Sheria za kibaguzi.
Watu ambao hawana uwezo wa kuwa na nyumba, wafanyakazi wa chini serikalini hawasaidiwi kupata makazi.
Watu wenye uwezo wa kuwa na nyumba hawa marais, tena wana nyumba zao tayari, ndio wanajengewa nyumba.
Kwake wanyonge hawana thamani labda mdomoni tuMbona hawaweki Sheria ya kuwajengea wastaafu WALIMU, MANESI au MADAKTARI? Upendeleo huo utawasaidia nini baada ya safari ya hapa DUNIANI?
Never ever entertain national resources wastage.mkuu,muache mzee JK ale maisha tuwe na shukrani wakati mwingine,kwani akijengewa hilo jumba itapunguza nini kwenye taifa ? mbona Nyerere alijengewa hamku mind
mkuu,muache mzee JK ale maisha tuwe na shukrani wakati mwingine,kwani akijengewa hilo jumba itapunguza nini kwenye taifa ? mbona Nyerere alijengewa hamku mind
Humuoni kwenye kampeni leo JK alikuwa Ukonga. Mwambie babako naye agombee uraisHilo haliwezi kumshawishi mzee JK ampigie Magu kampeni.
Fedha za WIZI za raia masikini. Kwanini hizo pesa wasipeleke kutatua shida mbalimbali za wananchi?
Dawa ya haya yote ni uwepo wa katiba mpya.Hapana huwezi kuwa na sheria mbili katika nchi moja, hawa wakistaafu walipwe 80% ya mshahara wa wakati huo kwa maana nyingine siku akija rais kichaa kuongeza mshahara 300% basi nao 80% ila kwa wastaafu wengine pamoja na kufanya kazi zaidi ya miaka 30 mazingira magumu lakini wanalipwa pesa ileile hata kama maisha yamebadilika. kama kuna mtu alistaafu 1990 sasa sijui mishahara ilikuwa kiasi gani usishangae kukuta mtu analipwa alfu 20. Hawa viongozi wamejenga nyumba nyingi tu walizipata kivipi sijui ila kwanini kuwajengea tena? Si walilipwa stahiki zao. kwa hili hapana basi ingekuwa hata nyumba ya kiasi nyumba utasema Mall. Wewe katizame wanajeshi wakistaafu utatamani kulia.
Serikali ilikiwa wapi kujenga nyumba hiyo mapema.wamesubiri mzew wa watu amebakiza miaka michacjhe ndiyo wanamjengea.ataaishi muda mfupi halafu itakuwa ya Ridhiwani na wadogo zake
ya Mwinyi inajengwa wapi,?
JK anastahili heshima kwa kazi nzuri aliyoifanyia Taifa letu.
Tuwaenzi wazee wetu.
Umeonesha mfano wa Kuigwa Dr. Magufuli.
Kwenda kipindi hiki cha kampeni ni kumsimanga JKRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli leo ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba maalumu ya Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.
Ujenzi wa Nyumba hiyo inajengwa na Serikali kwa mujibu wa Sheria namba 3 ya Mwaka 1999 inayoainisha ujenzi wa Nyumba maalumu kwa ajili ya makazi ya waheshimiwa Marais mara wanapostaafu.
View attachment 1604017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba ambayo Dkt. Kikwete anajengewa na Serikali eneo la Kawe Beach jijini Dar es salaam leo Jumapili Oktoba 18, 2020.
View attachment 1604019
View attachment 1604020
Kama rais amewatumikia vizuri wananchi Mimi nafikiri ni vyema kujengewa makaazi yenye hadhi yake.Ni jambo jema.