches.
 
Mfa maji haachi kutapatapa...kuamini Magufuli inakuwa ni ngumu Sana bill kusikiza upande huo mwingine.
 
Mikatabba ya Kiwanja cha ndege cha Chato, ya Stiegler's Gorge, ya ununuzi wa ndege pia viwekwe hadharani, ili watanzania wafanye comparisons!!!
Kwani hiyo mikataba ni ya wawekezaji kutoka nje?
 
Back
Top Bottom